mama firstborn
Member
- May 30, 2023
- 43
- 130
Habari za jioni.
Mimi ni mama mtu mzima nina watoto 4 kwa mume wangu wa ndoa kabisa.
Niende kwenye mada.
Miaka 10 iliyopita nilifumaniwa na mtoto wangu wa kiume (my first born). Sikuamini kilichotokea nilishituka sana kwa hile tukio lilotokea.
Mimi nafanya kazi kwenye wizara moja hivi nipo hapa dsm mpaka sasa. Miaka iliyopita niliingia mahusiano na Baba mmoja hivi anafanya kazi wizara nyingine tofauti na yetu, nilikutana naye kwenye kikao vya ofisini.
Mimi ni kawaida yangu kumcheat mume wangu, japo hajawahi kunitilia hofu kama nimewahi kumcheat maana mara nyingi navizia akiwa safarini ndo ninafanya hivyo. Maana ninajua kumcheta mwanaume ni hatari sana kwani wanaume wana wivu sana na hasira, kama mume wangu namfahamu ni mtu mwenye hasira sana, so nilijitahidi asijue kabisa.
Sasa kuna siku mimi nilienda kwenye duka langu maana kwenye duka langu kabla jioni ijafika lazima niwepo ndo nifunge na wafanyakazi waondoke pale. Sasa kipindi tunamaliza yule Baba alinipigia simu nikamwambia nipo sehemu falani, nikamuelekeza akafika na alipofika wafanya kazi wangu nao wakawa wanaondoka muda huo huo. Mimi nikamkaribisha mchepuka ndani, sasa kwenye duka kuna ofisi kwa ndani si nikaenda nae mapaka kwenye ofisi katika kuongea kama 20 minutes, kwa sababu ni mchepuka tukajisahau akaanza kunishika na kuanza kukiss each other katika kunishikashika nikajisahau.
Kumbe mtoto wangu wa kwanza alikuja pale dukani aliingia baada ya kuona mlango wa flemu moja haujarudishiwa mpaka chini kabisa, so akajua kuna mtu ndani. Aliingia moja kwa moja mpaka ofisini kwenye ndani ya duka, na mlango wa ofisi sikufunga, nilishituka sana mpaka kumtaja (mmiliki wa vyote) ile siku nilitetemeka pale pale, isitoshe mapaja yangu yote yalikuwa nje, japo nashukuru hatukufika ile stage ya kusexy.
Nilitetemeka sana na moyo kwenda mbio kwani yule ni mtoto wangu wa kumzaa. Alituangalia afu akaondoka, mchepuko akaniulize yule ni nani nikamwambia mwanangu, yeye mwenyewe alishituka. Akanishahauri kuwa tulia tuu tuongee tuyamalize nikamwambia subiri niende home kwani namjua atakuwa anaenda home. Akili iliruka siku ile. Nikafunga duka.
Nilikimbilia nyumbani ili kumuwahi mtoto maana Baba yake alikuwa Bagamoyo anarudi kesho, nilifikili ataenda kupiga simu ya nyumbani na kumwambia mume wangu, nilipofika home nilimkuta hajafika bado nilimsubiri alilofika. Nilimuita nje nikaongea nae sana. Nikajua yameisha. Kesho yake nikamwambia unataka nini nikununulie akasema hataki chochote.
Yule Baba akanipigia simu tukaongea sana akaniambia njoo uchukue pesa tumpe mtoto atanyamaza tuu. Yule Baba alinila 1,000,000 nimpe mtoto wangu ili asiseme, nilimpa zile pesa nikajua yameisha.
Sasa kadri siku zinazidi kwenda mtoto wangu alikuwa ananichukia, sana kuna kipindi alikuwa hata kunisalimia hataki kabisa. Nikimtuma hataki kabisa hata kwenda. Ila mimi niliewa kuwa ni lile tukio. Kuna siku alinisikia namuita mume wangu kipenzi, kijana wangu si akasikia aliniangalia sana. Mpaka mimi nikashituka, na nikajua yeye jinsi anavyo jisikia.
Kuna kipindi nililazwa hakuja hata kuniangali hospital. Mara nyingi tukiwa peke yetu nakuwa nakaa nae naongea nae namwambia mimi ni mama yako naomba unisamehe nimemkosea Baba yako, nimeacha sijarudia tena. Ila hanijibu chochote ananyamaza tuu. Najitahidi kumfanyia mambo mazuri ilimradi nirudishe mahusiano na mtoto wangu. Lakini inashidikana. Kuna siku namwambia unapenda nikufanyia nini mwanangu anasema tuu mimi nipo sawa mama. Tangu lile tukio niliacha kucheat.
Ki ukweli ananichukia sana mimi mama yake, huwa nakaa ne mara nyingi naongea nae ila inashindikiana.
Mwaka juzi nilimuona kuna rafiki yake ana gari na mimi nikasema ngoja nimnunulia kagari mtoto wangu. Kwa vile mimi nimeajiriwa na nina mshahara mzuri, nilijikusanya na kuchukua pesa baadhi kwenye biashara zetu na mume wangu, mwaka jana mwezi wa 8 nikaenda mlimani pale nikanunua gari, nikamfanyia kama surprise hivi alisema tuu asante akachukua.
Ila nilishangaa aliendesha kama 2 weeks baadae alilirudisha nyumbani na kuweka funguo mezani, hajaliendesha mpaka leo, mume aliniuliza gari vipi nikazuga zuga tu. Nilishangaa sana nilimuuliza kuwa unajua mimi ni mama yako nimekosa ila kumbuka mimi ni mama yako. Yeye sasa ana umri wa miaka 26.
Sasa wiki 2 zilizopita mume wangu aliniambia kuwa ninaona wewe na first born hamna mahusiano mazuri nawafatilia muda mrefu sana sijajua shida ni nini. Nimeshituka sana kwani sitaki mume wangu ajue hii ishu japo ilitokea 10 years ago ila baada ya kujiambia hivyo niliishiwa nguvu kabisa. Juzi nilijaribu kumuuita mtoto wangu niongee nae lakini still bado ana hasira nami.
Sasa jamani naomba msaada wenu kimawazo nideal vipi na hii kesi. Najua hawezi kumwambia Baba yake ila na mimi nikikaa kimya , mume wangu atajua tuu kuna something tunamficha maana hata juzi katoka kusema shida yenu ni nini nimemrukaruka tu. Mtoto wangu hataki kabisa kunisikiliza.
Nilitaka kushirikisha kiongozi wa dini mmoja ni mwanamke, tumuite ili tuongee nae ila naona haitakuwa siri tena inatavuja tu.
Msaada wa mawazo nahitaji.
Mimi ni mama mtu mzima nina watoto 4 kwa mume wangu wa ndoa kabisa.
Niende kwenye mada.
Miaka 10 iliyopita nilifumaniwa na mtoto wangu wa kiume (my first born). Sikuamini kilichotokea nilishituka sana kwa hile tukio lilotokea.
Mimi nafanya kazi kwenye wizara moja hivi nipo hapa dsm mpaka sasa. Miaka iliyopita niliingia mahusiano na Baba mmoja hivi anafanya kazi wizara nyingine tofauti na yetu, nilikutana naye kwenye kikao vya ofisini.
Mimi ni kawaida yangu kumcheat mume wangu, japo hajawahi kunitilia hofu kama nimewahi kumcheat maana mara nyingi navizia akiwa safarini ndo ninafanya hivyo. Maana ninajua kumcheta mwanaume ni hatari sana kwani wanaume wana wivu sana na hasira, kama mume wangu namfahamu ni mtu mwenye hasira sana, so nilijitahidi asijue kabisa.
Sasa kuna siku mimi nilienda kwenye duka langu maana kwenye duka langu kabla jioni ijafika lazima niwepo ndo nifunge na wafanyakazi waondoke pale. Sasa kipindi tunamaliza yule Baba alinipigia simu nikamwambia nipo sehemu falani, nikamuelekeza akafika na alipofika wafanya kazi wangu nao wakawa wanaondoka muda huo huo. Mimi nikamkaribisha mchepuka ndani, sasa kwenye duka kuna ofisi kwa ndani si nikaenda nae mapaka kwenye ofisi katika kuongea kama 20 minutes, kwa sababu ni mchepuka tukajisahau akaanza kunishika na kuanza kukiss each other katika kunishikashika nikajisahau.
Kumbe mtoto wangu wa kwanza alikuja pale dukani aliingia baada ya kuona mlango wa flemu moja haujarudishiwa mpaka chini kabisa, so akajua kuna mtu ndani. Aliingia moja kwa moja mpaka ofisini kwenye ndani ya duka, na mlango wa ofisi sikufunga, nilishituka sana mpaka kumtaja (mmiliki wa vyote) ile siku nilitetemeka pale pale, isitoshe mapaja yangu yote yalikuwa nje, japo nashukuru hatukufika ile stage ya kusexy.
