Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Mkutano wa CHADEMA viwanja vya NMC Arusha

Kila siku Arusha tu Makamanda jaribuni kujitanua kitaifa zaidi kuliko kikanda.

Lini tutasikia Chadema wameweka kambi maeneo mengine kama.

Kilwa.
liwale.
Ruangwa.
Nachingwea.
Newala.
Nanyumbu.
Tandahimba.
Ngara.
Karagwe.
Muleba.
Kyerwa.

ritz pole na kazi,
siku zote ukimshika popote iwe korodani,shingo ukiona analalamika oo kwa nini hushiki miguu jua roba imefika na usiachie.
na ukiona umeshika mahali halalamiki jua imekula kwako.

hata wakati wa uhuru nyerere aling,ang,ania sana dar ila aliposhtu alirudi arusha na moshi kwa kina mzee aikael mbowe kachukua nauli ya kwenda un.
 
Heche: inashangaza wabunge waliokataliwa na wananchi Kikwete anawateua kuwa mabalozi.
Anamteua Kamala kuwa balozi ubelgiji, kwanini asingempeleka uganda.
 
Mwanza sio tz? Mkutano wa lisu moro sio tz? Wa juz dom? Acha pumba.

hiyo miji uliyoitaja wanaendaga huko mara moja moja but tukubali wakitaka ku make a statement ni arusha or mwanza ambako am sure wana wafuasi wengi...wakitaka kuchukua nchi hii waanze kukusanya watu wengi, lindi, mtwara, huko kote nao wana hamu ya kuhudhuria mikutano yao
 
Heche!! Tunafurahi sana kuwa hapa leo!! Mara ya mwisho kuzungumza hapa ni wakati wa kufukuza madiwani wakorofi!!

Siku zote tulisema na tunaendelea kusema kuwa kwa miaka hamsini CCM imeshindwa kupambana na maadui watatu, tuwasamehe kina Millya kwani wametambua makosa na sasa wamejiunga nasi!!

Vyama vyote vingine vipo kwa maslahi ya chama tawala....

Juzi Kikwete ameteua wabunge na ameteua mwenyekiti wa chama kimoja cha upinzani na leo mnashuhudia watu tuliowasema sana wanjidhiri, tunakwenda Mtwara na Lindi kupokea wanachama kama tunavyofanya hapa!

Watu wanalalamika kuhusu maisha magumu, anavunja baraza la mawaziri 50 na kutengeneza la mawaziri 55, angalia mwandosya hana wizara maalumu na tunamuhudumia kwa kodi zetu hapa..

Sisi tunasema mawaziri walioiba kwa mfano Maige analeta Kiburi cha Chenge!! Anaona millioni mia saba ni kidogo, hii ni ishara ya kutuongezea hasira zaidi..

Moshi mjini Ndesamburo anapokea wenyeviti na mabalozi zaidi ya kumi na nane

Wenje yuko kitunda anaendelea kupokea wanaojiuzulu...

D. Kamara amekataliwa kijijini kwake anapelekwa ubelgiji

Serikali ya kishkaji inaliangamiza Taifa...

 
Mkuu ritz,
Ni lini tutasikia na CCM imepiga kambi Arusha, Mbeya, Mwanza na maeneo hayo uliyoyataja?

ritz ametoa hoja ya maana sana,maeneo aliyoyataja ni muhimu sana kwa CDM kujijenga,ritz anasema kutokana na uzoefu wake katika magamba,maeneo hayo ndiyo ngome kuu zilizobaki za ccm,nimetoka Liwale leo nimeshangaa sana kuona bendera za chadema vijijini,ni suala tu la makamanda kutia timu maeneo hayo
 
Nape hana ubavu wa kuzungumza zaidi ya kusema "hao tuliwachoka hata hivyo hatukuwa tunawahitaji". wakati hao hao ndo walioitwa dar kupongezwa kuhusu bidii yao ya chama.NAPE NI MNAFIKI NA WALA SI MWANASIASA MAKINI kuhusu propaganda zake hata machinga ana uwezo wa ku-propagate more than yeye.(NAPE)
 
dar es salaam ni mortuary ya mageuzi

Subiri kidogo, Dar moto wake bado kidogo sana, na siku hiyo Jua litasimama. Si wameanza na wamachinga, tayari jiji la dar halikaliki. Kutoka kona moja mpaka nyingine masaa 4. Halafu eti wanaleta mabasi yaendayo kasi spidi 500km/hr ngoja tuone.
 
Mbowe anwataka radhi watu kwa kuwa wakina dogo janja wamezungumza maneno makali na anasema kauli ya Dogo janja ya kuigawa nchi sio kauli ya chama na anasema CHADEMA haifikiri kuigawa nchi. Kwa hiyo anifuta kauli hiyo
 
Back
Top Bottom