Minyukano CCM: Ushauri wa bure kwa Bashiru na wenzako kokote kule mliko

Mabibi na mabwana kwa yanayotokea huko CCM kwa wengine kina sisi, hayo ni mambo ya Ngoswe.

Hata hivyo kama binadamu ambapo wengine huwa hawana huruma, wengine tumeumbiwa na roho za huruma. Ashukuriwe mola muweza wa yote.

Ni ukweli ulio wazi kuwa mh. Dr. Bashiru, Pole pole na vigogo wengine mliokuwa vinara kwenye awamu ile, tokea kuondoka kwa mwendazake kama mlikuwa hamjui, tathmini ya utendaji wenu na hata kukubalika kwenu katika jamii ndiyo hii mnayoiona sasa.

Bila ya shaka mtakuwa sasa mmejielewa vyema na pasi na shaka yoyote. Kwamba sasa mambo ni hadharani. Hakuna cha unafiki wala nini. Hii ni timamu kabisa ndani na nje ya CCM.

Ukweli mchungu:

"Ni wazi kuwa hamkuwa mkipendwa wala kukubalika kwenye chama wala katika jamii. Mlikuwa wababe mliopitiliza, mliokuwa mmejisahau. Hamkuukumbuka hata ule usemi wa kuwa - Dunia Mapito."

Kwani ni lini basi mwenye macho alisubiri kuambiwa tazama? Au ni lini afukuzwaye aliwahi kuambiwa toka? Labda kama ni mgeni na imegonga hadi siku ya kumi!

Ukweli mchungu zaidi ni kuwa, enyi machampioni kabisa wa awamu ile katika serikali na katika CCM, hamkuwa mkikubalika kabisa, kiasi kuwa katu hamuwezi kutosha tena kwenye awamu ya sita.

"Ni vipi awaye yote aweze kuwa rafiki wa Mungu na Shetani kwa wakati mmoja? Hii ndiyo changamoto ya wazi inayowakumba sasa."

Si mnamwona wanayemwita katelefoni anavyokuwa kama kanyeshewa mvua?

Muda wa kutumia busara zenu za kisomi ulikuwa sasa, kujiengua wenyewe kwa maslahi ya nchi na chama hiki, kama kweli mlivipenda.

Zaidi sana kama kweli mnadhani mliyokuwa mnayasimamia kwenye awamu ile yalikuwa na mashiko, bora mngefikiria kuanzisha hata chama chenu cha siasa chenye agenda hizo mkapata kuendelea kuzipambania.

Wakuu, kunyong'ong'onyezwa hivi mpaka mnatia huruma hadi lini? Hamjionei huruma wenyewe? Hata hamshauriani wenyewe kwa wenyewe?

View attachment 1771352

Mbona mko wengi wa kutosha mkisheheni hadi maaskofu wafufua wafu kwenye hilo ambalo leo linaitwa kuwa ni genge lenu?

Mh. Dkt Bashiru, pole pole na timu yenu, mbona kuvunjika kwa koleo si mwisho wa uhunzi?

Wapiganaji wanasema "Aluta Continua." Kazi inapoendelea, hebu mapambano na yakaendelee!

Ninawasilisha.
Da labda kwanza tukupe pole mtoa mada , inawezekana kabisa hujui mengi ila Daktari kayakanyaga mwenyewe mwishoni kabisa kwa kuonyesha nia ya kuisigina katiba ili aurithi ufalme, yaani kama Mchonga angekuwa presidaa daktari saa hizi alitakiwa awe detention kama Shekh Jumbe. Mama ana dini kaona kiroho safi wampeleke mjengoni.

Hawa watu ni wakatili sana kuliko unavyojua na ungewajua hawatakiwa hata kutajwa manake jalali ndio ameamua kuwe na mabadiliko haya baada ya kuona nafsi katili za viumbe hawa.
 
Mwingine huu hapa:

View attachment 1772301

Ukihitaji mwingine sema. Kukuongezea mwingine "itapendeza zaidi." - Dr. Shika.
Si Udaku wa ki blog cha Dar Mpya? Na wanaomshutumu Bashiru wengi mambo yao hayakwenda. Na kale ka mnec kaka yake alikatwa kwenye kura za Maoni. Mimi sitetei waovu hata kidogo. Wamefurahi wapi, Vyombo vya habari Vikubwa na vyenye weredi si vingeripoti? Tuache Nongwa. Bashiru aliifanya kazi yake mpaka hayati alimpotoa kwenye Chama. Wizi wa Mali za Chama ulizidi mno. Mpaka Chama kilikuwa kinashindwa kulipa Mishahara ya wafanyakazi wake. Ni aibu. Tumelogwa na nani kuwachafua wale wanaofanya mageuzi katika taasisi mbali mbali?
 
Si Udaku wa ki blog cha Dar Mpya? Na wanaomshutumu Bashiru wengi mambo yao hayakwenda. Na kale ka mnec kaka yake alikatwa kwenye kura za Maoni. Mimi sitetei waovu hata kidogo. Wamefurahi wapi, Vyombo vya habari Vikubwa na vyenye weredi si vingeripoti? Tuache Nongwa. Bashiru aliifanya kazi yake mpaka hayati alimpotoa kwenye Chama. Wizi wa Mali za Chama ulizidi mno. Mpaka Chama kilikuwa kinashindwa kulipa Mishahara ya wafanyakazi wake. Ni aibu. Tumelogwa na nani kuwachafua wale wanaofanya mageuzi katika taasisi mbali mbali?

Huu nao ni udaku wa Dar ipi?

IMG_20210328_223958_589.jpg
 
bashiru ana roho mbaya sana, amenyanyasa sana watumishi wa CCM makao makuu, huku yeye anayejinasabu mjamaa akiwa anapenda rushwa
Wewe sasa ndio unafahamu, Tulidhani Karma itawashughulikia miaka ijayo, 2025 na kuendelea imekuwa mapema zaidi ya tulivyodhani.

Hahah sasa hivi watakuja tuwahudumie kama wanachama wengine tu. wanachama wa mkopo hawakupaswa kuwa viburi na wanyanyasaji vile.

KM na NKM-Bara walikuwa wakiamua tu kuwa huna uwezo wa kushika ofisi fulani basi kesho barua inakufuata, WAGENI waliokuwa wanaamua kwa midomo fulani hafai na wanamleta fulani kutoka mikoa ya mbali kushika hiyo nafasi.

Karma mkali sana, wameondolewa wote hakuna salia hata moja, Wabara tuache roho mbaya tukipata nafasi, mbona wenzetu wa visiwano hawapo hivyo?

Eti kuna mtu anasema blah blah Bashiru na Polepole hawajakomolewa na chochote sababu wamepelekwa bungeni, Hivi mnajua ni kwa kiasi gani walizipenda ofisi walikotolewa!
 
Back
Top Bottom