Minyukano CCM: Ushauri wa bure kwa Bashiru na wenzako kokote kule mliko

Mabibi na mabwana kwa yanayotokea huko CCM kwa wengine kina sisi, hayo ni mambo ya Ngoswe.

Hata hivyo kama binadamu ambapo wengine huwa hawana huruma, wengine tumeumbiwa na roho za huruma. Ashukuriwe mola muweza wa yote.

Ni ukweli ulio wazi kuwa mh. Dr. Bashiru, Pole pole na vigogo wengine mliokuwa vinara kwenye awamu ile, tokea kuondoka kwa mwendazake kama mlikuwa hamjui, tathmini ya utendaji wenu na hata kukubalika kwenu katika jamii ndiyo hii mnayoiona sasa.

Bila ya shaka mtakuwa sasa mmejielewa vyema na pasi na shaka yoyote. Kwamba sasa mambo ni hadharani. Hakuna cha unafiki wala nini. Hii ni timamu kabisa ndani na nje ya CCM.

Ukweli mchungu:

"Ni wazi kuwa hamkuwa mkipendwa wala kukubalika kwenye chama wala katika jamii. Mlikuwa wababe mliopitiliza, mliokuwa mmejisahau. Hamkuukumbuka hata ule usemi wa kuwa - Dunia Mapito."

Kwani ni lini basi mwenye macho alisubiri kuambiwa tazama? Au ni lini afukuzwaye aliwahi kuambiwa toka? Labda kama ni mgeni na imegonga hadi siku ya kumi!

Ukweli mchungu zaidi ni kuwa, enyi machampioni kabisa wa awamu ile katika serikali na katika CCM, hamkuwa mkikubalika kabisa, kiasi kuwa katu hamuwezi kutosha tena kwenye awamu ya sita.

"Ni vipi awaye yote aweze kuwa rafiki wa Mungu na Shetani kwa wakati mmoja? Hii ndiyo changamoto ya wazi inayowakumba sasa."

Si mnamwona wanayemwita katelefoni anavyokuwa kama kanyeshewa mvua?

Muda wa kutumia busara zenu za kisomi ulikuwa sasa, kujiengua wenyewe kwa maslahi ya nchi na chama hiki, kama kweli mlivipenda.

Zaidi sana kama kweli mnadhani mliyokuwa mnayasimamia kwenye awamu ile yalikuwa na mashiko, bora mngefikiria kuanzisha hata chama chenu cha siasa chenye agenda hizo mkapata kuendelea kuzipambania.

Wakuu, kunyong'ong'onyezwa hivi mpaka mnatia huruma hadi lini? Hamjionei huruma wenyewe? Hata hamshauriani wenyewe kwa wenyewe?

View attachment 1771352

Mbona mko wengi wa kutosha mkisheheni hadi maaskofu wafufua wafu kwenye hilo ambalo leo linaitwa kuwa ni genge lenu?

Mh. Dkt Bashiru, pole pole na timu yenu, mbona kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi?

Wapiganaji wanasema "Aluta Continua." Kazi inapoendelea, hebu mapambano na yakaendelee!

Ninawasilisha.
Kipigo kitakatifu cha 2020 bado maumivu mnayasikilizia na haya japungua. Mungu awasaidie mumtunze huyo mmoja wa Nkasi awe mbegu. Bashiru na Pole pole oyeeeeeee.
 
Mabibi na mabwana kwa yanayotokea huko CCM kwa wengine kina sisi, hayo ni mambo ya Ngoswe.

Hata hivyo kama binadamu ambapo wengine huwa hawana huruma, wengine tumeumbiwa na roho za huruma. Ashukuriwe mola muweza wa yote.

Ni ukweli ulio wazi kuwa mh. Dr. Bashiru, Pole pole na vigogo wengine mliokuwa vinara kwenye awamu ile, tokea kuondoka kwa mwendazake kama mlikuwa hamjui, tathmini ya utendaji wenu na hata kukubalika kwenu katika jamii ndiyo hii mnayoiona sasa.

Bila ya shaka mtakuwa sasa mmejielewa vyema na pasi na shaka yoyote. Kwamba sasa mambo ni hadharani. Hakuna cha unafiki wala nini. Hii ni timamu kabisa ndani na nje ya CCM.

Ukweli mchungu:

"Ni wazi kuwa hamkuwa mkipendwa wala kukubalika kwenye chama wala katika jamii. Mlikuwa wababe mliopitiliza, mliokuwa mmejisahau. Hamkuukumbuka hata ule usemi wa kuwa - Dunia Mapito."

