Mh. Mnyika kwa hili umepotoka!...

Hapo kwenye red colour, angalia sana usije ukawa umenasa kwenya ntego wa unafiki wa hali ya juu sana.
Kabla ya kuandika hayo hapo kwenye red colour, ulitakiwa kufanya utafiti uone kama kweli katika nchi hii ya Tanzania jambo hili linafanyika, au ni theory tu inayotumika ili kunyonya wafanyakazi.

Kifupi hali katika Tanzania yetu hii iko hivi:-

  • pension schemes sio kwa ajili ya kukusaidia utakapo kuwa mzee, ila ni kwa ajili ya kukusanya pesa kwa ajili ya matumizi ya serikali, mfano, wafanyakazi wa iliyokuwa jumuiya ya afrika mashariki, wote sasa ni wazee, hebu niambie wanalipwa pension kiasi gani ???
  • je?, unajua pension wanayolipwa wastaafu kwa sasa ??? mfano, aliyewahi kuwa mkuu wa majeshi Tanzania, kwa sasa ni mstaafu anayelipwa Tzs. 50,000 (Tzs. elfu hamsini tu) kwa mwezi. Hii inamsaidiaje yeye kama mzee mstaafu.

Angalizo kwa wote:
Kabla ya kutoa maoni kwenye mada nzito kama hii ya maswala ya pension, fanya utafiti kwanza, vinginevyo, wewe ni mnafiki tu, au wewe pia ni mmoja wa wanaofaidika na udhalimu huu wa kunyima wafanyakazi haki yao ya mafao.


Be blessed, Naanza kuamini kuwa wananchi tumeshajua kuwa maisha yetu yako mikononi mwetu,no one cares for our future,labda hao SSRA wangetuambia vp thamani ya fedha uliyoweka kwa kipindi hicho itakuaje ukizingatia kuwa shilingi yetu inaporomoka kila uchao,pia kwa jinsi wastaafu wetu wanavyonyanyasika hadi sasa sijaona vivid example ya kujustify hicho kiini macho cha kuwa eti 'wanaamini hiyo pensheni itakusaidia',pia nataka suala la mfuko upi ujiunge nalo liwe kwa mtumishi manake mwajiri anakuamualia yeye na huna choice! wote wenye kudhani watatudanganya milele muda wao umekwisha, sema hapana kwa unafki na wizi wa jasho la wafanyakazi !
 
Kuna wachangiaji wanasema Mnyika alishindwa kuzuia mswada usiwe sheria kwa sababu wabunge wa wapinzani ni wachache. Swali, je sasa hivi anavyopeleka hoja bungeni wabunge wa upinzani wameshakuwa wengi kuliko wa CCM?
Mr Gamba!!!!! kwa vile wanatia sahihi tutawajua wale wanafiki. badala ya neno Ndiyooooooo ambalo huwa hatujui ni nani kasema
 
Wakuu kuna maneno yametumika humu ambayo yameutia ukakasi ubongo wangu!.. Kuna tofauti ya kumkosoa mtu na kumkejeli.. Kunafauti ya kukubaliana na mtu na kupingana na mtu.

Bado sijaelewa lengo la mtoa mada kuwa "MNYIKA AMEPOTOKA" na anatafuta "CHEAP POPULARITY". Naomba niwekwe sawa hapo ili nilete uzi wangu hapa.

Ahsanteni
 
Umejionyesha dhahiri ulivyo mfano halisi wa wataalam feki, usiyefahamu hata asilimia inayo changiwa na mwajiriwa na mwajiri! Analysis yako si ya kitalaam hata kidogo, ni uongo ambao siku zote mnautumia kuwahadaa watanzania ati wasichukue mafao yao wanapo maliza mikataba yao, ati wasubiri hadi uzeeni.
Si sahihi hata kidogo kumkatalia mtu anayemaliza ajira yake ya mkataba kabla ya umri wa kustaafu ati asichukue mafao yake. Nadhani njia mojawapo ya kuimarisha sekta binafsi ni kuwaruhusu wanaomaliza mikataba yao ya kazi kabla ya umri wa kustaafu kuchukua mafao yao na kujiajiri. Sasa hivi kuna vijana wengi sana wanamaliza vyuo vikuu na hawapati ajira kwa sababu kwa miaka mingi tumetegemea sekta rasmi kama mwajiri mkubwa! Sitaki watoto wangu wakimaliza elimu ya juu wahangaike kutafuta ajira serikalini ambazo hazipo. Si vibaya kuiga mambo mazuri kutoka kwa wenzetu wa magharibi; ambapo tumeona watoto wakiajiriwa kwenye biashara/kampuni ya familia. Sasa tukitegemea mfumo huu wa kufanya kazi na kulipwa mafao on retirement age hatufiki huko.
 
