Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Habari nilizozipata leo according to the dataz ni kwamba sasa makapa, Yona, na chenge wameamua kumtumia the same defence lawyer, sasa ni ana madhumuni yao ni nini hasa kama sio kujaribu ku-coordinate namna ya kuuficha na kuuuhalalisha ufisadi wao?

Rais mzima wa zamani wa taifa na jamhuri, anatafuta nini kwenye kutafuta wanasheria na mawaziri wake wa zamani? Na huko sheria tunazo habari kwamba mtoto wa makapa aliwekwa huko kwa makusudi ili aje avuruge uchunguzi, kwa hiyo tunawa-pressure wabunge wadai aondolewe mara maoja huko tuendelee na kazi ya wananchi!

Sasa kwa wale mlionao karibu huko Lushoto, na kwenye wazee wa vijisenti, tafadhalini waambieni kuwa wananchi tuko one step ahead, na tuko nao bega kwa bega, ni kwamba tutakula nao sahani moja mpaka
Mpaka kieleweke!

Wallahi siku za mwizi ni arobaini, sasa zimafikia mwanangu mpaka watinge tu kwenye mahakama ya wananchi Kisutu, tena tunamkumbusha waziri mkuu Pinda kwamba hawa wasipelekwe mahakama kuu, maana kesi yao ni sawa tu na ya wa wezi wa mbuzi na kuku, msiwape kichwa bure wakadhani tuhuma zao ni za kii-intellectualism na politicalism, no hawa ni wadokozi wakubwa yaani kwa jina lingine ni mijizi isiyokuwa na huruma na wananchi kabisaa, sasa kwa nini sisi wananchi tuwaonee huruma!

Hawa ni kuwaweka hapa Sanamu Monument ili wananchi tuwapige mawe, tena mchana kweupe! Off course hayana huruma haya wewe lijitu linaweka mihela yote nje, huku wananchi wanakufa na njaaa, dawa ni kuyapiga mawe!
 
barabara,shule mpya,madaraja,msamaha wa madeni..ametuachia national reserve kubwa kuliko wakati wowote...2 billion dollars...[mmeshauliza zimebakia ngapi siku hizi????]

pamoja na hayo natambua pia anayo makosa...sasa kikwete hadi saasa kuna mradi gani mkubwa katupa???

suala la uhuru wa vyombo vya habari alileta mzee mwinyi...kikwete hana sifa kwenye hili kwani inajulikana yeye ni mtu wa kununua waandishi....na magazeti...hilo sio siri!!!!

Ni lazima nchi ijue gharama ya barabara, shule mpya, madaraja na madeni.

Kama manunuzi ya radar yaliweza kuwanufaisha wao. Kuna uwezekano mkubwa kuwa ujenzi wa barabara, mashule na mafanikio katika reserve umewanufaisha wachache zaidi kuliko taifa. Na hii imejionyesha wazi kabisa katika kashfa ya BOT.
 
Wakuu kama wametumia same lawyer na tumeishajua kuwa Chenge tayari anavijisenti kila mahala mjue hata Mkapa vijisenti vyake si haba. Na kila alichofanya Chenge kilikuwa na baraka za Mkapa.

Hii itakuwa ni picha tosha za kuhakikisha tunaongeza nguvu ktk kuhakikisha tunapata kila UFIsadi walioufanya.
 
Ni lazima nchi ijue gharama ya barabara, shule mpya, madaraja na madeni.

Kama manunuzi ya radar yaliweza kuwanufaisha wao. Kuna uwezekano mkubwa kuwa ujenzi wa barabara, mashule na mafanikio katika reserve umewanufaisha wachache zaidi kuliko taifa. Na hii imejionyesha wazi kabisa katika kashfa ya BOT.


[B]....hayo madaraja,barabara,shule na madeni aliyosamehewa ameondoka nayo au wanatumia wananchi!!????..watanzania tufikie mahali mtu akifanya jema tukiri...kama vile tunavyoona mabaya...

....huyu kikwete hadi leo mwaka wa pili na nusu..ameshafanya jambo gani.....zaidi hata barabara ya km 2 ya ubungo to mwenge inamshinda kumalizia.....

...kikwete hana ubavu wa kupambana na ufisadi wakati ...pale benki kuu pesa zilichotwa kufinance kampeni yake....

.....nasisitiza mkapa ana makosa yake...lakini rekodi yake ya utumishi ina nafuu kubwa ...nakiri kusema kimaendeleo hadi sasa baada ya nyerere nii mkapa.....hata mkipinga ni chuki tu ...lakini huo ndio ukweli...

muhukumuni mkapa kwa makosa yake lakini na mazuri yake mengi muyakiri....

serikali ya kikwete hadi sasa haijafanya lolote zaidi ya kupindisha mawazo ya watanzania wenye akili nyepesi kwa propaganda mkwepesho!!!....sisi hatuangalii uzuri we want perfomance ...period!!!![/
SIZE[/B]]
 
...mkapa alituachia dola bilioni mbili kwenye national reserve account...zikitosha ku sustain matumizi ya nchi miezi 10....kumbuka alipokea nchi ikiwa na akiba isiyotosha hata wiki moja.....

wanaotaka tusimuone kikwete kituko watuambie kikwete ameongeza national reserve au anaendelea kuikwangua ...mbona siku hizi hatutangaziwi tuna dola ngapi akiba kama taifa kila baada ya miezi mitatu??
 
...mkapa alituachia dola bilioni mbili kwenye national reserve account...zikitosha ku sustain matumizi ya nchi miezi 10....kumbuka alipokea nchi ikiwa na akiba isiyotosha hata wiki moja.....

wanaotaka tusimuone kikwete kituko watuambie kikwete ameongeza national reserve au anaendelea kuikwangua ...mbona siku hizi hatutangaziwi tuna dola ngapi akiba kama taifa kila baada ya miezi mitatu??

Tunachotaka siyo kumuangamiza Mkapa. Tunachokitaka ni kuhakikisha wale wote wezi wa mali za umma hata kama ni wewe na mimi sheria inachukua mkondo wake. Hata kama ni JK lazima sheria ichukue mkondo wake.

Hakuna aliye juu ya katiba ya nchi. Juu ya dola la Watanzania.

Mambo yote yatakayofanyika yatafanyika kulingana na sheria zilizopo nchini ambazo hata Mkapa aliapa kuzifuata.

Hakuana kipya hapa. Kama watanzania tunaamua kufuata sheria na tuzifuate. Hatuwezi kuandika katiba na kuwa na viongozi walioapa kuzifuata na wasizifuate.

PM tunaelewa unasema nini lakini tunahitaji kujenga tanzania yenye uadilifu.

Lazimna hata mikataba yote irudi na iangaliwe upya kama hatuwezi kuivunja basi waliohusika wachunguzwe kulikoni.
 
...mkapa alituachia dola bilioni mbili kwenye national reserve account...zikitosha ku sustain matumizi ya nchi miezi 10....kumbuka alipokea nchi ikiwa na akiba isiyotosha hata wiki moja.....

wanaotaka tusimuone kikwete kituko watuambie kikwete ameongeza national reserve au anaendelea kuikwangua ...mbona siku hizi hatutangaziwi tuna dola ngapi akiba kama taifa kila baada ya miezi mitatu??


Phillemon Mikael,

Sijaelewa mpaka sasa hivi unazungumzia nini haswa , kwa hiyo kwa kuwa aliacha hizo hela alizoacha ina justify yeye kuiba hela au ? Hakuna mtu anayesema Kikwete amefanya mambo mazuri , nilimpinga JK hata kabla hajachukua nchi na nitaendelea kumpinga kuokana na kushindwa kutekeleza yale aliyoyasema.

