Michirizi ya Damu

Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 91

“Mimi ni kama wewe. Leo umechukua mtoto wa Kifaransa?” aliuliza Keith.
“Hapana! Ni Venezuela!”
“Aisee ni mzuri sana.”
Walikuwa wamseogea pembeni wakizungumza tu, waliwaacha wasichana wao katika meza nyingine kabisa. Maria alibaki akiangalia na demu wa Mendoza, hakumfahamu lakini kwa kuwa bwana wake alikuwa rafiki wa Keith, wakaanza kuzungumza kwa lengo la kuzoeana.

Wakati wakiwa hapo, ghafla akatokea mwanaume mmoja, aliyevalia suti, nywele alizipaka dawa, alionekana kuwa mwanaume mkakamavu, akawasogelewa wasichana wale na kisha kuwasalimia.
“Mna kampani?” aliuliza mwanaume huyo.
“Ndiyo! Tukusaidie nini?”

“Naomba unitafute,” alisema mwanaume huyo huku akimpa Maria kikaratasi kilichokuwa na namba yake ya simu.
“Mmh!”
“Usiogope! Mimi si muuaji! Naomba unitafute! Usihisi kwamba nakutaka, hapana, ila ninataka kuzungumza nawe mambo fulani kwa faida yako,” alisema mwanaume huyo.

“Mambo gani?”
“Ndiyo maana nimekupa namba yangu unitafute!” alisema mwanaume huyo, alikuwa akizungumza harakaharaka ili asionekane na wanaume wale wakajua kwamba alikuwa akiwamendea mademuu zao.

“Sawa.”
Hakuendelea kubaki mahali hapo, alichokifanya mwanaume huyo akaondoka zake mahali hapo. Wasichana hao walibaki wakimwangalia, alikuwa mzuri wa sura, alivalia suti iliyomkaa sana mwilini, mwili wake ulionekana kujazia, hakuwa na kitambi kama walivyokuwa mabwana zao.

Wote walimwangalia alivyokuwa akiondoka, alitembea kijeshi, akatoka ndani ya mgahawa huo na kutokomea zake. Japokuwa kikaratasi kile alipewa Maria lakini hata demu wa Mendoza naye alitamani kuwa na namba za mwanaume huyo.

Alikuwa na sura nzuri, alimpenda, hakutaka kuona akiacha mwanaume huyo aondoke zake kwani kwa jinsi alivyokuwa akivutia, hata moyo wake ulimchanganya.
“Ni mzuri!” alisema demu wake Mendoza.
“Sisi wengine tumezaliwa na bahati tu,” alisema Maria na kisha kukiweka kikaratasi kile mkobani.

Kichwa cha Maria kikachanganyikiwa, uzuri aliokuwa nao mwanaume yule ukampagawisha, moyoo wake ukahisi akianza kuanguka katika penzi la mwanaume yule, hata alipoondoka bado aliendelea kuhisi kitu cha tofauti moyoni mwake.
 
Back
Top Bottom