Mjue Rais wa zamani wa Haiti, François "Papa Doc" Duvalier aliyewahi kuwa mchawi kuliko Marais wote Duniani

TAJIRI MKUU WA MATAJIRI

JF-Expert Member
Dec 1, 2010
5,720
10,215
KUMBUKUMBU: JE, WAJUA? KWAMBA HAITI NDILO TAIFA LINALOSEMEKANA KUONGOZA KWA UCHAWI DUNIANI?

1684099594950.jpg


Rais wa zamani wa Haiti, Dikteta François "Papa Doc" Duvalier, aliyechaguliwa na wananchi wa taifa hilo kuwa rais wa 32 wa Jamhuri ya Haiti, kuanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1971, anasemekana kuwa mchawi kuliko marais wote wachawi duniani wa wakati wote.

Kwa mujibu wa makala ya runinga ya Evolution of Evil (),

Rais François Duvalier wa Haiti ndiye anayesemekana kusababisha kifo cha Rais John F. Kennedy wa Marekani kwa njia za kishirikina.

Kilichotokea ni kwamba Papa Doc alipoanza kufuja fedha za misaada za walipa kodi wa Marekani, akizitumia fedha hizo kuendesha nchi kichawi na kidikteta, kupitia kikosi-kazi chake cha Tonton Macoute, Rais Kennedy aliamua kusitisha misaada yote kwa taifa hilo kongwe ulimwenguni. Kitendo hicho kilimuudhi sana Duvalier, kiasi cha kuamua kuweka nadhiri ya kumuondoa Kennedy madarakani na duniani kwa msaada wa mungu wake aitwaye Bondye.

Tarehe 22/11/1963, siku moja tu baada ya Rais Kennedy kutangaza vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Haiti, Dikteta Duvalier alifanya tambiko akiwa nchini mwake la kumroga Kennedy kama alivyodhamiria. Siku hiyohiyo, yaani tarehe 22/11/1963, J. F. Kennedy aliuwawa na mtu asiyejulikana huko Dallas nchini Marekani.

Nchini Haiti Papa Doc alionekana kwenye vyombo vya habari akisherehekea kifo cha hasimu wake kwa kunywa shampeni na kucheza muziki na Tonton Macoute, kikosi chake maalumu kilichotesa au kuua mtu yeyote aliyepingana na Rais, huku akitamba kuwa yeye ndiye aliyemuua Kennedy.

Rais aliyefuata huko Marekani baada ya Rais Kennedy, Rais Lyndon B. Johnson, aliondoa mara moja vikwazo vya kiuchumi dhidi ya Haiti. Uhusiano kati ya Marekani na taifa hilo la Kikaribi, lililojipatia uhuru wake toka Ufaransa mnamo mwaka 1804, ukaendelea tena kama kawaida.

Haiti ina asilimia 70 ya Wakatoliki, asilimia 30 ya Waprotestanti, na asilimia 100 ya wachawi.
 
Kuna mwingine alikuwa na fimbo yake, hata ikija boom crane ya kubeba tani 1000 haiwezi kubeba hiyo fimbo. Boom inavunjika.

Nchini kwake wanapumbazwa na mamoshi ya kibatari kinachogharimu mabilioni ya mapesa.

Eti kibatari kinaleta amani, Congo maelfu ya watu wanakufa kutokana na vita, lakini wale mabwana hawataki kupeleka hicho kimashine chao cha kuletea amani.

Israel na Palestine kunawaka moto, lakini still jamaa wamegoma kabisa kupeleka mashine yao ya amani ikamalize vita.

Pale Ulaya mashariki, kuna vita kali inarindima, jamaa kamashine kao wanakafungia tu kwao wanakakimbiza kwa nyimbo na mapambio
Port-au-Prince kuna soko kubwa sana la kuuza bidhaa za uchawi
Hili nalijua tangu zamani na kuhusu uchawi wamo ila siamini

Nategemea kwenda siku moja huko nikajionee maajabu haya
 
Rais wa zamani wa Haiti, Dikteta François "Papa Doc" Duvalier, aliyechaguliwa na wananchi wa taifa hilo kuwa rais wa 32 wa Jamhuri ya Haiti, kuanzia mwaka 1957 hadi mwaka 1971, anasemekana kuwa mchawi kuliko marais wote wachawi duniani wa wakati wote.
Pamoja na uchawi wake kuna mwamba tapeli toka US alimtapeli Mara mbili na hakuweza kumfanya chochote,
 
Waprotestanti na Wakatoliki wote walikuwa ni vigagula. Kanisani walienda kumcheka mungu wa wazungu
Emu hapa fafanua kidogo mkuu umemaanisha nini maana umetukoroga koroga vibaya mno, Wakatoriki na Waprotestant ni wachawi 100% ndio umemaanisha hivyo ?
 
Kuna visa vingi vya kigagula alisimulia kwenye hotuba zake, miongoni mwa visa hivyo ni jinsi alivyomtengeneza mbuzi kikushi, mbuzi akawa anamfuata jamaa kwa nyuma kama wafanyavyo watoto wa bata
Hizi ni zile simulizi tulikua tunapeana uongo uongo njoo za watoto wakiimba chei chei Shangazi tufurahi Shangazi, hii ni chai Shangazi
 
stow away
 
Back
Top Bottom