Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Mkasa wa kweli: Kisiwa cha harishi

Kanungila Karim

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2016
Posts
20,746
Reaction score
25,672
16831207_1899205690105785_140789355008334865_n.jpg

MTUNZI : FAKI A FAKI


Sikuwahi kuona sherehe kubwa ya harusi kama ile niliyoiona katika visiwa vya Ngazija nchini Comoro mwaka mmoja uliopita.
Ilikuwa harusi ya binti wa Rais wa Moroco Yasmini binti Sharif Abdilatif aliyekuwa akolewa na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Comoro
Abubakar Mustafa Al- Shiraz aliyekuwa akiishi Ufaransa.
Sisi tulikuwa tumetoka Zanzibar. Mke wa mkuu wa majeshi ya Comoro Kulthum alikuwa Mzanzibari tena Mkojani wa Pemba, ndiye aliyetoa mwaliko kwa ndugu zake walioko Zanzibar.
Zilitolewa kadi kumi za mwaliko kwa watu kumi. Kwa vile na mimi nilikuwa na nasaba na Kulthum nikapata kadi moja na tiketi ya ndege ya kwenda Ngazija.
Wakati ule nilikuwa na umri wa miaka ishirini na minne(24). Nilikuwa bado kijana na shughuli zangu zilikuwa ni uvuvi. Nilikuwa sijaoa bado lakini nilikuwa katika maandalizi ya kutafuta mchumba.
Ndege tuliyosafiri nayo ilifika Comoro saa kumi jioni. Ndoa ilikuwa inafungwa saa mbili usiku baada ya swala ya Inshaa katika msikiti wa Riadha, msikiti mkuu wa Ijumaa nchini humo.
Nyumbani kwa bwana harusi kulikuwa kumejaa shamra shamra. Kadhalika nyumbani kwa Rais Sharif Abdulatif nako kulikuwa hakutoshi.
Kulikuwa na hoteli mbili kubwa zilizokodishwa siku ile kwa ajili ya sherehe za harusi. Na kulikuwa na hoteli nyingine kadhaa zilizokodiwa kwa ajili ya wageni walioalikwa kutoka nchi mbalimbali.
Sisi tulifikia katika hoteli ya Zaharani. Jina la hoteli hiyo lilifanana na jina langu. Jina langu ni Zaharani Shazume. Hoteli hiyo ilikuwa jirani na msikiti wa Riadha mahali ambapo ndoa ya Yasmin na Abubakar ingefungwa usiku ule.
Kwa kawaida msikiti wa ijumaa hujaa watu siku za ijumaa lakini siku ile kwa mara ya kwanza ulijaa watu katika swala ya Inshaa.
Kulikuwa na ulinzi mkali wa polisi na maafisa usalama waliokuwa na kazi ya kuhakikisha usalama unakuwepo katika eneo hilo.
Nilijitahidi sana nipate safu ya mbele lakini sikuweza. Safu hiyo ilikuwa imejaa masheikh na maafisa usalama. Nilibahatika kupata safu ya tatu yake.
Baadaya swala ya isha Rais wa Comoro Sharif Abdulatif alitakiwa kutoa idhini ya kumuozesha mwanawe.
Wakati anatoa idhini alipokea simu hapo hapo iliyomtambulisha kuwa binti yake Yasmin alikuwa ameanguka nyumbani na alikuwa akitokwa na povu mdomoni.
Shughuli ya ufungishaji ndoa ikasimama. Hapo hapo Rais Abdulatif na wasaidizi wake pamoja na maafisa usalama walitoka kwenda nyumbani.
Habari iliyopatikana baadaye ilieleza kuwa Yasmini alikuwa ameanguka na kupoteza fahamu huku akitokwa na povu midomoni. Baba yake alipofika na kumuona aliamrisha apelekwe hospitali haraka.