Hivi Mnyika alikuwa wapi wakati mswada unapitishwa bungeni?

nadhani mnyika sio wa kulaumu ila walioleta huo mswaada.na ukiangalia pia popularity ya wabunge ndo utajua wanye tatizo ni kina nani. ni mara ngapi wapinzani wemetoa hoja nzito na zenye maslahi kwa taifa wakasikilizwa? inawezekana wabunge walio wengi walikuwa tasyari wameshaaambiwa waupitishe mswaada huo kwa maslahi binafsi ya serikali. kama unakuwa na kumbukumbu serikali ndo mkopaji mkubwa wa fedha hizi za mifuko ya hifadhi ya jamii na ina deni kubwa sana. kuficha aibu ni lazima watu wengi wazuiwe kuchukua mafao ya kujitoa.

huyo ndugu aliyeanzisha thread hii inawezekana kuna mambo kayaoversee kwa kuwa kazi za bongo hapa ni za mashaka sana. mikataba ni mwaka mmoja, miezi sita n.k. sasa mtu kafanya kazi miezi sita/mwaka akaachishwa/akaacha asubiri mpaka miaka 55?walion na mikataba ya maisha kazini sheria hii inawafaa kini sio kwa mazingira haya ya ajira za tanzania. mfanyakazi amekuwa sehemu ya kufanyia mazorezi ya makato kwa kila kitu, ukija paye, kodi kwa kmila anachokiconsume, mifuko ya hifadhi nk,
 
Sober, Mnyika hajakosea isipokuwa wewe ndio unaonekana una masilahi ya moja kwa moja na jambo na wewe inaonekana umejawa na uccm zaidi kuliko utanzania na watu kama nyie hamtakiwi tanzania yetu,ukweli ni kwamba hii sheria lazima ibadilike kwa sababu nyingi pesa ya mtu unaipangiaje madhalani nimeamua kufanya kazi kwa miaka kumi and nichukue nijikite kwenye ujasiliamali wewe unazuia na life expectancy kwa taarifa yako haizidi miaka 48.

Na hao unaowasaidia wanataka hizo pesa kwa manufaa yao kupitia ufisadi mkubwa kwa tanzania tulipofikishwa wacha kila mtu atunze mali zake maana waliopewa dhamana hawaaminiki tena mbele ya macho ya watz.kwa hiyo hoja yako haina mashiko mchumia tumbo mkubwa wewe
 
Last edited by a moderator:
Mu-Israeli
Ungesubili kuchukua kwa hiyo miaka 55 mafanikio uliyoyapa sasa ungeyapata wapi? I real agree and inline with you.
 
Last edited by a moderator:
huyu mtoa mada ndo anapotosha watu.
mimi nina mshahara wa laki tano mkataba wangu ni wa miaka miwili sasa na nina miaka 40 kama sirika halijaniongeza mkataba ina maana nitaacha kazi nikiwa na 41 hivyo kwa mujibu wa sheria ya sasa nitasubiri miaka 14 ijayo mpaka mwak 2027 ndio nianze kulipwa tsh 500000;
turudi nyuma miaka 15 iliyopita 1997 kilo ya sukari ilikuwa sh ngapi sement,bati nyama,mchele nk chukua kiwango cha mwaka huo 1997 halafu angalia mwaka huu mfumuko ni kiasi gani zidisha miaka 15 ijayo kama hujakuta kama laki tano hata mfuko wa sukari kilo 50 haziwezi kununua,hapo utajua ni kwa nini watru wanaipigia kelele hii sheria.
nitakukubalia tu kama utamlaumu mnyika kuwa wakati sheria ikipitishwa alikuwa wapi.

vilevile usilinganishe mafao ya wenzetu ulaya na tanzania.
 
Mnyika ni MCHEMFU nasema kila siku humu ndani, na bado mtayaona mengi kwa huyu kijana. Angekuwa mti wa mbuyu tusingesema hafai kwa kuni wala kwa mbao:israel::israel:
 
Andika hivi "Nina maoni tofauti na ya mheshimiwa Mnyika kuhusu mafao ya kujitoa"


Sijui mwenzangu unalielewaje neno KUPOTOKA!

