Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

Michirizi ya damu-92

Akili yake ikahama, akaacha kumtafakari Keith, akaanza kuweka hisia zake kwa mwanaume ambaye hakuwa akimfahamu, hakujua alitokea wapi lakini kwa jinsi alivyoonekana, aligundua kwamba alikuwa mwanaume aliyekuwa na uwezo mkubwa kitandani.

Alikuwa akitafuta nafasi ya kuwasiliana na mwanaume huyo, alitaka kutumia hata usiku mmoja kulala naye kitandani na kufanya naye mapenzi, ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona lakini hakutaka kuona akimkosa, alikuwa tayari kufanya kitu chochote kile lakini mwisho wa siku kuwa naye.

“Usiku huuhuu lazima niongee naye,” alijisemea.
Huo ndiyo ulikuwa uamuzi wake, hakutaka siku hiyo ipite pasipo kuwasiliana naye, alichokifanya usiku huo ni kuamka usiku wa manane, akatoka kitandani huku akinyata na kuelekea chooni kwa lengo la kuzungumza na mwanaume huyo kwani pasipo kufanya hivyo asingefanikiwa kutokana na Kaith kumng’ang’ania kama ruba.

“Naomba upokee simu,” alisema wakati simu ikianza kuita, baada ya sekundee kadhaa tu, simu ikapokelewa.
“Bila shaka ni mrembo wa mgahawani,” alisema mwanaume huyo baada ya kupokea simu, alionekana kabisa kuwa macho japokuwa usiku ulikuwa umekwenda sana.

“Ndiyo! U mzima bebi,” alisema Maria, hakutaka kujivunga, alikuwa tayari mwanaume huyo ajue kwamba alikuwa akimpenda.
“Nipo poa.”

“Upo wapi nije tuzungumze kama ulivyotaka?” aliuliza Maria.
“Nipo hotelini! Ila nipo na mke wangu!”
“Jamani! Kumbe umeoa?”
“Yeah! Lakini nahisi hili haliwezi kuninyima kuwa na wewe,” alisema mwanaume huyo.

“Kweli kabisa. Umetokea kunichanganya sana mpenzi. Naomba nionane na wewe hata kesho!” alisema Maria.
“Haina shida. Wewe tu! Bye!”
“Bye! Nakupenda.”
“Nakupenda pia!”

Je, nini kitaendelea?
 
Back
Top Bottom