1.
- Uporaji wa mali za wananchi ni pamoja na kujiuzia Kiwira kwa bei poa, kama rais wa jamhuri huwezi kujiuzia mradi wa taifa kwa shillingi millioni 700 tu, mradi ambao unaingiza mamilioni ya dola za kimarekani kama faida, huu ni uporaji tena wizi wa mchana.
- TBL, NBC zimeuzwa kwa bei poa, chini ya uwaziri wa Yona, Mramba, na Idd Simba, hapa lazima uongeze Sumaye na Mkapa mwenyewe na yule mkulu wa ubinafsishaji wote wamehusika na kula mgawo. Sheria haimzuii kufanya biashara kama mwananchi wa kawaida, lakini inamzuia kupora mali za wananchi akiwa rais, hivi wananchi wengine mnakuwa mmerogwa nini? Katika urais wa Mkapa wa ten years tu ameweza kukusanya mali za kuwekea rehani mkopo wa ANBEN enough mpaka kuweza ku-secure mkopo wa dola laki tano mkuu uko serious au huelewi vizuri aliyoyafanya Mkapa Ikulu?
- Alitakiwa akafanyie nje ya Ikulu, taifa tumeamua kwamba rais wa jamhuri tutamtunza mpaka mwisho wa maisha yake ili kumuepusha na tamaa kama hizi za fisi, I mean tamaa gani hii mpaka unajinyakulia miradi ya taifa wewe mwenyewe rais wa Jamhuri? Sasa Yona na Mramba wanafanya nini Kisutu kama Mkapa aliyekuwa akiwatuma tunamuacha? Hivi unahitaji kuwa Doctor kama Kikwete kuelewa hili?
2.
- Hatusemi sheria iishie kwa Mkapa, tunasema hivi hata kama rais wa sasa au zamani atakutwa amevunja sheria zetu wote waende Kisutu, tutachyambua huko huko mbele kwa mbele, tunasema sheria ichukue mkondo hata kama Kikwete anahusika, yasemwe wazi na kila mmoja abebe mzigo wake au mshaurini Mkapa akifika Kisutu, aseme kama alishirikiana na Kikwete.
3.
- Hapa mkuu umechanganya ishus nyingi sana, kwanza unasema mapungufu ya katiba yetu, ukweli ni kwamba kwenye suala la kumfikisha Mkapa kwenye sheria zetu za jamhuri, at this point tatizo sio upungufu wa katiba isipokuwa ni interpretation tu ya sheria tuliyonayo tayari, ambayo pia wala sio ishu ila inasubiriwa amri ya rais tu.
- Hakuna mtu anayetaka kwenda bungeni kumtungia sheria Mkapa, sheria ipo tayari ila watu wanataka kwenda bungeni kufanya wajibu wao wa kazi ya ubunge, ambayo ni pamoja na ku-interprate sheria inapobidi as of this case. Kwenye Richimonduli tuliambiwa maneno kama yako na Takukuru, lakini tukafuata katiba na kuwakabidhi wabunge you know the rest of the story.
- Ya Mkapa kupora mali za wananchi hatukuyajua mpaka alipotoka Ikulu, kama vile ya EPA yote tumeyajua baada ya yeye kutoka Ikulu, lakini tungeyajua mapema basi angekiona cha moto kama tunachompa sasa, huyu Mkapa tunaye mpaka kieleweke, halafu it does not matter kuhusu time cha muhimu ni tumemshitukia kabla hajaenda mbali.
Ndugu zangu wananchi wengine naomba kuwaambia hivi wakati ni huu, rais wa sasa huwa ana-respond kunapokuwa na strong political pressure kutoka kwetu wananchi, ndio maana majuzi amemwambia Makamba kwamba hataki kumsikia Mbeya kwenye uchaguzi, tena point blank bila kumung'unya maneno wala diplomasia ni kutokana na pressure ya wabunge wa CCM na wananchi wa Mbeya kwamba hawataki not only Makamba bali viongozi wote mafisadi wasiguse huko, sasa amemuomba jm na kundi la viongozi wasio mafisadi kwenda huko na ni kweli wanaenda akiwemo kijana shujaa Nape na Kinana, my point ni kwamba hawa mafisadi wameshikwa pabaya sana na walahi tukifanya mchezo tukawakosa sasa basi hatutawapata tena, Kikwete ana respond only kukiwa na pressure ya nguvu kwa hiyo tuendelee ku-press tu mpaka kieleweke!
Mkapa hawezi kulisambaratisha taifa letu kwa kutakiwa kujibu mbele ya sheria jinsi alivyopora mali za wananchi na kujilimbikizia utajiri usio mfano kwa kipindi kifupi cha miaka kumi tu ninasema no way! Na likisambatratika then let it be on ourbloods, lakini huwezi wafikisha Mramba, Yona na Mgonja Kisutu bila baba yao Mkapa ni kuwaonea bure!
Mungu Aibariki Tanzania!