Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Ya Mkapa, David Martin na Kiwira

Johnson Mbwambo Aprili 9, 2008
Raia Mwema~Muungwana ni Kitendo

JUMATANO ya wiki iliyopita Rais Mstaafu Benjamin Mkapa (‘Bwana Msafi’) alifanya mahojiano na BBC (Network Africa) kuhusu masuala mbalimbali yanayoihusu nchi yetu.

Kwa kuwa katika kipindi chake cha urais Mkapa alishawaponda waandishi wa habari wa hapa nchini kwamba hawajui kuuliza maswali kama wafanyavyo kina Riz Khan, nilishawishika kuyasikiliza mahojiano hayo na BBC mwanzo hadi mwisho.

Nilijisogeza kwenye redio nikitarajia kwamba huyo bwana angeulizwa maswali mazito na BBC ambayo waandishi wa habari wa hapa nyumbani wasingeweza kumuuliza kwa sababu, kwa mtazamo wake yeye Mkapa, ‘hawana uwezo huo.’

Nilishangaa kwamba mahojiano hayo yalimalizika bila mama yule kumuuliza Mkapa japo swali moja tu kati ya mengi ambayo Watanzania wanasubiri kwa hamu kupata majibu kutoka kwake.

Hayo ni pamoja na skandali ya ufisadi ya EPA ambayo ilishamiri wakati yeye ni Rais na kuhusika kwake na waziri wake, Daniel Yona katika kununua kampuni ya umma ya mgodi wa makaa ya mawe ya Kiwira.

Mengine ni mauzo ya nyumba za serikali na ununuzi wa rada hususan zilikopotelea dola milioni mbili ambazo asasi ya uchunguzi wa ufisadi ya Uingereza iitwayo SFO ilidai zilipelekwa kwenye benki moja ya Uswisi kwa ajili ya rushwa kwa maofisa wa serikali yake waliohusika na ununuzi wa rada hiyo.

Nilijiuliza ni kwa nini mwandishi yule wa BBC hakumwuliza Mkapa japo swali moja tu kati ya hayo; angalau lile la ufisadi wa pesa za EPA ambalo limeziudhi hata nchi wahisani zinazochangia, kila mwaka, kiasi kikubwa cha pesa katika bajeti ya Tanzania.

Hisia zangu ni kwamba labda hilo lilikuwa ni sharti kubwa la kufanya mahojiano hayo. Kwamba mwandishi amuulize maswali yote – ya uchumi, biashara, huduma za jamii na demokrasia lakini asimuulize hayo ya tuhuma za ufisadi yanayomgusa moja kwa moja katika kipindi alichokuwa yeye rais.

Kwa hiyo, mwisho wa mahojiano, nilibaki na kiu yangu ile ile ya kutaka kumsikia Mkapa akifungua mdomo wake, kwa mara ya kwanza, kujitetea kuhusu tuhuma hizo nzito za ufisadi zinazomwandama; kiu ambayo pia naamini Watanzania wengi wanayo.

Nitaendelea kumlaumu mama huyo wa BBC kwa kutomuuliza Mkapa maswali hayo, kama ambavyo nitaendelea kumlaumu David Martin (Mungu amlaze pema peponi), kwa kutokufanya mahojiano ya pili na Mkapa baada ya kuwa amemaliza kipindi chake cha miaka kumi cha urais.

Wenye kumbukumbu nzuri watakumbuka kwamba mahojiano ya kwanza ya Mkapa mara baada ya kushinda urais, mwaka 1995, hayakuwa na mwandishi wa Tanzania; bali na Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti na Hifadhi ya Nyaraka Kusini mwa Afrika (SADRC), David Martin ambaye pia alikuwa rafiki yake wa miaka mingi.

Mahojiano hayo ya kwanza kabisa akiwa rais, yaliyofanyika Novemba 1995, yalichora picha ya Mkapa ambayo ni tofauti kabisa na picha tuliyoiona miaka 10 alipokuwa Ikulu.

