Umeelezea vizuri sana na analysis yako nimeipenda. But kuna vitu tunatofautiana kidogo.
Kwanza kumbuka kuwa nia ya compulsory pension scheme ni kwa ajili ya kukusaidia wakati wa uzee au kipindi ambacho huna uwezo wa kufanya kazi. Kufanya withdrawal ni kinyume na maana ya scheme yenyewe. Tungekuwa na voluntary/supplimentary schemes, ndio mtu ungeruhusiwa kutoa mafao yako muda wowote na pension yako ingetegemea na performance ya hiyo scheme.
Kuhusu formula, kila mfuko umeanzishwa na sheria yake na kila moja wakati wa kuanzisha walifanya analysis ya kutosha wakaona formula inayofaa ni ipi. Ukiangalia mifuko yetu, formula inayoumiza ni ya NSSF ambayo ni ya muda mrefu, ikufuatiwa na PPF ambayo ikikuja baada ya NSSF. PSPF na LAPF formula zao ni nzuri kwasabu mifuko ya hivi karibuni. Nafikiri hili suala SSRA wameshaliona na mifuko husika inarevise formula zao.
Sikubaliani na wewe kuwa actorial valuations zinaonyesha kuwa mifuko inakaribia kufa. Ukiangalia mifuko mingi inaidai serikali yetu kiasi kikubwa cha fedha. Ukijumlisha deni la serikali kwenye hesabu za haya mashirika unaona bao haya mashrika going concern yake ipo vizuri.
Kuhusu kuwekeza kwenye projects ambazo payback period yake ni ya muda mrefu, kumbuka kuwa pension fund zinawekeza kwa ajili ya kufulfil long term obligations. Wanachofanya ni matching ya cashflows zao na obligations zao. Nafikiri wanafanya vizuri kwenye portfolio zao na mixture of short term na long term assets ndio maana hatuwahi kusikia mfuko wowote umesuffer liquidity problems.
Nashukuru kwa majibu yako though hujajibu maeneo yote niliyopenda watanzania wapate majibu kwa mashaka ya fedha zao katika mashirika ya pendion.
Sheria hii unasema imejadiliwa April 2012 kwa nini haiku fanyiwa enough advocacy kwa wadau kabla ya kupelekwa bungeni kujadiliwa na kupitishwa? Vyama huru vya wafanyakazi vimekanusha kushirikishwa on behalf of employees. Lakini napata mashaka ya maelezo yako ktk hili, umesema pia kuwa katika sheria ya pension hapakuwepo clause ya withdrwal, je ipi ilijadiliwa April 12?
Act no 8 ya pension schemes iliyoiokoa PPF baada ya privatization ya parastotal organizations, sheria hii ilitangazwa sana na PPF kws sababu ilikuwa inawapa uhai wa kuishi wakati NSSF wakiipinga sababu ilikuwa inawanyima wanachama, kwa sababu walitegemea watumishi kutoka katika mashirika ya umma kuhamisha michango yao kwenda NSSF. Tunachojiuliza mbona hii haikufanyika kuelimisha wanachama mapema?
Katika mkutano wa mwaka 2006/2007 uliofanyika Golden Tulip organized by World Bank na ILO kutaka kutaka kuyaunganisha mashirika ya pension Tanzania baada ya kuwa utitiri wa mifuko yenye calculation tofauti, idea ya wafadhiri ktk mpango huu ni kutaka kuboresha pension system Tanzania, je hii imefikia wapi au imehujumiwa na mafisadi wansofadika na uwepo wa utitiri wa mifuko unaosababisha pension kuwa duni?
Katika majibu yako on investment policy esp on long term, the matching concept, ni sahihi, lakini je hizo fedha za wanachama mnazokopesha serikali za hazirudi kwa mujibu wa maelezo yako, je loan policy kwa govt inasemaje? Mnakopesha out of the policy or within the policy? Kama kuna loan policy je si wanakuwa na collateral ln the loan ambayo we can recover our money on default?
On the same, how do we project ufisadi and misuse of funds, is it part of our plans?