Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Kwa nini anaitwa Peter Samson Maro?, na sio Peter Mramba au Peter Mkapa?
 
phillemon mikael said:
sasa kama ni mkapa kashastaafu na hakuna ajabu kuwa na nyumba ngambo.mbona kuna viongozi wengine wa nje wana nyumba na miradi bongo? ili mradi mtupe proof kwamba amenunua na pesa hARAmu, kuhusu mtoto wa kufikia sio ajabu ukimkuta mkeo na mtoto ni mwanao,yeye vilevile,hakuna la ajabu,kama mmeshasema na yeye aliweka wake wawili..ukipenda tunda penda na mti wake.

hatukatai mkapa kafanya makosa,lakini pia meme yamezidi ,,,kuliko kupoteza muda kumjadili,tutakuwa tunamsaidia sitting president kwa kumpa constructive critisism,kwa sababu wapinzani si wamelala.

mkapa sasa amepokea kiti cha boutrous ghali cha chairman south commission mkumbuke mwalimu pia amewahi kuwa mwenyekiti wa tume ya kusini.

WANANCHI WANAMKUMBUKA MKAPA HUKU USWAHILINI.,


Kwani ile asilimia 29 ya rada ilitumika vipi? asilimia hii imetamkwa wazi na wazee wenyewe, kwa hiyo siyo majungu kama unavyoashiria kusema. Bado hatuelewi kama kick-backs kama hiyo ya rada zilitumika katika procurements za ndege ya Rais na pamoja na miktaba mingine bomu kama ITPL, TANESCO, ATC, NBC na mlolongo mrefu tu. Kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa South South Commisison isitumike kama warrant ya kumtetea Mkapa dhidi ya utwala wa rushwa alioendesha katika nchi yetu. Kwa taarifa yako, siri zote za mikataba yenye rushwa zilizoendeshwa na serikali ya Mkapa zitaibuliwa tu, hawawezi kuendelea kujificha.
 
Jamani,

Inawezekana jamaa ni smart tu hataki kuwa na familia za ajabu ajabu ndo maana anatumia "kinga" kila atokapo nje ya ndoa.......

Ogah, swali zuri sana, inawezekana ni katika kulinda heshima ya BWM, Nilivyosikia akina Maro wapo upande wa mama, kwahiyo inawezekana kijana anatumia jina la ujombani.

FD
 
Lini tutapata viongozi Malaika ? Kama haiwezekani basi tuwe na mstari wa kupima ili sio kila kiongozi akitoka madarakani awe kama Nyerere (maskini).
Kwani hii inatokana na historia mbaya ya wazee wastaafu wetu ambao walitumikia nchi hii kwa moyo na uaminifu wa kutukuka lakini wameishia kwenye chumba kimoja cha kupanga (mfano: Paul Sozigwa, Moses Nnauye, Timoth Apiyo n.k.).
 
kama Mkapa kanunua SA na kuweka hadharani hadi kumualika mzee Madiba basi tujue kuwa hiyo ni nyumba yake ya haki haina longo longo yote.

Kuhusu marais wa nchi nyingine kuja kununua nyumba hapa siyo lazima, maana kila mtu anapenda maeneo yake ndiyo maana wewe muandishi nyumba yako umeijenga Masaki mimi yangu ipo Mbande.

Viongozi kununua nyumba siyo Bongo tu popote pale na huwezi kukosa watu kulalamika kama Mh T Blair PM wa UK aliponunua Nyumba kule London watu walilalamika hivyo sishangai kwa wewe kuona maajabu.

Lakini rais ana tofauti gani na wakurugenzi wanao nunua nyumba nje za nje? Na zaidi ya yote hatujui hata gharama zao si bora huyu kama ameweka hadharani (kama habari hizi ni za kweli maana hakuna kivuli ku confirm hizi habari wala gazeti linalozungumzia hii habari kama lipo tafadhali tuwekee na sisi tusome jamani).
CIO
 
Kaka/dada kabla ya kujibu si unatakiwa usome mada yote toka mwanzo?

fd
 
On the other hand matajiri kununua property in SA (cape town to be specific) ni ni more rewarding than in TZ for obvious reasons

Location Location Location
 
Invisible,

Hamna noma, ila mimi huwa sipendi mtu anarukia rukia kisha anatoa lawama.