Lakini kwa vile hapa sio mashindano ya semantics, naomba upendekeze neno ambalo litakufurahisha wewe pamoja na wengine waliolichukulia negatively hilo neno.

Nami nitarekebisha title ya uzi huu.
 
Mimi ni mmoja wapo wa wachangiaji katika PSPF na fao la kujitoa halipo. lakini nionavyo wangeacha fao hilo liendelee kutolewa na mifuko iliyokuwa nalo ili mtu awe na choice ama kuchukua mafao mara anapojitoa au asubiri afikie umri wa miaka 55. lakini pia ingetusaidia na sisi wengine tuliopo kwenye mifuko kama PSPF pengine kuamua kuhamia mifuko yenye mafao kama hayo maana siku hizi sheria inaruhusu kuhama.
Nionavyo waliobadili sheria walilenga pia pamoja na mambo mengine kuondoa uwezekano wa wafanyakazi kuhamia mifuko fulani yenye mafao yanayopendwa kuliko mifuko mingine.
 
Kwa jinsi nilivyoelewa ni kwamba sheria mpya inataka mifuko hii kufanya kazi kwa kanuni ya solidarity kama ilivyo bima, kumaanisha kwamba iwapo mtu hatafikisha umri husika au kuchangia kwa muda wa miezi 180 basi anapoteza haki yote. Sio kwamba anasubiri afikishe miaka 55!
Tatizo lililopo ni kwamba utaratibu uliokuwepo awali ulikuwa ni mzuri zaidi kwa mchangiaji, na kuleta utaratibu unaombana mchangiaji inakuwa ni kutoka kwenye good kwenda kwenye bad. Hapo ndipo shida ilipo!
Ugomvi wangu mimi na wanasiasa wetu ni ujanjaujanja wa kutumia maumivu ya watu kujiingizia umaarufu. Mswada huu umejadiliwa bungeni. Ukaptishwa. Idadi ya wabunge haijabadilika. Kwanini mbunge aamke miazi kadhaa baada ya kupitishwa mswada kuwa sheria, akijidai kaguswa sana na jinsi unavyomuumiza mchangiaji? Mbona mswada wa katiba mpya ulipoonyesha mapungufu waliact promptly, hawakukubali mpaka kimeeleweka, (ingawa nusu kueleweka)?
 
Kwani, kwa nchi zote kusini mwa sahara kuwa na sheria aina moja kuhusu mafao ni lazima Tanzania ifuate? Halafu, huyu mtu anapofikisha miaka 55 na akawa na akiba ya mil 4, itamsaidiaje kumalizia sehemu ya maisha yake ikiwa mliamini kuwa alipokuwa na miaka 45 angeshindwa kumudu maisha yake baada ya mafao? Kama mtu huyu aliachishwa kazi akiwa na miaka 45 na akiba yake ni mil 4, na hakubahatika tena kuajiriwa, hapa kati anaishije? Ni lini serikali yetu ilifikia hatua ya kuwajali watumishi wake kiasi hiki? Unamjali kwenye mafao tu au unapaswa kumjali katika mchakato mzima wa maisha yake hapa Tanzania na duniani? Ndugu yangu Sober nawe kajipange tena.
 
Last edited by a moderator:
Kwa Tanzania, kwa vile majority ya watanzania hawana social security na wamesurvive, basi wamethibitisha kuwa it is possible to make it bila social security. Hivyo basi, swala la mtu kujiunga na social security liwe ni optional, anayetaka ajiunge asiyetaka aweke pesa yake mfukoni leoleo.
 
Mkuu haijalishi nipo wapi.

Ila ukiingia kwenye website ya PPF utaona sehemu inayosema mwanachama atachangia asilimia 5% ya mshahara na mwajiri atachangia asilimia 15% ya mshahara, ukijumlisha unapata hiyo 20% uliyoongelea. Na hata NSSF wanaweza kuchangiwa kwa uwiano huo huo kama mwajiri akiona inafaa. hivyo hoja ya kuwa kila mwezi unabakiwa na asilimia 95% ya mshahara tena bado ukiwa na nguvu zako inasimama.

Pensheni kwa wazee wote nchini ni wazo zuri sana, na hakika ni ndoto ya kila mtu. Ila kiukweli halitekelezeki ndani ya miaka 50 ijayo kwa ukuaji huu wa uchumi. Kwa Fertility rate yetu ya 5.4% na GDP Growth rate 7.5% itakua ni kujidanganya kuanza kuota kuwa sasa serikali itaweza kuwalipa pensheni ya kukidhi wazee wote.

