Mhe. Pinda aahirisha Bunge hadi Juni 12, 2012

Mhe. Pinda aahirisha Bunge hadi Juni 12, 2012

Jana huyu mama wakati akiliahirisha bunge ametoa kauli moja nzito sana ambayo nilitegemea palepale wabunge wote wangeng'aka lkn ikawa kimya.

Makinda alise" ndgugu zangu mawaziri mliosemwa hapa bungeni msichukie na kufika hatua ya kuumia bure, haya yaliyosemwa hapa ni maneno tu na yameishia hapahapa. Msiendelee kuyawaza sana wakati mwingine hata waliowasema wameshaondoka na hata hawayakumbuki"

Ndg. Zangu hii ni kauli inatolewa na spika tena mkuu wa bunge kwamba hawa wabunge wetu ni wapiga porojo tu, wakishatoka hapo yameisha na hata hawakumbuki nini walisema.

MY TAKE: kama wabunge hawataichukulia hatua kauli hii, natangaza rasimi mm sitakuwa na imani na mbunge yeyote tena.
Ana Makinda ni Mwanamke:smash:
 
Mimi nimechoshwa na unafiki wa wabunge wa ccm! Najipa subira kwenye hoja ya Zitto ya kutokuwa na imani na waziri mkuu. Kama hawatajitokeza kumuunga mkono na kufikisha idadi ya kumwondoa Pinda, idadi ambayo ni about 175, basi nitaamini kuwa walichokuwa wanakifanya bungeni na kwenye kikao chao ni igizo la kitoto sana na halichekeshi hata kidogo!

Na hapo nitawaunga mkono Zitto na wenzake kuzunguka nchi nzima kuwaelewesha wale waliowachagua wabunge hao maigizo wanayofanya ili watafakari upya kama walifanya sahihi au waliteleza. Bunge limekuwa likituonesha jinsi serikali inavyotudhalilisha watz na wabunge wanavyogeuka "mbwa koko" kwa kubweka bungeni na kufyata mkia kwenye vikao vya chama!
 
kama jadi yetu hatuna haja kuchukua hatua kwa maneno 'mazuri' yaliyosemwa na waziri mkuu.
Hiyo nayo itapita, hatupaswi kuitilia maanani ili tusiharibu utamaduni wetu tuliouzoea.
Hivyo chonde chonde tuisikilize tu ila tusichukue hatua kama ilivyo jadi yetu na serikari yetu ya ccm.
 
hebu nianze na kuomba samahani kwa mtazamo wangu,
inawezekana alimaanisha maneno yale ya kashfa waliyokuwa wakiambiwa ila si katika kuwajibika kwa waliyotenda, mfano swala la waachie ngazi hilo ni lazima wawajike hata spika aseme nini. maneno yenyewe labda ile kuitwa mchwa, goigoi, majambazi, nk japo bado mwizi hawezi tuchagulia adhabu ya kumpa

Laiti kama ungesikiliza ama kuangalia bunge ungeja ni nini huyu mdau anaongea, kuna maneno hajayabainisha hapo maana aliongeza pia kwa kusema, "kitendo cha ninyi mawaziri kusemwa bungeni ni sehemu ya uwajibikaji"....

Hiyo inaonesha hakuna waziri atakaye adabiwa na Bunge, labda muujiza tu utokee Mkuu wa Kaya atumie mamlaka yake.
 
Inapotokea wengi wetu tulikuwa na great expectations kuwa Pinda atazungumzia kuwajibika kwa mawaziri, kitendo cha kutozungumza lolote kuhusu hilo, then kwetu Pinda hajazungumza kitu.

Hivyo tumeshaipotezea!.
 
Sio jambo la ajabu kwa viongozi wetu kutoa majibu mepesi kwa maswali magumu. Huyo mama ameongea kana kwamba vikao vya bunge vinatumiwa kama kijiwe cha kukutana kwa ajili ya kupiga soga na kusogeza muda tu na sio kujadili mambo muhimu kwa mustakabali wa Taifa.

Kwa mtindo huo ni bora bunge likafutwa kabisa kwani hivyo vikao vinaonekana kama moja ya mambo yanayofanywa kwa minajili ya kuhujumu uchumi wa Taifa letu.
 
CCM wamelogwa na wamepigwa upofu pia hasikii wala kuona upepo wa kisulisuli unavuma kwa speed ngapi, hii ni ahueni yetu ya kufanyakazi, na waendelee kula na kunywa walewe tena wavimbiwe nasi tubebe mateka wetu.
 
Aliona cha maaana ni kuipongeza simba s.c!! ......Lol
 
Inapotokea wengi wetu tulikuwa na great expectations kuwa Pinda atazungumzia kuwajibika kwa mawaziri, kitendo cha kutozungumza lolote kuhusu hilo, then kwetu Pinda hajazungumza kitu.

Hivyo tumeshaipotezea!.


Hata sikumbuki vizuri jana waziri mkuu Pinda kazungumza kitu gani wakati akitoa hoja ya kuahirisha bunge.

Nimejitahidi kuvuta kumbukumbu nimekumbuka tu salamu za pongezi kwa Joshua Nassary na Cecilia Pareso pamoja na kuwaombea afya njema mawaziri Mwakyembe, Mwandosya na Magufuli.
 
Kama raisi amesema ni Upepo tu utapita,Spika atasema nini zaidi ya kuendeleza sera za serikali yao ya Kiswahiba?,Ipo siku tutafikia ya Tunisia,Misri,Libya kwani hakuna marefu yasiokuwa na ncha,M4C will take over,PEOPLEsssssssssssssssssssssssssssssssssss!
 
Inapotokea wengi wetu tulikuwa na great expectations kuwa Pinda atazungumzia kuwajibika kwa mawaziri, kitendo cha kutozungumza lolote kuhusu hilo, then kwetu Pinda hajazungumza kitu!.
 
Yeye anatimiza kazi yake kama kazi zingine.
Hana wajibu wowote kwa watanzania wa nchi hii au wa jimbo lake.
Yupo pale kwa maslahi ya chama kinachotawala na inabidi alinde serikari ili aendelee kuwa kazini.
Wananchi hawana masikio wala hawaoni.
 
Hasira za wananchi kwa wanamagamba ndio zinazidi kuongezeka siku hadi siku,wasifikiri kupotezea issue za msingi kutawaokoa hata siku moja.Leo nilikua naelekea kazini na katika daladala mjadala ulikua ni kwamba CCM sasa basi.Nakubaliana na mawazo ya sugu kwamba wajifunze ili wawe wapinzani bora
 
Napata hasira wadau..wametufanya mabwege..mbona uchaguzi mbali ivyo? MAMA MAKINDA KTK IYO POSITION ALIYOPO SI KWA MASLAHI YA WATZ YEYE NI 'MCHUMIA TUMBO'
 
Jana huyu mama wakati akiliahirisha bunge ametoa kauli moja nzito sana ambayo nilitegemea palepale wabunge wote wangeng'aka lkn ikawa kimya.

Makinda alise" ndgugu zangu mawaziri mliosemwa hapa bungeni msichukie na kufika hatua ya kuumia bure, haya yaliyosemwa hapa ni maneno tu na yameishia hapahapa. Msiendelee kuyawaza sana wakati mwingine hata waliowasema wameshaondoka na hata hawayakumbuki"

Ndg. Zangu hii ni kauli inatolewa na spika tena mkuu wa bunge kwamba hawa wabunge wetu ni wapiga porojo tu, wakishatoka hapo yameisha na hata hawakumbuki nini walisema.

MY TAKE: kama wabunge hawataichukulia hatua kauli hii, natangaza rasimi mm sitakuwa na imani na mbunge yeyote tena.

Asante mkuu kwa kulileta hili.Binafsi kauli hii iliniudhi sana,na kwa mtazamo wangu ilionyesha kuwa Bunge haliko tayari kuisimamia na kuiwajibisha serikali.Amejaribu ku-haribu vuguvugu linaloendelea kwa kuwapa nguvu mawaziri kwamba wanachofanya pale bungeni ni maigizo tu.Wasiwe na wasiwasi na lisiwakoseshe usingizi.....ni kauli ya kuudhi sana...
 
Haya maneno si dharahu kwa Wabunge tu bali kwa Watanzania wote hapo ndo tujue Bunge kimekuwa chombo cha kupuuzwa na serikali akisikilizwi tena na imani kwa wananchi kuhusu chombo hiki inaanza kupotea ebu tushikamane turudishe heshima ya Mbunge anapokuwa anakemea uwajibikaji mbovu wa serikali. M4C
 
CCM walidhani kumtosa SITTA wameweza lakini kumbe walijidanganya,kihistoria huyu mama Makinda tangu alipomaliza shule na kuingia serikalini hajawahi na hata leo hana chochote alichowahi kulifanyia taifa
 
A Makinda aliwekwa pale na MAGAMBA ili kutetea maslahi yao!
hivyo siwezi shangaa alichokiongea wakati wa kuhairisha bunge!
 
ccm imekwisha haina jipya na wanatudharau watanzania ...spika Hawezi kuongea kana kwamba anaongea na watu wasio na uelewa ...yana mwisho ..na ndio huu...
 
hutakuwa na Imani na MBUNGE WA CCM. kwakuwa wao ndio chanzo cha uozo kwa kuwa ndio walio wengi Bungeni. lakini kwa upande wa upinzani wamejaribu vya kutosha. mpaka kuweka itikadi za kichama na kutanguliza utaifa ili kuungana na wabunge wa ccm kutetea haki ya Mtanzania. lakini bado wabunge wengi wa ccm ni wachumia tumbo wanajali ya kwao.

ninashauri tufanye maandamano mpaka ikulu na nchi nzima ya kutokuwa na imani na rais, ikimaanisha kuwa hata yeye ni sehemu ya matatizo haya. uchaguzi urudiwe upya.

napenda kuwaunga mkono Chadema kwani wamejaribu kila linalowezekana ili kutetea maslahi ya watanzania lakini bado serikali haijaonyesha njia za dhati za kutetea rasilimali za taifa. Ikiwa mkakuzi wa hesabu za serikali amefanya kazi yake kwa nini vyombo vingine vya serikali vinashindwa, tatizo liko kwa rais. hata baraza la mawaziri likivunjwa bado naona matatizo kama haya kuendelea iwapo hatua za kisheria hazitachukuliwa kwa wezi hawa na sio kuishia kwenye kujiuzulu tu.
 
Back
Top Bottom