Ni wakati muafaka kwa viongozi wetu kuaanza kutupa majibu ya ukweli. watanzania tunataka kujua nini kilitokea, katika mazingira gani, na mshusika alichukua nafasi gani na kwa nini alifanya hivyo. Kuendelea kukana ni kuendelea kuwafanya watanzania wajinga na kuwadharau.
Pale mtu anapojiuzulu, halafu hatoi maelezo yoyote ya kuonyesha amekosea na kusikitishwa kwake na kosa hilo, bali kujitetea haileti maana kabisa. kimsingi mtu anajiuzulu pale anapoona kwa namna moja au nyingine hawezi tena kuitumikia nafasi yake kwa ufanisi. hapo inambidi aelezee kiundani. sasa hapa kwetu kila mtu anakana, na yaliyo wazi kabisa bado wanakana hii ni kutudharau kwa hali ya juu.
kwenye hili kama kweli Raisi Mkapa anataka kujisafisha, awaeleze watanzania kila kitu na kujibu yote yanayoelekezwa kwake. atuachie sisi tuchambue kama ni uongo ama la. sio yeye bila kutoa jibu lolote anataka tuamini kotowapendelea watu ndio wamemzushia. hao watu ni kina nani? na aelezee huo upendeleo ulikuwa on what.
kwa upande wangu bado Raisi Mkapa hajazungumza