Hamna noma nimeelewa. na msg delivered

FD
 
DrWHO said:
On the other hand matajiri kununua property in SA (cape town to be specific) ni ni more rewarding than in TZ for obvious reasons

Location Location Location
Viongozi wanakwenda kuwekeza nje halafu wao wanaita watu wa nje kuja kuwekeza nchini na kuwapa mikataba kichaa.
 
Jafar said:
Lini tutapata viongozi Malaika ? Kama haiwezekani basi tuwe na mstari wa kupima ili sio kila kiongozi akitoka madarakani awe kama Nyerere (maskini).
Kwani hii inatokana na historia mbaya ya wazee wastaafu wetu ambao walitumikia nchi hii kwa moyo na uaminifu wa kutukuka lakini wameishia kwenye chumba kimoja cha kupanga (mfano: Paul Sozigwa, Moses Nnauye, Timoth Apiyo n.k.).

Kwamba mifano ya hao wazee ndiyo imechochea rushwa hapa nchini. Nadhani jawabu lake lilikuwa ni kuweka taratibu za hifadhi kwa wastaaafu. Mtu kama rais wa nchi hawezi kuendesha rushwa kwa kuoogopa kuishia kwenye chumba cha kupanga; mbona mzee Jumbe bado anaishi kwa raha pale mji mwema tangu atoke madarakani miaka 23 iliyopita. Rais ndiye anatakiwa asimame madhubuti dhidi ya rushwa lakini hapa kwetu mambo yako kama kinyume vile.
 
Nobody is begrudging BM to buy a property in South Africa, but when you become a president of a nation it's different you need to take responsibilities. (Tanzania poor people are still looking after him, even though we know he sold most of our resources for nothing to South African companies) By the way why can't you stop collecting any payments from poor people?

BM stayed most of his time in USA representing Tanzania and after that he became to be a president. One wonders if this was his intentions, it does mean that he duped us to believe what he was preaching and he can't practise himself. What a shame.

No wonder is full of praise to JK because he knows he is the only one who can bring him to justice.

He used our resources to enrich his friends and himself. Please sell all your assets and leave bongo alone. Do not forget to return the 29% for the defective Rada because the British has uncovered the facts.

And we would like all cabinet members who want to do business to resign their positions instead of facilitating dubious deals etc. If they are so smart and well educated we welcome them out of the government and come to compete with us without uncles in the system.

How can you stay in government for all this years stealing from poor people – you guys are disgusting and should be ashamed of yourselves.

Tanzania will continue to be there but remember stolen money won't last and can't be carried to your graves.

You will leave Tanzania the same way you came and history will judge you. Shame on you.

____________________________________
Dua la kuku halimpati mwewe
 
Mkapa aponda wanaombeza

*Asema sera yake ya ubinafsishaji ilikuwa 'poa'

Na Charles Mwakipesile, Sumbawanga

RAIS mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bw. Benjamin Mkapa, amewataka wanaoponda sera ya ubinafsishaji aliyoianzisha waache, na badala yake waende kuangalia shamba la kisasa la mifugo na kiwanda kinachomilikiwa na mzalendo, Dkt. Chrisant Mzindakaya.

Alitoa kauli hiyo juzi mara baada ya kutembelea shamba la mifugo la Nkundi lililokuwa linamilikiwa na Serikali na kubinafsishwa kwa Dkt. Mzindakaya ambaye ni mbunge wa Kwela.

Rais mstaafu baada ya kulikagua shamba hilo na kujionea ng'ombe zaidi ya 3,000 wenye uzito wa zaidi ya kilo 500 kila mmoja, alisifu na kusema hilo ndilo lilikuwa lengo lake la ubinafsishaji kwa ajili ya kuwawezesha wazawa.

"Kwa mtindo huu kama kuna Mtanzania atakayediriki kuniponda kwa kuanzisha sera hii, mimi naona atafute jambo lingine, lakini si hili ambalo kwa sasa naweza kusema limefanikiwa kwa kiwango kikubwa na midomo ya watu sasa itafungwa," alisema.

Aliwataka wanahabari kutangaza mafanikio hayo ya wazawa waliofanikiwa katika uwekezaji, ili kuwafanya Watanzania waweze kufahamu kinachoendelea na mafanikio ya sera ya ubinafsishaji kwa maendeleo ya Taifa.

