Miaka kumi tangu kuhitimu shahada ya kwanza

Miaka kumi tangu kuhitimu shahada ya kwanza

Tuone ata kapicha kahiyo nyumba, maana desturi ya mswahili hasemi nyumba huwa tunasema kibanda sasa ww una nyumba inamaana ni kubwa zaidi ya Simba wa Madale
kiwanja nilinunua m16, nyumba mpaka ujenzi unakamilika iligharimu kama m55 hapo na fensi. ni ya kawaida tu vyumba vinne na vyenye space ya kutosha. Ujenzi kwa DAR kuna kupigwa pia ila kiukweli ina kila kitu cha muhimu ndani, Hizo nne na gharama nyinginezo ilinichukua miaka 3 kuikamilisha.

Kiwanja nilinunua mwaka 2015, nikajipanga kwa miaka 2 nikapata kama m14 hivi nikapandisha mpaka linter, nikatulia tena kama miaka mwaka hivi nikapata m12, nikapiga bati na nondo madirishani na milangoni, nikatulia mpk 2019 nikapata kama m 10 nikapiga plasta, gypsum na skimm, mwaka huu nikaona isiwe tabu nikazama benki nikabeba mpunga 25 m, nikapiga rangi, madirisha ya vioo, milango, marumaru, pavement, uzio, underground water tank, nikakamilisha. NI msoto inaitaji tu determination
 
USHAURI
Usipende kuelezea mafanikio yako katikati ya watu wenye matatizo/njaa. Sio tu utarogwa lakini pia mtu akikuangalia kwa jicho la husuda/ kukuwazia kwa roho ya kwanini tu ni uchawi tosha na inaweza kukurudisha nyuma. Kuna watu humu ndani wakiamua kuelezea mafanikio yao miaka 3 baada ya kumaliza chuo utashangaa sana na hata kujidharau.

Nakukumbusha mafanikio ni yako mwenyewe na familia yako huna haja ya kuwaelezea watu hapa maana haitakusaidia chochote zaidi ya kujitafsirisha tofauti mbele ya wengine. Ni ushauri tu unaweza kuubeba au kuuacha pia.
 
Kibongo bongo umetusua but in reality umechelewa......!!?
miaka yote kumi umepata hivyo tu daah.....
what a westage of time.....
waungwana msinielewe vibaya ni mtazamo tu

Ok mkuu una nyumba ngapi hapo sinza?
 
USHAURI
Usipende kuelezea mafanikio yako katikati ya watu wenye matatizo/njaa. Sio tu utarogwa lakini pia mtu akikuangalia kwa jicho la husuda/ kukuwazia kwa roho ya kwanini tu ni uchawi tosha na inaweza kukurudisha nyuma. Kuna watu humu ndani wakiamua kuelezea mafanikio yao miaka 3 baada ya kumaliza chuo utashangaa sana na hata kujidharau.

Nakukumbusha mafanikio ni yako mwenyewe na familia yako huna haja ya kuwaelezea watu hapa maana haitakusaidia chochote zaidi ya kujitafsirisha tofauti mbele ya wengine. Ni ushauri tu unaweza kuubeba au kuuacha pia.
Haya mambo ya kuogopa kurogwa ndo yanafanya vijana wasiwe motivated!!! Muache jamaa atoe motivation kwa vijana wewe endelea kujificha
 
Mie nimenaliza miaka 9 hata sijui vyeti vipo wapi fulu kupigika mishe zinagoma deile kazi niliomba nkachoka
 
USHAURI
Usipende kuelezea mafanikio yako katikati ya watu wenye matatizo/njaa. Sio tu utarogwa lakini pia mtu akikuangalia kwa jicho la husuda/ kukuwazia kwa roho ya kwanini tu ni uchawi tosha na inaweza kukurudisha nyuma. Kuna watu humu ndani wakiamua kuelezea mafanikio yao miaka 3 baada ya kumaliza chuo utashangaa sana na hata kujidharau.

Nakukumbusha mafanikio ni yako mwenyewe na familia yako huna haja ya kuwaelezea watu hapa maana haitakusaidia chochote zaidi ya kujitafsirisha tofauti mbele ya wengine. Ni ushauri tu unaweza kuubeba au kuuacha pia.
Ukijiamini huna haja ya kuhofu. sijarogwa na wanaonifahamu nije kurogwa na tusiojuana humu, hii ni imani na uoga usio na maana. Pia watu hatulingani kimafanikio niliamua tu kuweka hapa lakini si jambo jipya maana wanaonizunguka wanaona kama mm ninavyoona mafanikio zaidi ya wengine. Imani kama zako ndizo zinafanya wengi wetu tunaishi kama digidigi. Muamini Mungu na amini maisha yako hakuna mtu awaye yoyote anayeweza kuyarudisha nyuma zaidi yako mwenyewe.
 
Tufanye kazi kwa bidii, ndiyo theme niliyoipata hapo, ingawa sijui kazi gani unafanya, maana kwa mshahara tu, lets say wa ualimu, ni kazi kwelikweli kwasababu malupulupu si mengi.
 
Na wenzako waliomaliza degree zao 2015 mpk sasa wana miaka 5 mtaani na serikali sikivu ya JPM haina mpango nao wowote zaidi ya kujenga miradi tu.

So kwa sasa wana 5 years of experience ya kukaa kitaa na ku-bet ma bus yatakayowahi kufika stand.
Omba yasikupate Kuna siku na Mimi nta andika Uzi wangu Kama huu.......

MIAKA 5 maisha Yana kupiga mpaka unapagawa hauna unacho miliki zaidi ya begi....unalo hifadhia nguo...
Na nguo zikiwa busy ndio zinapauka Sasa
Asante Mungu kwa pumzi haya mengine Ni ya ziada tu
 
Hongera sana. Wanaokuponda ni wivu wa kike unawasumbua. Midume mingi humu inaishi kwa shemeji zao.
 
Omba yasikupate Kuna siku na Mimi nta andika Uzi wangu Kama huu.......

MIAKA 5 maisha Yana kupiga mpaka unapagawa hauna unacho miliki zaidi ya begi....unalo hifadhia nguo...
Na nguo zikiwa busy ndio zinapauka Sasa
Asante Mungu kwa pumzi haya mengine Ni ya ziada tu

Watoto wa mama hawawezi kuelewa unayoyapitia mkuu.

Hakuna kukata tamaa.
 
Omba yasikupate Kuna siku na Mimi nta andika Uzi wangu Kama huu.......

MIAKA 5 maisha Yana kupiga mpaka unapagawa hauna unacho miliki zaidi ya begi....unalo hifadhia nguo...
Na nguo zikiwa busy ndio zinapauka Sasa
Asante Mungu kwa pumzi haya mengine Ni ya ziada tu
Kuna ups/downs nyingi katika maisha ni wachache kwa aina ya familia zetu ambao hawajapita kipindi cha msoto...
 
Tangu kuhitimu degree ya kwanza huu ni mwaka wa kumi sasa na haya ndiyo nimeyafanikisha mpaka Leo hii.

Nimepata mke na watoto wawili

Nimeongeza elimu

Nimejenga jijini DSM nyumba ya familia iliyogharimu m75, kiwanja na ujenzi.

Nina kiwanja kimoja sqm 1250, kiligharimu m15

Nina usafiri kurahisisha mizunguko/uligharimu m13.

Nimeajiriwa serikalini

Nina kibanda cha mobile money kinaniiingizia kilo6 hivi.

Nina mikopo benki


Matamanio yangu zaidi
Kuwa na biashara zangu binafsi/kujiajiri/kuajiri ndani ya miaka 5

Kuongeza nyumba 2-3 ndani ya miaka 10.

Kumfungulia mzee wangu biashara ya kumuingizia kipato cha kila siku. Ndani ya miaka 2.

Mungu anipe uhai kutimiza haya yote.

Maisha ni matamanio, mipango, utafutaji na utekelezaji.
Haya na mimi ngoja niweke yangu maana miaka kumi imepita tangu nihitimu degree yangu ya kwanza.

Nina wake wawili na watoto wanne.Nina Nina nyumba tano na viwanja vitatu na gari moja.Nina chuo kimoja cha Vocational,Kampuni ya Ushauri-Consultancy.Nimefanya kazi ya kuajiriwa kwa miaka 7 na kujiajiri kwa miaka 9.Nimeongeza elimu sana na bado ninasoma.Interestingly kwa sasa nimeanza maisha upya kabisa nikiwa na malengo tofauti kabisa..
 
Back
Top Bottom