Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?
Mkuu hata wewe hujaokoka, au kweli umeokoka lakini hujakombolewa/uko kwenye kundi la wanaostahili maziwa(kwani umeshindwa kuchanganua jambo dogo namna hii). kama itatokea kwamba huo ni ubavu wako basi lazima umshirikishe Mungu na akupe assurance mbali na hivyo nakuhakikishia matatizo. Rudi kwenye angalia Isack alioa wapi!! au Israel alioa wapi!!! kama utaenda kinyume/sawa sawa na Neno itakuwa ndio majibu ya maswali yako yote, mtafakali Isack na Israel ukilinganisha na Samson itakusaidia.
 
Unajifanya unaijuwa sana Biblia ehehee!! Yesu alikufa msalababani kwa ajili ya dhambi zetu sasa utasemaje sisi tuache dhambu ni dhambi zipi hizo?

Na hata kama zipo kuna mlokole yeyote mwenye kipima dhambi ambacho kinaonesha hii ni dhambi na hii siyo dhambi?

Roho iliyoko ndani mwako haiwezi kukuruhuzu kuyaelewa maandiko matakatifu.
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?

mwache mtoto wa watu , utakuja kumnyanyasa tu wewe,,,,,,,,,,,,,

hapa hujamuoa umeshanza kuleta madilema.
 
ni sawa mkuu huyo dada sidhani kama hana hofu ya mungu. okey kama unawasiwasi piga goti kwa mungu muulize huyu ndiye mke wangua kwa imani yako nadhani mungu atakupa jibu.

napata mashaka kidogo kama we ni mlokole kweli uliyesimama katika neno sawa sawa, nadhani huwa mnaamini mke /mume hutoka kwa mungu basi yawezekana wewe hukumwomba mungu wakati unamtafuta huyo binti.

pili mawazo ya mwanadamu si ya mungu mrudie mungu wako anza upya na bwana katika uhusiano wako huu uone jibu la mungu ni lipi. akisema endelea fanya hivyo akisema mwache fanya ivyo katika bwana.
hivi huyu mungu wa helufi ndogo ni yupi? mbona mimi simfahamu au ulimaanisha Mungu?
 
hivi huyu mungu wa helufi ndogo ni yupi? mbona mimi simfahamu au ulimaanisha Mungu?

Ni mungu wa dunia hii ambaye ni Shetani na Ibilisi. Mungu wa herufi kubwa ndiye Mungu wa kweli aliyeumba mbingu na nchi.
 
Ni mungu wa dunia hii ambaye ni Shetani na Ibilisi. Mungu wa herufi kubwa ndiye Mungu wa kweli aliyeumba mbingu na nchi.

Asante mkuu kwani huwa inanitatiza sana mtu kuandika jina la Muumba mbingu na nchi kwa helufi ndogo wakati waisrael kuliandika jina hilo walinawa mala saba kabla hawajaliandika.
 
Mkuu, Mwalimu Mwakasege hajasoma?

Mkuu wangu nachotaka kusema hapa ni kwamba elimu inakusaidia hata kung'amua mambo madogo madogo...Sasa imagine mtu anasema akimuoa mtu wa dhehebu fulani hata enda mbinguni...? Hivi ni binadamu gani ambaye hatendi dhambi.....Hakika msomi kamwe hawezi sema upuuzi huo..
 
Watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa, hebu usiiaibishe efatha hapa, semina za vijana na ndoa kila wakati inamaana huudhurii hizo semina, basi we si mlokole mwombe mungu akupe jibu. Kujiita mlokole ni gharama, piga goti uombe sio maombi ya microwave, dakika mbili unataka jibu.
 
Mkuu wangu nachotaka kusema hapa ni kwamba elimu inakusaidia hata kung'amua mambo madogo madogo...Sasa imagine mtu anasema akimuoa mtu wa dhehebu fulani hata enda mbinguni...? Hivi ni binadamu gani ambaye hatendi dhambi.....Hakika msomi kamwe hawezi sema upuuzi huo..

Mambo ya rohoni hutambulika kwa njia ya roho. Unaweza kuwa profesa lakini kwa mambo ya rihoni ukazidiwa na ambaye hana elimu dunia.
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho? 1
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo? 2
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali? 3
je anaweza kuathiri wokovu wangu? 4
je naweza kwenda mbinguni? 5
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka? 6

kwanza unaonekana hujui nini maana ya kuokoka!!
pili hujui mambo ambayo yanamchukiza na kumpendeza mungu wako
tatu hujui msimamo wako wa maisha ya ndoa yatakuwaje
nne huna imani na wokovu wako
tano hujui njia za kwenda mbinguni
sita hujiamini na huna maamuzi ya kiimani

mwisho kabisa nenda kachukue ushauri kwa mchungaji na walokole wenzia hapa watakusumbua tu!!
 
