Naandika hapa huku machozi yakinitoka, nimeona niwashirikishe ndugu zangu labda ntapata faraja.
Ni wiki sasa nimejifungia ndani hata kazini siendi. Story iko hivi kwa kufupisha sana nisiwachoshe, mimi ni kijana nnaeishi na mwanamke na tumejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu, kwakweli nampenda sana huyu mtoto, maana ndio mtoto wa kwanza, wazazi mtakuwa mnanielewa.
Nakumbuka mwanamke wangu aliwahi kunianbia akija kugundua nachepuka basi ataondoka ataenda mbali, ataniblock mimi na ndugu zangu ili tusijue yupo wapi, akiolewa basi atabadilisha Jina la mtoto na kumpa la huyo mwanamme atakaemuoa na ndio atakua baba yake, asipoolewa mtoto akikua atamwambia baba yake alikufa na kumwonyesha kaburi.
Sasa wiki moja iliyopita nilisahau kufuta meseji za mchepuko bahati mbaya akapekua simu na kuzikuta, mimi natoka kuoga nakuta mtu analia nikajua hapa kuna shida. Kuangalia simu nakuta yale mameseji, kibaya zaidi meseji mbaya za kumsifia mchepuko na zingine za kumtumia hela, nikambembeleza lakin kaikusaidia.
Kesho yake nikaenda kazini kurudi sikumkuta, kupiga simu imeblockiwa, ndugu zangu kumpigia amewablock, ndugu zake nao hawajui alipo, kwahiyo nikajua kafanya kile kitu alichoniambia mwanzo angefanya.
Niwe mkweli tu, kuzingua nimezingua tena sana lakini nahisi adhabu alionipa ni kubwa mnooo, naombeni ushauri wakuu maana hali ni mbaya hapa, yaani naona nimejitwisha Dunia na ninachowaza mtoto wangu atapewaje baba mwingine, halafu mtoto wa kike, nashindwa kuelewa hata wanaotelekeza watoto huwa inakuaje.
Napokea ushauri pamoja na hata za mbavu sababu chanzo ni mimi hivyo hata za mbavu itakua kama adhabu ninayostahili.
Ni wiki sasa nimejifungia ndani hata kazini siendi. Story iko hivi kwa kufupisha sana nisiwachoshe, mimi ni kijana nnaeishi na mwanamke na tumejaliwa kupata mtoto mmoja wa kike mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi mitatu, kwakweli nampenda sana huyu mtoto, maana ndio mtoto wa kwanza, wazazi mtakuwa mnanielewa.
Nakumbuka mwanamke wangu aliwahi kunianbia akija kugundua nachepuka basi ataondoka ataenda mbali, ataniblock mimi na ndugu zangu ili tusijue yupo wapi, akiolewa basi atabadilisha Jina la mtoto na kumpa la huyo mwanamme atakaemuoa na ndio atakua baba yake, asipoolewa mtoto akikua atamwambia baba yake alikufa na kumwonyesha kaburi.
Sasa wiki moja iliyopita nilisahau kufuta meseji za mchepuko bahati mbaya akapekua simu na kuzikuta, mimi natoka kuoga nakuta mtu analia nikajua hapa kuna shida. Kuangalia simu nakuta yale mameseji, kibaya zaidi meseji mbaya za kumsifia mchepuko na zingine za kumtumia hela, nikambembeleza lakin kaikusaidia.
Kesho yake nikaenda kazini kurudi sikumkuta, kupiga simu imeblockiwa, ndugu zangu kumpigia amewablock, ndugu zake nao hawajui alipo, kwahiyo nikajua kafanya kile kitu alichoniambia mwanzo angefanya.
Niwe mkweli tu, kuzingua nimezingua tena sana lakini nahisi adhabu alionipa ni kubwa mnooo, naombeni ushauri wakuu maana hali ni mbaya hapa, yaani naona nimejitwisha Dunia na ninachowaza mtoto wangu atapewaje baba mwingine, halafu mtoto wa kike, nashindwa kuelewa hata wanaotelekeza watoto huwa inakuaje.
Napokea ushauri pamoja na hata za mbavu sababu chanzo ni mimi hivyo hata za mbavu itakua kama adhabu ninayostahili.