Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Tanganyika ni jina kutaka kutumanisha et itakuwa kama ya mkoloni ni uzezeta .
 
Wakoloni wapo mpaka leo, ndo maana mnakesha kutaka Tanganyika ya mkoloni kuliko nchi mliyoiunda wenyewe!
Nchi ipi hiyo? Tanganyika ni zao letu wenyewe , hiyo nyingine iliundwa na Mkoloni CIA wakati wa vita baridi ........
 
Nilichogundua mpaka sasa hivi viongozi wa tanzania (bara) na viongozi wa tanzania visiwani (zanzibar) wote kwa pamoja wanahofia kupoteza nguvu za kimadaraka na utawala.

Tanzania Bara wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.

Tanzania visiwani wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.

Kinachosikitisha hawa wananchi hawana nguvu za vitendo wana nguvu za maneno.
 
Hivi ni kwann watu awaongelei serikali 1 ?????? wanawaogopa waznz ??kwann wameng'ang'ania kwenye kupinga serikali 3 ?? mutujibu na sisi tunaosema serikali 1.Au ni vile hatuna mahala pakusemea ???????? Muunganano utakaodumu ni waserikali 1 tu.Mimi nataka siku 1 rais,m/rais au waziri mkuu siku wasimame watuambie ni kwann hawaongelei serikali 1 ??????? na kutokuongelea serikali 1 ni kuiogopa znz kwa msimamo wake kusema kwao serikali 1 ni bora muungano ufe.
 
Hana, tume ya uchaguzi ya Zanzibar inaitwa ZEC sio NEC ......ndio maana Tanganyika ipo na DED ila Zenji hakuna hao MADED ila kuna Masheha ........kama hujui ombi ufafanuzi Acha ubishi , hujui mfumo wa SMZ ila sio tatizo lako bali ni la watanganyika wengi......Pinda ni waziri mkuu wa Tanganyika , mamlaka yake inatisha kisiwa cha Chumbe........hairuhusiwi kufika Nungwi...

Wewe unamawazo ya kutawaliwa na sultani kwanini cc watanzania hatupendi ubunifu wetu
 
Hivi ni kwann watu awaongelei serikali 1 ?????? wanawaogopa waznz ??kwann wameng'ang'ania kwenye kupinga serikali 3 ?? mutujibu na sisi tunaosema serikali 1.Au ni vile hatuna mahala pakusemea ???????? Muunganano utakaodumu ni waserikali 1 tu.Mimi nataka siku 1 rais,m/rais au waziri mkuu siku wasimame watuambie ni kwann hawaongelei serikali 1 ??????? na kutokuongelea serikali 1 ni kuiogopa znz kwa msimamo wake kusema kwao serikali 1 ni bora muungano ufe.
Mkuu Zanzibar ni nchi tuliungana nayo mwaka 1964.

Suala la kuigopa halipo hapo.

Cha kufanya pambana na Pinda kuipata Tanganyika yako.
 
Nilichugundua mpaka sasa hivi
viongozi tanzania (bara) na viongozi wa tanzania visiwani (zanzibar)
wote kwa pamoja wanahofia kupoteza nguvu za kimadaraka na utawala.

Tanzania Bara wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao
hawataki wanataka serikali mbili.

Tanzania visiwani wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao
hawataki wanataka serikali mbili.

Kinachosikitisha hawa wananchi hawana nguvu za vitendo wana nguvu za
maneno.

salute u swahiba
 
Mamlaka ya nchi ipo kwenye katiba soma kwanza katiba ya znz toleo la 2010 .....

Mamlaka ya "nchi" ya Zanzibar sio absolute (not a sovereign state)! We muulize Ban Ki Moon kuwa kuna "nchi" inaitwa Zanzibar kama hatavunjika mbavu kwa kicheko! Ila nikimuuliza Maalim Seif kama kuna "nchi" ya Zanzibar atanikunjia uso kama unavyofanya wewe hapa mtandaoni!
Ila ukweli, hata kama utawauma kiasi gani, Zanzibar is NOT a sovereign state! Kuwa sovereign state hakuletwi na wording ya Katiba ya Nchi bali status ya entity katika International Law! Ukiwa na mentality hiyo tuko pamoja, ila ukiwa na mentality ya ki-maalim Seif, hapa tutakesha!
 
