Miaka 27 huna mtoto? Jichunguze

Miaka 27 huna mtoto? Jichunguze

Kama wewe ni mwanaume au mwanamke na umetimiza miaka 27 lakini huna hata mtoto wa kusingiziwa na hata kutoa mimba hujawahi basi unapaswa kujichunguza huenda una matatizo ya kizazi.

Haiwezekani mtu anaefanya ngono hadi kufikisha umri huo hana mtoto, hilo ni tatizo maana maisha ya sasa ni mafupi sana! Sasa kama hutaacha legacy basi ni hatari sana kwako au subiri tu kuitwa babu au bibi na watoto wako.

Wenzako wanaacha kuzaa wewe ndio unaanza
Sio kweli mkuu hata kidogo, kwani kutoa mimba ndio ujanja kuonesha kwamba una uwezo wa kuzaa?
Wanafunzi wengi wa vyuo Tanzania wanamaliza wakiwa na 24-26 yrs, so kwa bandiko lako ulipenda wazae wakiwa vyuoni huko au wazae baada tu ya kumaliza chuo wakiwa hawana hata ramani ya maisha?
Mi nafikiri suala la kuzaa na kua na familia ni personal sana na kila mtu anafanya kwa muda wake baada ya kujiandaa(hasa kwa wanaume)

Moja ya sababu ambazo zinatufanya sisi waafrica kua masikini ni kua na kundi kubwa katika jamii ambalo halizalishi(sio productive kiuchumi) ambalo ni watoto wadogo na kua na kundi dogo sana la watu wanaofanya kazi kuhudumia kundi hilo kubwa(watoto na wazee).Ukiangalia graph za population za nchi zilizoendelea utakua watu wazima ni wengi kuliko watoto wadogo.

Tukiiendelea na mitizamo kama hii kwamba ukiwa huna mtoto na una miaka zaidi ya 27 umaskini hautatuacha kamwe.
 
Sio kweli mkuu hata kidogo, kwani kutoa mimba ndio ujanja kuonesha kwamba una uwezo wa kuzaa?
Wanafunzi wengi wa vyuo Tanzania wanamaliza wakiwa na 24-26 yrs, so kwa bandiko lako ulipenda wazae wakiwa vyuoni huko au wazae baada tu ya kumaliza chuo wakiwa hawana hata ramani ya maisha?
Mi nafikiri suala la kuzaa na kua na familia ni personal sana na kila mtu anafanya kwa muda wake baada ya kujiandaa(hasa kwa wanaume)

Moja ya sababu ambazo zinatufanya sisi waafrica kua masikini ni kua na kundi kubwa katika jamii ambalo halizalishi(sio productive kiuchumi) ambalo ni watoto wadogo na kua na kundi dogo sana la watu wanaofanya kazi kuhudumia kundi hilo kubwa(watoto na wazee).Ukiangalia graph za population za nchi zilizoendelea utakua watu wazima ni wengi kuliko watoto wadogo.

Tukiiendelea na mitizamo kama hii kwamba ukiwa huna mtoto na una miaka zaidi ya 27 umaskini hautatuacha kamwe.
Wewe una miaka mingapi? Tueleze una kiasi gani benki hadi muda huu?? Harafu kwani nani kakwambia watu wote wanafika vyuo? Acha propaganda we zaa,maisha ni mafupi.unachojiandaa kikubwa ni nini?
 
dogo fikiri kabla ya kupost lazima ujue kila mtu ana mipango yake
Nina watoto watatu wa mama tofauti,wote nawahudumia vizuri tuu na mipango yangu inaenda kama kawaida,ukiwa na familia ndio akili ya kujipanga inatanuka coz unajua nyuma kuna watu wanakutegemea,,ukute hapo ulipo huna chochote cha maana ulichonacho
 
Sasa ndoa bila mtoto/watoto itakuaje tena mkuu? watoto wapo.
Safi.

Ujue ile kauli yako, nakunukuu, "Undhani kila mtu anataka kuzaa haramu?"

Nikajua wewe bado hujabahatika kupata Mtoto/Watoto, yaani na wewe umo kwenye lile kundi la kujipanga.

Na kingine ni kwamba, hakuna Mtoto Haramu.

Kumbuka Watoto ni Malaika na hawana kosa lolote, kwahiyo si vyema kuwaita Haramu
 
Hao wanasumbuliwa na nidhamu ya Uoga.

Wewe ujipange kwani una mkataba wa kuwepo kuishi hapa Ulimwenguni milele?

Maisha yenyewe haya mafupi.

Na watu wa hivyo wa kujipanga, kwa Mwanamme ikitokea bahati mbaya kimenasa, hawakawii kuwaambia Mademu zao wakacholopoe Mimba, na kama ni kwa Mwanamke halikadhalika wataenda kucholopoa.

Na kingine, hao wa kujipanga ndio wanaoongoza kwa kuwakana/kuwakataa Watoto wao.

Mtoto anapozaliwa hawakawii "sio Mwanangu", "sio wa kwangu"

Kumbe hawana lolote Uoga wa Maisha na Majukumu unawasumbua
Umeongea ukweli mtupuu
 
Waoga wa Maisha siku zote wanaogopa Watoto, wanakuambia wanajipanga.

Cha ajabu Umri unazidi kwenda, na bado hali yao kimaisha si Simba wala Yanga.

Sasa sijui wanajipanga nini!

Watoto wana raha yake, msiwe waoga.

Kama wewe unakula Tembele, na Mtoto atakula Tembele, hivyohivyo mpaka Mtoto anakua.

Jiulize, wewe unaeogopa Mtoto.

Wewe ulikuzwaje?

Lini Wazazi wako/wenu walilala nje eti kwasababu ya wewe Mtoto, nyie Watoto!
Kabisaa tena pengine mtoto akawa chachu ya maendeleo kukufanya ujishughulishe zaidi kwa kujua majukum yameongezeka.
 
Safi.

Ujue ile kauli yako, nakunukuu, "Undhani kila mtu anataka kuzaa haramu?"

Nikajua wewe bado hujabahatika kupata Mtoto/Watoto, yaani na wewe umo kwenye lile kundi la kujipanga.

Na kingine ni kwamba, hakuna Mtoto Haramu.

Kumbuka Watoto ni Malaika na hawana kosa lolote, kwahiyo si vyema kuwaita Haramu
Well said mkuu,hawa wanaoita haramu ndo hao akipata mimba au kumpa binti mimba wakati hawapo kwenye ndoa wanaenda kufanya abortion.
 
Mtoa mada vizur tukajua kiwango chako cha elimu. Maana kuna uhusiano mkubwa wa elimu ya mtu na umri wake wa kuoa, idadi ya watoto, bila kusahau aina ya mada anazopost mtu huyo.
Watu wanaweza kukulaumu bure kumbe level of education is direct promotional to thinking capacity when other factors remain constant.
 
Mtoa mada vizur tukajua kiwango chako cha elimu. Maana kuna uhusiano mkubwa wa elimu ya mtu na umri wake wa kuoa, idadi ya watoto, bila kusahau aina ya mada anazopost mtu huyo.
Watu wanaweza kukulaumu bure kumbe level of education is direct promotional to thinking capacity when other factors remain constant.
Sina muda wa kukwambia nina elimu gani,kikubwa we zaa kama ushafikisha umri huo,unless unataka kuitwa babu na wanao
 
Kabisaa tena pengine mtoto akawa chachu ya maendeleo kukufanya ujishughulishe zaidi kwa kujua majukum yameongezeka.
Ahsante sana.

Umemaliza.

Mtoto/Watoto wanakupa sana Spidi ya kutafuta, kwasababu kila ukikaa unajiambia,

'Wanangu sitaki waishi kinyonge'

Ujue kuna siri moja katika Maisha, Maisha ukijiambia inawezekana basi ujue itawezekana tu.

Wewe kuwa mpambanaji, halafu usiwe Mtu wa kukata tamaa inapotokea Mitihani.

Mitihani kawaida sana katika Maisha
 
Well said mkuu,hawa wanaoita haramu ndo hao akipata mimba au kumpa binti mimba wakati hawapo kwenye ndoa wanaenda kufanya abortion.
Umeona e...

Huo ndio unafiki wenyewe.

Na wapo wengi sana Watu wa sampuli hiyo.

Halafu baadae jitu litakuambia linajipanga.

Kumbe jitu lina kesi kibao za Vichwa
 
Mtoa mada vizur tukajua kiwango chako cha elimu. Maana kuna uhusiano mkubwa wa elimu ya mtu na umri wake wa kuoa, idadi ya watoto, bila kusahau aina ya mada anazopost mtu huyo.
Watu wanaweza kukulaumu bure kumbe level of education is direct promotional to thinking capacity when other factors remain constant.
Muangalieni huyu!

Watu wanazungumzia Watoto, wewe unazungumzia Elimu!

Kwani hakuna Watu ambao wanabukua na wana Watoto tayari?

Hebu tuliza kipago
 
mmmh..! lakini kuzaa mtoto bila ya kumjengea future ya kueleweka iv sasa ni janga kubwa kwa taifa pia"
 
mmmh..! lakini kuzaa mtoto bila ya kumjengea future ya kueleweka iv sasa ni janga kubwa kwa taifa pia"
Mkuu ukisubiri kumjengea future basi utazeeka bila watoto.future itakuja akizaliwa
 
Abraham na mkewe bi Sarah pia walijichunguza.
Mi siwajui hao,ila kama ni hadithi basi nakushauri tu usiishi kwa kufuata hadithi za zamani,watu ambao hujawahi kuwaona zaidi tu ya kusoma vitabu
 
Back
Top Bottom