Kuelewa hiki ninachotaka kukizungumza; ngoja nikukumbushe maswali mawili tu kati ya mengi aliyoulizwa na David Martin na majibu aliyoyatoa.

SWALI: Nimewasikia waandishi wa habari wakitumia maneno kadha wa kadha kukuelezea wewe. Lakini wewe mwenyewe unaweza kujieleza vipi?

JIBU: Sijui, kwa kweli sijui. Mimi ni mzalendo, mimi ni mtu wa kimataifa, mimi ni mwanademokrasia wa kijamaa, napendelea utawala safi na upanuzi wa uwajibikaji na dhamana ya majukumu ya jumuiya, kitaifa na kimataifa. Mimi ndimi.

SWALI: Hatimaye tukiangalia miaka mitano au kumi ijayo utakayokaa Ikulu, utapenda ukumbukwe vipi katika historia?

JIBU: Ningependa nikumbukwe kuwa nimeongoza serikali ambayo imepambana na rushwa na kuimarisha aina ya uongozi, utumishi wa umma, maadili na majukumu yanayojenga uongozi bora. Kwamba nimeongoza jitihada katika utawala wangu kuboresha nidhamu kwa maana ya sheria, kanuni na taratibu, lakini zinazoendana na uhuru wa msingi. Kwamba nimeendesha agenda ya vyama vingi bila madhara kwa taifa bali katika kukuza hisia za utaifa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Natumaini itajasemwa kuwa nimejitahidi kupata mafanikio hayo bila ya majivuno ambayo kwa kawaida huambatana na madaraka makuu nchini, ila kinyume, kwa uadilifu na unyenyekevu wa hali ya juu.

Hayo ndiyo majibu ya Mkapa kuhusu maswali mawili tu kati ya mengi aliyoulizwa na David Martin wiki ya kwanza tu baada ya kuwa rais. Na hapa, wala sijaweka maelezo yale muhumu aliyoyatoa kuhusu rushwa kwamba mtu anakuwa waziri (na hana mali) lakini baada ya muda mfupi wa uwaziri anakuwa na mali na majumba kadhaa kiasi cha watu kujiuliza alipata wapi pesa kipindi hicho kifupi tu?

Narudia kusema kwamba nitaendelea kumlaumu David Martin kwamba hadi mauti yalipomkuta (mwaka jana) hakupata kufanya mahojiano mengine na Mkapa baada ya kuwa amemaliza hiyo miaka 10 ya kukaa Ikulu.

Miaka 13 iliyopita, Mkapa alimwambia David Martin kwamba anataka akumbukwe kama Rais aliyepambana na rushwa. Hivi kweli kama David Martin angefanya sehemu ya pili ya mahojiano na Mkapa baada ya kuondoka Ikulu, na akamuuliza, kwa namna tofauti, maswali hayo hayo aliyomuuliza miaka 10 iliyopita, angejibu nini kuhusu rushwa na ufisadi?

Baada ya mahojiano hayo na David Martin, Novemba 1995, Mkapa alikwenda mbali zaidi na kutangaza mali zake; lakini miaka 10 baadaye wakati anaondoka Ikulu akagoma kutangaza tena mali zake licha ya shinikizo la vyombo vya habari la kumtaka afanye hivyo.

Hebu fikiria. Alipoingia Ikulu alitangaza, kwa hiari yake mwenyewe, mali alizokuwanazo; lakini wakati wa kuondoka, miaka kumi baadaye, akagoma kufanya hivyo licha ya shinikizo la vyombo vya habari. Kwa nini agome? Jibu linaeleweka.

Miaka 13 iliyopita alimwambia David Martin kwamba angependa akumbukwe kama Rais aliyeongoza serikali iliyopambana na rushwa. Ni rushwa ipi aliyopambana nayo wakati yeye mwenyewe na waziri wake Daniel Yona, walijiuzia kampuni ya umma ya Kiwira Coal Mines Limited kwa bei poa ya Sh. milioni 700 wakati thamani halisi ya mgodi huo ilikuwa Sh. bilioni 4 ? (Kulikoni – Aprili 2, 2008).

