george aloyce
JF-Expert Member
- Aug 22, 2017
- 1,177
- 1,822
CHOMBEZO: NILIPOFUNGWA GEREZA LA WANAWAKE KIMAKOSA
••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••
SEHEMU YA 01
"Na kesi imehairishwa mpaka tarehe ishirini na moja ya mwezi ujao, mtuhumiwa aende gerezani kwa sababu ya shtaka lake hili zito hatoweza kuwekewa dhamana, mpaka upelelezi utakapokamilika!" Hakimu aliongea akiinuka na mavazi yake ya kijaji na kofia yake maalumu kichwani
"wote simama!" yule askari maalumu aliamrisha watu wakasimama wote mahakamani kwa ajili ya Hakimu ambae alitoka, na mimi nikiwa na mavazi yangu ya kawaida ya uraiani nikashikwa na askari wawili wa kike nikiwa nimefungwa pingu mikononi kwa nyuma tayari kupelekwa kwenye karandinga la askari magereza ili wanipeleke gerezani kama mfungwa mahabusu nikisubiri kesi yangu kusikilizwa kwa mara ya pili
Kwakweli leo niliona kama dunia imenigeukia mimi, mbingu zimehamia chini na ardhi imehamia juu, nikiwa siamini kwa mara ya kwanza ndiyo ninaenda kuingia gerezani hata kama sijahukumiwa bado lakini ndiyo nitakaa wiki mbili mpaka tarehe ya kesi yangu itakapofika na kama ikihairishwa tena huenda nikakaa siku nyingine zaidi kama ujuavyo mambo ya kimahakama
Nilishushwa tukiwa tunatoka nje ya mahakama, nikiwa sipo peke yangu kama mtuhumiwa, nikiwa na wanawake wengine takribani saba wote tukiwa na kesi tofauti tofauti lakini zikishahabiana, mimi nikiwa na kesi ya kukutwa na madawa ya kulevya, wakati huo wakili na mwanasheria wangu alikuwa akinikimbilia nyuma nyuma akitaka kuongea kitu na mimi akawasimamisha askari
"una shida gani?" askari magereza mmoja wa kike alimwuliza
"nataka kuongea na mteja wangu sekunde chache!"
"haturuhusu!"
"kwa sheria gani?" wakili alimwuliza askari huyo aliyemtazama askari mwenzake ambae alitikisa kichwa kumruhusu wakili wangu azungumze na mimi akiogopa kufunguliwa vifungu vya sheria na wakili huyo msomi ambae sheria ipo kichwani
"naam kaka!" nilimwitikia nikibana sauti yangu kama mtoto wa kike kama kawaida yangu
"nitakuja kesho kutwa tuzungumze Reshma sawa?"
"sawa kaka wakili jitahidi ushughulikie mimi sijawahi kufungwa jamani?" niliongea kwa sauti ya kike huku nikijiliza
"sawa na kuna mzigo wako nitakueletea usijali hautokaa mda mrefu utatoka!"
"sawa nakuamini!"
Nilimjibu nikashikwa na askari safari kuelekea nje ya mahakama kwenye gari (karandinga) la askari magereza
Kiukweli kwa jinsi nilivyovaa hakuna ambae angejua kama mimi ni mwanaume, kwa kuwa nilikamatwa kwenye mazingira hayo, ilibidi tu nivumilie na kuendelea kujifanya mwanamke hivyo hivyo ilimradi nisikumbane na dhahama au kashkash wanazokutana nazo watuhumiwa wa kiume na kama ningegundulika kuwa mwanaume na nimejifanya kuwa mwanamke basi huenda ningeongeza kesi na kuonekana ni kweli mimi ni muhalifu kwa kitendo tu cha kujifanya mwanamke wakati wala siyo muhalifu lakini nilikuwa kwenye harakati tu za kukwepa kufanya tukio la uhalifu ambalo nililazimishwa kulifanya bila mimi kutaka
Mpaka nasomewa kesi kwa mara ya kwanza na kutolewa sasa kupelekwa kwenye karandinga la magereza nilikuwa na mavazi yangu, baibui jeusi na refu ambalo hapo awali wakati nakamatwa lilinifunika mpaka uso nikawa naonekana macho tu lakini mahakamani nilifunuliwa nikitakiwa uso uonekane lakini kutokana na make up nilizopakwa na urembo usoni niliopakwa na wabobezi wa mambo ya urembo ukichanganya na sura yangu nzuri niliyoirithi kutoka kwa mama yangu mzazi, hakuna ambae angedhani kuwa mimi ni mwanaume, maana ndefu zote zilikwanguliwa (nitawaeleza huko mbeleni kwanini nimekuwa hivi)
Na urijali wangu nikiwa mwanaume niliyekamilika kila kitu, nilikuwa ndani ya baibui langu refu nikipakizwa ndani ya karandinga la magereza, pamoja na watuhumiwa wa kike halisi, safari kuelekea gerezani kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu, nikiwa nimewahi kulala mahabusu tu kituo cha polisi lakini siyo gerezani kabisa, hii ndiyo ikiwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu
Nilikaa ndani ya basi nikitazama tu nje dirishani nikiwaza na kuwazua yatakuwaje maisha hayo ya gerezani ambayo ninasikia watu wakisema ni magumu sana sana na ya mateso, nikashusha pumzi ndefu nikijikaza kiume nikiwa nimekaa na mfungwa mwenzangu mwanamke ambae alikuwa yupo siriasi hacheki na mtu, akionekana ni mtu mkorofi sana aliyefanya matukio ya kutosha mtaani maana amekaa kiume kiume tu
"samahani hivi wewe nawe ni mara yako ya kwanza kuingia gerezani au!?" nilimwuliza nikijaribu kumsemesha akageuka na kunitazama kwa sekunde kadhaa na sura yake ya ukauzu
"mimi gerezani ni kama nyumbani!" alinijibu jibu lililonimaliza nguvu nikatikisa kichwa tu, na muda huo huo askari alipiga mayowe ya kuamrisha tushuke wote tukashuka kwenye karandinga hilo la magereza kumbe tulikuwa tumeshafika kwenye gereza na ndipo niliposhuhudia lango la gereza mbele yangu kwa mara ya kwanza nikiingia ndani ya gereza, tena gereza la wanawake na mimi ni mwanaume.......
Inaendelea
••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••••
SEHEMU YA 01
"Na kesi imehairishwa mpaka tarehe ishirini na moja ya mwezi ujao, mtuhumiwa aende gerezani kwa sababu ya shtaka lake hili zito hatoweza kuwekewa dhamana, mpaka upelelezi utakapokamilika!" Hakimu aliongea akiinuka na mavazi yake ya kijaji na kofia yake maalumu kichwani
"wote simama!" yule askari maalumu aliamrisha watu wakasimama wote mahakamani kwa ajili ya Hakimu ambae alitoka, na mimi nikiwa na mavazi yangu ya kawaida ya uraiani nikashikwa na askari wawili wa kike nikiwa nimefungwa pingu mikononi kwa nyuma tayari kupelekwa kwenye karandinga la askari magereza ili wanipeleke gerezani kama mfungwa mahabusu nikisubiri kesi yangu kusikilizwa kwa mara ya pili
Kwakweli leo niliona kama dunia imenigeukia mimi, mbingu zimehamia chini na ardhi imehamia juu, nikiwa siamini kwa mara ya kwanza ndiyo ninaenda kuingia gerezani hata kama sijahukumiwa bado lakini ndiyo nitakaa wiki mbili mpaka tarehe ya kesi yangu itakapofika na kama ikihairishwa tena huenda nikakaa siku nyingine zaidi kama ujuavyo mambo ya kimahakama
Nilishushwa tukiwa tunatoka nje ya mahakama, nikiwa sipo peke yangu kama mtuhumiwa, nikiwa na wanawake wengine takribani saba wote tukiwa na kesi tofauti tofauti lakini zikishahabiana, mimi nikiwa na kesi ya kukutwa na madawa ya kulevya, wakati huo wakili na mwanasheria wangu alikuwa akinikimbilia nyuma nyuma akitaka kuongea kitu na mimi akawasimamisha askari
"una shida gani?" askari magereza mmoja wa kike alimwuliza
"nataka kuongea na mteja wangu sekunde chache!"
"haturuhusu!"
"kwa sheria gani?" wakili alimwuliza askari huyo aliyemtazama askari mwenzake ambae alitikisa kichwa kumruhusu wakili wangu azungumze na mimi akiogopa kufunguliwa vifungu vya sheria na wakili huyo msomi ambae sheria ipo kichwani
"naam kaka!" nilimwitikia nikibana sauti yangu kama mtoto wa kike kama kawaida yangu
"nitakuja kesho kutwa tuzungumze Reshma sawa?"
"sawa kaka wakili jitahidi ushughulikie mimi sijawahi kufungwa jamani?" niliongea kwa sauti ya kike huku nikijiliza
"sawa na kuna mzigo wako nitakueletea usijali hautokaa mda mrefu utatoka!"
"sawa nakuamini!"
Nilimjibu nikashikwa na askari safari kuelekea nje ya mahakama kwenye gari (karandinga) la askari magereza
Kiukweli kwa jinsi nilivyovaa hakuna ambae angejua kama mimi ni mwanaume, kwa kuwa nilikamatwa kwenye mazingira hayo, ilibidi tu nivumilie na kuendelea kujifanya mwanamke hivyo hivyo ilimradi nisikumbane na dhahama au kashkash wanazokutana nazo watuhumiwa wa kiume na kama ningegundulika kuwa mwanaume na nimejifanya kuwa mwanamke basi huenda ningeongeza kesi na kuonekana ni kweli mimi ni muhalifu kwa kitendo tu cha kujifanya mwanamke wakati wala siyo muhalifu lakini nilikuwa kwenye harakati tu za kukwepa kufanya tukio la uhalifu ambalo nililazimishwa kulifanya bila mimi kutaka
Mpaka nasomewa kesi kwa mara ya kwanza na kutolewa sasa kupelekwa kwenye karandinga la magereza nilikuwa na mavazi yangu, baibui jeusi na refu ambalo hapo awali wakati nakamatwa lilinifunika mpaka uso nikawa naonekana macho tu lakini mahakamani nilifunuliwa nikitakiwa uso uonekane lakini kutokana na make up nilizopakwa na urembo usoni niliopakwa na wabobezi wa mambo ya urembo ukichanganya na sura yangu nzuri niliyoirithi kutoka kwa mama yangu mzazi, hakuna ambae angedhani kuwa mimi ni mwanaume, maana ndefu zote zilikwanguliwa (nitawaeleza huko mbeleni kwanini nimekuwa hivi)
Na urijali wangu nikiwa mwanaume niliyekamilika kila kitu, nilikuwa ndani ya baibui langu refu nikipakizwa ndani ya karandinga la magereza, pamoja na watuhumiwa wa kike halisi, safari kuelekea gerezani kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu, nikiwa nimewahi kulala mahabusu tu kituo cha polisi lakini siyo gerezani kabisa, hii ndiyo ikiwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu
Nilikaa ndani ya basi nikitazama tu nje dirishani nikiwaza na kuwazua yatakuwaje maisha hayo ya gerezani ambayo ninasikia watu wakisema ni magumu sana sana na ya mateso, nikashusha pumzi ndefu nikijikaza kiume nikiwa nimekaa na mfungwa mwenzangu mwanamke ambae alikuwa yupo siriasi hacheki na mtu, akionekana ni mtu mkorofi sana aliyefanya matukio ya kutosha mtaani maana amekaa kiume kiume tu
"samahani hivi wewe nawe ni mara yako ya kwanza kuingia gerezani au!?" nilimwuliza nikijaribu kumsemesha akageuka na kunitazama kwa sekunde kadhaa na sura yake ya ukauzu
"mimi gerezani ni kama nyumbani!" alinijibu jibu lililonimaliza nguvu nikatikisa kichwa tu, na muda huo huo askari alipiga mayowe ya kuamrisha tushuke wote tukashuka kwenye karandinga hilo la magereza kumbe tulikuwa tumeshafika kwenye gereza na ndipo niliposhuhudia lango la gereza mbele yangu kwa mara ya kwanza nikiingia ndani ya gereza, tena gereza la wanawake na mimi ni mwanaume.......
Inaendelea