Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,902
- 945
Mjumbe wa Baraza la Jumuiya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya UWT Taifa, Mhandisi Fatma Rembo akizungumza na Wanawake wa Mafinga Mji, Iringa amewaomba waendelee kushikamana kwani tunaelekea kwenye Uchuguzi wa Serikali za Mitaa mwaka 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 tunapaswa kushirikiana, tunapaswa kuandaa majeshi yetu, kuongeza wanachama, kuhakiki wanachama ili kuhakikisha tuna wanachama hai, tunatakiwa tujiandae vyema kwani wenzetu pia wanajiandaa chini kwa chini.
"Sisi mwaka 2025 tuna jambo letu, ambaye ni Dkt. Samia Suluhu Hassan na hakuna mwingine. Ninyi wenyewe mnaona mambo makubwa anayoyafanya siyo tu kwenye Taifa lakini pia kwenye Mkoa wa Iringa mnaona mambo makubwa anayoyafanya Mheshimiwa Rais" - Mhandisi Fatma Rembo, Mjumbe wa Baraza Kuu UWT Taifa
"Sisi tuna wajibu mkubwa wa kumbeba Mama Samia Suluhu Hassan kwa kumsemea mazuri anayoyafanya katika nchi hii. Wanawake ndiyo Jeshi kubwa analolitegemea, tumbebe Mama Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2025" - Mhandisi Fatma Rembo, Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa
Aidha, Mhandisi Fatma Rembo ametoa Shilingi Milioni Moja (1,000,000) mchango wa kikundi cha Wanawake wa Kata ya Nzihi kama kumuunga mkono Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Mhe. Rose Cyprian Tweve ambaye naye amechangia Shilingi Milioni Moja.
#UWT IMARA JESHI LA MAMA
#KAZIIENDELEE
"Sisi mwaka 2025 tuna jambo letu, ambaye ni Dkt. Samia Suluhu Hassan na hakuna mwingine. Ninyi wenyewe mnaona mambo makubwa anayoyafanya siyo tu kwenye Taifa lakini pia kwenye Mkoa wa Iringa mnaona mambo makubwa anayoyafanya Mheshimiwa Rais" - Mhandisi Fatma Rembo, Mjumbe wa Baraza Kuu UWT Taifa
"Sisi tuna wajibu mkubwa wa kumbeba Mama Samia Suluhu Hassan kwa kumsemea mazuri anayoyafanya katika nchi hii. Wanawake ndiyo Jeshi kubwa analolitegemea, tumbebe Mama Samia Suluhu Hassan ifikapo mwaka 2025" - Mhandisi Fatma Rembo, Mjumbe wa Baraza Kuu la UWT Taifa
Aidha, Mhandisi Fatma Rembo ametoa Shilingi Milioni Moja (1,000,000) mchango wa kikundi cha Wanawake wa Kata ya Nzihi kama kumuunga mkono Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Iringa, Mhe. Rose Cyprian Tweve ambaye naye amechangia Shilingi Milioni Moja.
#UWT IMARA JESHI LA MAMA
#KAZIIENDELEE