Migogoro mingi ya kijamii na kitaifa ni matokeo ya migogoro ya familia (mke na mume)

matunduizi

JF-Expert Member
Aug 20, 2018
6,586
15,369
Niliwahi kukaa katika taasisi moja. Kulikuwa na mazali kila siku. Chuki kutuhumiana, kuviziana na kila namna ya fyokofyoko kati ya wahusika.

Nilipozama kutafiti nikagundua chazo ni nyumbani hawa jamaa wanapotokea. Hawana amani, familia zimejaa magomvi, kufumaniana, mivurugano na taabu za kila namna.

Nimegundua watu wenye kuleta migogoro, taflani, debate nyingi zisizojenga, taharuki na magomvi katika jamii (Ofisini, kanisani, nzengo, vyama, na taifa kwa ujumla) ukichimba mzizi wa hizo tabia ni namna ya wao kujifariji kutokana na matifu na mabifu wanayopitia kwenye ndoa na familia zao.

Tumia nguvu kubwa kusimamisha ndoa na familia yako. Haitakusaidia wewe tu bali na popote utakapokua utakuwa mtu wa faida.
 
Kweli kabisa, mwenyewe nimewahi kuwa na mate ambae ndoa yake iliharibika baada ya wife kuhamishwa dodoma, jamaa anagubu usipime... Mnoko kwa wenzie, ili mradi na sisi tuwe hatuna Amani.. Serikali ione muhimu wa kuboresha familia kwa Ustawi wa jamii na maendeleo ya nchi.

Usiombe sasa ukute wa dada kazini wameachwa na watume zao... Yaani visirani vyao usipime 😁 😁 Kama secta ya familia haitakuwa kipaumbele. Ustawi wa jamii lazima usuesue.
 
Kweli kabisa, mwenyewe nimewahi kuwa na mate ambae ndoa yake iliharibika baada ya wife kuhamishwa dodoma, jamaa anagubu usipime... Mnoko kwa wenzie, ili mradi na sisi tuwe hatuna Amani.... Serikali ione muhimu wa kuboresha familia kwa Ustawi wa jamii na maendeleo ya nchi.
Usiombe sasa ukute wa dada kazini wameachwa na watume zao... Yaani visirani vyao usipime.... 😁 😁 Kama secta ya familia haitakuwa kipaumbele.. Ustawi wa jamii lazima usuesue.
Uwekezaji wa maana taifa linaweza kufanya ni katika familia imara.

Mtu asijua anatengeneza bomu ni yule inayekuta anaulimbukeni na kazi na biashara hadi anasahau familia. Hajui kufanya hivyo huko kazini anajitafutia visukari, presha na vifo ndebile (premature death).
 
Back
Top Bottom