Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

mm ni nduguye wa damu
ni sisi ni matwins
hvyo usishangae sana rafiki,
bora umejisemea ili nikwambie tukoje, una lingine la kusema?
Kwa avatar nilifikiri EMT nilivyosoma post ilibidi nihakikishe kuwa huyu kweli ni EMT ninaye mfahamu ndipo nilipogundua sio. Thank God
 
Kwani unaoa dini/dhehebu au unaoa binadamu? UPENDO WA KWELI HAUZUIWI NA VITU VIDOGO KAMA HICHO NA UKIKISHINDA HICHO KIKWAZO HIYO NDIO DINI SAFI,FUNGUKA.
 
waroma pia wana charismatic kama walokole vile haina tatizo biblia si ile japo ni maamuzi ya kila mmoja sehemu atakapo penda kuasali..
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?

Mshirikishe mchungaji wako. Ila mwenye maamuzi ni wewe mwenyewe kutokana ni imani yako.

Kwa upande wangu naona si sawa kwani tofuti za kiimani zitawaletea matatizo hapo baadaye.
 
kuokoka ni kumkiri Yesu kwa kichwa chako ya kua ni Mungu..na Kuacha dhambi
wewe uko Efatha yeye yuko RC sioni kama kuna shida yoyote kiroho hapo..as long as wote mnaamini katika Mungu mmoja kwa jina la Yesu kristo hayo mengine hayawazuii nyie kua pamoja na kujenga familia..
Mkuu hapo nilipobold ni typing error au huo ndio ukweli wenyewe
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?
Kazi kweli kweli , mtoa mada kazi kwako umeomba ushauri naona wengi wamekupa ushauri sasa ni wajibu wako kusoma na kuchuja yepi yanakufaa na kuyaweka kwenye matendo. Sitii neno naweza nikawa biased sababu mi ni mkatoliki na sioni sababu ya kuongeza kwani mengi waliotangulia wameshakwambia na ni mambo mazito na mazuri kama lengo lako lilikua kutafuta ushauri basi ufuate..
 
Mambo ya rohoni hutambulika kwa njia ya roho. Unaweza kuwa profesa lakini kwa mambo ya rihoni ukazidiwa na ambaye hana elimu dunia.

Maajabu ya dunia haya...Yani wewe kunyooshea kidole mwenzako na kumuita mdhambi ni mambo ya rohoni...Seriously...!!!!! Kama mkuu wangu unakipimo cha kupimia dhambi za watu huku kikuhakikishia wewe hutendi dhambi nakiomba maana nitakinunua kwa npesa yoyote.....Wacha kujkidanganya mkuu hakuna aliye mkamilifu hapa duniani ila Baba aliye mbinguni...Wote tu wasafiri katika hii dunia yenye kila aina ya uozo ndanio ytake....Tafadhali hebu usijidanganye eti kwasababu wewe ni mtu wa rohoni..
 
Ndugu mlokole unaoa mwanamke au uroma? Oa mwanamke anayefaa. Inaonekana wewe unataka kuoa dhehebu. Kasome Mithali 31:10-31 uone aina ya mwanamke wa kuoa. Usioe dhehebu hutapata mwanamke anayefaa kwani si wote hapo kwenu (kwenye ulokole) wana tabia inayofaa. Yesu alisema imani iendane na matendo. Kusema tu mimi ni mlokole wakati matendo ni tofauti si sawa. Angalia matendo zaidi kuliko ulokole au uroma. Namjua mtu mmoja alioa mwanamke akidhani ni mlokole kumbe balaa. Hiyo ndoa ilisambaratika na huyo bwana kaoa tena baada ya kuvumilia muda mrefu. Yule mwanamke alitoroshea watoto kenya. Alihangaika sana na sikumbuki kama aliwapata wote. Mtu anaweza akajifanya mlokole ili tu aolewe au aoe akibaini kuwa ulokole ni muhimu katika mada ya ndoa. So take your time and choose a good and intelligent wife not otherwise. By the way I am also a believer!! Read James 2:14-26.
Kumuoa mtu wa nje ya imani yako ni upungufu mkubwa wa kushindwa kuhimili mikiki ya shetani na maanisha shetani anakuwa amekutawala hadi kumfikilia huyo mtu!
Kama si kanisa unalo amini wewe akibadili dini na kuja kwako kwa akili yako unafikiri amefuata dini au wewe? na kama kakuona wewe ni zaidi ya Mungu wake aliyekuwa anamwabudu unafikiri wewe anashindwa kukusaliti? au unadhani huyo Mungu wako anashindwa kumsaliti? Usiishi kwa kumtegemea mwanadamu bali bwana aliye juu mbinguni, katika jina la Yesu naomba huyo pepo mchafu aliyeyatawala mawazo yako aondoke sema Ameni!!!!!!!!!
Usimuoe shinda tamaa zako za kimwili mrejee mwokozi wako na tubu kwa kuweka hisia nje ya maandiko unayo yaamini usijilinganishe na Muumba wako yaani dunia nzima umetafuta wa imani yako umekosa?
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali Efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
je anaweza kuathiri wokovu wangu?
je naweza kwenda mbinguni?
je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?

Wewe hujaokoka, ila unamajivuno ya kubatizwa kwa kile kinachoitwa eti 'maji mengi"

Sasa nikuuliza maji yana wingi? maji ya kwenye kijiko sisimizi anaona ni bahari.

Au nijibu haya yafuatayo.
-Maji ya kwenye kisoda na ya kwenye chupa yenyewe yapi mengi?
-Maji ya kwenye chupa na ya kwenye simtank yapi mengi?
-Maji ya kwenye simtank na ya kwenye bwawa yapi meni?
-maji ya kwenye bwawa na ya kwenye bahari yapi mengi?

hao wachungaji huwa wanawadanganya ndo mana huwa mnakiburi cha kujiona hamna dhambi, wakati huenda hata huyo binti ushamchakachua kabla ya ndoa.
 
Umempenda yeye au dini yake?.....acha uzinifu kijana hapo najua tayari umeshamaliza...
 
waroma pia wana charismatic kama walokole vile haina tatizo biblia si ile japo ni maamuzi ya kila mmoja sehemu atakapo penda kuasali..

Watu wengi wakiwemo wakatoliki wanakosea sana..Wanadhani ukarismatic ni aina fulani ya upentekoste au ulokole ndani ya kanisa..na wamefikia kuact kama vichaa wa kilokole na kipentekoste..charismatic siyo na wala haifanani hata kidogo na heresy kama za kilokole na waprotestanti
 
hatujaongea hilo kwa undani,ila yupo tayari kwenda na mimi efatha

hilo sio suala la kukurupuka.
Inabidi mkubaliane strongly sana ili msije kuwekeana nira huko mbele.
Suala la imani ni la msingi sana. Asikudanganye mtu kabisa.
 
wapendwa katika bwana
nimetatizwa na kitu hapa,mimi ni mlokole nasali efatha bible,nimejaribu kuomba na ku connect na baadhi ya wapendwa wenzangu lakini nahisi sikufanikiwa
ila imekuja kutokea nikaonana na mwanamke ambaye anasali roman catholic na tumependana sana japo sikutarajia wala sikua na plan yoyote ya kumwoa
naomba ushauri kwa yafuatayo:
Kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
Je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
Je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
Je anaweza kuathiri wokovu wangu?
Je naweza kwenda mbinguni?
Je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?

mmmmmmmmm haya maswali yako kiboko, majibu sasa:
1) kuathirika kiroho kivipi?
2) sidhani kama ukiwa mlokole au mpagani ndio guarantee ya kuishi miaka mingi: Mfano, marehemu bi kidude, mugabe, kingunge ngombalemwiru.
3)wokovu wako utauharibu mwenyewe kwa matendo yako.
4) mbinguni unajipeleka mwenyewe au umeambiwa waliooana wote kwa efatha wataenda mbinguni?
5)wakati unamshawishi uwe makini unaweza ukampoteza kimoja.
 
MMIE PIA NAOMBA NIKUJIBU KAMA IFUATAVYO-
1-kama nikioa mtu ambaye hajaokoka je nitaathirika kiroho?
JE NI MADHARA AU ATHARI ZIPI NULIZIPATA KABLA YA KUWA MLOKOLE..KAMA ZIPO ZITAJE NA NINI UNADHANI KILIKUWA CHANZO?

2-je naweza kumuudhi mungu kwa hilo?
NAINGIWA WASIWASI NA ULOKOLE WAKO..MAAANA MPAKA SASA HUJUI VITU VINAVYOMUUDHI MUNGU..NA PIA KUMBUKA MUNGU WETU YU MWEMA KIASI KWAMBA YUPO PALE KUKUOKOA KILA MARA UNAPOANGUKA KATIKA DHAMBI NA UKIMWOMBA MSAMAHA HUKUSAMEHE BILA KINYONGO. TAFAKARI KATIKA AMRI KUMI ZA MUNGU KAMA KUNAKITU UTAKUWA UMEKOSEA KWA KUMUOA MKATOLIKI BASI USIMWOE UTAMUUDHI MUNGU.

3-je maisha yetu huko mbele ya safari yatafika mbali?
KWANI MAISHA YENU "HUKO MBELE" MUMEPANGA YAFIKE WAPI?..NA KWANINI HUJAMSHIRIKISHA MWENZIO KUHUSU HILI LA MAISHA YENU HUKO MBELE NA UMEKIMBILIA KUTUULIZA SIE AMBAO HATA HATUJUI MUNA-MPANGO GANI HUKO MBELE..HUJACHELEWA MSHIRIKISHE MWENZIO MIPANGO YA UKO MBELE UMSIKIE NA YEYE ANASEMAJE NDIO UJUWE KAMA MTAFIKA MBALI.

4-je anaweza kuathiri wokovu wangu?
WOKOVU WAKO UMEJENGEKA KATIKA MISINGI IPI UNAYOHOFIA KUIVUNJA AU KUIATHIRI?..KAMA KWELI WOKOVU WAKO UMEJENGEKA KATIKA AMRI KUU YA MUNGU NAYO NI UPENDO BASI UKIMWOA HUYU NA HASA AKIWA NI CHAGUO LA MUNGU KWAKO UTAKUWA UNAIMARISHA ULOKOLE WAKO.

5-je naweza kwenda mbinguni?
KUNA WIMBO UNAIMBA"MBINGUNI HATUENDI KWA...........BALI WENYE MOYO SAFI WATRAENDAAAAA" TAFUTA HUO WIMBO USIKILIZE UJUWE JINSI UNAVYOTAKIWA KUFANYA ILI UUPATE UFALME WA MBINGU.."UZA KILA ULICHONACHO WAPE MASIKIN KISHA UNIFUATE".

6-je unafikiri naweza kumshawishi huko mbele ya safari akaokoka?
HUWA HAKUNA TOFAUTI KUBWA KATI YA WALOKOLE NA WAKRISTO WA MADHEHEBU MENGINE MAANA WOTE HUTUMIA KITABU KIMOJA CHA BIBLIA...NI TOFAUTI TU YA MITAZAMO NA UCHAMBUZI WA MAFUNDISHO YA MUNGU UNAOTUTOFAUTISHA NA PIA TAMAA ZA BAADHI YA VIONGOZI KUJITOA NA KUTAKA KUWA NA "MAKANISA YAO ILI WAPATE KUILA SADAKA YA BWANA"

ANGALIZO...MAMA AKIWA ANAIJUWA DINI VIZURI KULIKO WEWE(KITU AMBACHO UMEONYESHA HUUJUWI UKRISTO WALA ULOKOLE) JIANDAE KUMFUATA HUKOOO ROMAN CATHOLIC..ATAKURUDISHA KUNDINI WEWE ULIYEPOTELEA KWA MJASIRIA MALI MWINGIRA.

MASWALI YANGU KWAKO MKUU:-
1- KWANINI UMEOKOKA?
2- UNA MUDA GANI TOKA UOKOKE?
3- UNAIJUWA BIBLIA VIZURI?
5- USHAWAHI KUSOMA MAANDIKO HAYA "MKE MWEMA HUTOKA KWA MUNGU" "KUMCHA BWANA NI CHANZO CHA MAARIFA" "WATU WANGU WANAANGAMIA KWA KUKOSA MAARIFA...NA MENGINEYO MENGI TU
6- UNA UMRI GANI KWA SASA?
7- HUYU MKATOLIKI ULIMPATAJE?
8-HAUDHANI KAMA ULITENDA DHAMBI WAKATI UNAMTONGOZA MKATOLIKI WAKO
9-UMEJUWA LINI KAMA HUYU MTARAJIWA WAKO NI MKATOLIKI?
10- KABLA HUJAOKOKA ULIKUWA DHEHEBU GANI?

Tumsifu Yesu Kristu, umempa jibu la kumtosheleza. Ulokole ni njia ya kuwatenganisha mtu na ndugu zake, wazazi wake hata watoto wake kwa kisingizio eti.....nimempokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi wangu.......kwani wakristu wengine tunamwabudu nani kama si Yesu Kristu alifia msalabani kwa ajili yetu?
 
mh! hapa sasa tukushauri nini, kutamani kwenyewe dhambi tayari..., kama unataka ushaur nenda kwa padr wako sio um JF
 
mimi niongelee juu ya swali Zima la imani. Ninavyofaham mimi wokovu una misingi yake miiko yake. kwani wewe una miaka mingapi katika wokovu? kitu kilicho mfanya Mfalme Suleimani kukosana na Mungu ni pale alipooa wanawake wa mataifa mengine hao walikuwa wakiamini miungu mingine( imani tofauti na suleimani). Maandiko pia yanasema usifungiwe nira pamoja na wasioamini! wewe waamini wokovu yeye je? vipi siku moja akikwambia unanipigia makele ya kuomba mimi nimelala utajisikiaje? siku akija na bia home utasemaje? maana wakatoliki wanakunywa! uamzi ndugu unabaki kwako wewe mwenyewe maana yeye hatakuwa na shida hata kidogo ila wewe! hata hivyo wahenga walisema ndege wa rangi moja huruka pamoja! nawakilisha!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom