Mkoa gani ni mzuri kuishi?

Mkoa gani ni mzuri kuishi?

Yakheee nenda Tanga Raha, hao wote wanakudanganya tu. Ulishawahi kusikia mkoa wa Tanga kuna njaa?

Mvua mara mbili, matunda yote unayoyajua wewe utapata Tanga, mazao karibu yote yanakubali ardhi ya Tanga. Hao mademu waliosema wengine huku wapo wa kumwaga na maji ya hiliki na mdalasini utawekewa bafuni na ukitaka kubebwa mgongoni pia utabebwa.

Kule twala samaki wa maji chumvi unachoma na kula bila kuweka chumvi sio wengine wanakula perege hata nyama hawana.
 
Nenda Mpanda katavi, pale madina hotel........, semlwa, kashaulili, makanyagio, kabla ya reli, Mpanda hoteli, mapinduzi, kakese, sitarike na n.k yaan hapo laki 3 tuu lazima utoke kimaisha..
 
Jamani mimi natafuta mkoa mzuri wa kuishi ambako maisha ni ahueni! Nijuzeni waungwani!
Maisha popote ndugu.
Ndio sababu unakuta mtu katoka Mwanza, anafanya maisha Mtwara, Lindi, Kigoma n.k. Mtu anatoka Pemba, anafanya maisha Kyela au Mpanda. Ni matumizi ya fursa tu ndio yanayo matter.
 
Dar pananuka uchafu, watu nao ni uchafu maana wanapanga nyanya barabarani,akija obama wote mnakuwa mahaouse gal/boys, mnatimuliwa kila kona.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Tanga njaa tu, kila mwaka mahindi ya msaada, ladba matunda tu hasa msimu wa machungwa.
 
Umetisha,waambie wawahi upesi. Hapa kutakuwa university of medicine na hospitali. Huku mji ukipambwa na maziwa mawili kaskazini na kusini.
 
inategemea hali yako ya kimaisha ikoje unapopaona wewe ahuweni mwengine anaweza kupaona gharama.....Mi naona mikoa yote mizuri ili mradi uishi sehemu yenye huduma muhimu za kijamii kama hospitali,maji,pawe na usafiri n.k ahueni au gharama inatokana na kipata chako na kazi unayofanya.
 
Una shilling ngapi nikuonyeshe sehemu sahihi ya kukufa kuishi?usije kuta mtu huna hata senti kumi na pia ni mvivu usiyependa kazi halafu eti unaulizia sehemu nzuri ya kuishi!!! Abadan!! Hakuna sehemu/nchi/wala mkoa mzuri wa kuishi kwa mtu MASKINI,MVIVU,na MJINGA!!na maisha ni mazuri popote ikiwa umefanikiwa kuvipiga vita vitu hivyo hapo juu,au pambana hapo hapo ulipo na baada ya muda utaleta feedback kuwa huitaji tena kwenda popote.
 
na hasa ukichukulia
kujengwa kwa chuo kikuu kikubwa kabisa cha kilimo kanda ya nyanda za juu
kusini

duh,yaani kitakuwa kikubwa kuliko SUA?,nchi hii bwana ndo maana haiendelei kwa sababu mipango mingi hupangwa na wanasiasa badala ya wataalam,kuna ubaya gani kama wasingekiimarisha SUA?
 
Back
Top Bottom