Michirizi ya Damu

SEHEMU YA 96

Mtu wa kwanza kabisa aliyetaka kumuua alikuwa Bilionea Keith. Hakutaka kumuona mwanaume huyo akiendelea kuvuta pumzi ya dunia hii na wakati alimtenda vibaya. Mara ya mwisho kumsikia mwanaume huyo ni kwamba alikuwa na msichana mrembo mwenye asili ya Kinaigeria aliyeitwa Maria.

Alitaka kujua mahali alipokuwa, hakuendelea kuishi nchini Tanzania, akasafiri mpaka nchini Marekani, kwa kuwa bilionea huyo alikuwa akifahamika sana, hakupata kazi kuzipata data zake tena kutoka kwa watu walioonekana kuwa wa karibu sana.

Akaambiwa kwamba mwanaume huyo alikuwa akijiandaa na safari ya kuelekea nchini Italia kwa ajili ya kula bata na mpenzi wake na kuliona jengo kubwa la Collosseum.

HAkutaka kubaki nchini Marekani, ilikuwa ni lazima kwenda huko.
Alijiamini kwamba alikuwa na sura nzuri, mwili uliojengeka, alijua fika kwamba mara baada ya Maria kumuona ilikuwa ni lazima kumtamani na kutaka kulala naye. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa, alivyoonana na msichana huyo hotelini, akampenda na kuchukua namba yake ya simu.

Wakaanza kuwasiliana, alimdanganya kwamba alikuwa na mkewe hotelini, hakutaka kuona msichana huyo akipata muda wa kuwa naye kwa kujiachia, alitaka kumuingizia hofu ajue kwamba kweli mwanaume huyo alikuwa na mkewe hapo hotelini.

Mazungumzo yao yalikuwa ya kwenye simu, walitumiana meseji za mapenzi, kwa kipindi kifupi tu tayari Maria alionekana kufa na kuoza, hakutaka kuona mwanaume Fareed akiendelea kuwa na mkewe, alijipanga na alijipiza kwamba ni lazima alale naye kwa gharama yoyote ile.

“Siwezi kumuacha mwanaume mwenye mwili mzuri kama yule, nitamuachaje mwanaume mwenye sura nzuri kama yule?” alijiuliza.

Hakutaka kuona hilo likitokea, alijipiza kwamba ni lazima amfuate kitandani, alale naye na kufanya naye mapenzi. Ni kama Keith alijua, ukaribu kwa Maria ukaongezeka zaidi au kwa Kiswahili chepesi cha mtaani ni kwamba alikuwa akikaba mpaka penalti.

“Bebi naomba nionane na wewe,” aliandika ujumbe mfupi.
“Leo!”

“Ndiyo! Kesho tunaondoka!”
“Kwenda wapi?”
“Misri!”
“Kuna nini?”
Tunakwenda kuangalia mapiramidi ya Giza!”
 
SEHEMU YA 97

“Ooh! Nitakuweepo huko, nitakuja peke yangu kuonana nawe,” aliandika Fareed.
“Kweli?”
“Ndiyo!”
“Niahidi kama tutakuwa wote!”
“Nakuahidi!”

Moyo wa Maria ukaridhika, hakuamini kama hatimaye mwanaume huyo alikubaliana naye kwamba wangeonana na kufanya mambo yao. Moyo wake ukawa na furaha tele, akajitupa kitandani huku akiiona dunia yote kuwa yake kwani kile alichotaka kukisikia ndicho alichoambiwa na mwanaume huyo.

“Nitalala naye na kumuonyeshea kwa nini yule babu amepagawa kwa penzi langu,” alisema Maria na kujilaza kitandani huku akiisubiri kesho ifike, waondoke kuelekea Misri ambapo huko angeonana na mwanaume huyo.

**** Keith hakutaka kukaa sana na mpenzi wake nchini Italia, alichokifanya ni kuondoka na kuelekea katika Mji wa Giza, nchini Misri kwa ajili ya kuyatazama mapiramidi yaliyokuwa nchini humo.

Njiani, bado walionyesheana mapenzi ya dhati, walikuwa wakibusiana sana lakini mawazo ya Maria hayakuwa hapo, alimfanyia mwanaume huyo kila kitu lakini moyo wake, kichwa chake, vyote vilikuwa vikimfikiria Fareed, mwanaume ambaye hakujua kama alikuwa akitoka kimapenzi na mpenzi wake.

Ndege haikuchukua muda mrefu ikafika nchini Misri ndani ya Jiji la Cairo ambapo hapo wakachukua basi lililowapeleka mpaka katika Mji wa El Giza. Macho ya Maria yalishangaa, hakuamini kile alichokuwa kikiona, aliyaona mapiramidi makubwa ambayo alikuwa akiyasoma kwenye vitabu na wakati mwingine kuyaangalia kwenye televisheni.

Alishangaa mno, wakati mwingine alitamani kulia kwani furaha aliyokuwa nayo kipindi hicho ilikuwa kubwa sana. Akamkumbatia mpenzi wake, Keith na kumshukuru sana kwa kumsafisha macho kwa kumpeleka nchini Misri.

“Tutakwenda kule kesho, leo tulale hotelini,” alisema Keith, wakati huo waliyaona mapiramidi yale yakiwa mbali kabisa.

Walipoingia hotelini, kama kawaida wakaanza kucheza michezo ya kimahaba kitandani, kila mmoja alimtamani mwenzake, kila mmoja alihitaji sana kuwa na mwenzake wakati huo.

Japokuwa Maria alijitoa sana kama ilivyo kawaida yake lakini kichwa chake hakikuacha kumfikiria Fareed, kwake, mwanaume huyo alikuwa kila kitu, alikichanganya kichwa chake, muda mwingi alikuwa na mawazo tele juu yake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom