Mishahara ya Marais wastaafu ipunguzwe

Mishahara ya Marais wastaafu ipunguzwe

Hata kama hujasoma hesabu ama hisabati, tumia akili ndogo tu hii ifuatayo. Kwa mjibu wa TRA, kuna miezi makusanyo huishia milioni 800, ukitoa milioni 400+ ya rais aliye madarakani tu, unapata salio la milion 300+, hapo hujawalipa marais wastaafu, mawaziri wakuu wastaafu, waziri mkuu aliye madarakani na wastaafu wengine, je maendeleo ndiyo kusema yatategemea misaada tu?
Dyu!!!
 
Nilipata kuwa somewhere nikapata kuliweka hilo mbele ya wadau nikiwaambia mshahara wa prezida tz ni zaidi ya mil400 mbali na posho mbali na overtime hapo... Huwezi kuamini walin'gaka wengine wakaniambia kiasi hicho hakipo raisi analipwa mil arobaini na tano.
45m amekua coach wa team ya Taifa???
 
NI HAKI YAO ACHA WALIPWE.WEWE MTOA MADA NAZANI HUJAWAHI CHIMBA HANDAKI TOKA UZALUWE TUULIZE WENZIO VITA IKO KAGERA SISI TUNACHIMBA MAHANDAKI MTWARA.WAMEFANYA KAZI KUBWA HAO MARAIS YA KUTULINDA.LEO WATANZANIA WENGI WANAJUA ADUI NI KIBAKA NA MAJAMBAZI TU.
 
Hakuna wa kulitumbua kwa sababu ni mfumo na wameuweka kikatiba na kisheria wa kulaumiwa ni wabunge wetu wanoitikia NDIOOOOOOOOOOO hata bila kuusema mswada.
Naunga mkono hoja , lakini pia ofisi ya chadema pale ufipa ni mbaya mno napendekeza Mbowe apunguziwe mshahara, pia na ile kodi aliyopata baada ya kuuza chadema kwa lowasa nayo iwekwe wazi ili chama kijenge ofisi nzuri.

Ni aibu chama kina miaka 24 lkn ofisi yake utafikili ni bafu.



Wenu kinda la chadema
 
mgodi usishangae, kama viongozi ndio hao wanaingia madarakani wakiwa na umri wa miaka 55 inakuwaje kama kila miaka mitano anaingia mwingine na huyo aliyetoka madarakani akiwa na miaka 60 anakuja kuishi mpaka miaka 90 kama mzee Ruksa? Ni kwamba utafika wakati mna Rais na wastaafu kama 8 ambao mnawalipa 80% ya stahili zote za aliyeko madarakani. Kumbuka pamoja na stahili hizo mnazowapa wengine walisha tuumiza mfano migodi, makontaina, gesi nk nk
 
Hiyo ml 460 nina mashaka nayo. Hesabu kidogo, 80% ya ml 460 ni ml 368. Chukua ml 368 zidisha kwa marais watatu wastaafu walio hai unapata 1.104 trilioni, kisha jumlisha na ml 460 ya rais aliyepo madarakani unapata 1.564 trilion. Makusanyo ya mwezi yakizidi sana ni Trilioni 1.3, ambayo iko chini ya mishahara ya marais hao. Je, makusanyo yote ndiyo kusema huishia kwenye kulipa mishahara ya marais? Acheni usengerema.
Shukrani kwa Ufafanuzi,nilishangaa hii inaingia akilini kweli?
 
Hiyo ml 460 nina mashaka nayo. Hesabu kidogo, 80% ya ml 460 ni ml 368. Chukua ml 368 zidisha kwa marais watatu wastaafu walio hai unapata 1.104 trilioni, kisha jumlisha na ml 460 ya rais aliyepo madarakani unapata 1.564 trilion. Makusanyo ya mwezi yakizidi sana ni Trilioni 1.3, ambayo iko chini ya mishahara ya marais hao. Je, makusanyo yote ndiyo kusema huishia kwenye kulipa mishahara ya marais? Acheni usengerema.
mkuu kichwa chako ukitoka million unaenda trillion, billion haipo kichwa mwako piga vizur hesabu.
 
