Mkataba wa Bandari, Wabunge wasema waliburuzwa

Naenda kuwapokea mabosi wewe.

Lazima waje na mitandio na maabaya ya kijakazi wao.

Hivi nshawafunikia kondoo wawili ardhini, wakifika wanawafukuwa wenyewe.

Unaijuwa mandi wewe? Raha yake iliwe ya moto moto.

Cheza na kijakazi cha wenye Dirham zao wewe?
Haya bibie nenda kawape siyo kondoo tu wape na vyote watakavyotaka.Kumbuka wewe ni kijakazi wao na kazi yako ni kutii kwa kila kitu watakacjokuomba maboss wako.
Dirham za kazi gani kwangu,nahitaji na ninatunza Usd.
 
Inaweza kuwa fiction au non-fiction. Ukizingatia solid evidence hakuna, tukutane kwy roundtable kugonga cheers ku enjoy siku ya leo, ya nini kujichosha na siasa za kusadikika?!
Tutafute hela za kuhudumia familia zetu, kelele tumeshapaza, kama hawajasikia tufanyaje?!
 
Inaweza kuwa fiction au non-fiction. Ukizingatia solid evidence hakuna, tukutane kwy roundtable kugonga cheers ku enjoy siku ya leo, ya nini kujichosha na siasa za kusadikika?!
Tutafute hela za kuhudumia familia zetu, kelele tumeshapaza, kama hawajasikia tufanyaje?!
Hapana ukichoka kupaza sauti wewe,wengine bado wataendelea kupaza mpaka kieleweke.Pumzika tu na ugonge cheers ukimaliza mapumziko,karibu tena tuendelee kupaza sauti zetu.
 
Ni kweli waliburuzwa, tazama hii picha iliyotokea bungeni siku ile ya kupitisha ule mkataba wa hovyo..

Kwanza mwanasheria mkuu wa serikali hakuwemo ndani ya ukumbi wa bunge siku ile, wakati jambo lililokuwa linapitishwa lilihusu sheria, hili lilifanyika makusudi ili kumpa uhuru Spika Tulia auteke ule mkutano na kuupeleka atakavyo.

Matokeo yake kila mbunge aliyeonesha kupingana na hoja ya kuwapa waarabu bandari, Spika Tulia akawa anamshambulia kwa kutoa maelekezo potofu kisheria, na yaliyopo kwenye ule mkataba.

Samia asijidanganye kwa hii issue, hata kama atajitoa akili adai kuziba masikio ajue tu, watanganyika tunataka bandari zetu, kesi mahakamani zimeshaanza kufunguliwa, majibu yanasubiriwa, hao wajomba awarudishie alichowapa, haaminiki tena.
 
Kwamba DPW akichukua ndiyo mizigo haitapita au itaathiri kazi zingine?

Kwa maelezo ni kuwa itasaidia kuongeza wafanyakazi hadi 71,000

No body anakataa uwekezaji but at what cost? Wanyeji wanafaidika vipi na nchi ian faidika vipi?
 
Hili limenishangaza, kunishtua na kukatisha tamaa kabisa.

Nilikuwa na mazungumzo na wabunge wawili, mmoja ni mwanasheria, tena mzuri sana kwenye mambo ya corporate, akiwa amesoma miongoni mwa vyuo vikubwa na bora kabisa Duniani. Na mwingine alikuwa Naibu Waziri, kwa sasa yupo nje ya Baraza.

Hoja kubwa ilikuwa mjadala wa bandari, majibu yao, mmoja alisema hivi:

"hivi bwana ..........., unaamini, mimi na akili yangu, naweza kuunga mkono mkataba kama ule? Watu wanasema tu huko nje, hawajui kilichopo huku ndani. Ukiwa huku, unakuwa ni kama mtumwa. Tumeitwa kwenye kikao cha chama, tena tukaambiwa ni maelekezo. Bungeni pale kuna wachache, tena wale watu wao waliowekwa sawa, ndio waliokuwa wanaongea. Nakuhakikishia, wote ambao hatukuongea, kila mmoja alikuwa hataki, lakini kwa salama yako, unaamua kukaa kimya. Hawa watu wamejipanga hasa, na kila siku wanaoonekana ni kisiki mahali popote, wanaondolewa".

Mwingine aliyewahi kuwa naibu waziri, akasema:

"Wengine tumeondolewa, kwa sababu ya kuhisiwa tu kuwa tunaweza tusiunge mkono kila kitu. Tukawekwa pembeni. Na hapa, kwa hawa watu, si ajabu sisi wengine mwaka 2025, tukaondolewa kabisa hata kwenye ubunge. Na wakiwa wenyewe kabisa, itakuwa mbaya zaidi, maana hatutajua kabisa wanayopanga, hata wanayofanya. Kwa hiyo kwa namna fulani, ni afadhali hata ubakie kinafikinafiki, angalao tufahamu wanachofanya. Shida pia, ni wananchi wetu. Sisi tunapozitoa taarifa hizi, kuvujisha siri, tunatarajia wananchi waamke, lakini wananchi nao inakuwa kimya. Sasa ukiwa kimbelembele, upo pekee yako, nyuma yako hakuna watu, utafika wapi? Kwa kweli tumekwisha. Sasa hivi kila mahali wanapachikwa watu wao ili wapitishe haya. Na hao waarabu wanazidi kumiminika, wanapewa kila kitu, ukitazama mikataba yao, inatisha"

Walisema mengi, mpaka nashindwa kuelewa hii nchi kama hali ni hii, mwanga uko wapi?

Wananchi wanataka wabunge wafanye kitu kwa maslahi ya nchi na umma, wabunge nao wanatarajia wananchi ndio wafanye kitu kuiondoa nchi kwenye mkwamo, nao wananchi hawafanyi chochote. Na kama hali ni hiyo, sasa bunge ni la kazi gani?

Jamani, tupambane tupate katiba mpya lakini katiba yenyewe nayo tutaipataje wakati sisi sote ni waoga? Hata ikipatikana katiba mpya, wakiamua kutokuifuata, na watu tukawa waoga kuwawajibisha viongozi wanaoikiuka, itakuwa na msaada mkubwa? Uoga wetu, umekuwa mtaji mkubwa kwa watawala wenye dhamira mbaya ya kujineemesha wao na jamaa zao.
Tatizo mtego alioutega bwana yule,hakujua kama siku moja angenasa mwenyewe,alivuruga utaratibu wa kuwapata wabunge,akawapata anaowataka yeye.

Ingawa yeye alikuwa na uchungu na mali za umaa na hakuwapenda wabadhirifu,lakini nao wabaya wake wanapitia mulemule ingawa kwa nia mbaya zaidi
 
Hii habari yako Ni ya kutunga ,ya uongo na isiyo na ukweli wowote ule Zaid ya kutaka tu kuwadhalilisha waheshimiwa wabunge wetu.

Hakuna ushahidi wala hoja ya kuonyesha ukweli wa hoja yako,unasema waarabu wanaendelea kumiminika hapa nchini pasipo kuweka ushahidi wa namna ya wanavyoingia hapa nchini,hujaeleza wanaingia nchini kwa kufuata sheria au kwa kuvunja Sheria,hujaeleza Ni lini na kwa Tangazo lipi la serikali na la Tarehe ngapi na kupitia Nani lilipiga marufuku wageni wanaokuja kisheria nchini kuingia nchini.

Kwani Ni lini imekuwa jinai kwa mtu kuingia nchini kwa kuwa na vibali vyote na sababu ya kuja nchini? Watanzania wangapi wanasafiri kila Siku kwenda nje ya nchi? Wafanyabiashara wangapi wanaokwenda nje ya mipaka ya nchi? Je sisi watanzania hatutaki wafanyabiashara wa kigeni? Hatutaki wawekezaji wanaokuja kwa kufuata taratibu zote? Hatutaki wawekezaji? Hatutaki bidhàa zetu zipate soko nje ya nchi?

Mbona hujaeleza Kama hao wageni wanaoingia Kama wanavunja Sheria au wanazingatia Sheria? Nani kakwambia kuwa Tanzania haipokei watu wanaotaka kuja Tanzania? Hao wanaokuja ni magaidi? Wateka nyara? Ni majangili? Kama Ni watu wema na wanakuja kwa vihali rasimi kwanini unapata hofu na kusema wanamiminika? Na wanamiminikia wapi hapo ulipowakuta wamejikusanya na unashindwa hata kuwapiga picha au kutoa taarifa yenye ushahidi kuwa wamiminikaji wapo kinyume na sheria nchini

Mbona kipindi Cha corona ambapo baadhi ya nchi ziliposema raia wake wasije nchini kutokana na hofu ya Corona kwanini mlishangilia kwa kukenua meno yenu kuwa tunatengwa na Dunia na uchumi wetu utapolomoka? Kwanini leo wanapoingia kwa kufuata sheria unaanza Tena kulalama? Kwanini iwe nongwa? Kwanini iwe jinai mtu kuja kufanya biashara na Tanzania na kutoa fursa za ajira na kulipa Kodi?

