Mhe. Pinda aahirisha Bunge hadi Juni 12, 2012

Mhe. Pinda aahirisha Bunge hadi Juni 12, 2012

Hotuba iliyotolewa na Mh M.Pinda Waziri mkuu wa Tanzania inatufundisha Watanzania tuwe na mioyo ya kuvumiliana na kustahimiliana katika kuelekea katika maamuzi magumu kwa mustakabali wa amani na utulivu wa taifa letu.

Kwa Watanzania wapenda amani hutuba ya Pinda ya kuhairisha bunge ni hutuba ya kishujaa na ya kizalendo.

Vipi bwana? Inakuwaje usiku wote huu umelewa?
 
Shujaa anayedharauliwa?

Skendo ya Jairo ilimdhalilisha sana, na bado JK na Ikulu kwa kiburi walicho nacho wamegoma kutekeleza maazimio ya Bunge na ndo maana Spika wa Bunge alijua kwamba swala hilo lingejadiliwa lingewapandisha hasira wabunge.

Serikali yenu sio ya kubembelezana, ukiwabembeleza hakuna watakachotekeleza, na ndio maana mawaziri wanajibu mbovu na kujifanyia wanayotaka.

Wakati wa skendo ya Jairo, alisikika akisema kwamba hata wachonge sana hatatoka, na mpaka leo kweli bado yuko na hakuna walichomfanya.

Mbaya zaidi IKULU kupitia Luhanjo ikamsafisha na kumrudisha kwa mbwembwe na kupokelewa akisukumwa kwenye gari. Hayo kama sio matusi kwa Waziri Mkuu ni nini? Pinda alitutangazia watanzania kwamba kama angekuwa yeye ndo mwenye final say, angemfuta kazi Jairo. Juzi amekaa kwenye kikao mpaka usiku, wakakubaliana kwamba mawaziri 8 waondoke, nini kimetokea? Huyo ndo shujaaa? Angekuwa shujaa kweli angesema anajiuzulu, hapo ningemuona ni shujaa anayelinda heshima yake baada ya kudhalilishwa mara 2 tena mbele ya watanzania wote. Kwa kuwa kilichotokea sio kwamba ni vikao vya siri, bali ni maamuzi ya wazi yaliyotangazwa.

He is the weakest PM ambaye hajapata kutokea hapa Tanzania. JK anambuluza apendavyo na bado yuko tu amekomaa na u-PM! Halafu unakuja kusema eti ni shujaa!

umeongea point sana, leo hii kama kweli PM anaona maamuzi yake au direction anayotaka nchi na mawaziri wachukue haiendani na Rais basi alitakiwa ajiuzulu, ndivo nchi zingine zinavofanya. Watu hawampendi lowassa lakini nina uhakika lowassa angekua bado PM leo hii sidhani kama huu upuzi wa leo ungekuwepo. at least lowasa alikua anaweza kusimama vizuri na kubishana na rais huyu wa sasa hawezi ni mpole mno
 
Hotuba iliyotolewa na Mh M.Pinda Waziri mkuu wa Tanzania inatufundisha Watanzania tuwe na mioyo ya kuvumiliana na kustahimiliana katika kuelekea katika maamuzi magumu kwa mustakabali wa amani na utulivu wa taifa letu.

Kwa Watanzania wapenda amani hutuba ya Pinda ya kuhairisha bunge ni hutuba ya kishujaa na ya kizalendo.

noted.
 
Ushujaa Gani aliouonyesha badala ya yeye kuzungumzia matatizo yaliyopo yeye akawa anaipongeza Simba.

it was crup. Tuvumilie nini wakati wameshaimaliza nchi?
 
Mke wa Pinda ulikuwepo bungeni, huwezi kumshauri mumeo ajiudhuru ili angarau alinde heshima yake? Hana jamaa, ndugu au wazazi wake??? Pinda mbona unadharauliwa sana na jeykey?? We vipi wewe?? Mbona huna maamuzi magumu wewe?? Unatisha sana mtoto wa mkulima, sijui mkulima gani huyo! Utaficha wapi uso wako?
 
kusoma au kusikiliza hotuba ya pinda ni sawa na kupoteza muda
 
Hotuba ya Kishujaa hotuba ya kizalendo. Nilishasahau maana ya maneno mzalendo na shujaa, mwenye kuyajua naomba anisaidie.
 
Pinda kwa nini usijitambulishe kwa jina lako halisi? Pamoja na hayo, sijaona waziri mkuu aliyepwaya katika nchi hii tangu uhuru kama wewe. Sijui kwa nini huchukui uamuzi wa kujiuzuru. Rais anakudharau, mawaziri wanakudharau na wananchi wanakudharau. Wewe mwenyewe huoni!?
 
Natangaza rasmi kutokusoma thread za mr emmy, tume ya katiba na wengine kwani zinafanya uwezo wa kuchambua mambo ushuke. Hata post nitakuwa naziruka.
 
Hotuba iliyotolewa na Mh M.Pinda Waziri mkuu wa Tanzania inatufundisha Watanzania tuwe na mioyo ya kuvumiliana na kustahimiliana katika kuelekea katika maamuzi magumu kwa mustakabali wa amani na utulivu wa taifa letu.

Kwa Watanzania wapenda amani hutuba ya Pinda ya kuhairisha bunge ni hutuba ya kishujaa na ya kizalendo.

Bila hiana, kweli inahitaji ushujaa wa ziada kutetea magamba ya nyoka yasiyokubali kukoboka. You are very right mkuu. Sio siri. Unatakiwa kuwa gamba gumegume zaidi ya magamba hayo.
 
mtoa nada unapima hasira za watz. Hv kweli ushujaa uko hivo ; unamfumania mkeo unasema nitatoa maamuz siku za mbelen! we kweli hamnazo!!!
 
Natangaza rasmi kutokusoma thread za mr emmy, tume ya katiba na wengine kwani zinafanya uwezo wa kuchambua mambo ushuke. Hata post nitakuwa naziruka.

Unadhani itakuwa solution? Mbona unataka kukimbia tatizo dogo kama hili badala ya kulitafutia ufumbuzi. Kwa mtindo huu basi na ww huna haja ya kumlaumu pm kwa hotoba yake
 
Jana huyu mama wakati akiliahirisha bunge ametoa kauli moja nzito sana ambayo nilitegemea palepale wabunge wote wangeng'aka lkn ikawa kimya.

Makinda alise" ndgugu zangu mawaziri mliosemwa hapa bungeni msichukie na kufika hatua ya kuumia bure, haya yaliyosemwa hapa ni maneno tu na yameishia hapahapa. Msiendelee kuyawaza sana wakati mwingine hata waliowasema wameshaondoka na hata hawayakumbuki"

Ndg. Zangu hii ni kauli inatolewa na spika tena mkuu wa bunge kwamba hawa wabunge wetu ni wapiga porojo tu, wakishatoka hapo yameisha na hata hawakumbuki nini walisema.

MY TAKE: kama wabunge hawataichukulia hatua kauli hii, natangaza rasimi mm sitakuwa na imani na mbunge yeyote tena.
 
Wewe ni kama kipofu aliyeona Punda. Unaona kuwa kila kitu ni JF tu.

Pinda ana mambo ya kumpindisha zaidi ya JF.

Fikiri!
kwa hiyo huo utumbo uloandika unaona umefikiri,!hotuba yake ya kipuuzi ya jana haiwezi kupongezwa na tahaira yoyote isipokuwa mwenyewe & u!
 
effect za kupotezea hii issue ni kubwa kwa CCM kuliko wangechukua hatua, wananchi wengi wamekuwa disappointed sana , hasira za wananchi dhidi ya magamba zinazidi kushika kasi kwani serikali inadhihirisha kuwa haina nia ya dhati ya kupambana na viongozi wasio waadirifu, watatambua madhara ya hii kitu ikisika siku ya kudumbukiza kura kwenye box
 
Kinachofuata ni M4D (Movement for Destruction) wasubiri yatimie.
 
hebu nianze na kuomba samahani kwa mtazamo wangu,
inawezekana alimaanisha maneno yale ya kashfa waliyokuwa wakiambiwa ila si katika kuwajibika kwa waliyotenda, mfano swala la waachie ngazi hilo ni lazima wawajike hata spika aseme nini. maneno yenyewe labda ile kuitwa mchwa, goigoi, majambazi, nk japo bado mwizi hawezi tuchagulia adhabu ya kumpa
 
Back
Top Bottom