Nilitetemeka sana na moyo kwenda mbio kwani yule ni mtoto wangu wa kumzaa. Alituangalia afu akaondoka, mchepuko akaniulize yule ni nani nikamwambia mwanangu, yeye mwenyewe alishituka. Akanishahauri kuwa tulia tuu tuongee tuyamalize nikamwambia subiri niende home kwani namjua atakuwa anaenda home. Akili iliruka siku ile. Nikafunga duka.
Nilikimbilia nyumbani ili kumuwahi mtoto maana Baba yake alikuwa Bagamoyo anarudi kesho, nilifikili ataenda kupiga simu ya nyumbani na kumwambia mume wangu, nilipofika home nilimkuta hajafika bado nilimsubiri alilofika. Nilimuita nje nikaongea nae sana. Nikajua yameisha. Kesho yake nikamwambia unataka nini nikununulie akasema hataki chochote.
Yule Baba akanipigia simu tukaongea sana akaniambia njoo uchukue pesa tumpe mtoto atanyamaza tuu. Yule Baba alinila 1,000,000 nimpe mtoto wangu ili asiseme, nilimpa zile pesa nikajua yameisha.
Sasa kadri siku zinazidi kwenda mtoto wangu alikuwa ananichukia, sana kuna kipindi alikuwa hata kunisalimia hataki kabisa. Nikimtuma hataki kabisa hata kwenda. Ila mimi niliewa kuwa ni lile tukio. Kuna siku alinisikia namuita mume wangu kipenzi, kijana wangu si akasikia aliniangalia sana. Mpaka mimi nikashituka, na nikajua yeye jinsi anavyo jisikia.
Kuna kipindi nililazwa hakuja hata kuniangali hospital. Mara nyingi tukiwa peke yetu nakuwa nakaa nae naongea nae namwambia mimi ni mama yako naomba unisamehe nimemkosea Baba yako, nimeacha sijarudia tena. Ila hanijibu chochote ananyamaza tuu. Najitahidi kumfanyia mambo mazuri ilimradi nirudishe mahusiano na mtoto wangu. Lakini inashidikana. Kuna siku namwambia unapenda nikufanyia nini mwanangu anasema tuu mimi nipo sawa mama. Tangu lile tukio niliacha kucheat.
Ki ukweli ananichukia sana mimi mama yake, huwa nakaa ne mara nyingi naongea nae ila inashindikiana.
Mwaka juzi nilimuona kuna rafiki yake ana gari na mimi nikasema ngoja nimnunulia kagari mtoto wangu. Kwa vile mimi nimeajiriwa na nina mshahara mzuri, nilijikusanya na kuchukua pesa baadhi kwenye biashara zetu na mume wangu, mwaka jana mwezi wa 8 nikaenda mlimani pale nikanunua gari, nikamfanyia kama surprise hivi alisema tuu asante akachukua.
Ila nilishangaa aliendesha kama 2 weeks baadae alilirudisha nyumbani na kuweka funguo mezani, hajaliendesha mpaka leo, mume aliniuliza gari vipi nikazuga zuga tu. Nilishangaa sana nilimuuliza kuwa unajua mimi ni mama yako nimekosa ila kumbuka mimi ni mama yako. Yeye sasa ana umri wa miaka 26.
Sasa wiki 2 zilizopita mume wangu aliniambia kuwa ninaona wewe na first born hamna mahusiano mazuri nawafatilia muda mrefu sana sijajua shida ni nini. Nimeshituka sana kwani sitaki mume wangu ajue hii ishu japo ilitokea 10 years ago ila baada ya kujiambia hivyo niliishiwa nguvu kabisa. Juzi nilijaribu kumuuita mtoto wangu niongee nae lakini still bado ana hasira nami.
Sasa jamani naomba msaada wenu kimawazo nideal vipi na hii kesi. Najua hawezi kumwambia Baba yake ila na mimi nikikaa kimya , mume wangu atajua tuu kuna something tunamficha maana hata juzi katoka kusema shida yenu ni nini nimemrukaruka tu. Mtoto wangu hataki kabisa kunisikiliza.
Nilitaka kushirikisha kiongozi wa dini mmoja ni mwanamke, tumuite ili tuongee nae ila naona haitakuwa siri tena inatavuja tu.
Msaada wa mawazo nahitaji.