Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 152,998
- 453,871
MICHIRIZI YA DAMU 01- Nyemo Chilongani
GIZA, Misri
Zilisikika kelele kutoka ndani ya piramidi moja lililokuwa katika Mji wa Giza uliokuwa nchini Misri. Watu waliokuwa humo ambao asilimia kubwa walikwenda kutalii wakatoka huku wakikimbia kwani mbali na kelele hizo, piramidi hilo halikuwa la kawaida, lilikuwa linatisha kiasi kwamba hata watalii waliokuwa wakiingia, walishikana mikono kama njia mojawapo ya kutokutana kuuawa na majini yaliyosadikiwa kwamba yalikuwepo ndani ya piramidi hilo.
Mwanamke yule aliyekuwa amepiga kelele akatoka huku akitetemeka, kijasho chembamba kikimtoka, walinzi waliokuwa mahali hapo wakamsogelea kwa lengo la kutaka kufahamu kilichomfanya mpaka kupiga kelele kiasi hicho hadi kuwaogopesha watu wengine.
Walipomuuliza mwanamke huyo wa Kiingereza akawaambia kwamba aliiona maiti ndani ya piramidi hilo kitu kilichomtisha kila mtu.
“What?” (nini?) aliuliza mwanaume mmoja.
“A deadbody!” (maiti)
“Are you sure?” (una uhakika?)
“Yes!” (ndiyo) alijibu mwanamke huyo huku akiendelea kutetemeka kwa hofu.
Watu wote waliotoka ndani ya piramidi hilo wakaanza kumwangalia mwanamke yule, wengine hawakuridhika, wakamsogelea na kumuuliza kilichokuwa kimetokea ndani ya piramidi lile, hakuficha, aliwaambia wazi kwamba aliiona maiti ikiwa chini kitu kilichomfanya kupiga kelele na kukimbia.
“Siyo kwamba umeona mauzauza?” aliuliza jamaa mmoja.
“Kwani mauzauza siyajui? Nimeona maiti!” “Sasa kwa nini ulikuwa peke yako na wakati hairuhusiwi?” aliuliza mwanaume mwingine.
“Niliingia na mume wangu! Yeye alikwenda upande mwingine na mimi kwenda mwingine,” alijibu mwanamke huyo na mumewe kutokea hapo, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia mkewe.
Walinzi waliokuwa hapo wakachukua tochi zao na kuingia ndani ya piramidi hilo, walitaka kuona kile alichokiona mwanamke huyo. Kwa miaka mingi, tangu karne ya ishirini ilipoingia hakukuwa na mtu yeyote aliyekufa ndani ya piramidi hilo japokuwa kulikuwa na tetesi za kuwepo kwa majini. Kama hakukuwa na mtu aliyekufa! Iliwezekanaje mwanamke huyo kuona maiti humo?
GIZA, Misri
Zilisikika kelele kutoka ndani ya piramidi moja lililokuwa katika Mji wa Giza uliokuwa nchini Misri. Watu waliokuwa humo ambao asilimia kubwa walikwenda kutalii wakatoka huku wakikimbia kwani mbali na kelele hizo, piramidi hilo halikuwa la kawaida, lilikuwa linatisha kiasi kwamba hata watalii waliokuwa wakiingia, walishikana mikono kama njia mojawapo ya kutokutana kuuawa na majini yaliyosadikiwa kwamba yalikuwepo ndani ya piramidi hilo.
Mwanamke yule aliyekuwa amepiga kelele akatoka huku akitetemeka, kijasho chembamba kikimtoka, walinzi waliokuwa mahali hapo wakamsogelea kwa lengo la kutaka kufahamu kilichomfanya mpaka kupiga kelele kiasi hicho hadi kuwaogopesha watu wengine.
Walipomuuliza mwanamke huyo wa Kiingereza akawaambia kwamba aliiona maiti ndani ya piramidi hilo kitu kilichomtisha kila mtu.
“What?” (nini?) aliuliza mwanaume mmoja.
“A deadbody!” (maiti)
“Are you sure?” (una uhakika?)
“Yes!” (ndiyo) alijibu mwanamke huyo huku akiendelea kutetemeka kwa hofu.
Watu wote waliotoka ndani ya piramidi hilo wakaanza kumwangalia mwanamke yule, wengine hawakuridhika, wakamsogelea na kumuuliza kilichokuwa kimetokea ndani ya piramidi lile, hakuficha, aliwaambia wazi kwamba aliiona maiti ikiwa chini kitu kilichomfanya kupiga kelele na kukimbia.
“Siyo kwamba umeona mauzauza?” aliuliza jamaa mmoja.
“Kwani mauzauza siyajui? Nimeona maiti!” “Sasa kwa nini ulikuwa peke yako na wakati hairuhusiwi?” aliuliza mwanaume mwingine.
“Niliingia na mume wangu! Yeye alikwenda upande mwingine na mimi kwenda mwingine,” alijibu mwanamke huyo na mumewe kutokea hapo, kitu cha kwanza kabisa kilikuwa ni kumkumbatia mkewe.
Walinzi waliokuwa hapo wakachukua tochi zao na kuingia ndani ya piramidi hilo, walitaka kuona kile alichokiona mwanamke huyo. Kwa miaka mingi, tangu karne ya ishirini ilipoingia hakukuwa na mtu yeyote aliyekufa ndani ya piramidi hilo japokuwa kulikuwa na tetesi za kuwepo kwa majini. Kama hakukuwa na mtu aliyekufa! Iliwezekanaje mwanamke huyo kuona maiti humo?