Gari la hospitali lilikuwa limeshafika. Yasmin alipakiwa na kukimbizwa hospitali. Gari hilo la hospitali lilifuatana na gari la maafisa usalama na gari la rais mwenyewe.
Lakini gari alilopakiwa Yasmin likapata ajali kabla ya kufika hospitali. Tairi lake la mbele la upande wa kulia lilipasuka na kusababisha gari hilo kuyumba na kuligonga gari jingine kabla ya kupindukia kwenye mtaro uliokuwa kando ya barabara.
Heka heka ikawa kubwa!. Magari ya maafisa usalama yakasimama. Maafisa hao wakashuka na kukimbilia kutoa msaada. Dereva wa gari la hospitali alipotolewa alikutwa akiwa ameshakufa. Yasmin mwenyewe hakuonekana. Wauguzi wawili waliokuwa naye walikutwa wamezirai. Tukio hilo lilizua taharuki kubwa.
Rais Abdulatif hakuamini macho yake, akawa anauliza kwa ukali “Binti yangu yuko wapi?”
Lakini hakukuwa na aliyejua. Yasmin alikuwa ametoweka ghafla. Kila aliyeshuhudia alishangaa.
Harusi ikavunjika. Badala ya furaha sasa ikawa huzuni. Bwana harusi na mke wa Rais Sharif Abdullatif Bi Kulthum
walikuwa wanalia kutokana na muujiza huo.
Usiku ule ule Rais Abdullatif aliita masheikh Ikulu na kuwauliza kama walikuwa wanajua kilichomtokea binti yake.
Kila sheikh alisema lake. Wako waliomwambia kuwa binti yake alikuwa amechukuliwa na wachawi. Wako waliomwambia kuwa haikuwa muafaka kwa binti yake kuolewa na Abubakar ndiyo sababu tukio hilo limetokea. Na wako waliomwambia kuwa Yasmin alikuwa amechukuliwa na jini aliyekuwa amemchunuka.
Rais Abdullatif hakujua ashike kauli ya sheikh yupi. Kwa vile lilikuwa limeshamfika alikubaliana na masheikh wote na kuwataka masheikh hao kutumia elimu zao kumrudisha binti yake. Aliahidi mamilioni ya shilingi za ki Comoro kwa sheikh yeyote atakayefanikiwa kumrudisha Yasmin.
Licha ya Rais Abdullatif kusubiri kwa zaidi ya miezi mitatu. Hakukuwa na sheikh yeyote aliyefanikiwa kumrudisha Yasmin! Yasmin akabaki kuwa historia kwani hakupatikana tena. Ulikuwa msiba ambao kila mkazi wa Comro alihisi kuwa hautasahaulika.
Hivi sasa mwaka mmoja umeshapita tangu tukio hilo la kuhuzunisha litokee. Tangu wakati ule sikuwahi tena kurudi Comoro. Nilikuwa Unguja nikiendelea na shughuli zangu za uvuvi.
Sasa siku moja ambayo sitaisahau maishani mwangu tulikuwa kwenye boti letu tukielekea maji makuu kuvua samaki. Ndani ya boti hilo tulikuwa wavuvi saba.
Ilipofika saa nne asubuhi tulikuwa mbali sana. Boti yetu ilipigwa na dharuba kali. Mashine ya boti ikazima ghafla. Tilijaribu kuiwasha lakini boti haikuwaka. Ikawa inakokotwa na maji.
Tulipumzika kidogo kisha tulijaribu kuiwasha tena na tena lakini hatukufanikiwa kuiwasha Mashine ilitugomea kabisa. Hatukujua ilikuwa imepatwa na hitilafu gani.
Je nini kitawatokea wavuvi hao?
 
SEHEMU YA 02


Hapo ndipo tulipoanza kufadhaika. Hatukuwa na la kufanya, tukawa tunatazamana!.
Tulikuwa tumepelekwa mbali sana kiasi kwamba hatukuweza kuona vyombo vyovyote ambavyo vingeweza kutusaidia. Tukakata tama kabisa.
Injini ya boti inapozima boti inakuwa kwenye hatari ya kupigwa na dharuba na kupinduka. Kama hilo lingetokea ungekuwa ndio mwisho wetu!
Hata hivyo bahari ilikuwa tulivu. Tatizo letu ni kuwa safari yetu haikuwa na mwisho wala muelekeo maalumu. Boti yetu ilikuwa inakokotwa kufuata upepo unakokwenda.
Mpaka jua linakuchwa hatukuwa tumetokea kwenye nchi yoyote wala kisiwa chochote. Ndani ya boti tulikuwa na vyakula vya akiba lakini hakukuwa na yeyote miongoni mwetu aliyesikia njaa.
Usiku ukapita kwa taabu huku tukiendelea kupelekwa. Asubuhi tuliendelea tena na jitihada ya kuiwasha injini lakini injini ilikataa katakata kuwaka. Tukaendelea kukokotwa hadi jioni. Hapo tukatoa vyakula vyetu na maji tukala kidogo tu.
Tulilala tena kwenye boti hadi siku ya tatu na ya nne. Vyakula vikatuishia licha ya kwamba tulikuwa hatuli sana. Tulibakisha maji kidogo tu.
Sasa tukahisi kwamba kama hatutakufa maji tutakufa kwa njaa kwani kwa siku hizo nne tulizokuwa baharini tulikuwa tumekonda.
Alfajiri ya kuamkia siku ya tano ndipo tulipotokea kwenye kisiwa. Sote tukashukuru ingawa hatukujua kilikuwa kisiwa gani na kilikuwa katika eneo gani.
Kilikuwa kisiwa kikubwa ingawa hakikuwa kikubwa sana. Kwa vile tulikitokea wakati wa usiku hatukukiona kwa sababu ya giza. Tulikiona kulipoanza kucha. Wakati tunakiona tulikuwa tumekikaribia sana. Sote tukapata furaha na matumaini ya kuokoka.
Mawimbi yaliendelea kutusukuma kidogodogo na kutufikisha kwenye maji madogo kabisa.
Suala kwamba kisiwa hicho kilikuwa kisiwa gani na kipo wapi halikuwa na umuhimu kwetu. Kilichokuwa muhimu ni kuwa tumefika mahali ambapo tungeweza kuyasalimisha maisha yetu nap engine kupata msaada wa kutuwezesha kurudi kwetu.
Tulishusha nanga na kushuka kwenye boti. Maji yalikuwa yakitufikia kwenye magoti. Tukaliacha boti na kutembea kwa miguu kwa kuyasukuma maji hadi tukafika ufukweni mwa bahari. Mahali tulipotokea hapakuwa na muinuko mkubwa. Tukapanda kwenye nchi kavu na kuanza kutembea kwemye vichaka huku tukiangaza macho huku na huku.
Kulikuwa na kunguru wengi waliokuwa wakiruka ruka kwenye miti. Jinsi walivyokuwa wakipiga kelele walikuwa kama wanaotukaribisha katika kisiwa hicho kilichokuwa kimya.
Tukaendelea kutembea tukiingia ndani zaidi ya kisiwa. Mtarajio yetu yalikuwa kupata mji au kijiji kilichokuwa kinakaa watu ili tuweze kusaidiwa.
Baada ya mwendo wa kama nusu saa tulianza kuona vibanda vilivyokuwa vimebomoka. Tukapata matumaini kuwa kulikuwa na watu waliokuwa wanaishi katika kisiwa hicho. Pia tulikuta visima viwili vya maji ambavyo vilikuwa vimekauka.
Wakati tunaendelea kwenda ghafla tuliona tumetokea kwenye barabara pana ya changarawe. Tukaifuata ile barabara mpaka tukatokea katikati ya mji. Ulikuwa mji mzuri uliokuwa na barabara na majumba. Lakini nyumba zote zilikuwa zimechakaa na kubomoka. Baadhi yake zilionekana kama mahame.
Jambo ambalo lilitushangaza ni kuwa hatukuona mtu hata mmoja. Mji wote ulikuwa kimya kabisa. Tulikuwa ni sisi peke yetu tu. Tulikatiza mtaa hadi mtaa kutafuta wenyeji wa kisiwa hicho lakini hatukuona mtu.
Udadisi ukatufanya tuanze kuingia katika zile nyumba. Tuliingia katika
nyumba ya kwanza. Tukakuta vitu vya ndani vilivyochakaa na kukongoroka. Vilikuwa kama vitu vya zamani visivyotumika tena. Katika kutafiti tafiti tulishituka tulipokuta mafumvu na mifupa ya binaadamu. Kuna iliyokuwa imelala kwenye kitanda na mengine ilisambaa ovyo.
Tukatoka haraka katika nyumba ile na kuingia katika nyumba nyingine, nako tulikuta vitu mbalimbali vya ndani ya nyumba vilivyokuwa vimechakaa na mifupa ya binaadamu.
Tukawa tunatazamana kwa hofu. Kila mmoja wetu alikuwa akijiuliza moyoni mwake, kulikoni? Lakini hatukupata jibu.
Katika mitaa mengine tulikuta mafuvu na mifupa ya binaadamu ikiwa barazani mwa nyumba na kando kando ya barabara. Tulivyozidi tena kwenda mbele tulikuta mifupa ya mikono nay a miguu ya binaadamu ikining’nia kwenye miti. Tukawa tunazidi kuitazama ile mifupa huku tunazidi kwenda.
Ghafla tukatokea kwenye jumba moja kubwa. Jumba hilo ndilo lililokuwa kubwa na zuri kuliko jumba lolote katika kisiwa hicho.
Mbele ya jumba hilo kulikuwa na bustani ya maua na miti ya vivuli. Kutokana na uzuri wa jumba hilo tukaona tuingie ndani ili tuangalie lilivyo.
Tulipoingia tu pua zetu zilikaribishwa na harufu nzuri ya manukato yaliyokuwa yananukia humo ndani. Tulitembea katika sakafu ya marumaru iliyonakishiwa maua ya kupendeza.
Tulikuwa tumeingia katika ukumbi mpana uliokuwa na madirisha na mapazia ya hariri. Tulikuta meza, viti na makabati. Zilikuwa fanicha za kifahari sana.
Baada ya kuupita ukumbi huo tulitokea katika kumbi nyingine ndogondogo zilizokuwa na vyumba vipana. Tukawa tunaingia kila chumba kuchunguza.
Katika chumba cha kwanza tulikuta kitanda kilichotandikwa vizurii. Pia tulikuta makabati ya vioo yaliyokuwa yanapendeza.
“Inaelekea kuna watu wanaoishi ndani ya jumba hili” Mwenzetu mmoja akasema.
“Lakini mbona hatuwaoni hao watu?” Mwingine akauliza.
“Ndiyo hatuelewi sasa” aliyesema mwanzo akamjibu.
Je wavuvi hao wametokea kwenye kisiwa gani hicho na ni kitu gani kitakachowatokea?
 
SEHEMU YA 03



Tulitoka katika kile chumba tukaingia katika chumba kingine. Pia tulikuta kitanda na makabati. Tukawa tunatazamana kwa mshangao. Kutoka hapo tulichangukana. Kila mmoja akawa anafungua chumba alichotaka na kuangalia ndani.
Mimi niliingia katika vyumba viwili. Nilipoingia chumba cha tatu nilishituka nilipomuona msichana mzuri amelala kitandani. Alikuwa amelala usingizi kabisa huku amejifinika shuka kuanzia miguuni hadi shingoni. Uso wake uliokuwa wazi ulikuwa umeelekea upande wangu.
Nilipomuona nilisita kwenye mlango na kujiuliza msichana huyo ni nani na kwanini alikuwa peke yake katika jumba hilo.
Baada ya kusita kidogo niliingia ndani. Nilikuwa nataka kuhakikisha kama alikuwa hai kweli au amekufa.
Nilipofika karibu yake, msichana huyo alifumbua macho ghafla. Akashituka aliponiona.
“Wewe nani?” akaniuliza kwa mshangao akitumia lugha ya kingazija ambayo nilikuwa siijui vizuri. Lakini nilimjibu kwa Kiswahili.
“Mimi ni mgeni katika kisiwa hiki na katika jumba hili, je wewe ni nani?”
Alikuwa anajua Kiswahili. Akanijibu kwa Kiswahili cha kipemba.
“Miye ni Yasmin, binti wa Rais Shariff Abdilatif wa Comoro!”
SASA ENDELEA
Nilishituka sana aliponiambia yeye ni binti wa Sharif Abdulatif wa Comoro.
Papo hapo nikakumbuka ile harusi iliyovunjika kati ya binti wa rais wa Comoro na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi nchini humo.
Mimi nilikuwa mmoja wa waalikwa kutoka Zanzibar na nikashuhudia maajabu. Yasmin alitoweka katika mazingira ya kutatanisha baada ya gari iliyokuwa inampeleka hospitali kupasuka tairi na kuingia kwenyenye mtaro. Yasmin alikuwa anakimbizwa hospitali baada ya kuanguka ghafla wakati baba yake Rais Sharif Abdulatif anataka kutoa idhini ya kumuozesha binti yake.
Baada ya kutoweka ghafla kwenye gari, Yasmin hakupatikana tena na sasa mwaka ulikuwa umeshapita.
Ingawa sikuwahi kuonana naye uso kwa uso lakini niliona picha zake katika magazeti na televisheni wakati habari zake zilipokuwa zinaandikwa na kutangazwa.
Alikuwa ndiye Yasmin kweli binti wa Rais Sharif Abdulatif wa Comoro.
Kwa kweli tukio la kumkuta ndani ya jumba hilo na katika kisiwa kile kisicho na watu, mbali ya kunishitua, liliniongezea hofu mara dufu.
“Wewe ni binti wa Rais wa Comoro” nikamuuliza kwa mshangao.
Huku akinyanyuka kwenye kitanda na kuketi msichana huyo alinijibu.
“Ndiye mimi. Rais Sharif Abdulatif ni baba yangu”
Nikiwa kwenye mshangao niliendelea kumtazama msichana huyo bila kummaliza. Alikuwa amevaa shumizi inayoonya. Alipoketi alijifunga ile shuka kwenye mwili wake kama mtu aliyekuwa anaona baridi. Lakini nilijua alikuwa anajisitiri kwa sababu sumizi aliyovaa ilikuwa inaonya.
Kwa tamaduni za kiislamu na za kule Comoro mwanamke hatakiwi kuonekana mwili wake pamoja na kichwa chake.
