Mkaka mzuri, ana magari na kazi nzuri ila amenikosa kwa utongozaji wake wa kitoto

Ederra

Member
Mar 2, 2022
91
528
Nilikuwa nimekaa zangu kwenye mgahawa fulani. Akaja mkaka mzuri tu na alikuwa amependeza. Akakaa kiti cha mbele yangu.

"Mambo? Nimependa nikae na wewe hapa." Akaniongelesha.

"Haina shida." Nikajibu.

"Mbona huna kinywaji au chochote? Agiza chochote. Usikae kinyonge hivyo" Aliuliza.

Nikamjibu "Nimeagiza chakula. Ndio nakisubiri."

"Oh sawa. Vizuri tufahamiane. Me naitwa James, naishi (******). Nafanya kazi hapo (****) Bank kama branch manager. Nikufahamu na wewe please!"

"Naitwa Ederra. Naishi (******).". Nikajitambulisha.

Akaendelea na stori nyingine kwa dakika chache kisha akainuka na kusema angerudi pale punde. Baada ya dakika tatu akarudi.

"Nimerudi Ederra. Nilienda kuangalia gari yangu. Nilikuwa na wasiwasi kama nilikuwa nimepandisha vioo." Akasema huku akikaa tena kwenye kiti.

"Sawa. Karibu tena."

"Asante. Nilikuwa naogopa isije kunyesha mvua au watu wakaniibia KiBMW changu. Unajua gari yenyewe ni mpya nisije kupata hasara. Nilichoka kutembelea Harrier nikaona ninunue na hii"

"Yeah wasiwasi ndio akili." Nikamuunga mkono.

Chakula kikafika. Na yeye akaagiza. Nikawa naendelea kula huku nikisikiliza stori za magari yake, kazi yake nzuri, anapoishi na nyingine kama hizo mpaka nikamaliza kula.

Mhudumu alipokuja kuleta chakula cha jamaa nikamuomba bill.

"Acha tu nitalipa Ederra. Unalipaje wakati mimi niko hapa?" James akaingilia kati.

"Oh sawa. Nashukuru sana."

Nikamuaga kuwa naondoka. Akaniomba namba ya simu. Nikamwambia anipe yake ningemtafuta. Akanipa business card yake na kung'ang'ania nimpigie pale pale lakini nikamwambia asijali ningemtafuta tu. Nikaondoka.

Ile business card niliitupa kwenye dustbin baada ya kupotea kwenye upeo wa macho yake. Nisamehe James. Sio kwa ubaya.

Mwanaume unapotumia nguvu kutaka kuonesha magari unayoendesha, kazi yako unayoiona nzuri, unapoishi na mafanikio yako mengine kwa mwanamke ambaye ndiye kwanza unakutana naye unadhani ndiyo utamvutia?

Hii tabia haivutii. Meseji ya nje unayoileta kwa kufanya hivyo ni kuwa wewe ni mtu wa maana sana na mwenye mafanikio. Meseji hii ya nje sio inayoathiri mvuto wako kwenye akili ya mwanamke.

Meseji iliyojificha (ya ndani kabisa) ndio inayoathiri mvuto wako. Hiyo ni kwamba hujiamni na unadhani huna thamani wewe kama mwanaume na hivyo unalazimika kutumia vitu kama magari, kazi, mafinikio ili uonekane una thamani. Hakuna mwanamke anayejielewa anavutiwa na mwanaume wa hivi.

James asante kwa kunilipia chakula. Lakini wewe na wanaume wengine wenye akili kama zako badilikeni. Itawasaidia.

Jifunzeni kuwa na tabia zinazowavutia wadada. Mnaweza kusoma vitabu hivi viwili mtanishukuru baadae.

1) "UNLOCK HER LEGS: How to Effortlessly Attract Women..." By Dominic Mann

2) "MWANAUME WA DHAHABU : Jifunze Namna ya Kuwatawala Wanawake na Kutawala Mahusiano." By Anita Shija

Mwanaume tafuta uvisome yasije kukukuta ya James. Hasa hicho cha Kiswahili.
 
"UNLOCK HER LEGS: How to Effortlessly Attract Women
Si utuweekee tuu hapa utafanya mambo kuwa mepesi Sanaa
1646289630394.png
 

Attachments

  • Attract Women_ Unlock Her Legs_ How to Effortlessly Attract Women and Become the Man Women Unl...pdf
    484.9 KB · Views: 116
Back
Top Bottom