Halafu ndugu usijisifie katika kutenda dhambi. Hiuo ni sifa ya Shetani ambaye ni mwasisi wa dhambi. Tena ni ole kwa anayewakosesha watu wa Mungu. Leo utajiona kijogoo. Lakini hatimaye itakuwa ni kilio na kusaga meno. Hujui ni lini unamaliza muda wako ukizingatia kuwa kifo hakuna kanuni. Mtu wa umri wowote aweza kufa wakati wowote. Siyo sifa kuwa jasiri katika dhambi.

Nimependezwa sana na busara zako kwa jins unavyojaribu kumwelewesha huyo aliyeteleza ulimi,hongera kwa hilo maana binaadam tumejisahau sana ktk matendo mabaya bila wenyewe kuzingatia kwamba hatujui siku wala saa.
 
hivi ukipanda na daladala na mtu asiye okoka una athilika nini?
kuna tatizo hapa katika sisi walokole ni kwamba tunaamini katika kujitenga kwetu ndio tunamwabudu MUNGU vizuri na watu wengine ni wapuuzi.
tunashindwa kuelewa kuwa watu wote wameokolewa kwa DAMU YA YESU.
tunashindwa kukumbuka kuwa wajibu wa mtu aliyeokoka ni kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wa YESU. bali tunajiona dhamira yetu kuwa wanafunzi wa YESU peke yetu na wengine hawastahili.
japo si mahala pake lakini naimani naelekezwa niyaseme haya. na wengi tutakubaliana imefika wakati walokole hata tukienda magerezani kuwatendelea wafungwa tunaenda kutoa msaada si kwa kadri na shida na mahitaji ya watu bali tunatoa kwa walokole wenzetu tu.
hii ni shida.
back to major topic
kutoka rohoni ningekushauri ni bora usimuoe kwakuwa hofu ya ndoa yako naiyona ipo kwenye uroma wake, huu unaweza kuwa mlango katika kutotulia na ndoa yako kwni hujiamini na kibaya zaidi unaonekana unataka kuingilia uhuru wake wa kuabudu bila kushiriki zaidi katika maombi na roho wa MUNGU akamwongoza.
umeweka shaka kubwa kuhusu imani yake na unaonyesha ubaguzi na hauko tayari kumtayarisha kuwa mnyenyekevu kwa MUNGU akiwa ndani ya dhehebu lake na unaamini kwako ndio kuna wokovu zaidi kwahiyo hii ni shida umekwenda zaidi na akili zako na sio roho anavyokuongoza.
hivyo ingia kwenye maombi upate kibali usije ukarudi hapa ukatusumbua ili hilo gereza la dhehebu linalokuletea hofu liondoke.
pole inawezekana nimeonekana nimekuhukumu lakini halikuwa lengo langu na MUNGU anisamhe kama nimefanya hivyo lakin lengo ni kutoa mawazo ambao pia yanaweza kuleta upana wa uchangiaji.

Very well said Chiwa

CC Kongosho Kaunga snowhite cacico
 
Last edited by a moderator:
Angalia msimamo wako juu ya wokovu wako soma warumi 12:2
maandiko yanasema kuwa usifungwe nira na wasioamini, hivyo nawe
jua kuwa wewe ni hekalu la roho mt, hivyo ukijitambua ukoje
utajua namna ya kufanya juu ya jambo hilo. UAMUZI NI WAKO

Kwa avatar nilifikiri EMT nilivyosoma post ilibidi nihakikishe kuwa huyu kweli ni EMT ninaye mfahamu ndipo nilipogundua sio. Thank God
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: EMT
hivi ukipanda na daladala na mtu asiye okoka una athilika nini?
kuna tatizo hapa katika sisi walokole ni kwamba tunaamini katika kujitenga kwetu ndio tunamwabudu MUNGU vizuri na watu wengine ni wapuuzi.
tunashindwa kuelewa kuwa watu wote wameokolewa kwa DAMU YA YESU.
tunashindwa kukumbuka kuwa wajibu wa mtu aliyeokoka ni kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wa YESU. bali tunajiona dhamira yetu kuwa wanafunzi wa YESU peke yetu na wengine hawastahili.
japo si mahala pake lakini naimani naelekezwa niyaseme haya. na wengi tutakubaliana imefika wakati walokole hata tukienda magerezani kuwatendelea wafungwa tunaenda kutoa msaada si kwa kadri na shida na mahitaji ya watu bali tunatoa kwa walokole wenzetu tu.
hii ni shida.
back to major topic
kutoka rohoni ningekushauri ni bora usimuoe kwakuwa hofu ya ndoa yako naiyona ipo kwenye uroma wake, huu unaweza kuwa mlango katika kutotulia na ndoa yako kwni hujiamini na kibaya zaidi unaonekana unataka kuingilia uhuru wake wa kuabudu bila kushiriki zaidi katika maombi na roho wa MUNGU akamwongoza.
umeweka shaka kubwa kuhusu imani yake na unaonyesha ubaguzi na hauko tayari kumtayarisha kuwa mnyenyekevu kwa MUNGU akiwa ndani ya dhehebu lake na unaamini kwako ndio kuna wokovu zaidi kwahiyo hii ni shida umekwenda zaidi na akili zako na sio roho anavyokuongoza.
hivyo ingia kwenye maombi upate kibali usije ukarudi hapa ukatusumbua ili hilo gereza la dhehebu linalokuletea hofu liondoke.
pole inawezekana nimeonekana nimekuhukumu lakini halikuwa lengo langu na MUNGU anisamhe kama nimefanya hivyo lakin lengo ni kutoa mawazo ambao pia yanaweza kuleta upana wa uchangiaji.


:amen:
da mkuu umeongea vizuri mpka natamani kurudia kusoma tena na tena!
HILI JICHO PANA HIVI KIIMANI TUNGEKUWA NALO WOTE HAKIKA DUNIA INGEKUWA MAHALA SALAMA SANA PA KUISHI!
mi mwenyewe mekupenda bure kama kina Kaunga na Kaizer
 
Last edited by a moderator:
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?
naomba nikujibu kama ifutavyo
POKEA HIVYO HIVYO HATA KAMA MACHUNGU NA UYAFANYIE KAZI!na hakika nakujibu kulingana na ulichokiandika hapa

-Ulianza mahusiano naye ukiwa HUNA PLAN YOYOTE YA KUMUOA,huoni kuwa wewe mwenyewe ni tatizo hata kabla hujaanza mahusiano na huyu dada?SO PENGINE IMANI YAKO BADO HAIJAKUSAIDIA!

-KUOKOKA ni nini?TAFSIRI YAKE NI IPI?MAWANDA YAKE NI YAPI?UNAKUSAIDIA NINI ?UNAWASAIDIA WANAOKUZUNGUKA KUWAJE?

-MUNGU ni nani kwa tafsiri yako?ANACHUKIZWA NA YEPI?ANAPENDEZWA NA YEPI?

-Maisha yako yanachangiwaje na imani yako,imani yako inachagiza kwa kiasi gani maisha yako!imani yako na maisha yako vinatengana mahali gani?

-Wokovu ni wapi na ni kwa nani?lini?kwa wakati upi?

-Njia ya kwenda mbinguni unaamini inaanzia na kuishia wapi?abiria na vyombo vya usafiri vya kwenda mbinguni ni nani na nini?Nauli je?Unayo wewe au mwenzio?

-Imani yako ni chumvi au ni maji kwenye maisha ya mwwingine
episodes NISOME KWA MAKINI THN UNIJIBU AHALAFU TUTAENDA SAWA!
 
Last edited by a moderator:
mi naamini ungeweza kupeleka hizo hoja kwa wasimamizi wako wa kiroho ingekuwa vema zaidi, kuliko kuzileta hapa, mahala ambapo shetani anapatawala kwa zaidi ya asilimia 90...(taking into consideration mitusi inayomwagwa hapa daily),.....pia, kwa jibu la swali kuwa endapo utaenda mbinguni..i guarantee you, even mwingira cant tell u that, and if he does, atakuwa ametenda dhambi ya uongo...kama unaijua biblia, utakuwa umepitia maneno ya Mungu ambayo watu kwa namna nyingi wamekuwa wakiifafanua tofauti kwa mitazamo tofauti yenye mlengo wa kupotosha, kukataza ama kutawala watu...wapo waliotafsiri baadhi ya maneno ya Bible kuwa yanatutaka tusifungamane na watu wasioamini...ila jiulize, Yesu alipokuja, alifungamana na watu wa aina gani?, je alihangaika na watu gani....Maria magdalene alikuwa mwanamke wa aina gani??, Lazaro alikuwa mtu yupi??.....Pia jiulize, wakati wa NUHU, ni yeye pekee ndiye alikuwa mwaminifu kwa Mungu, hatukuelezwa habari ya wanawe wala wakwe zake...lakini wakwe za Nuhu waliokolewa kwa imani ya Nuhu na uaminifu wa Nuhu kwa Mungu......kiufupi, Imani yako kwa Mungu, inaweza kuwa chachu ya wokovu kwa mtu utayefungamana naye.....Wakristo wote, ilimradi tunamkiri Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wa Maisha yetu, na kuwa alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, akafufuka, akapaa mbinguni, na atarudi tena kuhukumu.....basi wote tu sawa, tunatofautiana mitazamo ambayo imewekwa na binadamu kwa milengo tofauti tofauti......

brilliant I love it, stay blessed
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom