Sheikh Ponda: Jamii ya sasa inataka Tanganyika iwepo.

Sheikh Ponda: Jamii ya sasa inataka Tanganyika iwepo.

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
5,614
Reaction score
21,303
Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania leo Septemba 07, 2026, Sheikh Issa Ponda amesema suala la muungano linahitaji kufanyiwa maridhiano.

"Kwa hivyo, jamii ya sasa, ndio hata tunapozungumzia G55, wao wanataka angalau hata hiyo nadharia iliyoelezwa ionekane, kwamba Tanganyika iwepo. Matarajio kwa mujibu wa nadharia hii ilikuwa ni lazima tuwe na ikulu tatu, tuwe na ikulu ya Zanzibar ambayo yuko Rais mzanzibari mzanzibari halisi, anakusanya kodi Zanzibar anaijenga Zanzibar, na tuna ikulu ya Tanganyika ambayo yuko Rais halisi Mtanganyika, anakusanya kodi Tanganyika anaijenga Tanganyika, halafu kwa pamoja hizi nchi mbili zinachangia katika kuendesha ile serikali ya muungano. Haipo. Hiki ndicho ambacho kizazi cha sasa kinafikiria juu ya suala zima la muungano, angalau ingekuwa na sura hiyo."


Source: The Chanzo
 
Kwenye ikulu ya Zanzibar na mzanzibar halisi, ikulu ya Tanganyika na mtanganyika halisi imekaa poa sana ila ikulu ya tatu kwa lugha nyingine muungano mkono wa thank you itapendeza.
 
Anaongea ukweli kabisa, mgogoro wa Urusi na Ukraine sababu yake ni kama hayo anayoongea shekhe Ponda, Rais wa Muunganiko wa Soviet wakati huo 1954, Bwana Nikita Khrushchev Ambaye ana asili ya Ukrane , alichukua eneo la Urusi Liitwalo crimea na kulihamishia kwao ukraine , sasa baadae baada ya muunganiko kuvunijka , krimea ikaenda ukraine na urusi wanataka Eneo lao ndo kisa cha vita kati ya ukrane na Urusi. Mambo anayofanya Samia siku akiingia mtanganyika atayadai, huko kuuza mbuga, ufisadi wa hela za tanganyika, watazitapika, mifano tunayo ya umoja wa soviet.

Machungu waliyonayo watanganyika ipo siku yataisha na yatalipiwa
 
Akizungumza katika mkutano ulioandaliwa na Kituo cha Demokrasia Tanzania leo Septemba 07, 2026, Sheikh Issa Ponda amesema suala la muungano linahitaji kufanyiwa maridhiano.

"Kwa hivyo, jamii ya sasa, ndio hata tunapozungumzia G55, wao wanataka angalau hata hiyo nadharia iliyoelezwa ionekane, kwamba Tanganyika iwepo. Matarajio kwa mujibu wa nadharia hii ilikuwa ni lazima tuwe na ikulu tatu, tuwe na ikulu ya Zanzibar ambayo yuko Rais mzanzibari mzanzibari halisi, anakusanya kodi Zanzibar anaijenga Zanzibar, na tuna ikulu ya Tanganyika ambayo yuko Rais halisi Mtanganyika, anakusanya kodi Tanganyika anaijenga Tanganyika, halafu kwa pamoja hizi nchi mbili zinachangia katika kuendesha ile serikali ya muungano. Haipo. Hiki ndicho ambacho kizazi cha sasa kinafikiria juu ya suala zima la muungano, angalau ingekuwa na sura hiyo."
View attachment 3665226

Source: The Chanzo
Huyu sheikh yuko smart sana
 
Back
Top Bottom