Lakini lazima naye Mkapa awajibishwe kwani yeye alichaguliwa ili aidefend constitution yetu na ameshindwa kufanya hivyo , haya mambo mengine uliyoyasema ni mazuri for Historians they are going to judge him on that .
 
Habari nilizozipata leo according to the dataz ni kwamba sasa makapa, Yona, na chenge wameamua kumtumia the same defence lawyer, sasa ni ana madhumuni yao ni nini hasa kama sio kujaribu ku-coordinate namna ya kuuficha na kuuuhalalisha ufisadi wao?

Rais mzima wa zamani wa taifa na jamhuri, anatafuta nini kwenye kutafuta wanasheria na mawaziri wake wa zamani? Na huko sheria tunazo habari kwamba mtoto wa makapa aliwekwa huko kwa makusudi ili aje avuruge uchunguzi, kwa hiyo tunawa-pressure wabunge wadai aondolewe mara maoja huko tuendelee na kazi ya wananchi!
!

Huyo wakili ni Joseph Mbuna au wametafuta wakili mwingine?

Kama wakili wao ni Mbuna basi hapo hakuna kitu kwani inaeleweka wazi kabisa uhusiano wa Mkapa na Mbuna ulivyo.
Nicholaus Mkapa (Mtoto wa Ben Mkapa) amemwoa Mtoto wa Joseph Mbuna. Joseph Mbuna, Mkapa, Yona na Chenge wote wana share Kiwira Mining.
 
Huyo wakili ni Joseph Mbuna au wametafuta wakili mwingine?

Kama wakili wao ni Mbuna basi hapo hakuna kitu kwani inaeleweka wazi kabisa uhusiano wa Mkapa na Mbuna ulivyo.
Nicholaus Mkapa (Mtoto wa Ben Mkapa) amemwoa Mtoto wa Joseph Mbuna. Joseph Mbuna, Mkapa, Yona na Chenge wote wana share Kiwira Mining.

Hivi na Chenge yupo? Jamani hapa lazima tusimame kidete kweli. Kumbe ndo maana anasema 1bilioni ni vijisenti?

Hawa watu wanatakiwa waandaliwe makazi pale segerea mapema sana.
 
Tunachotaka siyo kumuangamiza Mkapa. Tunachokitaka ni kuhakikisha wale wote wezi wa mali za umma hata kama ni wewe na mimi sheria inachukua mkondo wake. Hata kama ni JK lazima sheria ichukue mkondo wake.

Hakuna aliye juu ya katiba ya nchi. Juu ya dola la Watanzania.

Mambo yote yatakayofanyika yatafanyika kulingana na sheria zilizopo nchini ambazo hata Mkapa aliapa kuzifuata.

Hakuana kipya hapa. Kama watanzania tunaamua kufuata sheria na tuzifuate. Hatuwezi kuandika katiba na kuwa na viongozi walioapa kuzifuata na wasizifuate.

PM tunaelewa unasema nini lakini tunahitaji kujenga tanzania yenye uadilifu.

Lazimna hata mikataba yote irudi na iangaliwe upya kama hatuwezi kuivunja basi waliohusika wachunguzwe kulikoni.

kindo nakubaliana na wewe ..what we need is a sustainable solution sio hii ya kikwete...aunde PCCB ...Huru ambayo haitangiliwa hata na ikulu...bunge liweke sheria nzuri za maadili....nadhani hata zitti alipendekeza hili juzi bungeni..utaratibu pia uweke nanna ya kushughulikia marais na viongozi wa umma pale wanapotenda makosa ya kifisadi...kinga ibakie kwa makosa mengine ya kiutendaji mfano hata uvunjaji wa haki za binadamu katika kutekeleza majukumu kwa manufaa ya umma....mara nyingi rais wengi makosa kama haya huyafanya kwenye maamuzi.....

what i mean ni kuwa tuweke system imara ya kushughulika na haya ....na tuache kufanya as if mkapa ndio mkosaji na tukishamshughulikia yeye ..tumemaliza matatizo ya leo na ya kesho!!
 
kamanda ..unasema mkapa ameiba pesa nyingi kupitia miundombinu...barabara zikaisha...sasa kikwete amekula zote nini mbona hata barabara moja haijaisha??...teh teh kama holiday yake moja inagharimu milioni 500...na anapumzika zaidi ya mara 6 kwa mwaka mnategemea nini!!?
 