Lakini Yasmin kwa sababu ya kutaharuki alisahau kujifinika kichwa. Nywele zake za mawimbi zilizokuwa ndefu zilikuwa zimeshuka na kumfikia mabegani.
“Yasmin umefikaje huku?” nikamuuliza.
Yasmin akanitazama. Macho yake makubwa yenye mboni za rangi ya kahawia yalinifanya nikiri kimoyomoyo kuwa Yasmin alikuwa mzuri.
Badala ya Yasmin kunijibu, na yeye akaniuliza.
“Kwani wewe umefikaje hapa?”
“Mimi siko peke yangu, nina wenzangu na tumefika hapa kwa bahati mbaya. Sisi ni wavuvi kutoka Zanzibar. Chombo chetu kilipigwa na dharuba kikapata hitilafu. Kwa siku nne kilikuwa kinaelea kwenye maji, hatujui tunakokwenda. Leo siku ya tano ndio tumetokea kwenye kisiwa hiki”
“Huko ulikopita hadi umetokea hapa, umeona nini?”
“Tumekuta nyumba hazina watu. Pia tumekuta mafuvu na mifupa ya watu kila mahali”
“Basin a nyinyi ndio mtakuwa hivyo hivyo, hamtapona”
Yale maneno yalinitisha na kunifadhaisha.
“Yasmini kwanini unaniambia hivyo. Mimi ni ndugu yako wa Zanzibar. Hata katika harusi yako na mwana wa mkuu wa majeshi ya ulinzi wa Moroco nilialikwa na nilikuja Comoro lakini wewe ulitoweka katika mazingira ya ajabu. Na leo ndio nakuona hapa” nikamwambia Yasmin kwa hofu.
“Nashukuru kwamba leo nimetembelewa na ndugu yangu wa Zanzibar na nashukuru kwamba umenijua lakini naona uchungu kuwa nitayashuhudia mauti yako muda si mrefu”
>Kwanini unaniambia hivyo Yasmin?. Niambie”
Yasmin bdala ya kunijibu aliangua kilio.
Wenzangu mmoja mmoja wakaanza kuingia mle chumbani na kushangaa kumuona yule msichana akilia.
“Je ni nani huyu?” Mmoja wa wale wenzangu akaniuliza wakati wenzetu wengine walikuwa wamepigwa na butwaa.
“Ni msichana nimemkuta amelala humu chumbani. Nilipoingia alizinduka na kuniambia anaitwa Yasmin. Ni binti wa Rais wa Comoro” nikawaeleza.
“Ni binti wa Rais wa Comoro?” Baadhi ya wenzangu wakaniuliza kwa mshangao. Walidhani labda nilikosea kusema.
“Ndiyo, mwenyewe ameniambia hivyo na mimi pia namfahamu. Nilihudhuria katika harusi yake nchini Comoro mwaka uliopita.
“Si ilisemekana kuwa yule binti alitoweka?” Mmoja wa wenzangu akauliza.
“Ni kweli. Mimi pia nimeshangaa kumkuta katika kisiwa hiki, tena akiwa peke yake. Na amenieleza kitu cha kutisha”
“Kitu gani?”
“Mh! Ameniambia anaona uchungu kuwa atayashuhudia mauti yetu muda si mrefu!”
Wenzangu wote wakashituka, ndipo nilipojua kuwa hakuna mtu anayependa kufa.
“Kwanini amekwambia hivyo?” Sautu za kuuliza zilisikika kutoka kwa wenzangu.
“Ndio nilikuwa namuuliza, naona analia”
“Asilie, atueleze ili tujue…”
“Usilie dada yangu, nyamaza utueleze ili tujue jinsi ya kujihami” nikamwambia msichan huyo.
“Pia atueleze jinsi alivyofika katika kisiwa hiki cha ajabu” Mtu mwingine akasema.
 
Back
Top Bottom