Rushwa ipi aliyopambana nayo wakati ufisadi uliendelea kila kona katika serikali yake ukiwemo huo wa mwisho mwisho wa EPA ambao ni wa aina yake katika historia ya Tanzania?

Ninachojaribu kueleza hapa ni kwamba picha ile ya Mkapa tuliyochorewa na David Martin mwaka 1995 si picha ya Mkapa tuliyemwona baadaye Ikulu.

Alitaka akumbukwe kama kiongozi aliyepambana na rushwa; lakini picha tuliyoiona ni ya Rais aliyeutamani utajiri wa haraka haraka kiasi cha kufanya biashara angali bado Ikulu; huku akinunua shirika la umma kwa bei poa.

Na naambiwa alikuwa pia akikimezea mate kiwanda cha sukari cha Mtibwa na mashamba yake makubwa ya miwa!

Kwa ufupi, ujumbe wangu ni kwamba wanasiasa hubadilika wakishaingia Ikulu; hivyo si jambo jema hata kidogo kuendelea na katiba ya nchi inayompa rais mstaafu kinga ya kushitakiwa kwa makosa aliyoyafanya akiwa madarakani.

Kinga ile ya kikatiba inakuwa na maana ukiwa na rais mwadilifu wa aina ya Mwalimu Nyerere, lakini nusu karne inaweza ikapita bila kumpata kiongozi mwingine wa aina ya Nyerere.

Kinga hiyo ya kikatiba haina maana hata kidogo unapokuwa na marais wa sampuli ya Mkapa wanaofanya biashara na mashirika ya umma wakishaingia Ikulu, na wakitoka Ikulu baada ya kumaliza muda wao bado wanaendelea kulipwa marupurupu yote ya Rais mstaafu!

Nionavyo; tukiliacha suala hili la kinga ya kushitakiwa ya rais mstaafu kuendelea kuwa open ended, tunaweza siku moja tukampata rais mwizi kupindukia wa aina ya Sani Abacha, na bado akimaliza kipindi chake cha urais tukashindwa kumfikisha mahakamani kwa kuwa tu ana kinga ya kikatiba.

Wakati umefika kwa Watanzania kuanza kulijadili suala hili. Wakati umefika kwa wabunge wetu kuliangalia hili; na ikibidi atokee jasiri mmoja awasilishe hoja binafsi bungeni juu ya suala hili ili mwishowe kinga ya rais mstaafu isiachwe open ended; hasa inapokuja kwenye kuhusishwa na ufisadi.

Ni lazima kinga hiyo iwe na mipaka kwa kuweka mazingira fulani fulani yanayoweza kuifanya kinga hiyo kuvuliwa ili kulinda fedha na mali za umma dhidi ya marais wa aina ya Abacha tunaoweza kuwachagua.

Tunaweza kumpigia kura mwanasiasa anayeonekana mwadilifu kweli kweli; lakini mwaka mmoja tu akiwa Ikulu akaanza kupora huku na kule kwa sababu tu anajua ana kinga ya kikatiba ya kutokushitakiwa.

Maana, kama nilivyosema mwanzo, wanasiasa hubadilika wanapoingia Ikulu. Na mfano mzuri ni Mkapa. Mkapa yule aliyehojiwa na David Martin Novemba 1995, si yule aliyetoka Ikulu miaka 10 baadaye.

Tafakari.

Email: mbwambojohnson@yahoo.com
 
Nimefurahishwa na makala hii 'Mkapa David Martin na Kiwira'.Zaidi ya alichosema, wanazuoni wa sheria wanadai kinga ya kumshtaki rais ni kwa mambo ya kikazi, kwa hiyo Mkapa hawezi kushtakiwa kwa mauaji ya Januari 27 Zanzibar kwa sababu aliua kama rais, lakini anaweza kushtakiwa kwa kukwapua Kiwira kwa sababu aliikwapua sio kama rais bali kama Ben Mkapa.

Tafakari.
 
Kazi Ipo Na Ukweli Utakuja Kujianika Hadharani...mimi Nasubiriaa Shinikizoo..la Kimataifa Ili Epa Na Kiwira,richmond Na Mengineyo Yafanyiwe Kazi Wambane Huyo Jk Hakuna Pesa,hadi Uwajibishe Hao Marafiki Zako....waliokuweka Hapo Ulipo...el,ra Nani Hajui?
 
I have tried hard during my term of office to engender, by my conduct, a better public perception of politicians. We have to be more truthful and people of integrity.

The story is told of an older couple with a son who was still living with his parents. The parents were a little worried, as the son was still unable to decide about his future career. They decided to do a small test. They took a ten-thousandshilling note, a Bible, and a bottle of whisky, and put them on the front-hall table, and hid, retending they were not home.

The father’s plan was: ‘If our son takes the money, he will be a businessman, if he takes the Bible, he will be a priest, but if he takes the bottle of whisky, I’m afraid our son will be a drunkard’. So the parents waited nervously, hiding in the nearby closet.

Peeping through the keyhole, they saw their son arrive. The son saw the ten-thousand-shilling note they had left. He took it, looked at it against the light to be sure it was genuine, and slid it in[to] his pocket. After that, he took the Bible, flicked through it, and took it. Then he grabbed the bottle, opened it, and took a whiff to get assured of the quality. Then he left for his room, carrying all three items.

The father slapped his forehead and said: ‘Darn. Our son is going to be a politician’! This is the kind of reputation I would not want Tanzanian politicians to be defamed with.
Mkapa 2005, Boston, USA.


Hivi si ndiyo alivyotuachia akina Lowassa, Chenge etc.?
 
Rais mtaafu Mkapa, mkewe waumbuliwa bungeni kwa mgodi wa Kiwira
Na Muhibu Said, Dodoma

MBUNGE wa Vunjo, Aloyce Kimaro (CCM), amewatuhumu Rais Mstaafu, Benjamin Mkapa, mkewe Mama Anna Mkapa na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Daniel Yona, kuwa walinunua mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira, wilayani Rungwe, Mbeya kwa kificho.

Mbunge huyo alidai bungeni jana kuwa mwaka 2004, Mkapa kwa kushirikiana na mkewe pamoja na Yona, walianzisha Kampuni ya TanPower Resources Ltd na mwaka mmoja baadaye wakauziwa machimbo ya Kiwira kimya kimya.

Kimaro alitoa madai hayo alipokuwa akichangia Muswada wa Sheria ya Umeme wa Mwaka 2008, bungeni, mjini hapa juzi jioni.

Alidai kuwa katika mauziano hayo ya siri, Kampuni ya TanPower Resources Limited,

ilikuwa iilipe serikali Sh700milioni katika mradi huo uliogharimu, zaidi ya Sh4bilioni, lakini kampuni hiyo ilifanya malipo ya awali ya Sh70milioni tu.

"Waliuziwa kwa Sh700milioni bila kutangazwa na wao wakalipa down payment (malipo ya awali) Sh70 milioni," alisema Kimaro.

Aliendelea kudai kuwa mwaka 2006, Mkapa, Anna na Yona, waliingia mkataba na Shirika la

Umeme nchini (Tanesco) kwa ajili ya kufua umeme kwa makubaliano ya kulipwa Gharama za uwekezaji ('capacity charge') Sh146 milioni kila siku, bila kujali kwamba wamefua umeme au la.

"Sasa mimi nauliza huu ni uadilifu kweli? Haya ni maadili kweli? Tufike mahala tuseme inatosha. Hivi tunawafundisha nini vijana hawa ambao ni mawaziri?," alihoji

Kimaro na kuongeza:

"Rais Jakaya Kikwete alisema urais wake hauna ubia na mtu. Basi aseme huu ni mwisho kwa wanaotuhujumu, tuwaambie basi na washughulikiwe kwa mujibu wa sheria."

Awali, akichangia muswada huo, Kimaro alisema ipo haja ya kuwa makini katika kuupitisha muswada huo kwa kuwa wawekezaji watakaokuja kuwekeza katika umeme, si rahisi kwenda vijijini kusambaza nishati hiyo.

Kutokana na hali hiyo, aliitaka serikali kuifufua Tanesco kwa kuipa fedha ili (serikali) iwe na chombo chake cha kuzalisha umeme.

Naye Mbunge wa Mpanda Kati (Chadema), Said Amour Arfi, alishangazwa namna serikali inavyotumia nguvu nyingi kuupitisha muswada huo.

Alisema haafiki kupitishwa kwa muswada huo na kuongeza kuwa nguvu inayotumika kuharakisha kupitishwa muswada huo si ya kawaida.

Alisema hoja ya kuwa muswada huo ukipita, wananchi wa vijijini watapata umeme wa bei rahisi, haina nguvu.

Alitoa mfano wa Kampuni ya Artumas ambayo baadhi ya wabunge waliipigia debe, kwamba haitaweza kuondoa matatizo ya umeme.

"Tanesco itaingiaje katika ushindani wakati ikiwa hoi? Tanesco inavishwa majukumu ya kisiasa," alisema na kuonya kwamba wawekezaji watakaokuja si ajabu wakafanana na hadithi ya ubinafsishwaji wa Benki ya NMB.

Alikumbusha kuwa wakati NMB inabinafsishwa, ilisemwa kuwa itakuwa benki ya wananchi na itawafikia watu wengi, lakini leo hii ukitaka kufungua tawi vijijini wana vigezo vyao na si jambo rahisi kufika huko.

"Na hao (wawekezaji) wakija, wataweka vigezo vyao vya kusambaza umeme vijijini ambavyo havitawawezesha wananchi wa huko kunufaika na huduma hiyo," alibainisha.

Naye Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela alimwangaliza Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja, kutambua aina ya wawekezaji wanaotarajiwa kuwekeza katika sekta ya umeme baada ya sheria mpya ya sekta hiyo kupitishwa, kwani ndiyo watakaomwangusha ama kumwinua.

"Nakupa angalizo Mheshimiwa Waziri, ujue kuwa aina ya wawekezaji watakaoingia katika sekta ya nishati ndiyo watakaokuangusha au kukuinua, wapo Watanzania wenzetu wanajiandaa kuingia katika biashara hiyo, wengine ni wale walionufaika na mikataba mibovu kama ule wa Richmond," alitahadharisha Mbunge huyo.

Alidai kuwa baadhi ya Watanzania, hususani walionufaika na mikataba inayolitia hasara Tanesco, wameanza kujiandaa kuwekeza kwenye sekta hiyo.

Alisema kuwa, kimsingi ni muhimu kwa serikali kuhakikisha kuwa Tanesco inakuwa imara katika kipindi hiki cha ushindani, ambacho kinahitaji nguvu zaidi kwa shirika hilo la umeme ili kukabiliana na ushindani utakaotokana na kupitishwa kwa sheria hiyo.

Aliangaliza kuwa serikali inatakiwa kutambua kuwa Mtanzania wa leo anaitambua nchi yake na hivyo kuna umuhimu mkubwa kuwa na ufahamu kwamba mageuzi ya kiuchumi ni muhimu na sharti yajengwe palipo na mfumo imara wa usambazaji wa umeme.

Kwa upande wake Mbunge wa Moshi Mjini (Chadaema), Philemon Ndesamburo ambaye mbali ya kuunga mkono hoja hiyo alishauri kuwa umeme usiwe kitu cha anasa na badala yake kiweze kupatikana kwa kila mtu anayekihitaji.