Nadhani bado unakumbukumbu ya mgomo wa juzi wa madaktari na baadae waalimu. Serikali imeshasema ingawa nia ya kuwaboreshea mishahara wanayo lakini uwezo hauruhusu. Hili la pensheni kwa wazee wote litakua far fetched kweli.
Mimi nashindwa kuelewa unaongelea mshahara wa mfanyakazi wa wapi kama ni Tanzania basi unasahau makato mengi tu

maana tunalipa kodi pia (PAYEE) achilia mbali VAT za mtaani kwa kila manunuzi! huwezi kubaki na 95%.

Alafu asilimia itabaki hivyohivyo hata kama Gross ni 300,000/=, 250,000/= au 1,000,000/=. Lakini net pay zitatofautiana tu.

Usiongelee asilimia kwa ujumla kama wote tunalipwa sawa!.

Kuna watu net pay yao haitoshi matumizi kwa mwezi.

Hii unayoelezea hapa ni sawa na kusema "kama umeshindwa kununua mkate wa kula nunua keki ule"

HAKIKA ALIYESHIBA HAMJUI MWENYE NJAA!.
 
Wewe unaiga ya wenzako tu? Kwani sisi tz hatuwezi kuanzisha ya kwetu na tukawa pioneers? Kila Siku ni copy and paste tu. Hivi huoni ni tatizo mtu usubiri mafao mpaka uzeeke? Wewe ndio umpotoka sana saba. Unapenda kudesa kilavkitu,, hutaki tuanze Malta, shame o you.
 
Wakuu kuna maneno yametumika humu ambayo yameutia ukakasi ubongo wangu!.. Kuna tofauti ya kumkosoa mtu na kumkejeli.. Kunafauti ya kukubaliana na mtu na kupingana na mtu.

Bado sijaelewa lengo la mtoa mada kuwa "MNYIKA AMEPOTOKA" na anatafuta "CHEAP POPULARITY". Naomba niwekwe sawa hapo ili nilete uzi wangu hapa.

Ahsanteni


Lengo la mtoa mada ni kumnanga mh. Mnyika.

Ametumia neno kapotoka - kakosea, kaenda kombo, anafachofanya si sahihi nk.

Katumia neno anatafuta cheap popularity...- kuutaka umaarufu miongon mwa watanzania kwa hoja zisizo na mantiki (hoja butu/dhaifu)

Mim si mtaalam wa lugha kakini hivyo ndivyo nilivyomuelewa mtoa mada.

Kwa mtazamo wangu, mtoa mada hajatenda haki kwa kugeuka hakimu kumhukum mnyika. Sifaham makosa ya mnyika, na pia sioni kama mnyika anatafuta umaarufu kwasababu kama mbunge niwajibu na jukum lake kuwakilisha maoni ya wanainchi inapobainika kuna utata au manung'uniko ya yakutoridhishwa na jambo flani.

Ni matokeo ya ndiyooo.
 
Na hii huruma kwa wazee wastaafu kwamba wapate hela yao kipindi hawajiwezi ili ziwasaidie imeanza lini?Tunaona wazee wastaafu wanavyohangaika kupata hizo fedha zao na wengine kufariki kwenye process za kufuatilia hayo malipo yao.

Mbona hawa wasionewe huruma?Kusema kuwa serikali ina nia njema na wastaafu ni kupotosha ukweli wa hali halisi.Huruma kwa wazee isitumike kama sababu ya kuipa nguvu hii sheria kwani kiuhalisia hiyo huruma haipo.

Kusema kuwa watanzania tuige mambo yanayofanywa na nchi zingine kwa nini viwe vitu selective kama hivi?Kwa nini tusiwaige hao kwa kuwajali watumishi kwa kuwapa mishahara inayokidhi na kuwapunguzia kodi na kuwa na sera za kiuchumi zinazozuia au kupunguza mfumuko wa bei?Kwa nini tunaiga mfumo wa mifuko ya hifadhi ya jamii na hatuigi mifumo ya kuwajali watumishi wakiwa bado kazini?

Sielewi ni kwanini kama wafanyakazi wenyewe hawataki mfumo huo wa kinyonyaji serikali iendelee kung'ang'ania ikijifanya inamjali mfanyakazi kuliko anavyojijali!

