LiverpoolFC
JF-Expert Member
- Apr 12, 2011
- 11,496
- 3,389
tangu asubuhi spika alionyesha dhahiri kuiua hoja ya zitto..lakini hoja iko pale pale
Haki haijawahi kushindwa hakika!
tangu asubuhi spika alionyesha dhahiri kuiua hoja ya zitto..lakini hoja iko pale pale
Mkuu vuta subira kanuni zitafuatwa, gharama za kuteua waziri mpya ni kubwa sana lazima ufanye kwa uangalifu mkubwa.Hio ndo sirikali. Hakuna cha kujiuzulu wl nn
Haya sasa, hayo ndiyo majibu ya waziri mkuu. Mko wapi mliotuletea uongo hapa mkidai mko jikoni? Kwanza mlianza na kikao cha wabunge wa CCM Kilichoongozwa na waziri mkuu, mkatuambia mawaziri nane wamejiuzulu.. Wajinga wakaamini. Leo mkaleta habari kutoka jikoni kuwa waziri mkuu anajiuzulu, tumesikia kilichotokea. Siku chache zilizopita niliweka bandiko hapa kuwa wananchi na wabunge wetu wazalendo, anayepaswa kuwajibishwa ni rais. Watu wakanipigia kelele hapa. Nchi za wenzetu wana akili kuliko sisi. Tunisia waliandamana moja kwa moja kwa ajili ya kumtoa rais, wakafanikiwa. Misri nako vilevile. Sisi tunalia na waziri mkuu, mtu anayopokea amri kutoka kwa mkuu wake. Nilitoa mfano pia kuwa, timu ya mpila ikifungwa tunalia na kocha? Au kapten wa timu. Nikaongeza pia, nyoka akikuingilia unapaswa kupiga kichwa au mkia? Bila kuchukua hatua zinazostahili. Tutaishia kupiga kelele, lazima tujiulize. Mawaziri hawa kiburi wanapata wapi? Nadhani majibu tunayo..
Kumbe ile habari iliyokanushwa jana na Ikulu juu ya kilichoandikwa na Tanzania Daima ilikuwa ni ya kweli? Basi hii ni balaa. Hapo wabunge wa CCM waliosaini petition matumbo moto.
Sasa tufanyaje? Toa muelekeo mkuu
Mkuu huko tunisia, misri hakuwezi kuwa model ya TZ,
huku ni ushabiki wa kisiasa na vyama. kule ilikuwa wananchi wote kwa ujumla dhidi ya Serikali.
kwa hiyo ni vitu viwili tofauti.
JK ni mwanajeshi wa kweli kimafunzo wakuu sio uamiri jeshi wa kupewa na katiba kama kina ben na mwinyi.
Pengine anamsubiri mkuu wa kaya arejee mazikoni amkabidhi barua ya kujiuzulu.
That's my wish and only hope, at the moment.
Waziri Mkuu katoa hotuba ya kufunga bunge (Hotuba nzima ipo post ya pili chini).
Hakuna Waziri hata mmoja aliyejiuzulu wala kuwajibishwa kama wengi walivyotarajia.
Spika kahitimisha kwa kuwataka wabunge wasichukiane nje ya Bunge kwakuwa yaliyojadiliwa bungeni ni sehemu ya kazi.
Ndugu . Pinda anazungumza kufunga kikao cha bunge.
Hotuba yake hii: