Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Hivi mpaka sasa mbona Sumaye naona yuko clean? Magazeti yalikuwa yanamuonea Sumaye bure nini? Ni karibu miaka miwili naona hakuna mambo ya Sumaye yanayoandikwa au ni kweli huko nyuma Mtandao ndio walikuwa wanampaka matope?
 
Duh!
Kwa mtaji huu Tanesco itakufa kama walivyoiuwa TIPER.

Sasa naanza kupata mawazo Inawezekana BM hakuishia kwenye KIWIRA COAL power Project. Kwenye makampuni ya madini(Bariki na mengineo) ANBEM Ltd inaweza kuwepo, hii 97%ya mwekezaji kwenye madini bado haiingii akilini.
 
Siamini kama JK atatoa tamko lingine kumtetea Ben

Atakuwa punguani akifanya hivyo maana kashfa tulizozijua tangu yuko madarakani mpaka hizi ambazo pamoja na kuwa alizifanya akiwa madarakani ndiyo kwanza zinazoibuka kila siku kama uyoga. Atamtetea kwa ushahidi gani aliokuwa nao, haitoshi tu kusema mwacheni mzee wetu astaafu kwa amani!!! je mwenyewe yuko wapi kujitetea!? Ama ndio katudharau Watanzania kwa kujua hakuna lolote atakalofanywa maana wote wanajuana kashfa zao!!!
 
Duh!
Kwa mtaji huu Tanesco itakufa kama walivyoiuwa TIPER.

Sasa naanza kupata mawazo Inawezekana BM hakuishia kwenye KIWIRA COAL power Project. Kwenye makampuni ya madini(Bariki na mengineo) ANBEM Ltd inaweza kuwepo, hii 97%ya mwekezaji kwenye madini bado haiingii akilini.

Nakubalina nawewe kabisa inabidi mikataba yote ya huyu mzee alipokuwa serekalini ipitiwe,maana share ni za wao kwa wao tu.
Hasa hasa huko kwenye madini ambako Yona alimpigia pAsi Senkoro
 
Kuna mawazo mengi ya msingi yametolewa hapa. Shukrani kwa waliyoyatoa. Viko vipengele vingine vinahusu hii ishu ambavyo bado havijatajwa.

Umeme wa mafuta ni ghali sana. Kwetu sisi tusio na mafuta, umeme huo hautufai hata kidogo.

Tuna hydroelectric potential kubwa, gesi na mkaa wa mawe. Hatuna sababu ya kutegemea umeme wa mafuta. Unatumalizia forex, na unachangia sana kuyumbisha dhamani ya shilingi yetu.

We have not exhausted our hydroelectric potential. Tutafute wawekezaji (sio lazima watoke nje) wa upande huo. Wajue kabisa Watanzania wenye mitaji (kama wenye NICO) kwamba unaweza kujenga bwawa ukauza umeme. Ikibidi tutalazimisha TANESCO wanunue huo umeme wako.

Ni vizuri kwamba tunazalisha umeme wa gesi, lakini tulikosea sana pale tulipokubali kupewa ruzuku badala ya kuwa wamiliki washiriki. Kama atatokea Mtanzania mwenye fedha nyingi (wapo, na mikopo ipo) akainunua kabisa SONGAS tungeshangilia sana. Kwa sasa, inatugharimu FOREX nyingi kuzalisha huu umeme wa gesi, kwani SONGAS wanahamishia fedha zao nje. Wakina Mkapa, Mengi, etc, tunaomba mtafute mbinu ya kununua hiyo kampuni iwe ya Watanzania. Tutawashangilieni.

Kama Umeme wa Kiwira ni wa Wamakonde na Wapare, basi tutaupata bila kutumia forex nyingi. Hiyo ni AHUENI kubwa. Ni sababu ya kufurahi, si ya kulalamika.

Wako Watanzani wenye mtaji wa kutuwezesha kupunguza kasi ya utumiaji wetu wa FOREX kwenye nishati. Tukipata ushahidi kwamba fedha walizo nazo ni za wizi, basi tutaujadili. Kabla ya hapo, tuwapongeze.

Tumezoea mno kuona biashara ya Mtanzania ni ya baa ya kuuza sanduku nne na kuku sita, au daladala mbili na lori moja. Akitokea anayefanya uwekezaji wa kikweli, asitukoseshe raha. Si lazima awe ameiba. Mbona wanapokuja wageni kuwekeza hatusemi wameiba?

Kuhusu Mwalimu kutokuwa na fedha, naomba niseme hivi: Mwalimu alipunguza hata mshahara wake. Kuna watu hawapendi fedha, period. Sasa sio lazima kila mtu awe kama Mwalimu. Rais ambaye anahudumiwa kila kitu na serikali kwa nini asiwe na savings? Lazima awe na savings za mamilioni mengi tu. Kwa vingine ni mpuuzi. Msisahau hawa watu wana marupurupu mengi sana. Badala ya kulalia hayo mapesa ni vema hawa wastaafu wanunue makampuni wazalishe mali na kuinua uchumi wetu.

Augustine Moshi
 
Naomba kuuliza...

Maoni yenu ni nini sasa? Ndio hivyo mambo yanafunuka one after the other, about BM and practically speaking, all those who at any one point wameshika madaraka in Afrika. BM, hayupo peke yake na hatakuwa wa mwisho. Kama common mwananchi nauliza, tutafika kweli?[/FONT]
 
Waungwana, ili kuwa na mtiririko mzuri wa uchangiaji nashauri hii thread iunganishwe na ile ya "KIWIRA COAL POWER PROJECT: ANBEM ..."
 
Augustine Moshi
Mwalimu alipunguza hata mshahara wake. Kuna watu hawapendi fedha, period. Sasa sio lazima kila mtu awe kama Mwalimu. Rais ambaye anahudumiwa kila kitu na serikali kwa nini asiwe na savings? Lazima awe na savings za mamilioni mengi tu. Kwa vingine ni mpuuzi. Msisahau hawa watu wana marupurupu mengi sana. Badala ya kulalia hayo mapesa ni vema hawa wastaafu wanunue makampuni wazalishe mali na kuinua uchumi wetu.

Awali nilishasema ndugu yetu AM bora usimtetee maana unavyotetea unazidi kumtia katika kitanzi. Unaposema kuna watu hawapendi pesa kama Mwalimu, kwa hiyo una maana Mkapa alipenda pesa sana? Kwanini aliingia katika siasa kama alipenda pesa, siasa si mahali pa kupata pesa (japo imekua kinyume kwa sasa). Unaposema wasipokusanya mapesa ni wapuuzi, hapo unamtukana Mwalimu JKN na hapo humsaidii Mkapa.

Lakini AM umeanza kwa kuingiza suala la uzawa kama alivyofanya Mkono katika kutetea biashara yake ya Bank M. Kwa kweli hakuna ubishi kwamba Watanzania tunahutaji wawekezaji Wazalendo kama Mkapa, Mengi, Mkono, Massawe (wote hao ni MMMMMMM) lakini, ndugu yangu hoja hapa si uwekezaji, hoja hapa ni RAIS BENJAMIN MKAPA, akiwa Rais na mkewe, ameanzisha Kampuni inaitwa ANBEM, akamfundisha mwanae Nicholas, naye na mkewe (FOSTER)wakaanzisha kampuni ikaitwa FOSNICK na tena akamhusisha na rafiki yake Waziri wa Nishati na MAdini, Daniel Yona, am baye naye na familia yeke wakawa na kampuni ambayo hapo sasa ikapewa mradi wa Kiwira. Hapo hujaona tu tatizo? Tatizo si wawekezaji WAZALENDO, tunawataka sana. lakini SIASA na BIASHARA vina walakini.. TUTAJUTA SANA BAADAYE
 
...mr clean kumbe ana deal chafu kiasi hicho,lakini hizi tamaa mbaya sana...huyo Yona ni rushwa tupu na hii kama kweli hawa kina JK na tume yake ya rushwa na kelele zao za kupigia rushwa kelele lazima hii waichunguze na kama kuna foul imechezwa lazima wafikishwe mahakamani la sivyo tutaendelea kuwa maskini,hawa lazima wawe mifano ya kudhibiti rushwa na wizi
 
kwa kweli hawa watu ni wezi sana na inabidi wachunguzwe na kama kuna uhalifu umefanyika wafikishwe mahakamani,maana kila kitu ni kasfa tupu kuanzia mikataba ya madini,Presidential jet,fake radar,BOT building,huu umeme wa kiwira/IPTL/Richmond yaani ni balaa tupu na ukiangalia vizuri cost ya hizo deals zote lazima nchi izame lakini hao waungwana wala hawashtuki na sasa ndio mjue mliempa nchi (CCM) ni majizi tuu na wala hayajali chochote kuhusu ile nchi...sijawahi kuona upuuzi kama wa kununulia wabunge wote landcruisers za million 100...kama wanataka magari si wakakope Bank kama wengine kwanini serikali inajiingiza kwenye biashara ya kukopa watu magari...only in Tanzania!
 
It is corruption pure and simple. Asingekuwa Ikulu angeweza kumshinikiza nani ndani ya TANESCO wasaini mkataba na hizo kampuni zao feki?
 
Kuna habari kwamba jalada la kampuni ya TANPOWER halionekani kwa Msajili wa Makampuni (BRELA)... Kwa kawaida jalada likipotea linapoonekana huwa na mabadiliko fulani... Hawa jamaa wa THISDAY na wengine wanaofuatilia sakata hili lazima wawe waangalifu sana.

Hayo ni maneno yaliyosikika yakisemwa na ofisa mwandamizi wa SIRIKALI
 
Kuna mawazo mengi ya msingi yametolewa hapa. Shukrani kwa waliyoyatoa. Viko vipengele vingine vinahusu hii ishu ambavyo bado havijatajwa.

Umeme wa mafuta ni ghali sana. Kwetu sisi tusio na mafuta, umeme huo hautufai hata kidogo.

Tuna hydroelectric potential kubwa, gesi na mkaa wa mawe. Hatuna sababu ya kutegemea umeme wa mafuta. Unatumalizia forex, na unachangia sana kuyumbisha dhamani ya shilingi yetu.

We have not exhausted our hydroelectric potential. Tutafute wawekezaji (sio lazima watoke nje) wa upande huo. Wajue kabisa Watanzania wenye mitaji (kama wenye NICO) kwamba unaweza kujenga bwawa ukauza umeme. Ikibidi tutalazimisha TANESCO wanunue huo umeme wako.

Ni vizuri kwamba tunazalisha umeme wa gesi, lakini tulikosea sana pale tulipokubali kupewa ruzuku badala ya kuwa wamiliki washiriki. Kama atatokea Mtanzania mwenye fedha nyingi (wapo, na mikopo ipo) akainunua kabisa SONGAS tungeshangilia sana. Kwa sasa, inatugharimu FOREX nyingi kuzalisha huu umeme wa gesi, kwani SONGAS wanahamishia fedha zao nje. Wakina Mkapa, Mengi, etc, tunaomba mtafute mbinu ya kununua hiyo kampuni iwe ya Watanzania. Tutawashangilieni.

Kama Umeme wa Kiwira ni wa Wamakonde na Wapare, basi tutaupata bila kutumia forex nyingi. Hiyo ni AHUENI kubwa. Ni sababu ya kufurahi, si ya kulalamika.

Wako Watanzani wenye mtaji wa kutuwezesha kupunguza kasi ya utumiaji wetu wa FOREX kwenye nishati. Tukipata ushahidi kwamba fedha walizo nazo ni za wizi, basi tutaujadili. Kabla ya hapo, tuwapongeze.

Tumezoea mno kuona biashara ya Mtanzania ni ya baa ya kuuza sanduku nne na kuku sita, au daladala mbili na lori moja. Akitokea anayefanya uwekezaji wa kikweli, asitukoseshe raha. Si lazima awe ameiba. Mbona wanapokuja wageni kuwekeza hatusemi wameiba?

