Mitaa korofi na hatari mikoani

Iringa... Kitanzini
Songea....Lizaboni
Mwanza ..... Sahara,mabatini,pasiansi
Mbeya ...nonde makaburini
 
Sultan Area sio kiivyo, Vibandani siku hizi pamekuwa na unafuu kidogo ingawa zamani palikuwa hakupitiki usiku. Hiyo barabara ya kwenda Moro hotel nilishawahi kukabwa maeneo ya uwanja wa gofu walikuwa kama saba hivi, wale vibaka karibu wote nilikuwa najuana nao ila wao hawakunitambua usiku huo nikiwa natoka mazoezini, walichukua wallet iliyokuwa na IDs, kesho yake waliniletea wenyewe vitu vyangu bila hata kuwatafuta. Huwa nawalinda sana na hizi mia mbili mia mbili wakiwa na njaa zao, ndio maana sikupata tabu ya kupata vitu vyangu.
 
Makambako -Ubena huku ndiko nondo zilikozaliwa !!
 
Kwa kura za harakaharaka mwanza inaongoza ikifuatiwa na Arusha.

Mmh, Arusha every street is potentially unsafe. Sehem yoyote tu unaweza ukageuzwa firigisi anytime, kuna namba zina roho ngumu sijaona, toka kitambo, mi nikienda Arusha , usiku mguu sawa staki kabisaa mazoea
 
Kwa arusha kuna matejoo, ngarenaro, eso,ungalimited,daraja mbili bila kusahau kwa mworombo wezi wa bodaboda

Daaaah umenikumbusha mbali sanaaaa morombooo pale daaah acha tuuuu
 
Siku moja msomali mmoja alitekwa njoro ya Pepsi kule Moshi alipiga karate walikimbia na pikipiki wakaiacha
 
Arusha ungalimited ni nouma kabisa ikifika saa kumi jion pesa cm unaacha kwenye jiwe moja maarufu sana. Na sanawari eneo maarufu mbwa chini
 
mbezi beach dar es salaam ni hatari sana!...unakuta mzee anakaa jumba kubwa ukiona kibinti kinaingia humo ujue kinaenda kutatuliwa marinda!....kwingine ni masaki na oysterbay maeneo ya coco beach
 
Enzi hizo Shinyanga mjini kulikua na mtaa unaitwa Fanta, hapo kulikua na kundi la vijana ambalo lilisumbua sana mji.
Jamaa walikua na timu yao inaitwa Fanta Sc, ilikuwa vizuri sana.
Sidhani kama siku hizi bado wana hizo mambo, mana wengi wa wale jamaa ni either wachezaji, viongozi, mashabiki, au wamiliki wa Stand United inayoshiriki Ligi Kuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…