Shujaa anayedharauliwa?
Skendo ya Jairo ilimdhalilisha sana, na bado JK na Ikulu kwa kiburi walicho nacho wamegoma kutekeleza maazimio ya Bunge na ndo maana Spika wa Bunge alijua kwamba swala hilo lingejadiliwa lingewapandisha hasira wabunge.
Serikali yenu sio ya kubembelezana, ukiwabembeleza hakuna watakachotekeleza, na ndio maana mawaziri wanajibu mbovu na kujifanyia wanayotaka.
Wakati wa skendo ya Jairo, alisikika akisema kwamba hata wachonge sana hatatoka, na mpaka leo kweli bado yuko na hakuna walichomfanya.
Mbaya zaidi IKULU kupitia Luhanjo ikamsafisha na kumrudisha kwa mbwembwe na kupokelewa akisukumwa kwenye gari. Hayo kama sio matusi kwa Waziri Mkuu ni nini? Pinda alitutangazia watanzania kwamba kama angekuwa yeye ndo mwenye final say, angemfuta kazi Jairo. Juzi amekaa kwenye kikao mpaka usiku, wakakubaliana kwamba mawaziri 8 waondoke, nini kimetokea? Huyo ndo shujaaa? Angekuwa shujaa kweli angesema anajiuzulu, hapo ningemuona ni shujaa anayelinda heshima yake baada ya kudhalilishwa mara 2 tena mbele ya watanzania wote. Kwa kuwa kilichotokea sio kwamba ni vikao vya siri, bali ni maamuzi ya wazi yaliyotangazwa.
He is the weakest PM ambaye hajapata kutokea hapa Tanzania. JK anambuluza apendavyo na bado yuko tu amekomaa na u-PM! Halafu unakuja kusema eti ni shujaa!