Kuhusu Mwalimu kutokuwa na fedha, naomba niseme hivi: Mwalimu alipunguza hata mshahara wake. Kuna watu hawapendi fedha, period. Sasa sio lazima kila mtu awe kama Mwalimu. Rais ambaye anahudumiwa kila kitu na serikali kwa nini asiwe na savings? Lazima awe na savings za mamilioni mengi tu. Kwa vingine ni mpuuzi. Msisahau hawa watu wana marupurupu mengi sana. Badala ya kulalia hayo mapesa ni vema hawa wastaafu wanunue makampuni wazalishe mali na kuinua uchumi wetu.

Augustine Moshi

Ndugu yangu AM
Kuna key issue ambazo ziko wazi, moja ni mgongano wa ki-maslahi.
Inakuwa kama kesi ya nyani umpeleke tumbili.
Au let me put it like this u r the prosecuter na Judge at the same time. Sasa hapo haki itakuwepo?
Tumia akili yako ya kawaida tu sio ya kwenda Shule.
Pili ukitumia ya kwenda shule, sasa bahati mbaya sijui fani yako, lakini kila fani inataratibu zake ili ku-uphold high standard za utendaji kazi na kuweka heshima ya hiyo Profession.
Na hata ukiwa mfanya biashara yule ambaye hakwenda shule, anajua the basic principle ya Biashara ni kuweka undugu ktk biashara inaweza kuwa moja, nyingine ni kukopesha bila kuji-shield na uwezekano wa kutolipwa, au ule utaratibu wa kumjua mtea wako.
So hata ukienda Bar ya mtu yoyote, unless u r are regular customer, ndio anaweza kukukopesha kwa dharura au atakwambia acha saa yako au simu.
Tukirudi kwa Kaka Ben etc kuna issue ya kuwa kiongozi unapitisha sera na maamuzi kwa faida ya watu sio ya kwako.
Kampuni unajiuzia mwenyewe, then tarriffs una set mwenyewe, kweli kutakuwa na haki kwa wengine?
Tatu nitakupa mifano ya Hotel zetu za kitalii zilivyo kufa sababu hiii hiii ya wa conflict of interest, Hotel ina stock nzuri tu ya kuku, lakini kwa sababu waziri au mjumbe wa Board au ndugu au rafiki, ana kuku wameisha kuwa na hawezi kuendelea kubeba cost ya kuwalisha , anaiuzia hii hotel, matokeo yake wanakaa saana kwenye fridge, then kinakuwa chakula cha staff kabla hawajaharibika, hasra kwa hotel, matokeo yake hao hao wajomba zetu, dada zetu na kaka zetu ambao walikuwa wana kazi kwenye hizo hotel wakawa hawana kazi.
so ukiwa mtu mzima na akili zako timamu usifurahie furaha ya dakika tatu wakati mbele ni mauti.
wasio na kazi ambao huko nyuma walikuwa na kazi ni wengi, angalia kwenye textile mill , NMC, Ugawaji , TWICO etc. mifano ni kingi na wewe mwenyewe unaijua.
Usiwe na ile sera ya mkuki kwa nguruwe ni sawa kwa binadamu ni mchungu. Hope umenielewa.

wa
 
Jasusi, ina maana nzito sana, ila nadhani tutajua siku si nyingi... Kuna uwezekano mkubwa wa kufanyika kwa mchezo mchafu.. Kama una mtu pale BRELA wasiliana nao, uangalia je, majalada ya Makampuni yaliyotajwa na THISDAY kwa sasa yapo? kama hayapo yako wapi? maana aliyezungumza hayo alisema:

"Hawa THISDAY wamepata wapai hayo majalada maana kule BRELA hayapo! Lakini kila walichoandika ni kweli kwa asilimia 99.99 lakini watu wamechanganyikiwa wamepataje ukweli huo?"

HILI SI SUALA DOGO HATA KIDOGO maana Mzee wa watu (BEN) amekaliwa pabaya. Je,yeye anajiandaa kwa mbinu gani kujihami? Tunaambiwa pale BRELA kuna mtoto wa ndugu yake anayeitwa Andrew Mkapa, ambaye ni Assistant Register, lakini Andrew amekua akitajwa kama mtu anayefanya kazi yake kwa uadilifu wa hali ya juu na hata mara moja hajawahi wala hatawahi kumtetea Ben, na sababu kubwa ni kwamba kila mtu akiona jina la Mkapa ataamini kwamba atamtetea, na ndio maana anajitahidi asiharibu taaluma yake, kwani mwenzake amekula vyake na ameng'atuka yeye bado kijana na ana uwezo mkubwa wa kufanikiwa. Andrew anaelezwa kuwa ndiye nguzo kuu ya BRELA katika uchapaji kazi. Sasa swali linakuja ni nani atakayemlinda Ben ikiwa mtoto wa ndugu yake anajali taaluma?
 
Halisi said:
Huu ni mfano hai wa jinsi serikali ya JK ilivyokua haijajiandaa kutawala na kujikuta inakamilisha na kutekeleza mambo yaliyokwisha kamilishwa na Ben. Mchakato wa Kiwira ulianza kipindi cha mwisho cha Ben na Baraza la Mawaziri chini ya Ben (japo JK na EL walikuwamo)na kwamba mbali ya THISDAY kuandika, kuna taarifa kwamba katika hali ya kushangaza Kaburu wa NET GROUP alikataa kusaini hadi akagombana na Msabaha na TANESCO wallilazimishwa kusaini. Kaburu huyo anaelezwa alianza kuwageuka waliomleta Tanzania hata katika kukataa kuagiza vifaa toka Afrika Kusini ambavyo vinaweza kupatikana Tanzania. Mwezi Machi ni kipindi ambacho bado WANAMTANDAO walikua wamelewa USHINDI WA KISHINDO na kwamba baadhi walijipa likizo baada ya kazi mpya na wengine walikua wakijipanga kushika nyadhifa mbalimbali na kupeana ulaji. Hapo ndipo wenye kujua michezo waliitumia nafasi hiyo na kuchangamkia zabuni hiyo.

Halisi,
sijaridhika na haya majibu yako. msabaha alikuwa naibu waziri wakati wa serikali ya mkapa. lau masha alikuwa ni mwanasheria na ame-deal kwa muda mrefu na makampuni ya madini. hayo naamini ni maandalizi tosha kabisa kuongoza wizara ya madini na nishati.

ni katibu mkuu wa wizara peke yake ndiye unaweza ukasema he was new to the job. makamishna wote na wakurugenzi naamini walikuwa hawajabadilishwa.

vilevile umeeleza kwamba Tanesco walikuwa forced. mimi napenda kuelewa walikuwa forced na nani? kwa uchache, kwa uelewa wangu, mwenye uwezo wa kuwa-force Tanesco kufanya atakavyo ni Raisi,Waziri Mkuu,Waziri au Katibu Mkuu wa Nishati na Madini.

1.FEDHA ZA KU-FINANCE HUU MRADI ZIMETOKA WAPI?

2.JE HAO KIWIRA WALISHINDANISHWA NA KAMPUNI ZIPI KTK KUPATA TENDER HIYO?
...INAWEZEKANA TANESCO SASA HIVI IKO KTK KU-DERVERSIFY VYANZO VYA UMEME NA WATU WANACHANGAMKA TU.

3.KWANINI TANESCO HAWAPEWI UMILIKI WA HUU MRADI[Kiwira Coals] KAMA AMBAVYO WANAMILIKI KIDATU?
 
Joka Kuu,

Maneno yako yanazidi kunogesha mjadala.... Naamini kama THISDAY wanasoma JF hapo kuna story zaidi ikiwa watatafuta (ama kama wanayo) majibu ya maswali yako na kuyaandika
 
jokaKuu,
TANESCO wakipewa umiliki wa huo mradi wajanja watakula wapi?
TANESCO inaonekana imegeuka kuwa cash cow. IPTL, Net Group Solutions, Richmonduli na sasa Kiwira-ANBEM
 
Mkapa alipoingia madarakani, alitamka wazi kuwa alikuwa na magari matatu (mojawapo likiwa shangini la ubunge), nyumba mbili (moja iko kijijini kwake Masasi na moja iko Kiluvya). Hizo ndizo mali kubwa alizotaja na akawataka mawaziri wake pia wafanye hivyo. Wakati huo alikuwa anajua mali zake na zilikuwa za kwawaida kwa mfanyakazi wa serikali. Miaka kumi baadaye, mali zake zimekuwa nyingi sana kiasi kuwa hata hawezi kuzifahamu, na wala hakuweza kuzitangaza tena hadharani kama alivyofanya wakati anaingia madarakani.

Maswala hapa siyo utajiri wake, ila jinsi utajiri huo ulivyopatikana:
  • Sehemu kubwa ya utajiri wake inaonekana kutokana na kuikamua TANESCO kupitia miradi kama ITPL, NETGROUP na huu wa Kiwira. Yote hiyo ilitumia nafasi yake kama president. Matokeo ya kuikamua TANESCO ni kwa watumiaji wa umeme kujikuta wanalipa umeme kwa bei ya juu zaidi ya kawaida, na TANESCO yenyewe kushindwa kujiendesha kwa ufanisi wa kutosha, jambo linaloweza kupelekea kupunguka kwa umeme uzalishwao na hivyo kulazimisha zimwi lan MGAO wa UMEME.
  • Sehemu nyingine ya utajiri wake imetokana na rushwa ya moja kwa moja katika manunuzi ya serikali ambayo inatokana na kodi ya wananchi. Mifano inayojulikana wazi ni pamoja na ununuzi wa ndege ya rais, ununuzi wa rada, ujenzi wa benki kuu, nadhani na ukarabati wa ikulu. Hii inapunguza pesa za serikali na hivyo kuipunguzia serikali uwezo wa kutoa huduma kwa jamii. Ndiyo maana tunakuwa na shule ambazo hazina sakafu wala waalimu.
  • Sehemu nyingine kubwa sana ya utajiri huo ni kutokana na mikataba ua uuzwaji wa raslimali za taifa kama ardhi yenye madini, na mashirika ya umma. Raslimali hizi ziliuzwa kwa bei ya chini sana kwa vile kuna wasiwasi kuwa wanunuaji walikuwa wakitoa malipo mengine kwa viongozi waliohusika na zoezi la uuzwaji wa raslimali hizo. Mkapa akiwa Rais aliyesimamia uuzwaji ule alikuwa na stake kubwa sana na hiyo, na nadhani ndiyo imechangia sana kwa yeye kujipatia utajiri huu. Matokea ya mauzo haya ni kuwa wananchi wamebaki hawana sauti katika raslimali zao. Wale waliokuwa wakichimba dhahabu na tanzanite kwenye migodi waliondolewa kwa nguvu sana badala ya serikali kubuni namna ya kuwandeleza, leo hii wananchi hao ni maskini kabisa
Sasa kwa vile vyanzo vikuu vyote vya utajiri wake vinagusa maisha ya kawaida ya kila mwananchi, tuna haki ya kuhoji alikopata utajiri huo.

Sumaye kweye sakati hilo:


Sumaye ni mtu aliyelaumiwa sana kwa kuendesha rushwa. Tatizo la Sumaye ni kuwa alikuwa anafanya mambo madogo madogo hadharani sana, kama vile kukopa kutoka NSSF na "kununua" ardhi kutoka kwa wanavijiji huko Morogoro na Dodoma. Mkapa alifurahia hali hiyo ya Sumaye kuchunguzwa sana kwa mambo madogomadogo kwa vile ilimsaidia yeye asichunguzwa kwa mambo makubwa aliyokuwa akifanya wakati huo. Ndiyo maana kila wakati jina la Sumaye lilikuwa likitajwa, alikuwa msitari wa mble sana kumtetea. Mpaka leo haijulikani Sumaye alichukua dili gani kubwa, labda kama na yeye alipata migao kwenye ununuzi wa ndege, uuzwaji wa ardhi ya madini na mashirika. Kama kweli na yeye alijipatia mgao ule, basi inawezekana alikuwa akipewa tu, lakini hakuwa na tamaa kama aliyokuwa nayo bosi wake ambaye tangu wakati huo ameendelea na libeneke wakati Sumaye mweywe ametulia na kuachana na mambo ya aina hiyo
 
Back
Top Bottom