Mbunge huyo wa Moshi Mjini alishauri kuwa pamoja na umuhimu wa serikali kuingia katika mfumo huo mpya, jambo muhimu ni kuhakikisha kuwa maeneo ya mipakani yakatumia fursa ya kuwepo umeme kutoka nchi jirani.
 
Wasi wasi ni kama atapona ndani ya CCM.Nadhani karibi sasa spika ataanza kusema kabla ya kuongea Bungeni ukaseme ofisini then urudie maneno yale yale wakati wa kuchangia .

Mimi yangu macho wacha nione mwelekeo .Huyu Mbunge kaleta balaa huenda asifike mwisho wa mwaka huyu .
 
Hili ni zimwi hata wakilificha vipi litatoka na kuonekana kwa wananchi, huyu mbunge nafikiri Spika ameshamuita kwa sasa na kumwambia hana ruhusa ya kuongea mpaka aongelee ofisini kwakwe kwanza. Wakati utafika watajikuta hawawezi kulificha hili zimwi tena.
 
laana kubwa iliyo wakumba wana CCM akiwemo Chenge ni kwenda Butiana na kuzuru kaburi la Mwalimu wakiajiamini kwamba kafa hana madhara kwao tena .They made a huge mistake na madhara ni haya .Nakwambia huu ni Mwanzo tu .Mengi utayasikia .
 
Kikwete nilikuandikia hii barua hapo chini, sijui ulipata muda wakuipiti, kama hukupata muda , basi si vibaya ukiirudia tena

Pole sana na safari na karibu tena hapa nyumbani, ningependa pia kukupa hali halisi ya hewa ya hapa nyumbani (nikiamini kabisa wapambe wako hawawezi kukupa ukweli halisa maana bado they will simply tell you what you like to hear na pia bado wako juu hawajui hali halisi ya huku chini), moto bado ni mkali, ndo kwaaanza umeanza upya, hali ni mbaya na ni ngumu

Pongezi sana kwa kusoma alama za nyakati kwa kusikiliza watakacho wananchi kwa kutaka Chenge Cents kuitikia watakacho wananchi, nyoosha mkono sasa na kuruhusu achukuliwe hatuna pamoja na wale wote waliohusika katika sakata hili (Unawajua vizuri sana) Jopo uonekane uko serious kidogo

Jambo kuu lililonifanya nikuandikie waraka huu ni kukutahadharisha na kukuamsha kuwa KWANINI UMENYAMAZE MAOVU YA MWIZIO… ooops Sorry MWENZIO BENJAMIN WILLIAM MKAPA??
Hivi ni kweli toka moyoni mwako huoni kama huyu jamaa anakuchafulia?? Hivi huoni kama machafu yote haya ni ya enzi yake naye anahusuka moja kwa moja??


Binafsi nakuonea huruma sana maana hiyo energy unayotumia kumprotect Mkapa, badala ya kukusaidia kujiprotect mwenyewe, mwenzako kule anapeta wakati wewe unaungua, kwanini ubebe mzigo wa mwenzio?? Kwanini nawe usimwage mboga tu mzee???

Hebu njoo mbele yetu, ungama kwa makosa uliofanya (I promise you waTZ watakuwa nyuma yako na watakupa nafasi nyingine), pangua kila kitu, achia vyombo vya sheria vifanye kazi yake(na kabla havijaanza kazi kwamza kabisa mtoe, Hosea na Mwanyika maana sisi wapigakura hatuwaamini) Muweke jamaa (MKAPA) hadharani, mwite mbele yetu aje kujibu maswali, mbona Zambia iliwezekana???

Chukua nafasi ya pekee kumchunguza Mkullo nauone kama anafaakuwepo hapo alipo, nakuapi ahii niaibu nyingine juu yako inakuja, tumia wakati huu wakumteua atakayeziba nafasi ya Cents kumtoa huyu jamaa Mkullo nauweke mwingine ALIE SAFI,

Kwa leo naishia hapa, nasubiri kuona mwitikio wako juu ya waraka wangu kwako

NIKUTAKIAE MEMA
MWANAJAMBOFORUMS.
 
