Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

Mimi ni Mlokole nataka kuoa Mroma

eti utamuudhi Mungu walokole mna perception mbaya.
 
Ok, kama mmekubaliana kuhusu imani sioni tatizo kwa upande huo.

Kwa upande wangu ningepata shida sana na hayo mahusiano ya mama wa Ex na mchumba wako, lakini pia ukaribu wa baba na mtoto, manake kuna ukaribu na Ex wake, Mimi kama Renegade sipendi kuoa mwanamke aliyezaa na mtu mwingine, kwa kuwa najua kuwa kutakuwa na connection ya kudumu na ex wake, wakati wote kwenye tatizo la mtoto lazima watakuwa pamoja, hivyo ni kama kuwa na mke mwenye waume wawili, that is how i feel,Nakumbuka hata wazee waliwahi kuniambia juu ya jambo hili.
Duh..hapa ndio haya mambo yanapokuaga magumu...ila ndio hivyo sometimes huwa hayana formula...unaweza kuyapeleka peleka tu yakaenda vizur tu
 
namwona ni mwanamke mnyenyekevu sana KULIKO WENGI NILIOKUTANA NAO MAKANISANI

kumbe walokole hamna kitu,ndomana mapepo hayawaishi kila kukicha. nimejifunza kitu.[/QUOTE]

Elimu yako juu ya Mungu wa kweli ni zero. Pepo hukaa kwa wenye dhambi. Huyu jamaa kama kweli ameokoka na anasali Efata kama siyo mwongo na ameamua kuleta ngonjera hapa anashindwa nini kuwaona vionhozi wa kanisa? Mwongo mkubwa. Unatumik na Ibikisi kuleta uongo ili wasiomjua Mungu waje na makufuru yao. Angalia usijitafutie balaa.
 
Tatizo la walikole ndio hili..kujifanya wao ni watakatifu na mbinguni ni kwao..ss km kwa style hii ya ubaguzi mbinguni mtafika.??? Umejihakikishiaje au kwa kujifanya umeokoka huku unabagua..yesu mwenyewe aliwapenda wabaya kwa wema..tena wale wabaya aliwapenda zaidi ili apate kuwakomboa na waweze kumpenda muumba..iweje nyinyi mnaoabudu/kutumikia kina mwingira mjione boora....maana ukiuliza unasali wapi..nasali kwa mwingira. .kwa rwakatale..kwa mzee wa upako..fungukeni enyi misukule mnatumiwa bila kujijua..KANISA NI MOJA TU NALO NI LA YESU KRISTO...sasa kanisa la fulani fulani..ndo ushetani wenyewe pendaneni muache kubagua wakristo wenzenu..mm nawapenda sana wasabato huwa wanaishi maisha yao..hawakebehi wenzao...hawadharau..hawakulazimishi uwafate km hizi dhehebu za kibiashara zinavyofanya kuutwa

Zungumza kwa maandiko na siyo kuleta ngonjera, hisia n matusi. No research no right to speak abiut walokole.
 
Angalia msimamo wako juu ya wokovu wako soma warumi 12:2
maandiko yanasema kuwa usifungwe nira na wasioamini, hivyo nawe
jua kuwa wewe ni hekalu la roho mt, hivyo ukijitambua ukoje
utajua namna ya kufanya juu ya jambo hilo. UAMUZI NI WAKO

kuhusu kumwoa tumeongea sana na yupo tayari,mahusiano alikuwa nayo kwa sababu ana mtoto mmoja na hawajawahi kuishi pamoja,kuhusu usumbufu mbele ya safari nahisi ndugu inaweza kuwa hivyo lakini namwona ni mwanamke mnyenyekevu sana kuliko wengi niliokutana nao makanisani
 
kumbe walokole hamna kitu,ndomana mapepo hayawaishi kila kukicha. nimejifunza kitu.

Elimu yako juu ya Mungu wa kweli ni zero. Pepo hukaa kwa wenye dhambi. Huyu jamaa kama kweli ameokoka na anasali Efata kama siyo mwongo na ameamua kuleta ngonjera hapa anashindwa nini kuwaona vionhozi wa kanisa? Mwongo mkubwa. Unatumik na Ibikisi kuleta uongo ili wasiomjua Mungu waje na makufuru yao. Angalia usijitafutie balaa.[/QUOTE]

Asante sana Mkuu.
 
mke mwema anatoka kwa bwana, ayo ni madhehebu tu mungu ni mmoja. ila kwa kuwa wewe mlokole unajitambulisha inabidi upate kitu kipya ambacho hakijaliwa ili ukiombee kabla ya kukifumua.
 
Mkuu nahisi unaelewa sana kinachonitatiza
kuhusu baba wa mtoto walishamalizana kwani alishaoa mwanamke mwingine,lakini ana uhusiano wa karibu na yule bibi wa mtoto wake yaani mama wa x wake
kuhusu mtoto atabakia na uhusiano na baba yake kwani hata sasa hivi wana uhusiano mzuri
kuhusu imani yupo tayari kunifata kwa ,Mwingira

Tafuta mke wako, tangaza hata hapo kanisani kwako watajitokeza kibao tena mabikira.
 
episodes, Mke mwema hutoka kwa bwana, matokea ya ndoa hiyo yatatokana na Roho Mtakatifu atakavyowaongoza na mtakavyofuata maelekezo
1) Utamuudhi Mungu kama utatenda dhambi
2)Tunaokoka kwa neema, ukiomba Neema hiyo ataokoka
3) Kwenda Mbinguni ni kwa Utakatifu

Piga Goti ili uone Mungu anakwambia nini juu ya huyo mke, USITUMIE AKILI YAKO
 
Last edited by a moderator:
hivi ukipanda na daladala na mtu asiye okoka una athilika nini?
kuna tatizo hapa katika sisi walokole ni kwamba tunaamini katika kujitenga kwetu ndio tunamwabudu MUNGU vizuri na watu wengine ni wapuuzi.

Kimtokacho mtu ndicho kilichoujaa moyo wake (Luka 6:45), wewe kama kweli ni mlokole usingeandika uongo huu. Je, ni kweli walokole hawapandi daladala na wengine? Je, walokole wamejitenga kiasi gani na wengine? Nifahamuvyo mimi maisha ya maombi huwafanya wengi wawwachukie walokole bila sababu za msingi. Mlokole huishi maisha ya ushuhuda na hapa ukikutana naye atataka mzungumze habari za Yesu Kristu, na hili huwa na chukizo kwa waumini wa jumapili hadi jumapili.

tunashindwa kuelewa kuwa watu wote wameokolewa kwa DAMU YA YESU.
tunashindwa kukumbuka kuwa wajibu wa mtu aliyeokoka ni kuwafanya watu wote kuwa wanafunzi wa YESU. bali tunajiona dhamira yetu kuwa wanafunzi wa YESU peke yetu na wengine hawastahili.

Naha ndipo lilipo tatizo lako, hupendi maisha ya ushuhuda ya walokole. Hupendi wanavyojitahidi kumbeba Kristo katika maisha yao ya kila siku. Utawafanyaje watu wote kuwa wanafunzi wa Yesu kama hujawashuhudia matendo makuu ya Mungu? Hatuenendi kwa hekima ya kibinadamu, bali twaongozwa kwa hekima itokananyo na Roho wa Mungu. Pia Ukweli ni kwamba Kristu alikufa kwa ajili ya wanadamu wote, bali wale waliomwamini ndio waliokoewa. Hebu soma hapa:

Matendo 16

29
Askari akaitisha taa iletwe, akaingia ndani ya chumba cha gereza, akapiga magoti akitetemeka miguuni mwa Paulo na Sila.
30 Kisha akawatoa nje akasema, "Ndugu zangu, nifanye nini ili nipate kuokoka?" 31 Wakamjibu, "Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka, wewe pamoja na jamaa yako."32 Wakawaambia neno la Bwana yeye pamoja na wote waliokuwa wanaishi nyumbani kwake.


japo si mahala pake lakini naimani naelekezwa niyaseme haya. na wengi tutakubaliana imefika wakati walokole hata tukienda magerezani kuwatendelea wafungwa tunaenda kutoa msaada si kwa kadri na shida na mahitaji ya watu bali tunatoa kwa walokole wenzetu tu.
hii ni shida.

Shutuma nyingine zinashangaza sana kuzitoa kwa ujumla wake namna hii. Kwamba kwa kuwa "wewe unayejiita mlokole" unasaidia ndugu zako tu, basi kila mmmoja hufanya hivyo? Hebu kuwa logical kidogo tu ndugu yangu.

Fahamu kwamba Bwana ametoa uzima buree, ni kazi yako kuamua kuchagua kati ya uzima au mauti.
 
mke mwema anatoka kwa bwana, ayo ni madhehebu tu mungu ni mmoja. ila kwa kuwa wewe mlokole unajitambulisha inabidi upate kitu kipya ambacho hakijaliwa ili ukiombee kabla ya kukifumua.
Uongo uongo nimekula walokole kibao, wote nimekuta used
 
Hii thread ipo very interesting....uzuri wa thread hii umegusa taasisi mbili muhimu sana kwenye Ukristo nayo ni IMANI na NDOA.
Usipokuwa makini na hii mambo unaweza jikuta unaoa au unaolewa na BOMU....hatari sana!!!
 
Uongo uongo nimekula walokole kibao, wote nimekuta used

Hao ni wazinzi na waasherati wenzako hawamjui Mungu na wala hawajawahi kuokoka. Kumbuka siyo kila anayesali kanisa la walokole ameokoka. Mtu haingii mbinguni kwa kusali kwenye kanisa la kilokole. La hasha. Wanaoingia mbinguni ni wale waliotubu dhambi na kumwamini Yesu Kristo kuwa ni Bwana na Mwokozi wa maisha yao na kuacha dhambi. Full stop.
 
Uongo uongo nimekula walokole kibao, wote nimekuta used

Halafu ndugu usijisifie katika kutenda dhambi. Hiuo ni sifa ya Shetani ambaye ni mwasisi wa dhambi. Tena ni ole kwa anayewakosesha watu wa Mungu. Leo utajiona kijogoo. Lakini hatimaye itakuwa ni kilio na kusaga meno. Hujui ni lini unamaliza muda wako ukizingatia kuwa kifo hakuna kanuni. Mtu wa umri wowote aweza kufa wakati wowote. Siyo sifa kuwa jasiri katika dhambi.
 
kikubwa ni upendo tu ila sidhani kama dini apo inatatizo wote ni wakristo ni swala la uaminifu na kuheshimiana.
 
Acha kujidanganya. Ingekuwa hivyo mapapa wasingewauwa mitume wa Bwana Yesu.
Acha kuskiliza conspiracy theories.Papa gani kamuua nani? hizo attacks tunazijua sanaa...Yesu aliacha organised hierachy mapemaa maana alijua tu kutakuwa na migogoro tu....akamweka peter kama leading figure..kukawa na succession hadi leo unaona papa, makadinali, maaskofu na mapadri..acheni kujidanganya na conspiracy theories ukristo halisi ni ukatoliki na unaendelea kuwa persecuted kutoka kila angle...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom