SEHEMU YA 89
Kupitia mlango wa nyuma, kulikuwa na gari lake, akampakiza na kuondoka naye. Safari ilikuwa ndefu na walipofika sehemu iliyoonekana kuwa na takataka nyingi, akasimamisha gari lake na kumwangalia Fareed aliyekuwa hoi japokuwa nguvu zilianza kumjia.
“Nisamehe tu! Shetani aliniingia. Amekuwa akinitesa sana katika mchezo huu, uliponiambia shida yako, nilizidiwa kabisa, naomba unisamehe,” alisema Padri Luke huku akimwangalia Fareed aliyekuwa akilia tu.
“Nitakuua! Nitakuua padri!” alisema Fareed, akaufungua mlango na kuteremka, hakupiga hatua nyingi, akadondoka na kupoteza fahamu. Padri Luke akaliwasha gari lake na kuondoka mahali hapo huku akimwacha Fareed akiwa hoi. ***
Bado bilionea Keith alikuwa kwenye penzi la dhati na msichana Maria, moyo wake ulichanganyikiwa, ulikufa na kuoza, hakutaka kusikia kitu chochote, kwake, msichana huyo alikuwa kila kitu.
Alitumia kiasi kikubwa cha pesa kwa msichana huyo, hakutaka kabisa kumuona akipata tabu ya aina yoyote ile. Alimpenda, alimpeleka nchini Ufaransa, Italia, Dubai na sehemu nyingine nyingi kwa ajili ya kula naye maisha.
Msichana huyo hakutaka kuleta uvivu kitandani, alifanya kila linalowezekana kumchanganya mzee huyo, alijua kucheza na kiuno chake, alijua kucheza na mdomo wake uliomchanganya mzee huyo na kuona dunia yote ilikuwa yake.
Maria hakurudi nchini Nigeria, aliendelea kubaki nchini MArekani huku akiendelea kutanua na mwanaume huyo. Penzi likamchanganya mno Keith, wakati mwingine hakuwa akifanya kazi zake, alitamani sana kuendelea kuwa na mwanamke huyo kwani kila alipomuacha hata kwa saa tano, alihisi kulikuwa na mwanaume aliyekuwa akiliiba penzi lake.
“Have you ever seen collossium?” (Umewahi kuliona Collessium?) aliuliza Keith.
“I’ve just seen it but I’ve not touched it!” (nimewahi kuliona lakini sijawahi kuligusa) alijibu msichana huyo.
“Are you serious baby?” (kweli bebi?)
“Yeah!” (ndiyo)
“I want to take you there!” (nataka nikupeleke huko)
“I real want to touch it,” (natamani sana niliguse) alisema msichana huyo.