Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Pinda aache kupotosha wamanchi; Tanganyika ni jina la nchi iliyopata uhuru wake 9/12/1961 na tunaendelea kusherekea siku hii kila mwaka. Pinda anapoibeza Tanganyika na kuendelea kusherekea na kuienzi December 9 kila mwaka huu ni unafiki kwa sababu hakuna nchi juu ya uso wa dunia hii inayoitwa Tanzania iliyopata uhuru wake tarehe 9/12/1961. Kama kweli Pinda na ccm wanania nzuri ya muungano wangezungumzia muungano wa serikali moja hapo tungewaelewa. Pinda unaitwa waziri mkuu wa serikali ya JMT lakini huna hata chembe ya mamlaka yeyote Zanzibar; sasa huo wazari mkuu wako wa JMT uko wapi!! Hata Rais waJMT naye pia hana madaraka yeyote kwa serikali ya Zanzibar. Na vipi Rais wa Zanzibar naye hawezi hata kumkemea naibu waziri wa JMT. Tangayika anayoibeza Pinda na ccm ni sawa na kulikataa jina la baba yako la ukoo kwasababu kabatizwa au kaslimu akaitwa Joseph au Said jina la Kayanza ulikatee!!!

Ni kweli Zanzibar ni wajanja zaidi wao chao ni chao tu lakini cha Tanganyika ni cha wote
 
Ningemsifu ka ma angeuliza swali hilohilo kwa Zanzibar. Unafiki ni mbaya sana. Anawaogopa?
PInda hana ubavu kuzungumzia Zanzibar pumba hiyo, anajua historia ya matokeo ya uropokaji wake kuhusu Zanzibar, ungedhania hajasomea sheria. Labda ndio madhara ya elimu zetu katika shule za Bongo. Ndio maana waccm wamepelekwa wengi sana bungeni ili kuhakikisha serikali mbili inaendelezwa. Hata katika kura ya wananchi watatumia nguvu za dola kuipitisha hoja ya serikali mbli na hapo ndipo katiba mpya itakapojilikana kama katiba ya ccm. Hawajui hilo au wanajua lakini hawajali. Watakapokuwa wao ndio wapinzani kama Zambia na Malawi watalialia kama watoto wadogo vibao vitakapogeuka.
 
Mawazo ya kijinga kabisa haya. Cha ajabu hayatoki kwa mjinga! Pathetic
 
Mheshimiwa kateleza tena,safari hii kaitelekeza Tanganyika badala ya Zanzibar, hay a sasa ni zamu ya Watanganyika kusema au kuteta na jamaa yao ,naona kwa hili ni bora akabwaga manyanga na kujiuzulu.
 
Kung'ang'ania mfumo wa serikali mbili ni janja ya watanganyika kuitawala zanzibar kijanja! Mfano watanganyika wanatumia bunge la muungano kwa manufaa ya tanganyika badala ya tanzania! Watanganyika wengi wanajifanya kutetea serikali mbili kwa lengo la kuikandamiza zanzibar na si vinginevyo!

Tunataka Serikari Moja tu yaani Zenji atawale Gavana Pia Bara atawale Gavana kisha Rais mmoja tu akae Dodoma ili kupunguza foleni jijini kupisha misafara
 
Hawa wazee Nape alisemaje tena:bump2:?
 
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba anayetamka maneno haya ni waziri mkuu ambae anajua wazi kwamba hana hata mamlaka ya kwenda kukagua miradi ya maendeleo zanzibar. Kwa maana nyingine, zanzibar haimtambui waziri mkuu ingawa anaitwa "waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania"; Hivi ameshindwa kabisa kugundua kwamba kinachombeba ni koti analozungumzia jaji warioba (Tanganyika)?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Hivi Pinda ni Waziri Mkuu wa serikali ipi? Wa Tanzania Bara au Jamhuri ya muungano wa Tanzania? Kama ni wa JMT, mbona hana mamlaka ya kwenda kufanya ziara au kukagua miradi ya maendeleo kwenye upande mwingine wa jamhuri ya muungano wa Tanzania (zanzibar)? Je hii haitoshi kumwelimisha kwamba yeye ni Waziri Mkuu wa muungano uliovishwa koti la Tanganyika?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
zanzibar iwe nchi huru na Tanganyika iwe kivyake
na mm huo muungano tangu uwepo cjaona la maana zaidi ya kuwapora wazanzibar
 
Pooor Pinda. kweli hii nchi ina viongozi mizigo. uwezo wake na akili yake na uzoefu wake ameweza kuchambua off-points kama hizi. kweli tuna kazi. Kwanza hafahamu kwamba muda ni kitu muhimu katika kila jambo. Ni vigumu kuwashawishi watu waamini jambo ambalo limeshindwa kurekebishika kwa miongo mitano au nusu ya karne, halafu utuambie bado linazungumzika. Ukweli ni kuwa sisi kizazi kipya tunaona muungano hauna maslahi tena na kwa hakika umepitwa na wakati. istoshe muungano unatokana na pilika pilika za vita baridi vya wakati ule ambapo wababe wa vita ile walishasahau na athari zake zote zilishafanyiwa marekebisho makubwa. rejea ukuta wa Berlin na kuvunjika kwa USSR au Soviet Russia na reforms au mageuzi yaliyofanika China. Watu wengi wa aina ya Mtoto wa Mkulima wanaogopa mabadiliko kwa vile; mosi, wanafaidika na mfumo wa hovyo uliopo na hawana uhakika iwapo wata-sustain ulaji iwapo mabadiliko yatatokea. pili, watu wengi hawana taaluma ya kuona mambo ya mbele au jamii yetu haina taasisi za kufanya strategic studies ambazo huweza kufanya prdictions kuhusu expected outcomes for any reforms in 50 to 100 years ahead. Kwa hiyo katika hali ya kila kitu kwenda gizani ndio maana kina Pm na nyinyiem yake wanaogopa mabadiliko.

nitawapa mfano, nchi ya China ambayo leo ni tishio kwa uchumi wa dunia, baada ya kuwa na uchumi wa kijamaa kwa miaka 30 tokea 1948 baada ya mapinduzi ya kizalendo, walifanya utafiti na kuona iwapo mfumo ule ulikuwa sahihi na iwapo ungewapeleka kuwa China ya karne ya 21. Ile study iligunduwa kuwa China ilikuwa na nafasi kubwa ikiwa mabadiliko makubwa yangefanyika na ndani ya mika 50, mabadiliko yale yangeifanya kuwa uchumi mkubwa wa dunia. mwaka 1978, bila kusita, China ilifanya mageuzi makubwa ya kiuchumi, kutoka uchumi wa kijamaa kwenda uchumi wa soko. Miaka thelathini baadaye, nyote ni mashahidi. kila kitu, whether uko Los Angeles, Cape Town, Glasgow, au Hokkaido, MADE IN CHINA ndio habari ya mjini. si nguo, tab pc, super computer wala smart phone unayoitumia kusoma uzi huuu.

Mimi namhamsisha Mkuu Pinda na wenzake magamba, wasiogope mabadiliko, hawawezi kuyazuia. Istoshe, dunia inabadilika kila sekunde nao hawezi kuuzuia muda kwa mikono, ila ni wao kubadilika ili waendelee kuwa "relevant".

Sorry kwa post ndefu anyway.

Capital
 
Nyerere na karume waliasisi Muungano huu wa Analojia wakitarajia Kuwa Muungano utakuwa ukiboreshwa kulingana na wakati kisha Lengo Lao lije Litimie yaani Serikari Moja tu ( muungano Digtal ) lakini Lengo limekuwa Kinyume sasa ni Miaka 50 muungano upo vile vile Analojia huku Wajanja wakijipatia Pesa kupitia Bajeti za Wizara ya Muungano kwa kisingizio eti ni pesa za kutatua kero za muungano na hii pesa imewafanya wajanja waendelee kung'ang'ania Serikari mbili ili waendelee kuneemeka na Pesa za Vipofu wa Tanga nyika .yaani hadi sasa matokeo ya Kufaidi matunda ya muungano ni 7 - 0 yaani Zanzibar anaongoza kwa 7 -0 ya Tanganyika kwa kweli Zenji wamejipanga vizuri sana wana Aridhi ndogo na watu wachache lakini wana wabunge wengi na viongozi wengi sana wanaofaidi pesa za Hazina kisha wanasimama na kulalamika kwa speed ya radi huku Tanganyika ikilea muungano kwa mamilioni pasipo kujielewa
 
Mimi naona jambo la muhimu kwa sasa ni kuangalia upya mfumo huu wa serikali mbili na kuufanyia marekebisho lakini mfumo wa sijui serikali Tatu,Nne ,Tano Mara shirikisho ni kujiongezea matatizo yasio ya msingi

MUNGU aliembinguni atusaidie,Muundo wa sasa una walakini lakini suluhisho sio serikali tatu,mie najiuliza kwanini Tume imetoa mara mbili hili swala????Tume umeleta serikali tatu umeleta posho nzito,wewe Tume wewe...Tuangalie tu sie wananchi
 
zanzibar iwe nchi huru na Tanganyika iwe kivyake
na mm huo muungano tangu uwepo cjaona la maana zaidi ya kuwapora wazanzibar

Sioni cha kupora huko Zanzibar! Au yale mafuta ya kujipaka?
 
Mamlaka ya "nchi" ya Zanzibar sio absolute (not a sovereign state)! We muulize Ban Ki Moon kuwa kuna "nchi" inaitwa Zanzibar kama hatavunjika mbavu kwa kicheko! Ila nikimuuliza Maalim Seif kama kuna "nchi" ya Zanzibar atanikunjia uso kama unavyofanya wewe hapa mtandaoni!
Ila ukweli, hata kama utawauma kiasi gani, Zanzibar is NOT a sovereign state! Kuwa sovereign state hakuletwi na wording ya Katiba ya Nchi bali status ya entity katika International Law! Ukiwa na mentality hiyo tuko pamoja, ila ukiwa na mentality ya ki-maalim Seif, hapa tutakesha!

Ni kitu kigumu kwa mtu au kiongozi kujitangazia kwenye eneo lake kuwa ana nchi na eneo la mipaka kisha kuwa na vikosi vyake vya ulinzi,katiba,bunge,bendera,mahakama,wimbo wa taifa n.k,hebu nambie mkoa gani huko tanganyika unaoweza kufanya hivyo?kwa akili za kawaida tu unapata picha kuwa hao jamaa wanaojitangazia kuwa ni nchi kuwa hawataki muungano,zanzibar kwanza.
 
Cha kusikitisha zaidi ni kwamba anayetamka maneno haya ni waziri mkuu ambae anajua wazi kwamba hana hata mamlaka ya kwenda kukagua miradi ya maendeleo zanzibar. Kwa maana nyingine, zanzibar haimtambui waziri mkuu ingawa anaitwa "waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania"; Hivi ameshindwa kabisa kugundua kwamba kinachombeba ni koti analozungumzia jaji warioba (Tanganyika)?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Sasa kama hamumtambui kauli zake zinawauma nini, mnakula posho za Bunge la Katiba huku hamumtambui anayewapa posho! Wazenj watu wa ajabu sana!
 
Hivi Pinda ni Waziri Mkuu wa serikali ipi? Wa Tanzania Bara au Jamhuri ya muungano wa Tanzania? Kama ni wa JMT, mbona hana mamlaka ya kwenda kufanya ziara au kukagua miradi ya maendeleo kwenye upande mwingine wa jamhuri ya muungano wa Tanzania (zanzibar)? Je hii haitoshi kumwelimisha kwamba yeye ni Waziri Mkuu wa muungano uliovishwa koti la Tanganyika?



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums

Ofisi ya waziri Mkuu ipo Tanganyika tu kule Visiwani Hana Ofisi kule kuna Makamu wa Rais wawili mmoja anaact Kama waziri Mkuu kimtindo hv lakini kiujumla Pinda Pale Zenji hapagusi ni Kama Magufuri hagusi miladi ya Barabara za Zenji ingawa yeye wakati wa Bunge la Bajeti Dodoma wabunge wa Zenji hukaa kwenye vikao na kuvuta posho kwenye vikao vya Wizara ambazo si za muungano lakini Hakuna Mbunge wa Bara ananusa Bunge Lao la zenji ambalo ni kubwa sana japo Aridhi Yao ni ndogo lakini wao wanawachuna buzz watanganyika kupitia Utitiri wa Viongozi kisha wanafurumusha malalamiko kibao ili kuwasahaulisha haraka
 
Mheshimiwa kateleza tena,safari hii kaitelekeza Tanganyika badala ya Zanzibar, hay a sasa ni zamu ya Watanganyika kusema au kuteta na jamaa yao ,naona kwa hili ni bora akabwaga manyanga na kujiuzulu.

Mkuu safari hii PM hajateleza, anamaanisha anachosema na of course ni msimamo wa Chama!
 
Mheshimiwa Pinda ameshindwa kabisa kutambua kwamba, moja wapo ya kero za muungano ambazo ni lazima zitatuliwe ni kero ya "Serikali Mbili". Kulingana na mimi, hii ndio kero mama ambayo inazaa kero nyingine nyingi. Bila kutatua hii, wasitarajie Watz kutosheka na hali itakavyokuwa. Kama wanaona serikali tatu itavunja muungano, basi wafanye serikali moja ili tujue kabisa kwamba hakuna Tanganyika wala Zanzibar, bali Tanzania pekee. Hii mambo ya kutuambia hakuna Tanganyika, bali kuna Zanzibar na Tanzania ni kitu kilichopitwa na wakati.
 
Ni kweli Zanzibar ni wajanja zaidi wao chao ni chao tu lakini cha Tanganyika ni cha wote

Hawana ujanja wowote ni makosa ya CCM kuendelea kubishia hoja ambayo kwa zaidi ya miaka 30 wanabisha wakati jibu lipo.
 
Back
Top Bottom