Nadhani kwa mwendo huu, tutayajua mengi. Lakini kinachosikitisha ni kwamba raia karibu million 40, tumekosa azma ya kuijenga Tanzania yenye neema kwa kila raia na vizazi vijavyo. Hivi jamani, hawa viongozi wetu wapewe nini kusudi waweke maslahi ya wananchi na taifa mbele? naombeni mwenye mawazo anipe. Tuwape nini? Pension ya wanasiasa Tanzania ni kubwa kuliko popote, maisha yao ni ya neema mno (kulinganisha na hali ya wanaowaongoza), sasa jamani tufanye nini? Ama kweli kama jamaa alivyosema ITS ALL ABOUT IQ, IQ, IQ ya mwafrika akiwa Africa! Zaidi ya hili, utaelezeaje huu ufedhuli wa hawa viongozi wetu (wengi wao wakiwa na utumishi uliotukuka nje ya nchi, lakini baada ya kurudi nyumbani wamekuwa majuha?)
Naomba wanaforum humu na watanzania, tusiwe wepesi wa kusahau, kila anayepita humu, ayaweke na kuyatunza haya madudu ya hawa wazee kichwani, 2010 tusidanganywe tena. Tafadhali sana, maana ugonjwa wa watanzania ni kusahau haraka. Kashfa za hawa wazee zimezidi mno, na madhara ya hizi rushwa ndo tunayaona, kipindupindu ambacho hakiishi kilometa mbili toka nyumbani kwa mkuu wa nchi, uchafu na ukosefu wa huduma za msingi kabisa ambazo binadamu inabidi azipate kwa kuwa raia! si mara mia wangekuwa wanakula lakini wanawamegea wananchi wao? Taifa kama taifa tukae chini tutafute mstakabali wa hili taifa, tuache theories na ndoto za kutumia usomi wetu kuihujumu nchi na hawa raia wake wanaotambulika kwa namba na idadi tuu za kuombea misaada. Tutafanya hivi kwa kila mtu kugundua wajibu wake kama kiumbe aliyepewa utashi na Mungu wa kuamua mema na mabaya. Tuna silaha moja nayo ni KURA (its our last democratic right in Tanzania), Hii ikiondolewa, basi we shall be banished in the dustbin of history.
THISDAY have played their part, wewe na mimi je? ukitaka kuwaita wenye majungu, or whatever name, wewe ndo mwamuzi.