Mimi sina chama, halafu hapa ndiyo watanzania tunaonyesha unafiki wetu, watawala ni wachache sana watanzania wamefanya jitihada gani kuidai Tanganyika yao, hili suala mpaka viongozi wa dini wanapingana nalo kwa maslahi yao haujamsikia Pengo?Watawala kutoka chama chako cha CCM wameshindwa kusoma alama za nyakati kwasababu Tanganyika haizuiliki ni kama mafuriko. Mpaka sasa wanapinga bila hoja zozote za msingi ambazo wanaweza kutuonyesha wenye akili kwamba sasa tumepata mworobaini wa kero za muungano.
Ritz msaidie chama chenu kujiondoa ktk aibu ambayo itakuja kukiandama ktk uhai wake wote. Toka 1984 mpaka leo hakina majibu ya kero za muungano lakini bado wanalazimisha hata kutuchafulia Katiba yetu mpya!
Kama swala ni kupunguza gharama na kuimarisha umoja wetu, kwa nini tusiwe na serikali moja? Mbona ccm hawaongelei kuhusu serikali moja?
Kama Tanganyika haitarudi na zikabaki serikali mbili baada ya kua moja nafikiria kudai Uhuru wa visiwa vya Ukerewe kutoka kwa wakoloni wa kitanzania. Wanaokubaliana nami wanipe like ili baadae tuweze kujadiliana jinsi ya kupata Uhuru wa UKEREWE.
Nilichogundua mpaka sasa hivi viongozi wa tanzania (bara) na viongozi wa tanzania visiwani (zanzibar) wote kwa pamoja wanahofia kupoteza nguvu za kimadaraka na utawala.
Tanzania Bara wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.
Tanzania visiwani wengi wao wanataka serikali tatu lakini viongozi wao hawataki wanataka serikali mbili.
Kinachosikitisha hawa wananchi hawana nguvu za vitendo wana nguvu za maneno.
Tanganyika ni zao la Mjerumani (mambo ya Tanganyika Mandate na Baadaye Tanganyika Territory). Alipokuja Mwingereza akachukua hiyo kitu Tanganyika mpaka alipomkabidhi Julius, ambaye alipoona nchi "haitoshi" akaamua "kuiongeza" kidogo na kuipa jina jipya! Hongera sana Mwaaaaalim (RIP) kwa ubunifu! Wengine wanakuonea wivu tu, hamna lolote!
dahhhhh......yani hadi hapo nimeona kuna haja ya pinda kukaa na kupitia upya alicho kisema.....baada ya hapo kama tutakuwa na serikali mbili ma pemba nao wakae kudai uhuru wao uliopotelea mikonini mwa unguja...
serikali tatu kiboko
Ulishasema Zanzibar siyo nchi, sasa ungetaka tukuelewe ungesema ni MUUNGANO wa serikali moja wala tusingekuuliza TANGANYIKA tunayoitaka
ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ha ah ah haaaaaaaah, mkuu umenichekesha sana hapa, kwa hiyo teacher hapa alikuwa mjanja sana, labda wenye kipande chao washagutuka ndo maana wamekomaa kukitaka
Pinda kama unataka selikali mbili tuambie na majibu haya mbona zanzibar kwenye katiba yao wameainisha kuwa zanzibar ni nchi, wana wimbo wao, bendera yao, katiba yao inaruhusu wazanzibari ndio wanahaki ya kumiliki ardhi tu? Sasa tanganyika haina katiba, wimbo, bendera huu ni muungano gani? Hivi ni vizazi vingine tunahitaji majibu