...mkapa alituachia dola bilioni mbili kwenye national reserve account...zikitosha ku sustain matumizi ya nchi miezi 10....kumbuka alipokea nchi ikiwa na akiba isiyotosha hata wiki moja.....

wanaotaka tusimuone kikwete kituko watuambie kikwete ameongeza national reserve au anaendelea kuikwangua ...mbona siku hizi hatutangaziwi tuna dola ngapi akiba kama taifa kila baada ya miezi mitatu??


Sijuhi inabidi tuanze kuulizana madarasa ya shule. Hoja unazotoa ni za emotion na mapenzi yako lakini ni utumbo katika uwanja wa sheria na ethics. Serikali kutumia na kuacha reserve haina kitu au negative sio kosa la jinai. Na kiongozi hashitakiwa kwa kuacha hazina haina kitu.

Kwa mfano: Clinton aliacha nchi ina surplus na kwa hesabu zilizopo sasa Bush ataacha nchi ikiwa deficit. Pamoja na peformance yake katika uchumi, watu hawakumwachia Clinton kuendeleza ufuska wake akiwa kama rais.

Vilevile hesabu zako za reserve kutosha miezi 10 sio sahihi. Kama dollar billioni 2 zilitosha miezi 10 mwaka 2005 basi dollar millioni 800 zitatosha zaidi ya miezi minne mwaka 1995 na hiyo ni hesabu ya mashine za matendo tu.

Kama kutakuwa na uchunguzi au mashitaka dhidi ya Mkapa hawezi kujitetea kwa kusema aliacha reserve, alijenga barabara, alijenga shule mpya au uwanja wa taifa. Itabidi ajitetee kwa kuonyesha sheria za nchi zilivyompa ruhusa kufanya kile alichofanya.

Na wewe kama mtetezi wake tuletee misingi ya sheria kuonyesha alichofanya kilikuwa katika misingi ya kisheria
 
Mimi nilichokiangalia siyo kwamba sheria au taratibu hazipo. Kila kitu kipo ndio maana tuna tume ya maadili ya viongozi. Mkapa alijua hili ukiangalia ujumbe ulioweka hapa utagundua sheria inayommaliza Mkapa siyo kwamba itatungwa na Jk hapana ipo. Ila tu ni suala la Rais kuacha sheria ifuate mkondo wake ambacho Mkapa kama alivyokuwa dictator FISADI asingetaka.

Jk kazi yake siyo kutunga sheria mpya ni kusimamia sheria zilizopo kama alivyoapa.

Mkuu Nchi yoyote bila Kanuni na sheria ni kama imekufa. Hatujui kama Mkapa ana Makosa au ana tofauti na Jk. Tunachojua kuna baadhi ya mambo ambayo hayakwenda sawa kipindi chake na yalifanyika hivyo makusudi.

Bado kuna ubinafsishaji wa Makampuni ambayo watanzania bado tunajiuliza kulikoni(NBC et al). Lakini najua watanzania ni watu wazuri sana uchunguzi utafanyika na haki itatendeka.

Mkapa atapata haki yake kama Raia yeyote mtiifu wa Tanzania.
 
kamanda ..unasema mkapa ameiba pesa nyingi kupitia miundombinu...barabara zikaisha...sasa kikwete amekula zote nini mbona hata barabara moja haijaisha??...teh teh kama holiday yake moja inagharimu milioni 500...na anapumzika zaidi ya mara 6 kwa mwaka mnategemea nini!!?