NI HAKI YAO ACHA WALIPWE.WEWE MTOA MADA NAZANI HUJAWAHI CHIMBA HANDAKI TOKA UZALUWE TUULIZE WENZIO VITA IKO KAGERA SISI TUNACHIMBA MAHANDAKI MTWARA.WAMEFANYA KAZI KUBWA HAO MARAIS YA KUTULINDA.LEO WATANZANIA WENGI WANAJUA ADUI NI KIBAKA NA MAJAMBAZI TU.
Tunachojaribu kukijadili hapa ni namna ya kuangalia upya mizigo isiyokuwa ya lazima kwa serikali kwa mtiririko huo wa malipo ya 80% kwa watu 3 mbali na viongozi wengine wakiwemo mawaziri wakuu n.k, unaambiwa privilege tu peke yake kwa viongozi hao watatu inatosha kabisa kuwaweka sawa maisha yao... Kama vipi walipwe kila baada ya miezi 3 basi kama siyo sita.
 
Watanzania ni watu wa ajabu wameshindwa kumpa EL nchi ni yeye pekee ndiye alisema mshahara wa rais ataupunguza sasa munalalamika nini? Acheni unafiki
 
mambo mengine ndio hupelekea taaluma nyingi hapa nchini kuwa inferior. maadam rais haombwi kuongoza taifa bali hushindana(kampeni) kuipata kama wafanyavyo wafanyakazi wengine kwenye kada mbalimbali(usahili)alitakiwa alipwe mafao yake tu kama wafanyiwavyo watz wengine. hakuna sababu ya msingi kwanini wastaafu kwenye nyadhifa nyingine waendelee kulipwa 80% ya mishahara utadhani enzi ya utumishi wao walijitolea au waliombwa kuongoza. tuondoeni huu upendeleo wa kijinga.

























































































































































]
 
Elimu Elimu Elimu! Tangu lini tshs 368 milion x 3 = 1. 104 trilion? Jibu sahihi ni 1.104 billion. Elimu elimu elimu!
 
Ilitakiwa wasilipwe kabisa mshahara baada ya kustafu ila wakiwa watumishi basi wachangie katika mifuko ya jamii,,,wakistafu ndio mifuko hiyo iwatunze wawe kama watumishi wengine
 
mambo mengine ndio hupelekea taaluma nyingi hapa nchini kuwa inferior. maadam rais haombwi kuongoza taifa bali hushindana(kampeni) kuipata kama wafanyavyo wafanyakazi wengine kwenye kada mbalimbali(usahili)alitakiwa alipwe mafao yake tu kama wafanyiwavyo watz wengine. hakuna sababu ya msingi kwanini wastaafu kwenye nyadhifa nyingine waendelee kulipwa 80% ya mishahara utadhani enzi ya utumishi wao walijitolea au waliombwa kuongoza. tuondoeni huu upendeleo wa kijinga.

























































































































































]
Formula hiyo ya kulipa marais wastaafu iliwekwa kwa mategemeo kwamba punde rais akiwa madarakani aongoze nchi vizuri bila kujitumbukiza katika ufisadi kwa kuwa ana uhakiki marupurupu yake baada ya uongozi yanamuwezesha kuishi kwa raha mustarehe. La kujiuliza ni je marais hao wamefanya kilichotarajiwa?
 
Kuweni wa kweli, Mshahara wa Raisi Tanzania hauzidi Milioni 30tsh.Unaweza fika milioni 40 au 50 kama atakua na kazi nyingi au mitoko Mingi sana.Nafikiri analipwa kutokana na utendaji wa kazi na allowance za kutosha.Kama waziri Mkuu analipwa 25Milion Sina uhakika sana hapa(Pinda aliwai Kusema) basi Raisi atakua Mara Mbili ya waziri Mkuu.
 
Back
Top Bottom