Sikupenda ule ushabiki wa hoja aliounyesha Wenje, jinsi alivyofoka na kufurahia hisia za unyonge waliopata baadhi ya wabunge wateule. Sikupenda, LAKINI Wenje alikuwa na ujumbe MZITO SANA.
Madai ya Wenje ni uwepo wa vikao haramu vikiongozwa na viongozi wa serikali ambao wamekuwa wakiwapiga msasa hawa wabunge! Hii ndio tatizo. Dr Kawambwa - alitaka kulia huyu- alivyokuwa anajieleza kwamba yeye hakuwaita bali watu wale kutoka kwenye taasisi za elimu waliomba kukutana naye. Inawezekana huyu rafiki yangu anasema kweli, lakini Shukuru amekuwa anatumiwa- yeye sio mwanasiasa- lakini kutokujua kusema HAPANA ndio kunamtesa. Inawezakana sana baadhi ya haya mapandikizi ndani ya kundi la 201 ndio wamemponza kwa kuhamasisha wenzao waende kwa waziri naye akawakubalia. Agenda za huko nyumbani kwa mawaziri hawa ndio alizokuwa anazilenga Wenje.
Kwa nini makundi kama haya yasikutane kwenye uwazi na mchana, maana kazi za Bunge ni aidha jioni kuanzia saa 10 au saa 4 had 7. Kama agenda ni za wazi wangekutana ndani ya majengo ya bunge tuseme saa 2-4, au 8-10. Mbona inawezekana. Lakini pongezi Prof Jumanne -- yeye alikiri kukaribisha na kuwakarimu! Yote ni mamoja tu, ni jinsi ya kuchochea fikira. Na ndugu zangu wengine kina Dr Michael Francis- ni muhimu wakaelewa wametumwa na taasisi zao na wala sio kwenda kufanya makundi kwa kujikusanya kwa wanasiasa! Mtachafuliwa.
Nilimsikitikia sana yule Mama wa Kimasai maana hakujua kinachoendelea. Ulikwenda kupigwa msasa Mama na umeshapigika na kwa kuwa hukuwa na shida na vijisent vyao kwa sababu una vyakula na mifugu ya kutosha, walikufaidi kikweli kweli. Umekuwa mfuasi wao kwa gharama ndogo sana. Kwa lugha nyingine UMEJIUZA! Wenje alikuwa sahihi lakini lugha ndio shida hasa kwa ndugu zangu wa kipande kile cha Wenje