Acheni unafiki wenu na kuandika vihabari vya kuokoteza na kuunga unga kwa maslahi yenu binafsi,Acheni chuki zenu binafsi,acheni kutumika kijinga ,acheni uchonganishi wenu wa kitoto na kijinga,acheni ushamba wenu, acheni kuishi nyuma ya wakati na acheni ukasuku.
Crap. We argue with sound minds.
 
Tatizo huna uelewa. Wenzako hatutafuti ajira mahali popote. Hatua hizo tulikwaishazipita.

Kama nimefanya kazi nje ya bara hili kwa miaka 21 tena kwenye managerial positions, nikaacha kwa kuamua. Nikajenga businesses zangu, nikaajiri watu 300, halafu kwa fikra zako, unadhani nafanya kazi bandarini!! Kweli mmeishiwa fikra. Kwa sababu mnayawaza yaliyo madogo tu.

Mimi kwa sasa nafikiria kulinda utu wangu, utu wa jamii yetu na proud ya nchi yangu. Na pia kufikiria vizazi vyetu vijavyo.
Ungekua kweli umefanya kazi nje ya Africa kwa muda wote huo tena kwa position ya managerial usingepinga uwekezaji bandarini kwa sasa.
 
Ungekua kweli umefanya kazi nje ya Africa kwa muda wote huo tena kwa position ya managerial usingepinga uwekezaji bandarini kwa sasa.
Mimi sipingi hata kidogo masuala ya uwekezaji.

South Korea, hapo zamani ilikuwa duni sana ukilinganisha na North Korea. Leo South Korea, GDP yake ni kubwa kuzidi ya Russia. Yote ni kutokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na makampuni ya Marekani na mataifa mengine ya Magharibi.

China kwa miaka mingi, uchumi wake ulikuwa duni sana. Lakini kuanzia miaka 1990 kwenda mbele ukuaji wa uchumi wake ulikuwa wa juu kabisa mpaka kufikia 12% kwa sababu ya kuruhusu uwekezaji mkubwa wa mataifa ya Ulaya na America. Mpaka leo China ndiyo inayoongoza kwa kuvutia wawekezaji wa nje kuliko Taifa lolote.

Dubai kama sehemu ya UAE lilikuwa Taifa maskini ambalo kwa sehemu kubwa likiwa jangwa. Ndani ya miaka 15 tu, Dubai ilibadilika sana na kupata maendeleo makubwa kutokana na sera nzuri zilizovutia wawekezaji wengi wa nje na ndani. Mpaka leo wanaendelea kuvutia wawekezaji.

Mimi nitakuwa wa mwisho kupinga uwekezaji wa kampuni yoyote ile, ya Taifa lolote lile kuja kuwekeza Tanzania. Tunahitaji uwekezaji mkubwa maeneo mengi.

Suala la DP, tatizo siyo DP, tatizo siyo kwa sababu ya kampuni ya nje, bali mkataba ulioegemea upande mmoja. Siwalaumu DP, wao wameangalia maslahi yao. Tatizo lipo kwetu, hatukuea makini kuangalua maslahi yetu. Hizo nchi za kiarabu, nyingi, wewe mgeni huruhusiwi kuwekeza pekee yako mpaka uungane na wakurugenzi wenye nchi au local company. Lengo ni nini? Ni kuwainua watu wao. Wanaangalia maslahi ya watu wao na mataifa yao.

Kuwait, mzalishaji mkubwa wa mafuta, visima vyote vinamilikiwa ama na mtu anayemiliki ardhi au Serikali. Makampuni yote yanayochimba mafuta, licha ya kwamba visima hivyo vimechimbwa na makampuni wawekezaji, bado yanakuwa yamekodishiwa tu, lakini hayamiliki:

Who owns oil wells in Kuwait?

Unless explicitly separated by a deed, oil and gas rights are owned by the surface landowner. Oil and gas rights offshore are owned by either the state or federal government and leased to oil companies for development.
 
Wewe ni mjinga

Bandari haikuletei chakula mezani, wala kukulipia umeme au maji.

Fanya kazi
Au kaandamane
Ni ukweli usiopingika wapiga kelele na watetezi wa rasilimali za taifa hawana njaa kama nyie machawa msio na mbele wala nyuma zaidi ya kulipwa 2,0000 day.
 
Back
Top Bottom