Nilichugundua mpaka sasa hivi viongozi tanzania (bara) na viongozi wa tanzania visiwani (zanzibar) wote kwa pamoja wanahofia kupoteza nguvu za kimadaraka na utawala.

Tanzania Bara wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.

Tanzania visiwani wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.

Kinachosikitisha hawa wananchi hawana nguvu za vitendo wana nguvu za maneno.
Agreed, ila tatizo ni unafiki wa viongozi hasa CCM kwani wao ni vinara wa malalamiko kuwa znz imevunja Muungano wanape fursa wanaleta unafiki wao
 
Mamlaka ya "nchi" ya Zanzibar sio absolute (not a sovereign state)! We muulize Ban Ki Moon kuwa kuna "nchi" inaitwa Zanzibar kama hatavunjika mbavu kwa kicheko! Ila nikimuuliza Maalim Seif kama kuna "nchi" ya Zanzibar atanikunjia uso kama unavyofanya wewe hapa mtandaoni!
Ila ukweli, hata kama utawauma kiasi gani, Zanzibar is NOT a sovereign state! Kuwa sovereign state hakuletwi na wording ya Katiba ya Nchi bali status ya entity katika International Law! Ukiwa na mentality hiyo tuko pamoja, ila ukiwa na mentality ya ki-maalim Seif, hapa tutakesha!
Tanganyika iliungana na nchi gani vile 1964? Mbona wewe ndio hujitambui hapa ? Maalim Seif yeye anataka Muungano wa Nkataba .......
 
Nchi ipi hiyo? Tanganyika ni zao letu wenyewe , hiyo nyingine iliundwa na Mkoloni CIA wakati wa vita baridi ........

Tanganyika ni zao la Mjerumani (mambo ya Tanganyika Mandate na Baadaye Tanganyika Territory). Alipokuja Mwingereza akachukua hiyo kitu Tanganyika mpaka alipomkabidhi Julius, ambaye alipoona nchi "haitoshi" akaamua "kuiongeza" kidogo na kuipa jina jipya! Hongera sana Mwaaaaalim (RIP) kwa ubunifu! Wengine wanakuonea wivu tu, hamna lolote!
 
Mimi naona jambo la muhimu kwa sasa ni kuangalia upya mfumo huu wa serikali mbili na kuufanyia marekebisho lakini mfumo wa sijui serikali Tatu,Nne ,Tano Mara shirikisho ni kujiongezea matatizo yasio ya msingi

Hakuna dawa ya kutibu na kuukarabati mfumo wa Muungano wa serikali mbili uliopo sasa.Yaani kama ni mgonjwa sasa umeshaambiwa na daktari wenu mrudisheni nyumbani akafie huko!!

Kosa la msingi hapa lililofanyika katika harakati hizi za uandishi wa katiba mpya ni kuruka hatua ya kwanza ambayo ni kura ya maoni ya wananchi kuulizwa kama wanautaka Muungano au la. Jibu ambalo hata wewe unalo kwamba HAKUNA MTU ASIYEPENDA MUUNGANO na kama wapo basi ni wachache sana ambao sisi tunaoutaka tungewashinda tu!!.....Swali la mwisho lingekuwa ni sisi kuamua sasa kwa mtindo uleule wa kura ya maoni NI MUUNDO GANI WA MUUNGANO TUNAOUTAKA!

Honestly,hili likifanyika kwa uhuru na uwazi wakaachwa wananchi wenyewe kuamua aina ya muungano wanautaka,hakika muungano wa hizi nchi mbili za TANGANYIKA na ZANZIBAR na kupata JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA,basi hii JMT itadumu milele na milele!!

LAKINI, kwa mtindo huu tunaoenda nao chini ya uratibu wa Chama kinachoongoza serikali CCM wa kulazimisha mambo na kuwafanya wenye nchi wote ni mataahira,HUU MUUNGANO UTAKUFA TU hata kama sio kwa kisu cha rasimu ya Warioba,lakini si muda mrefu miaka ijayo.......na milele hautalindwa kwa mitutu ya bunduki!!....Hii ya kina PINDA ni unafiki mtupu kwani ni yaleyale ya kuwafanya wananchi vichwa vyao havina akili ila vina nywele tu kwa ajili ya kunyolewa na kina PINDA na CCM, HIKI NDICHO TUNACHOKIKATAA kwa manufaa ya MUUNGANO WETU.....Otherwise tujiandae kugawana mbao!!
 
Tanganyika iliungana na nchi gani vile 1964? Mbona wewe ndio hujitambui hapa ? Maalim Seif yeye anataka Muungano wa Nkataba .......

Japokuwa unauliza kwa kejeli lakini jibu unalo na historia nzima unayo! Huo muungano wa "Nkataba" ni idea ya Seif ya baadaye lakini idea original ni Serikali 3! Kifupi Maalim anaamini kuwa tayari Zanzibar ni sovereign state, labda kama siku hizi kabadilika, maana babu kigeugeu, si mchezo!
 
Watanganyika wenzangu kwa maneno ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, suala la Tanganyika litabakia kuwa historia.

Cc; Nguruvi3 Mag3 Mzee Mwanakijiji JokaKuu WildCard Mkandara Ngongo

Tutabaki kupambana kwenye forums tu, wako wapi Watanganyika watakaoweza kuirudisha Tanganyika yao.

Watawala kutoka chama chako cha CCM wameshindwa kusoma alama za nyakati kwasababu Tanganyika haizuiliki ni kama mafuriko. Mpaka sasa wanapinga bila hoja zozote za msingi ambazo wanaweza kutuonyesha wenye akili kwamba sasa tumepata mworobaini wa kero za muungano.

Ritz msaidie chama chenu kujiondoa ktk aibu ambayo itakuja kukiandama ktk uhai wake wote. Toka 1984 mpaka leo hakina majibu ya kero za muungano lakini bado wanalazimisha hata kutuchafulia Katiba yetu mpya!
 
Last edited by a moderator:
Japokuwa unauliza kwa kejeli lakini jibu unalo na historia nzima unayo! Huo muungano wa "Nkataba" ni idea ya Seif ya baadaye lakini idea original ni Serikali 3! Kifupi Maalim anaamini kuwa tayari Zanzibar ni sovereign state, labda kama siku hizi kabadilika, maana babu kigeugeu, si mchezo!

Umeandika sana ktk hii thread lakini bado hujasema ni kwanini wewe hutaki serikali 3? Toa hoja badala ya kutujazia mashudu!
 
Watawala kutoka chama chako cha CCM wameshindwa kusoma alama za nyakati kwasababu Tanganyika haizuiliki ni kama mafuriko. Mpaka sasa wanapinga bila hoja zozote za msingi ambazo wanaweza kutuonyesha wenye akili kwamba sasa tumepata mworobaini wa kero za muungano.

Ritz msaidie chama chenu kujiondoa ktk aibu ambayo itakuja kukiandama ktk uhai wake wote. Toka 1984 mpaka leo hakina majibu ya kero za muungano lakini bado wanalazimisha hata kutuchafulia Katiba yetu mpya!

Mwarobaini ni SERIKALI MOJA! SERIKALI MBILI au TATU ni Panadol tu ya kutuliza maumivu! Nguvu ya dawa ikiisha maumivu yanarudi pale pale tu!
 
[h=1]
asietaka-mbili-apigwe-430x300.jpg
[/h]
Na Fidelis Butahe, Mwananchi

Jumapili,Februari23 2014

Dodoma. Wakati mjadala mkali ndani ya Bunge Maalumu la Katiba ukitarajiwa kuwa muundo wa Muungano, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda amesisitiza Serikali mbili.
Akifungua semina ya Jumuiya ya Wazazi ya CCM jana, Pinda alihoji sababu za baadhi ya watu kudai kufa kwa Serikali ya Tanganyika wakati ilishatoweka miaka 50 iliyopita.
Pinda alisema Tanganyika ilidumu kwa miaka mitatu baada ya uhuru, kuanzia mwaka 1961 hadi 1964 na kuungana na Zanzibar.

Alisema kwa msingi huo, Watanzania wengi hawajui lolote kuhusu Tanganyika kwa sababu baadhi yao walikuwa hawajazaliwa.
“Suala hili najua litaleta mvutano mkali katika Bunge la Katiba. Binafsi hata ukinikurupusha usiku nitakwambia nataka Serikali mbili,” alisema.

Alisema hata Rais wa Awamu ya Kwanza, Hayati Mwalimu Julius Nyerere aliwahi kueleza wazi kwamba, alikuwa kiongozi wa Tanganyika kwa muda mfupi na ilikuwa Tanganyika ya wakoloni ndiyo maana likaibuka wazo la kuungana na Zanzibar.
“Hivi sasa tuna miaka 50 ya Muungano wetu lakini wapo watu wanadai Tanganyika, hivi hiyo Tanganyika wanayoida ni ipi, unalalamika kuikosa Tanganyika ipi,”alihoji.
Alisema kasoro zilizopo katika Muungano zinaweza kujadiliwa na ikapatikana suluhu ya kudumu.

Tayari CCM imeshatoa waraka maalumu kwa wanachama wake ikisisitiza msimamo wake wa Serikali mbili, msimamo ambao pia wataingia nao bungeni wakati wa kujadili rasimu ya Katiba ambayo imependekeza muundo wa Serikali tatu.

Rushwa

Akizungumzia rushwa Pinda alisema, “Jumuiya inatakiwa kuwa mstari wa mbele kusimamia uendeshaji wa chaguzi ndani ya chama kwa misingi ya maadili kwani wanaomwaga fedha ili kupata uongozi ndani ya chama wanatuvuruga na hiyo siyo njia ya kukijenga chama.”

Alisema viongozi wanaopatikana kwa njia ya rushwa siyo viongozi bora na kuhoji, “Hivi mtu anayetumia fedha kuingia madarakani akipata madaraka fedha hizo atazirudishaje.”
Katika hotuba yake Pinda aliwagusia wanachama wa CCM wanaopanga nani agombee na nani asigombee na kufafanua kuwa hali hiyo hujenga makundi ndani ya chama hicho.

“Tunahitaji kupata viongozi kwa kuzingatia umoja wetu na mshikamano miongoni mwa wanachama. CCM ikiwa imara itaunda Serikali imara. Chama kikiwa dhaifu ni wazi kuwa hata Serikali yake nayo itakuwa dhaifu” alisema.
Pia aliitaka Jumuiya hiyo kujipanga kwa kuimarisha mali zake ikiwa ni pamoja na shule ili siku za usoni shule hizo ziwe miongoni mwa shule 10 zinazofanya vizuri nchini, kuitaka kutumia majengo, viwanja na ardhi inayofaa kwa kilimo ili kuitumia kuimarisha jumuiya hiyo.

Aiponda Chadema
Katika mkutano huo Waziri Pinda alikipiga kijembe Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuwa licha ya kufanya kampeni zake kwa kutumia helkopta tatu, kiliambulia ushindi katika kata tatu tu, kwenye uchaguzi wa madiwani uliofanyika hivi karibuni katika kata 27.
“Chama ni kujipanga na wakati mwingine fedha siyo kila kitu. Chadema wameruka kwa helkopta tatu na wameambulia ushindi katika kata tatu tu.
 
Umeandika sana ktk hii thread lakini bado hujasema ni kwanini wewe hutaki serikali 3? Toa hoja badala ya kutujazia mashudu!

Ni kweli nimeandika sana na nimetoa mawazo yangu kwenye Topic hii, labda kama hujafuatilia! Mwanzoni nilikuwa naunga mkono Serikali 2 lakini baadaye nikapima nikaona nayo itaendeleza matatizo hayo hayo yaliyokuwepo! Hatimaye nikaona FINAL SOLUTION ni Serikali MOJA! REASON: USISI utaisha na tutaana kuongea lugha moja! Kumbuka huko nyuma nako tulikuwa na baadhi ya makabila yalitaka kuimega nchi yetu lakini leo hawapo!
Serikali 2 au 3 zitaongeza USISI na kero zitaendelea!
 
Back
Top Bottom