Kwani ni lini basi mwenye macho alisubiri kuambiwa tazama? Au ni lini afukuzwaye aliwahi kuambiwa toka? Labda kama ni mgeni na imegonga hadi siku ya kumi!

Ukweli mchungu zaidi ni kuwa, enyi machampioni kabisa wa awamu ile katika serikali na katika CCM, hamkuwa mkikubalika kabisa, kiasi kuwa katu hamuwezi kutosha tena kwenye awamu ya sita.

"Ni vipi awaye yote aweze kuwa rafiki wa Mungu na Shetani kwa wakati mmoja? Hii ndiyo changamoto ya wazi inayowakumba sasa."

Si mnamwona wanayemwita katelefoni anavyokuwa kama kanyeshewa mvua?

Muda wa kutumia busara zenu za kisomi ulikuwa sasa, kujiengua wenyewe kwa maslahi ya nchi na chama hiki, kama kweli mlivipenda.

Zaidi sana kama kweli mnadhani mliyokuwa mnayasimamia kwenye awamu ile yalikuwa na mashiko, bora mngefikiria kuanzisha hata chama chenu cha siasa chenye agenda hizo mkapata kuendelea kuzipambania.

Wakuu, kunyong'ong'onyezwa hivi mpaka mnatia huruma hadi lini? Hamjionei huruma wenyewe? Hata hamshauriani wenyewe kwa wenyewe?

View attachment 1771352

Mbona mko wengi wa kutosha mkisheheni hadi maaskofu wafufua wafu kwenye hilo ambalo leo linaitwa kuwa ni genge lenu?

Mh. Dkt Bashiru, pole pole na timu yenu, mbona kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi?

Wapiganaji wanasema "Aluta Continua." Kazi inapoendelea, hebu mapambano na yakaendelee!

Ninawasilisha.
Nimegundua humu tuna watoto wadogo sana ama akili ni ndogo za kuwaza au wavivu wa kufikiria. Bashiru alitolewa kwenye Chama na kupelekwa serikalini. Hakuna namna Bashiru angerudi kuongoza Chama. Samia kampeleka Bungeni. Nini shida hapo? Polepole aliteuliwa kuwa Mbunge. Baada ya uteuzi alikuwa anasubiri mtu ateuliwe kuja kuchukua nafasi yake ya Uenezi. Nafasi ni kwamba Mtu mmoja nafasi moja. Walishatolewa kufanya kazi za Chama. Alikuwa anataftwa katibu mkuu wa chama pamoja na mwenezi. Mbona watu mna nongwa? Wenzio wapo Bungeni na wamekitumikia Chama wamepambana sana. Hata Mungu akiwachukua leo wamefanya jambo na jamii inaona. Wewe unayeandika haya bila kufikiria umefanya nini? Kiufupi kama ni Maslahi Bashiru na Polepole wanapata zaidi kuliko walivyokuwa wanapata ndani ya Chama kama Malipo ya kazi. Tutumie akili muda mwingine. Ni sawa sasa kwa level yangu nianze kumnanga Mbowe wakati Mbowe ka achieve mengi. Ingekuwa unawasema kwenye masuala ya hoja sawz lakini huu udaku unakupunguzia hadhi.
 
Bashiru aliisaliti taaluma yake kisa ni njaa. Sidhani kama anaweza kutoa mhadhara wa kisomi na akaeleweka leo kama zamani. From critical thinker to compromise thinker!
mwenzio anapiga mshiko. Angebaki katika taaluma asingepata hayo. Lakini pia alikuja ku practice politics. Mmuache Bashiru
 
Nimegundua humu tuna watoto wadogo sana ama akili ni ndogo za kuwaza au wavivu wa kufikiria. Bashiru alitolewa kwenye Chama na kupelekwa serikalini. Hakuna namna Bashiru angerudi kuongoza Chama. Samia kampeleka Bungeni. Nini shida hapo? Polepole aliteuliwa kuwa Mbunge. Baada ya uteuzi alikuwa anasubiri mtu ateuliwe kuja kuchukua nafasi yake ya Uenezi. Nafasi ni kwamba Mtu mmoja nafasi moja. Walishatolewa kufanya kazi za Chama. Alikuwa anataftwa katibu mkuu wa chama pamoja na mwenezi. Mbona watu mna nongwa? Wenzio wapo Bungeni na wamekitumikia Chama wamepambana sana. Hata Mungu akiwachukua leo wamefanya jambo na jamii inaona. Wewe unayeandika haya bila kufikiria umefanya nini? Kiufupi kama ni Maslahi Bashiru na Polepole wanapata zaidi kuliko walivyokuwa wanapata ndani ya Chama kama Malipo ya kazi. Tutumie akili muda mwingine. Ni sawa sasa kwa level yangu nianze kumnanga Mbowe wakati Mbowe ka achieve mengi. Ingekuwa unawasema kwenye masuala ya hoja sawz lakini huu udaku unakupunguzia hadhi.

Watoto hao unaowaongelea CCM nako wapo? Au hawa nao ni wakubwa wenzio?

IMG_20210502_111926_138.jpg



Hawa nao je? Ni wakubwa wenzio?

IMG_20210502_112021_041.jpg



Nyuso zao je? Nazo hazikufumbui lolote?

IMG_20210501_130541_775.jpg


Ni uzwazwa kudhani mnaweza wadanganya watu wote siku zote. Bashiru, pole pole na genge lao walilikoroga awamu ya tano. Sasa wanavuna walichopanda.

Huu ulikiwa ushauri kwao binafsi. Labda kama wewe ni Bashiru au Polepole au mshirika katika genge lao.

Tumekuwa wazi vilivyo ya Ngoswe (CCM) yatuhusu sisi wengine vipi?

Awamu ya sita haikubaliani na yao ya awamu ile. Kama waliyosimamia yalikuwa na mashiko taabu gani kuendelea kuyapigania?

Pamoja na kutoyaona au kuyafumbia macho yote hayo ninashawishika kukuona kuwa, wewe ni kubwa zima lenye akili za kitoto.

Mwendazake alipenda kusema, "mtanzania wa leo mbona si yule wa jana?"

Au nasema uongo ndugu zangu?

Hiiiiii bagosha!
 
Mwacheni Mwl. Balozi Bashiru amalize kwanza majonzi ya msiba wa kipenzi chake. Bado anamachungu. Kidonda hakijapona.
Mimi ukiachia mambo mengine yote ya hovyo aliyoyafanya Bashiru dhidi ya watanzania kwa lengo la kumfurahisha Mwenda zake, ikiwemo kauli yake kuwa watatumia dola kubaki madarakani.

Kubwa zaidi ni lugha na maneno yake ya kejeli dhidi ya Lissu kwa tukio lililompata kwamba eti Lissu anadeka.

Yaani kweli hawa watu kiburi cha uzima na madaraka viliwalevya sana.
 
Bashiru haamini kili hotokea kama kukufurualishakufuruuu.....haamini ukuu Mungu anaona anaota hadi leo change over ( change kota) .....haelewiiii
bashiru ana roho mbaya sana, amenyanyasa sana watumishi wa CCM makao makuu, huku yeye anayejinasabu mjamaa akiwa anapenda rushwa
 
bashiru ana roho mbaya sana, amenyanyasa sana watumishi wa CCM makao makuu, huku yeye anayejinasabu mjamaa akiwa anapenda rushwa

Kwa tathmini kama hizi kwa watendaji hawa wa awamu ile bado hamsikii tu? Wajameni, hamtufai!

Mmekomaa kama luba bado, au mpaka mtumbuliwe au kufurushwa kwa fedheha?

Cc: mparamagamba, katelefoni, bashiri, pole pole na dream team yote inayounda lile genge lenu pendwa la wasukuma uchwara wa imani.

Hiiiiii bagosha!
 
kuna watu walikuwa wanaserereka tu utafikiri wamepanda treni ya mwendokasi, leo katibu mkuu wa chama, kesho katibu mkuu kiongozi utafikiri nchi ilikuwa mali yao binafsi..
Hiyo kawaida,kila zama/utawala kuna watu watapeta wengine wataumia

Ova
 
Kwani mkuu wale vijana wanaowahamasisha kila leo kujiajiri, kwani wao wanaishi je?

Hawa watu mbona tayari wako vizuri tu?
Na ndio msemo wao huo,wakati wao wanang'ang'ania kwenye nafasi ambazo hawafit, kiufupi hawana uwezo wa kupambana huku mtaani,ni sawa na samaki akitupwa nchi kavu lazima afe
 
Leta ushahidi wa uharibifu wao hapa. Naomba ulete hapa wana Jamvi wauone. Hizi zote ni chuki binafsi hizi.

Mwingine huu hapa:

IMG_20210503_083816_092.jpg


Ukihitaji mwingine sema. Kukuongezea mwingine "itapendeza zaidi." - Dr. Shika.
 
Back
Top Bottom