"Huu ni ndio uwezeshaji niliokuwa naupigania kwa nguvu zangu zote kwa maendeleo ya Taifa, sasa naweza kusema nimetua mzigo kwa amani na kwa hakika napumzika nikiwa na raha kubwa moyoni mwangu, kutokana na kuacha wazawa wakiwa wawekezaji wakubwa kama Mzindakaya," alisema.

Alisema wakati anatangaza sera ya ubinafsishaji mali za Serikali watu wengi hawakuelewa lengo lake na hivyo kuzua mijadala mingi, lakini kwa sasa wataelewa kutokana na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika shamba hilo ambalo awali lilikuwa limekufa .

Bw. Mkapa alisema ili kumaliza ubishi huo, waliokuwa wanaiponda sera hiyo kama wanataka kuhakikisha kuwa kuna kitu kimefanyika waende katika shamba hilo wajionee jinsi lilivyo na ng'ombe wa kisasa, ambao ilikuwa ndoto kwa Mtanzania kumiliki shamba kama hilo.

Baada ya kufika, alipewa taarifa fupi ya mradi huo na Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni inayomiliki shamba hilo na kiwanda cha kisasa cha kusindika nyama ya Sumbawanga Agriculture and Animal Food Industries (SAAFI), Dkt. Mzindakaya alisema alichokifanya katika mradi huo ni kumdhihirishia Rais mstaafu kuwa hata Watanzania wanaweza.

"Nakumbuka mzee, ulianiambia nilipokuja Ikulu siku moja, kuwa uliumia moyo ulipokwenda Uganda na kupelekwa na Rais Yoweri Museveni kwa mzawa wa Uganda aliyefanya uwekezaji mkubwa, sasa na mimi leo niliona uje uone kuwa hata sisi Watanzania tunaweza na akija atakuta mambo ya ajabu," alisema Dkt. Mzindakaya.

Alisema wakati akiadhimisha miaka 40 ya kukaa bungeni, aliona aunganishe kwa kumwalika Rais mstaafu ili ajionee sera aliyoianzisha na kuiacha, wakati akiondoka madarakani ikilenga kuwawezesha wazawa kumiliki uchumi na kupunguza umasikini.


Bwana Mkapa anasema uwongo:

(1) Sera ya kubinafsisha siyo kwamba aliitunga yeye. Ilikuwa ni shinikizo la vyombo vya fedha duniani na ilianza wakati wa Mwinyi, na ni rais Mwinyi aliyemaarufisha neno "kubinafsisha". Kwa hiyo Mkapa anataka kujizolea sifa kama ndiye mtu aliyeleta sera ya kubinafsisha wakati tunajua kuwa Mkapa ameondoka bila kuwa na signature initiative yoyote pale nchini. Alichofanya yeye ni kutekeleza sera hiyo bila kutumia akili yoyote.

(2) Lengo la sera ya kubinafsisha ilikuwa ni kuifanya serikale ichane na shughuli za biashara. Lengo halikuwa kuwafanya Watanzania wawe matajiri kama anavyodai.

(3) Sera haikuwa na ubaya wowote, anacholaumiwa ni kwenye utekelezaji. Kama sera ingetekelezwa vizuri bila kutumia njia za rushwa ni kweli ingeweza kuleta faida kubwa kwa nchi na bila shaka sehemu kubwa ya mashirika ya umma ingekuwa inamilikiwa na watanzania wenyewe. Hebu aangalia nchi zilizowahi kuwa na mashirika ya umma halafu yakabinafsishwa. Mifano mizuri ni pamoja na Japan na China; hakuna shirika la umma lililobinafsihwa na kupewa watu wa nje. Badala yake China iliyaambia makampuni ya nje kuwa fungueni viwanda vyenu nchini halafu viwanda vyetu vitajifunza technologia na mbeinu kutoka kwenu. Japan nayo ilipoamua kuuza mashirika kama NEC, JR ni wajapani tu walioruhusiwa kuyanunua wakati huo, siyo watu wa nje.

(4) Mzindakaya ni mmoja kati ya wachache sana waliobahatika kununua mashirika ya umma na wote wale walikuwa connected na serikali. Mzindakaya alikuwa mkali sana wa kuibana sana serikali bungeni kwa hiyo hatushangai kuwa serikali ilifanya jambo fulani kumnyamazisha kusudi waendelee kuuza kinyemela mashirika ya umma. Ni dhahili kuwa baada ya kumwuzia shamba hilo, Mzindaka hakuwahi tena kuulizia chochote kuhusu uuzwaji holea wa mashirika ya umma.

Mimi naona kama Mzee Mkapa anasumbuliwa na sense of guilt kutokana na serikali ya rushwa aliyoeendekeza na ndiyo maana tangu alipokaribia kuondoka madarakani amekuwa katika kampeini ya kujitetea na kujiandikia historia yake apendavyo badala ya kuachia historia yenyewe ichukue mkondo wake. Mabomu la rada ya asilimia 29 rushwa na mikataba bomu kama ile ya ITPL na madini vyote ni matokeo ya utawala wake wa rushwa. Pamoja na upungufu wa Kikwete, kuna ukweli kabisa kuwa amerithi mzigo mkubwa sana kutoka kwa Mkapa kwa vile mikataba mingi ilyofanywa na Mkapa haiwezi kubadilishwa bila kuiweka serikali kwenye matatizo ya kisheria. Mkapa alipokuwa akiambiwa kuhusu rushwa serikalini mwake alikuwa akibweta kwamba leta ushahidi huku akijua kabisa kuwa hakuna raia atakayefanya hivyo; ngija sasa ushaidi utatoka uingereza kuhusiana na rada.
 
Kichuguu,
No wonder you are a Professor. Uchambuzi murua kabisa wa huyu kuwadi wa soko huria. Sentensi yako moja inayosema, "alitekeleza ubinafsishaji bila kutumia akili yeyote ina sum up kila kitu." Iko siku dhihaka zake hizi zitakuja pata majibu sahihi
 
Huyu mnafiki mkubwa huyu amezoea kudanganya wananchi, na hata baba wa taifa alimdanganya kuwa ni mjamaa kumbe ni mtoto wa kuotea mbali,

Ni huyu huyu Mkapa, aliyemtukana Dk. Mzindakaya katika kikao cha wabunge wa CCM, kwenye issue ya Idd Simba na rushwa ya sukari ya jeshi, alimtukana kama mtoto mdogo na kumuita pumbavu, kwa hiyo baada ya kustaafu sasa Dk.Mzindakaya amekuwa mfano wa kuigwa?

Mkapa anede Ulaya akale mapesa aliyokomba kwenye ubinfsishaji, na marafiki zake Yona, Idd Simba, Kigoda, na Ruhinda, wabongo hatujalala ila ni waungwana!
 
Idd Simba tena ? Mzee Es hebu nimegee kidogo ya huyu aliyekuwa akipiga debe la uzawa.
 
Huyu MKapa jambazi tu kama majambazi mengine.

Hana jipya zaidi ya kusifia sera zilizoliingia taifa hasara kubwa.

Yeye shamba lakeliko wapi? Kazi kuzunguka Ulaya na kukusanya michuzi ya
Wafadhili badala ya kusaidia kuendeleza taifa.
 
Huyu MKapa jambazi tu kama majambazi mengine.

Hana jipya zaidi ya kusifia sera zilizoliingia taifa hasara kubwa.

Yeye shamba lakeliko wapi? Kazi kuzunguka Ulaya na kukusanya michuzi ya
Wafadhili badala ya kusaidia kuendeleza taifa.

Nasikia kile kiwanda cha miwa cha Mtibwa au Kilombero ni chake. Labda na yeye analima miwa kule.
 
Jamani,

BENJAMIN WILLIAM MKAPA, former president of Tanzania ought to undergo psychotherapy that'll ease his suffering from his gulity conscience. He can't have a sound sleep kama anapata muda wa kusoma forum hii.. the man was nepotist, corrupt.......
 
Mkapa anachokifanya sasa ndicho matapeli wengi wanachokifanya. Hakuweza kugundulika/aliweza kudanganya watanzania kwa muda mrefu akijibanza kwenye mgongo wa utandawazi. Alivyotoka kwenye Urais akagundua kuwa watu walikuwa wamemgundua. akaamua kukaa kimya. watanzania walikuwa na shakuku kubwa ya kuwa na mabadiliko ya haraka. Mkapa ameona sasa mabadiliko ya haraka hayajatokea ni kama alivyoacha nchi. amepata nguvu ya kuanza fix zake tena kwa sababu anajua kuwa wanaanza kusahau.

Hila watu walio makini hawawezi kumsahau mapema. Tunashukuru kwa kazi nzuri aliyoifanya. ametengeneza Historia nzuri ktk Mashirika yetu na ubinafsishaji kwa ujumla.
 
Back
Top Bottom