Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mshikaji alienda comoro alimuoa yule Demu wakapata Mtoto wa kike, mtoto wa kike naye kaolewa akataga mtoto wa kiume, mshikaji alizeeka sana mwisho Akavuta akiwa na miaka 80 alimuacha mkewe Bibi.
 
Wavuvi wanapenda kula hawa sijapta kuona, wako kwenye hatari lakini wanagonga menu tu!!
 
16831207_1899205690105785_140789355008334865_n.jpg

MTUNZI : FAKI A FAKI


Sikuwahi kuona sherehe kubwa ya harusi kama ile niliyoiona katika visiwa vya Ngazija nchini Comoro mwaka mmoja uliopita.
Ilikuwa harusi ya binti wa Rais wa Moroco Yasmini binti Sharif Abdilatif aliyekuwa akolewa na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Comoro
Abubakar Mustafa Al- Shiraz aliyekuwa akiishi Ufaransa.
Sisi tulikuwa tumetoka Zanzibar. Mke wa mkuu wa majeshi ya Comoro Kulthum alikuwa Mzanzibari tena Mkojani wa Pemba, ndiye aliyetoa mwaliko kwa ndugu zake walioko Zanzibar.
Zilitolewa kadi kumi za mwaliko kwa watu kumi. Kwa vile na mimi nilikuwa na nasaba na Kulthum nikapata kadi moja na tiketi ya ndege ya kwenda Ngazija.
Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka ishirini na minne(24). Nilikuwa bado kijana na shughuli zangu zilikuwa ni uvuvi. Nilikuwa sijaoa bado lakini nilikuwa katika maandalizi ya kutafuta mchumba.
Ndege tuliyosafiri nayo ilifika Comoro saa kumi jioni. Ndoa ilikuwa inafungwa saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa katika msikiti wa Riadha, msikiti mkuu wa Ijumaa nchini humo.
Nyumbani kwa bwana harusi kulikuwa kumejaa shamra shamra. Kadhalika nyumbani kwa Rais Sharif Abdulatif nako kulikuwa hakutoshi.
Kulikuwa na hoteli mbili kubwa zilizokodishwa siku ile kwa ajili ya sherehe za harusi. Na kulikuwa na hoteli nyingine kadhaa zilizokodiwa kwa ajili ya wageni walioalikwa kutoka nchi mbalimbali.
Sisi tulifikia katika hoteli ya Zaharani. Jina la hoteli hiyo lilifanana na jina langu. Jina langu ni Zaharani Shazume. Hoteli hiyo ilikuwa jirani na msikiti wa Riadha mahali ambapo ndoa ya Yasmin na Abubakar ingefungwa usiku ule.
Kwa kawaida msikiti wa ijumaa hujaa watu siku za ijumaa lakini siku ile kwa mara ya kwanza ulijaa watu katika swala ya Inshaa.
Kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na maafisa usalama waliokuwa na kazi ya kuhakikisha usalama unakuwepo katika eneo hilo.
Nilijitahidi sana nipate safu ya mbele lakini sikuweza. Safu hiyo ilikuwa imejaa masheikh na maafisa usalama. Nilibahatika kupata safu ya tatu yake.
Baadaya swala ya isha Rais wa Comoro Sharif Abdulatif alitakiwa kutoa idhini ya kumuozesha mwanawe.
Wakati anatoa idhini alipokea simu hapo hapo iliyomtambulisha kuwa binti yake Yasmin alikuwa ameanguka nyumbani na alikuwa akitokwa na povu mdomoni.
Shughuli ya ufungishaji ndoa ikasimama. Hapo hapo Rais Abdulatif na wasaidizi wake pamoja na maafisa usalama walitoka kwenda nyumbani.
Habari iliyopatikana baadaye ilieleza kuwa Yasmini alikuwa ameanguka na kupoteza fahamu huku akitokwa na povu midomoni. Baba yake alipofika na kumuona aliamrisha apelekwe hospitali haraka.
Gari la hospitali lilikuwa limeshafika. Yasmin alipakiwa na kukimbizwa hospitali. Gari hilo la hospitali lilifuatana na gari la maafisa usalama na gari la rais mwenyewe.
Lakini gari alilopakiwa Yasmin likapata ajali kabla ya kufika hospitali. Tairi lake la mbele la upande wa kulia lilipasuka na kusababisha gari hilo kuyumba na kuligonga gari jingine kabla ya kupindukia kwenye mtaro uliokuwa kando ya barabara.
Heka heka ikawa kubwa!. Magari ya maafisa usalama yakasimama. Maafisa hao wakashuka na kukimbilia kutoa msaada. Dereva wa gari la hospitali alipotolewa alikutwa akiwa ameshakufa. Yasmin mwenyewe hakuonekana. Wauguzi wawili waliokuwa naye walikutwa wamezirai. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa.
Rais Abdulatif hakuamini macho yake, akawa anauliza kwa ukali “Binti yangu yuko wapi?”
Lakini hakukuwa na aliyejua. Yasmin alikuwa ametoweka ghafla. Kila aliyeshuhudia alishangaa.
Harusi ikavunjika. Badala ya furaha sasa ikawa huzuni. Bwana harusi na mke wa Rais Sharif Abdullatif Bi Kulthum
walikuwa wanalia kutokana na muujiza huo.
Usiku ule ule Rais Abdullatif aliita masheikh Ikulu na kuwauliza kama walikuwa wanajua kilichomtokea binti yake.
Kila sheikh alisema lake. Wako waliomwambia kuwa binti yake alikuwa amechukuliwa na wachawi. Wako waliomwambia kuwa haikuwa muafaka kwa binti yake kuolewa na Abubakar ndiyo sababu tukio hilo limetokea. Na wako waliomwambia kuwa Yasmin alikuwa amechukuliwa na jini aliyekuwa amemchunuka.
Rais Abdullatif hakujua ashike kauli ya sheikh yupi. Kwa vile lilikuwa limeshamfika alikubaliana na masheikh wote na kuwataka masheikh hao kutumia elimu zao kumrudisha binti yake. Aliahidi mamilioni ya shilingi za ki Comoro kwa sheikh yeyote atakayefanikiwa kumrudisha Yasmin.
Licha ya Rais Abdullatif kusubiri kwa zaidi ya miezi mitatu. Hakukuwa na sheikh yeyote aliyefanikiwa kumrudisha Yasmin! Yasmin akabaki kuwa historia kwani hakupatikana tena. Ulikuwa msiba ambao kila mkazi wa Comro alihisi kuwa hautasahaulika.
Hivi sasa mwaka mmoja umeshapita tangu tukio hilo la kuhuzunisha litokee. Tangu wakati ule sikuwahi tena kurudi Comoro. Nilikuwa Unguja nikiendelea na shughuli zangu za uvuvi.
Sasa siku moja ambayo sitaisahau maishani mwangu tulikuwa kwenye boti letu tukielekea maji makuu kuvua samaki. Ndani ya boti hilo tulikuwa wavuvi saba.
Ilipofika saa nne asubuhi tulikuwa mbali sana. Boti yetu ilipigwa na dharuba kali. Mashine ya boti ikazima ghafla. Tilijaribu kuiwasha lakini boti haikuwaka. Ikawa inakokotwa na maji.
Tulipumzika kidogo kisha tulijaribu kuiwasha tena na tena lakini hatukufanikiwa kuiwasha Mashine ilitugomea kabisa. Hatukujua ilikuwa imepatwa na hitilafu gani.
Je nini kitawatokea wavuvi hao?
Shikamoo msimuliaji.
 
Back
Top Bottom