Hapa Mkuu naona kama waziri fulani wa JK mnataka pia kumdondosha.
 
mkapa alituachia dola bilioni mbili kwenye national reserve account...zikitosha ku sustain matumizi ya nchi miezi 10....kumbuka alipokea nchi ikiwa na akiba isiyotosha hata wiki moja.....

wanaotaka tusimuone kikwete kituko watuambie kikwete ameongeza national reserve au anaendelea kuikwangua ...mbona siku hizi hatutangaziwi tuna dola ngapi akiba kama taifa kila baada ya miezi mitatu??

Mkuu tunakusikia sana tena kwa masikio mawili, lakini one at a time, kwanza tulianza na Lowassa, halafu akaja Chenge, sasa tunaelekea kwa baba yao makapa, huenda in the process na wasiokuwemo sasa hivi wakaingia, lakini kwanza one at a time sasa ni zamu ya kichwa cha ufisadi, makapa mwenyewe, wananchi tukiongozwa na wabunge tumeshayavulia maji nguo, sasa ni kuyaoga tu, hata kama aliacha biilioni mia, lakini swali ni alichukua ngapi? Alichukuaje? Na ziko wapi?

Wakuu tuendele kumkomalia nyani wakati ni huu tukiwakosa this time hatuwapati tena, tuwaunge mkono wabunge kina Kimaro, walioamua kuwa hata kama shemeji anatoka kabila lao, lakini taifa mbele!
 
Kama kutakuwa na uchunguzi au mashitaka dhidi ya Mkapa hawezi kujitetea kwa kusema aliacha reserve, alijenga barabara, alijenga shule mpya au uwanja wa taifa. Itabidi ajitetee kwa kuonyesha sheria za nchi zilivyompa ruhusa kufanya kile alichofanya.


He! He! He! mweee jamani! Kwani hela za bara bara na shule ni zake kama Ndesamburo? Mbona hata mtandao wamejenga shule na bara bara?
 
Wakuu hebu acheni siasa na shule kwenye wizi wa makapa, kama Chenge amechota hela zote zile kwenye deal ya Radar, makapa alipewa ngapi? Makapa ameiba hela nyingi sana za taifa letu kupitia Miundo Mbinu, in fact kuna menngi ambayo hayajasemwa bado ya uchafu wake, kama ni msafi kwa nini asiombe kuondolewa immunity akajisafishe mahakamani?

Hivi ni lini bingwa wa kujenga hoja Mwalimu, aliwahi kujificha nyuma ya political immunity?

Mkuu ni angalizo tu, spelling za hili jina unatukwaza wengine. Anaitwa Mkapa, hakuna "a" kabla ya "k".
 
Hawa watu wanatakiwa waandaliwe makazi pale segerea mapema sana.

Mkuu K,

Maneno mazito hayo, na Mkuu Kithuku vipi mkuu huna lolote la kuongeza kuhusiana na mafisadi?, nafikiri the focus hapa iko very clear mkuu inakaribia kuundwa kamati ya bunge ya uchunguzi, umeisikia hiyo mkuu!
 
Kumbe mpaka mabalozi wa nje bongo, walienda bungeni kuwauliza wakulu wana mpango gani na ufisadi wa awamu ya tatu ndoio maana tunasikia kina Pinda wakijipinda na ishu?

Tafuta gazeti la Mwanahalisi, tarehe 23-29, Jumapili April 2008, toleo namba 094, yaani utaridhika na roho yako, maana ufisadi wote wa mkapa uko wazi na hatua ambazo zimeshachukuliwa na zitakazochukuliwa, huku wafadhili wetu wakifuatilia kwa makini, that is all we could ask kutoka kwa serikali yetu,

Mungu Ashukuriwe!
 
Back
Top Bottom