Congratulations Mbunge wa CCM, Mkapa is a next victim simuoni kumaliza huu mwaka bila kuumbuliwa, let us wait and see.

Ila ninajiuliza usalama wa huyu Mbunge masikini, tumsaidieje jamani? Hawa mafisadi wa CCM watamuacha hivi hivi? Mungu amrinde AMEN
 
Congratulations Mbunge wa CCM, Mkapa is a next victim simuoni kumaliza huu mwaka bila kuumbuliwa, let us wait and see.

Ila ninajiuliza usalama wa huyu Mbunge masikini, tumsaidieje jamani? Hawa mafisadi wa CCM watamuacha hivi hivi? Mungu amrinde AMEN

Hawawezi kumuacha maana amesaidia mkapa ameingia kwenye ansadi kuwa ni mwizi wa mali za umma, sasa hivi nafikiri wako nyumbani kwakwe wanamkomesha, lakini time will tell mkapa ameiba sana hawezi kupita hivihivi wataizima hiyo lakini itatoka tena.
 
Congratulations Mbunge wa CCM, Mkapa is a next victim simuoni kumaliza huu mwaka bila kuumbuliwa, let us wait and see.

Ila ninajiuliza usalama wa huyu Mbunge masikini, tumsaidieje jamani? Hawa mafisadi wa CCM watamuacha hivi hivi? Mungu amrinde AMEN

Aaa wapi hawana ubavu wakuua mtu hawa maji yameshawafika shingoni, labda tuu nawasi na usalama wa JK nasikia ameshapokea na vitisha bwana

Tayari Kikwete anaelezwa kupokea maelezo, ushauri, lawama na hata vitisho baada ya kuibuka kwa tuhuma na uchunguzi wa masuala yote yanayohusishwa na ufisadi ambayo yameibuka mfululizo na yakaitikisa Serikali yake
http://www.raiamwema.co.tz/08/04/16/1.php
 
ni vizuri kuona kwamba hawa wabunge wengine wa CCM na upinzani wanatanguliza uzalendo mbele ya maslahi yao binafsi, lazima wapewe majibu ili wakawajibike wa wananchi wao. Wengi ndani ya CCM wamechukizwa sana na mambo yalivyoenda hasa kwenye uongozi wa chama. tuwasaidie hawa rogue wabunge kuanika mengine mengi bungeni wananchi wawajue wahusika.
 
ni vizuri kuona kwamba hawa wabunge wengine wa CCM na upinzani wanatanguliza uzalendo mbele ya maslahi yao binafsi, lazima wapewe majibu ili wakawajibike wa wananchi wao. Wengi ndani ya CCM wamechukizwa sana na mambo yalivyoenda hasa kwenye uongozi wa chama. tuwasaidie hawa rogue wabunge kuanika mengine mengi bungeni wananchi wawajue wahusika.

Hilo ndo bunge linalotakiwa kwa Tanzania, tunapoongelea masirahi ya nchi wasigawanyike na kuwa na vyama, CCM wanawaziba sana midomo wabunge wao.
 
Jamani Bunge sindilo lenye mamlaka ya kutunga sheria, Kwanini wasipige kuondoa immunity ya Mkapa from prosecution...
 
hamjajiuliza imekuwaje Kimaro anaibuka kuwa shujaa... mapambano ya fikra yanazidi kushinda taratibu.....
 
Kalipa 70 millioni tu, anangoja malipo yake ya shilingi 146 millioni kwa siku toka TANESCO ili amalizie deni lake! Fisadi mkubwa. JK rudisha Kiwira chini ya umiliki wa serikali haraka iwezekanavyo na huo mkataba wa mafisadi Mkapa na Yona uubatilishe.
 
penye ukweli panakuja wala msiwe na wasiwasi, wazalendo tutarudishiwa kila kilichoporwa...
 
Back
Top Bottom