Kwa nini basi angalau mfanyakazi asipewe option ya kuchagua wakati anajiunga na mfuko husika ama atachukua fedha mpaka astaafu au atachukua muda wowote atakapoamua kufanya mabadiliko yoyote kwenye ajira yake?Kwa nini iwe compulsory miaka 55 au 60?

Na kwa nini tunashuhudia hali hii huku mifuko kama NSSF ikitumika kwenye uwekezaji mwingi wa serikali na ambayo mingine ni kama wizi tu kwa wafanyakazi?Tunakumbuka Mkapa alipojibinafsishia mgodi wa Kiwira kwa mamilioni ya fedha za NSSF.

Wafanyakazi wanaamini kuwa mifuko hii sasa ndo kimbilio la serikali iliyofilisika kwa ufisadi na kwahivyo sheria hii mpya inalenga kuwadhulumu haki wafanyakazi wengi ambao wataacha au kuachishwa kazi miaka mingi kabla ya kustaafu kwani wengi hawatafika miaka hiyo na hata ambao watafika watapewa fedha ileile waliyotakiwa kupewa miaka 20 iliyopita!Kwa hii inflation rate nani yupo tayari kuacha fedha miaka yote hiyo?Kama sukari kilo ilikuwa sh.600 mwaka 2005 na sasa sh 2000 vipi thamani ya hela itapungua kwa miaka 20 ya kuisubiria?

Wafanyakazi wasikilizwe wanachokitaka na sio kuwaburuza kama majuha tu kwa kisingizio vyenye maneno ya kitaalamu na pembuzi yakinifu.

Mnyika yupo sahihi na anapaswa kuungwa mkono.
 
so·cial se·cu·ri·ty
Noun:
Any government system that provides monetary assistance to people with an inadequate or no income
(in the US) A federal insurance program that provides benefits to retired persons, the unemployed, and the disabled

Pen·sion/ˈpenSHən/
Noun:
A regular payment made during a person's retirement from an investment fund to which that person or their employer has contributed...
A boardinghouse in France and other European countries, providing full or partial board at a fixed rate
Verb:
Dismiss someone from employment, typically because of age or ill health, and pay them a pension

Hapo kwenye red colour, angalia sana usije ukawa umenasa kwenya ntego wa unafiki wa hali ya juu sana.
Kabla ya kuandika hayo hapo kwenye red colour, ulitakiwa kufanya utafiti uone kama kweli katika nchi hii ya Tanzania jambo hili linafanyika, au ni theory tu inayotumika ili kunyonya wafanyakazi.

Kifupi hali katika Tanzania yetu hii iko hivi:-

  • pension schemes sio kwa ajili ya kukusaidia utakapo kuwa mzee, ila ni kwa ajili ya kukusanya pesa kwa ajili ya matumizi ya serikali, mfano, wafanyakazi wa iliyokuwa jumuiya ya afrika mashariki, wote sasa ni wazee, hebu niambie wanalipwa pension kiasi gani ???
  • je?, unajua pension wanayolipwa wastaafu kwa sasa ??? mfano, aliyewahi kuwa mkuu wa majeshi Tanzania, kwa sasa ni mstaafu anayelipwa Tzs. 50,000 (Tzs. elfu hamsini tu) kwa mwezi. Hii inamsaidiaje yeye kama mzee mstaafu.

Angalizo kwa wote:
Kabla ya kutoa maoni kwenye mada nzito kama hii ya maswala ya pension, fanya utafiti kwanza, vinginevyo, wewe ni mnafiki tu, au wewe pia ni mmoja wa wanaofaidika na udhalimu huu wa kunyima wafanyakazi haki yao ya mafao.

Hapo juu angalia sana.
Mimi naona huo 'wendawazimu' ni kwa serikali kushindwa kukusanya kodi kwa ajili ya matumizi yake, na badala yake kukimbilia kuchulua pesa kwenye mifuko ya pension.
Mimi nimeshachukua 'withdrawal' yangu mwaka jana, na sasa nimeanzisha mradi unaoniletea mapato ya kutosha tu. Nimejiajiri. Niambie kama kufanikiwa kujiajiri ni 'wendawazimu', au serikali kuogopa kukusanya kodi kwenye makampuni ya madini ndio 'wendawazimu' ???
Humu JF kuna watu wa ajabu sana.

Kwa mamlaka niliyojipa natangaza rasmi hizi posts tatu ni posts of the decade. Na pia nawatangaza Mu-Israeli na King Kong III kama ma Griit Thinkaz bora wa mwaka 2012
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom