UWT yamchangia Samia Suluhu Hassan Tsh milioni 2 kwa ajili ya kuchukulia fomu ya urais ifikapo mwaka 2025

Hamduni

Senior Member
Apr 25, 2020
155
108
🗓️ 26 Machi, 2024

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda kwa pamoja wametimiza ahadi yao kwa kumpatia Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiasi cha Tsh Milioni 2,000,000/= kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea nafasi ya Urais ifikapo mwaka 2025.

UWT wamefanya hivyo ikiwa ni ishara ya kukubali na kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 kwa kishindo kikubwa katika miaka 3 ya uongozi wake tangu mwaka 2021 - 2024.

Fedha hizo wamezikabidhi kwa Ndugu. Issa Haji Gavu ambaye ni Katibu wa NEC, Idara ya Oganaizesheni wa CCM Taifa, aliyekuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Kumshukuru Rais Samia lililofanyika katika Ukumbi wa Mkuki House Jijini Dar es salaam.
 
Fomu ya kugombea Urais CCM inauzwa shilling ngapi?

Kwa nini UWT hii pesa wasipeleke kusaidia watoto yatima.

Rais anapaswa kukemea huu uchawa uliopitiliza, tunajenga Taifa la hovyo kabisa la walaghai wachawi na wanafki.
 
Endeleeni tu kumchuria
photo_2021-08-11_09-06-26.jpg
 
Hao wanawake wapuuzi kwelikweli kwa kipi alichokifanya Hadi agombee urais. Wakilazimisha wajiaNdae kupata kura 2 kati ya watz milioni zaidi ya 16. Na uzuri uchaguzi Huu wananchi tutazilinda kura zetu kama walivyofanya Ivory Coast
 
Sijui kwanini kujikomba imekuwa fasheni kiasi hiki.

Hiyo Fomu ni sh ngapi?

Hadi sasa kachangiwa na magroup zaidi ya 3, ambapo Walimu walianza mwaka jana walipokuwa kwenye vikao vyao kule Mwanza.
 
🗓️ 26 Machi, 2024

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda kwa pamoja wametimiza ahadi yao kwa kumpatia Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiasi cha Tsh Milioni 2,000,000/= kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea nafasi ya Urais ifikapo mwaka 2025.

UWT wamefanya hivyo ikiwa ni ishara ya kukubali na kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 kwa kishindo kikubwa katika miaka 3 ya uongozi wake tangu mwaka 2021 - 2024.

Fedha hizo wamezikabidhi kwa Ndugu. Issa Haji Gavu ambaye ni Katibu wa NEC, Idara ya Oganaizesheni wa CCM Taifa, aliyekuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Kumshukuru Rais Samia lililofanyika katika Ukumbi wa Mkuki House Jijini Dar es salaam.
Akili za macc shida sana, wengine ni kuimba mama, mama tu hata hawajielewi huku wengine ni majitu mazima kuliko huyo mama☹️. Sasa hapa nchi lazima iwe ya kilevilevi tuu!
 
Juzi alikataa ye Hana chawa,makundi Wala upande!!

Sasa anaruhusuje haya!!?

Hawa ndio wanamsaidia mpinzani wake apite bila kupingwa na chama!!
 
UWT YAMCHANGIA DKT. SAMIA SULUHU HASSAN KIASI CHA TSH MILIONI 2 KWA AJILI YA KUCHUKULIA FOMU YA URAIS IFIKAPO MWAKA 2025

🗓️ 26 Machi, 2024

Jumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT) ikiongozwa na Mwenyekiti wake Ndugu. Mary Chatanda kwa pamoja wametimiza ahadi yao kwa kumpatia Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, kiasi cha Tsh Milioni 2,000,000/= kwaajili ya kuchukulia fomu ya kugombea nafasi ya Urais ifikapo mwaka 2025.

UWT wamefanya hivyo ikiwa ni ishara ya kukubali na kuunga mkono juhudi za Rais Dkt. Samia katika utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020 - 2025 kwa kishindo kikubwa katika miaka 3 ya uongozi wake tangu mwaka 2021 - 2024.

Fedha hizo wamezikabidhi kwa Ndugu. Issa Haji Gavu ambaye ni Katibu wa NEC , Idara ya Oganaizesheni wa CCM Taifa , aliyekuwa Mgeni rasmi katika Kongamano la Kumshukuru Rais Samia lililofanyika katika Ukumbi wa Mkuki House Jijini Dar es salaam.
IMG-20240327-WA0027(1).jpg
IMG-20240327-WA0026.jpg
 
Nia ni njema mama achukue fomu ya mi5 tena. Ninachoomba kusaidiwa hapa nikwamba hizi jumuiya hazifahamu kuwa swala la fomu lilishamalizwa na makundi flani ikiwemo waalimu? Au zoezi la kumchangia mama fomu halina kikomo?
 
Hata wakuu wa shule tanzania walichangishwa hela kwa ajli ya kumchungulia fomu huyo mama
 
Kuna mkutano mwingine wamechanga milioni 26. Kweli CCM ni tajiri ila watanzania ni maskini
 
Back
Top Bottom