Mh. Mnyika kwa hili umepotoka!...

Kimsingi fao la kujitoa liachwe kuwa hiari kwa anayetaka kuacha michango(fedha) yake au anayetaka kuchukua haki yake aruhusiwe kufanya hivyo. Kwa kuwa terms za ajira hutofautiana kati ya mwajiriwa mmoja na mwingine,basi pia hata strategy au style ya kuweka akiba hutofautiana pia. Kwa mfano kuna watu wengi tu kutokana na mishahara yao na majukumu, 10% inayochukuliwa na mfuko wa pensheni ndio savings yake,hiyo 90% inayobaki baada ya kukatwa pensheni hawawezi ku-save kutokana na hali ya maisha.(Na hawa ndio wengi).
Kwa mchanganuo huo ni wazi kwamba mtu atakapoacha ama kuachishwa kazi atategemea ile akiba ndio aanzie maisha kwa wakati husika,sasa kama mtu ana miaka 35,kusubiri miaka 20 ndio achukue haki yake,huu ni ukatili! Na kipindi chote hichi (miaka 20) kama hakuajiriwa tena huyu mtu ataendesha vipi maisha yake.? Hata hivyo,hata kama kutakuwa na interest kwa kipindi NSSF/PPF...wanapokaa na hela yako,sidhani kwa mfumo wa ukuaji wa uchumi wetu kama itaweza kushindana na inflation rate!

Kama tunataka watu wengi wawe na ajira,lazima tu encourage watu kuwa wajasiriamali. Mtu anapoacha kazi na kwenda kuanzisha project yake,kama ni kuku,mgahawa,duka,basi,kilimo,real estate n.k,ni nafasi nyeti ya kuwapa watanzania wengine ajira. Na pale alipoacha kazi pia ni nafasi ya Mtanzania mwingine kuajiriwa. Hizi ndio ajira zenyewe,na sio zile tunazodanganywa na wanasiasa,eti ntawapa vijana ajira,..liers!Sasa tukiweka mfumo huu ni kuwatisha watanzania wasithubutu au waogope kujiajiri na badala yake wajishike kwenye ajira miaka nenda rudi hata kama ajira hiyo haibadilishi maisha yake. Watu waachwe wachukue haki yao mara tu wanapoacha au kuachishwa kazi bila kujali kama ataajiriwa tena au la! Wanaotaka kuendelea kubaki kwenye hii mifuko nao rukhsa.
 
Mh. Mnyika siku zote nimekua namuona ni mbunge makini sana na anayejishughulisha kujua mambo.

Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.

Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito.

Pili, ukiondoa PPF na NSSF, Tanzania ina mifuko mingine pia, nayo ni LAPF, PSPF na ZSSF, huko kote hakuna hilo fao la kujitoa na halikuwahi kutolewa. Mtu ukiacha kazi hata baada ya miaka 15 ukapata kazi kwenye private sector, utatakiwa kurudi kwa ajili ya mafao yako pale tu umri wako utakapofika miaka 55 au 60.

Tatu hili jambo la kutumia "ujinga" wa watu(nikimaanisha kutojua sekta hii vizuri) ili kujitengezea umaarufu wa mpito ndio jambo ambalo kizazi hiki kilianza kuonekana kuchoshwa nacho, lakini Mh. Mnyika anaonekana kurudia kosa lilelile la kutumia "ujinga" wa watu kujinufaisha. Kumwambia mtu ajitoe at 46yrs ni kumhakikishia uzee usiokua na uhakika wa staha. Mheshmiwa hebu pita BRELLA wakupe data za biashara zinazofunguliwa kwa mwaka, halafuna baada ya miaka mitano asilimia ngapi ya hizo biashara bado zinakuwepo sokoni. Nakuhakikishia utaweza kuanguka kwa mshtuko! Kuna data inaongelea 67% ya biashara mpya zitapotea sokoni ndani ya miaka mitano. Hivyo kusema watu watajifungulia biashara ni wishful thinking ambazo kila mtu yupo entitled kuwa nazo, ila we need a reality check hapa. Huwezi kuwa mwajiriwa miaka nenda rudi halafu siku ukapewa bulungutu, bila kuwa na basic entrepreneurial skills ukategema kusurvive sokoni.

Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).

Hivi mh. Mnyika anajua kuwa kwa kung'ang'ania kurudishwa kwa mafao ya kujitoa ni kuwaumiza wafanyakazi kuliko kama wangesubiri pensheni? Chukulia mfano, mtu aliyeanza kazi na miaka 25, akatumika kwa miaka 20. Atakuja kulipwa mafao ya kujitoa kwa kutizama kilichopo kwenye account yake kama kilivyo!!!... inawezekana kabisa huyu mtu kipato chake kilipanda sana ndani ya miaka mitano ya mwisho kutokana na experience, lakini kitakacholipwa ni kilichopo kwenye account yake kama kilivyo. Hapa utakuta kuna miaka ile 15 ya mishahara midogo akiwa bado junior officer ndio atakayojumlishiwa kama ilivyo na hii miaka mitano ya mishahara mikubwa. Wakati kama angekuwa ni wa kupokea pensheni angelipwa kufuatana na mishahara yake ya miaka ya mwisho kabla hajastaafu, ambayo mara nyingi ndiyo mikubwazaidi katika career ya mtu. Sijui mheshmiwa unalisemeaje hili...

Ukiwa kijana na nguvu zako, siku zote unaona kama kuwa mzee na kikongwe ni kitu cha mbali sana na kwamba unaweza kujipanga vizuri ili usizeeke kwa dhiki. Lakini ni muhimu tujiulize mh. Mnyika, kama ukiwa na nguvu na mshahara wako unachukuliwa asilimia 5% kwa ajili ya akiba ya uzeeni. Kwanini basi ushindwe kujipangilia maisha kwa hiyo asilimia 95% unayobakiwa nayo? Jamani tusipende cheap popularity, tuwawaingiza watanzania wenzetu kwenye dimbwi la dhiki wakati wa uzee, ambapo hata nguvu za kujishughulisha zimekwisha.

Hivyo ni vyema Mh. Ukakaa na wataalam wa kwenye hii mifuko, na hasa wataalamu wenye kufanya tathmini za mifuko ya pensheni na ujue kiundani nini hasa maana ya mifuko ya pensheni. Malengo na madhumuni yake. Ni vizuri na huwa nafarijika sana ninapoona mwanasiasa kijana akijishughulisha kutaka kujua mambo yanayokua ya kitaalam kwa kukaa na kujifunza kwa wataalam badala ya kuzunguka kusaka saini za wanasiasa wenzake ili kurudisha nyuma juhudi za muda mrefu za wataalam, wenye nia safi ya kuweka safety net kwa ajili ya wazee wa kitanzania na vizazi vyao.

Mimi nafkiri, badala ya kutaka kifungu cha mafao ya kujitoa kirudishwe na hivyo kujihakikishia kuona vurugu za wazee mitaani kama wale wa jumuiya ya afrika mashariki siku za usoni. Ni bora tukaacha sheria ibaki kama ilivyo(kwa maana ya kuzuia mafao ya kujitoa) ILA iongeze kifungu kitakachomtaka mwajiri awe na scheme ya kuchangia wafanyakazi ambayo ni over and above the basic pension scheme, ambayo mtu ataweza kuacess fedha zake pale atakapoacha kazi.

Bottom Line, pensheni ni muhimu muhimu sana... Kila siku ukienda kwenye fukwe za Zanzibar utakuta vizee vya kizungu vimejazana vinakula maisha. Na hii siyo rocket science. wenzetu waliona mbali, wakaamua kwa makusudi kufuta mafao ya kujitoa kama bado una nguvu zako. Ili unapozeeka uzeeke kwa heshma!

Niishie hapo, naomba tujadili bila matusi.
ee UDHAIFU mwingine huu,
]
 
Mh. Mnyika siku zote nimekua namuona ni mbunge makini sana na anayejishughulisha kujua mambo.

Lakini kwa hili la kutaka sheria ipitiwe upya na kurudisha mafao ya kujitoa naona amepotoka sana. Nashawishika kuamini kuwa nayeye kwenye hili ameingia kwenye mkumbo wa kusaka cheap popularity kwenye mambo ya kitaalamu zaidi. Najua nitashambuliwa kwa mtizamo huu ila nieleze sababu za mtizamo huu wangu.

Kwanza, katika nchi zote za Afrika kusini mwa Jangwa la Sahara, hakuna kitu kinaitwa mafao ya kujitoa kwa mfuko wowote wa pensheni. Hiki kituko kipo hapa Tanzania tu na chanzo chake ni wanasiasa wa aina za mh. Mnyika wanaokua tayari kuweka maisha ya maelfu ya wazee wa miaka ijayo kwenye maisha ya dhiki na hivyo kufa mapema baada ya kustaafu kwa ajili ya umaarufu wao(wanasiasa) wa mpito.

Pili, ukiondoa PPF na NSSF, Tanzania ina mifuko mingine pia, nayo ni LAPF, PSPF na ZSSF, huko kote hakuna hilo fao la kujitoa na halikuwahi kutolewa. Mtu ukiacha kazi hata baada ya miaka 15 ukapata kazi kwenye private sector, utatakiwa kurudi kwa ajili ya mafao yako pale tu umri wako utakapofika miaka 55 au 60.

Tatu hili jambo la kutumia "ujinga" wa watu(nikimaanisha kutojua sekta hii vizuri) ili kujitengezea umaarufu wa mpito ndio jambo ambalo kizazi hiki kilianza kuonekana kuchoshwa nacho, lakini Mh. Mnyika anaonekana kurudia kosa lilelile la kutumia "ujinga" wa watu kujinufaisha. Kumwambia mtu ajitoe at 46yrs ni kumhakikishia uzee usiokua na uhakika wa staha. Mheshmiwa hebu pita BRELLA wakupe data za biashara zinazofunguliwa kwa mwaka, halafuna baada ya miaka mitano asilimia ngapi ya hizo biashara bado zinakuwepo sokoni. Nakuhakikishia utaweza kuanguka kwa mshtuko! Kuna data inaongelea 67% ya biashara mpya zitapotea sokoni ndani ya miaka mitano. Hivyo kusema watu watajifungulia biashara ni wishful thinking ambazo kila mtu yupo entitled kuwa nazo, ila we need a reality check hapa. Huwezi kuwa mwajiriwa miaka nenda rudi halafu siku ukapewa bulungutu, bila kuwa na basic entrepreneurial skills ukategema kusurvive sokoni.

Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).

Hivi mh. Mnyika anajua kuwa kwa kung'ang'ania kurudishwa kwa mafao ya kujitoa ni kuwaumiza wafanyakazi kuliko kama wangesubiri pensheni? Chukulia mfano, mtu aliyeanza kazi na miaka 25, akatumika kwa miaka 20. Atakuja kulipwa mafao ya kujitoa kwa kutizama kilichopo kwenye account yake kama kilivyo!!!... inawezekana kabisa huyu mtu kipato chake kilipanda sana ndani ya miaka mitano ya mwisho kutokana na experience, lakini kitakacholipwa ni kilichopo kwenye account yake kama kilivyo. Hapa utakuta kuna miaka ile 15 ya mishahara midogo akiwa bado junior officer ndio atakayojumlishiwa kama ilivyo na hii miaka mitano ya mishahara mikubwa. Wakati kama angekuwa ni wa kupokea pensheni angelipwa kufuatana na mishahara yake ya miaka ya mwisho kabla hajastaafu, ambayo mara nyingi ndiyo mikubwazaidi katika career ya mtu. Sijui mheshmiwa unalisemeaje hili...

Ukiwa kijana na nguvu zako, siku zote unaona kama kuwa mzee na kikongwe ni kitu cha mbali sana na kwamba unaweza kujipanga vizuri ili usizeeke kwa dhiki. Lakini ni muhimu tujiulize mh. Mnyika, kama ukiwa na nguvu na mshahara wako unachukuliwa asilimia 5% kwa ajili ya akiba ya uzeeni. Kwanini basi ushindwe kujipangilia maisha kwa hiyo asilimia 95% unayobakiwa nayo? Jamani tusipende cheap popularity, tuwawaingiza watanzania wenzetu kwenye dimbwi la dhiki wakati wa uzee, ambapo hata nguvu za kujishughulisha zimekwisha.

Hivyo ni vyema Mh. Ukakaa na wataalam wa kwenye hii mifuko, na hasa wataalamu wenye kufanya tathmini za mifuko ya pensheni na ujue kiundani nini hasa maana ya mifuko ya pensheni. Malengo na madhumuni yake. Ni vizuri na huwa nafarijika sana ninapoona mwanasiasa kijana akijishughulisha kutaka kujua mambo yanayokua ya kitaalam kwa kukaa na kujifunza kwa wataalam badala ya kuzunguka kusaka saini za wanasiasa wenzake ili kurudisha nyuma juhudi za muda mrefu za wataalam, wenye nia safi ya kuweka safety net kwa ajili ya wazee wa kitanzania na vizazi vyao.

Mimi nafkiri, badala ya kutaka kifungu cha mafao ya kujitoa kirudishwe na hivyo kujihakikishia kuona vurugu za wazee mitaani kama wale wa jumuiya ya afrika mashariki siku za usoni. Ni bora tukaacha sheria ibaki kama ilivyo(kwa maana ya kuzuia mafao ya kujitoa) ILA iongeze kifungu kitakachomtaka mwajiri awe na scheme ya kuchangia wafanyakazi ambayo ni over and above the basic pension scheme, ambayo mtu ataweza kuacess fedha zake pale atakapoacha kazi.

Bottom Line, pensheni ni muhimu muhimu sana... Kila siku ukienda kwenye fukwe za Zanzibar utakuta vizee vya kizungu vimejazana vinakula maisha. Na hii siyo rocket science. wenzetu waliona mbali, wakaamua kwa makusudi kufuta mafao ya kujitoa kama bado una nguvu zako. Ili unapozeeka uzeeke kwa heshma!

Niishie hapo, naomba tujadili bila matusi.
Sober naona na wewe ni mmoja wa watu wanaokuwa wanapinga hoja za watu bila kutoa mapendekezo yoyote kitu ambacho hujitokeza kwa jamii isiyokuwa na elimu na uelewa wa kutosha. Mnyika ana haki kwa maoni yake binafsi nawe toa maoni yako. Kusema eti aachie wataalamu wakati hao wataalamu ndio wametufikisha tulipo hapa. Hata kama mtu una utaalamu mkubwa kama sio kwa manufaa ya jamii hauna maana na ndio wataalamu wetu wa TZ walivyo. Ufisadi mwingi unafanywa na watu ambao majina yao yanaanza na Prof/Dr n.k.
Hicho kigezo cha kusaidia wazee kimetoka wapi, wafanyakazi ni chini ya asilimia 10 ya watanzania wote hao walioko kwenye asilimia 90 serikali ina mpango gani na ndio wengi. Acha ushabiki wa kijinga eti wazee!!!!. Hii sheria ingeanza kazi baada ya kutoa kanuni zake ili watu wasianze kuhangaika. Wewe miaka 55/65 utafika lini wakati serikali haijaweka mazingira ya kufika huko. Hospitali za rufaa hazina vifaa/wataalamu/madawa n.k. Watu wanafanya kazi katika mazingira magumu bila ya serikali kulinda na kuzingatia afya za wafanyakazi. Ajali barabarani kila serikali haisimamii sheria zake vizuri sababu ya rushwa. Tunakula vitu ambavyo havina ubora na serikali imeshindwa kulisimami hilo, rushwa kwenda mbele. Watu wanamisongo ya mawazo, shinikizo la damu kutokana na serikali kushindwa kufanya mipango endelevu kulinda afya za watu.
Ukiangalia mifuko kama hii nchi za nje wafanyakazi wanapokuwa hawana kazi hulipwa mishahara mpaka siku wanapopata kazi. Hapa kwetu wanakula wakijua hawatakuwepo kipindi hicho cha baadae. Serikali wanatakiwa kushirikisha wadau wenye pesa zao na wanachama wanatakiwa kuchagua viongozi wa mifuko. Rais anateua viongozi wa mifuko, na pia anateua viongozi wa mamlaka ya kudhibiti hii mifuko, unategemea hapo kutakuwa na ukweli.
Watu inabidi mbadilike na jinsi ya kufikiri, ila mie nashauri serikali iondoe hiyo sheria wakati ikiendelea na mchakato wa kuboresha hii mifuko.

Kuhusu 95% ya mshahara mtu anapata kila mwezi ni ishu nyingine. Kwanza nikusahihishe siku hizi hata PPF makampuni mengi yanachangia 10% tu. Na wala mtu hapati hiyo 90% bali anapata 63% (90%x70%) baada ya kukatwa kodi. Sasa hii pesa ndio mtu aanzishe biashara? Haitoshi na ndio maana kuna mabenki ya kutoa mikopo otherwise mtu uweze kufanya biashara, usile vizuri, usilale sehemu bora yaani kwa ujumla maisha bora. Fanya tafiti ya maisha ya mtanzania utajionea mwenyewe. Mishahara midogo halafu toa matumizi yako ya mwezi kwenye hiyo asilimia 63% utajikuta huna kitu.

SOBER, SIJUI KAMA ULIKUWA SOBER WAKATI UNAANDIKA HIYO MSG YAKO
 
Jamani kiukweli wale wote wanaopinga hoja hii hawaguswi au ndo vibaraka wenyewe wa SSRA kama sivyo ni kati mafisadi wanaokusanya pesa zetu. Sasa huyo anaposema pension anayopewa mtu haijalishi kama aliajilwa au hakuajiliwa inaaply wapi Tanzania. Tanzania ni lazima uajiriwe na ufanye kwa muda wa miaka si chini ya kumi ndo unakuwa pensionable. Acha kukosoa vitu usivyokuwa na uhakika navyo rofa wewe.
 
Mkuu,sijui utafiti wako umeufanyia wapi lakini kiufupi unasikitisha.
1.Unaposema kwamba PPF ,mwanachama anachangia 5% siyo kweli kwani inasema kwamba mwajiri anaweza akachangia "up to" 15%. Kwa hiyo utaona kwamba waajiri walio wengi wanachangia 10% na wafanyakazi wanakatwa 10%. Hii ni simple logic ambaya kama kweli ulikuwa makini ungekuwa umeliona.
2. Unamshauri Mnyika akutane na wataalam wapi? Hawa ni kwamba wamesoma mashuleni na wanajua walichotakiwa kufanya lakini siasa zimejaa vichwa vyao( na allowances) kwa hiyo hawawezi kutoa ushauri wa kweli. Hivi unajua kwamba wakati wa fao la kujitoa lipo,mwanachama alikuwa anapewa michango yako na kuongezewa 5% ( kwa NSSF) na PPF hawakuongezei chochote regardless umechangia miaka mingapi? Kwa ufupi hela yako inakuwa imepungua thamani kwa kiasi cha kutisha . Mi nilichangia 22,000 kwa mwezi mwaka 1998 halfau mwaka 2011 narudishiwa 23,100 halafu unasema tuna wataalam wa mifuko hii? Wako wapi kama siyo waeishageuzwa matapeli?
3.Unaongelea mifuko kama LAPF kutokuwa na hili fao,je umefanya utafiti ni kwamba wanachama wa mifuko hii ni asilimia ngapi wanapoeteza ajira ukilinganisha na NSSF? Naoamba ufanye utafiti huo ndo utagundua kwamba mifuko mingine haikuwa na ulazima wa kuwa na hili fao
4.Hivi unajua kwamba kuna kibarua anafanya kazi miezi mitatu anakatwa NSSF an baada ya hapo ndo kazi kwake mwisho na ana miaka 20. Asubiri miaka 35 ili apate pensheni? Je unajua ili upate pensheni lazima uchangie miezi mingapi?
5. Pensheni za hao wazungu unaowaona hapo beach siyo lazima iwe ni michango yao. Ukishakuwa mwananchi wa nchi za wenzetu,hata kama hukuchangia mifuko hii ni kwamba utapata pensheni kwa haki yako ya kuzaliwa ukuwa mnorway,msweden,mjapan etc
 
Jamani wewe kapimwe damu hivi ni mtanzania kweli wewe au unacopy na kupest from Nchi za wenzenu zilizoendelea ambao huna kazi unapewa allowance ya kujikimu mpaka upate kazi nyingine Tje Tanzania hiyo ipo. Na je Tanzania uliona mtu anakuwa pensionable pasipo kuajiliwa ili mradi ni mzee tu basi wazee wetu akiwemo babu yako wasingekuwa nadhiki. Kama ndo mmoja kati ya illegal beneficiaries wa mifuko hii sasa imekula kwako wafanyakazi tupo imara na maiki kama wewe hauhusiki na jambo ile toka kwenye uwanja waachie wahusika usiwe kama SSRA anliyewaconsult Mifuko , Vyama vya waajiri n Vyama vya wafanyakazi japo nao wamekanusha badala ya kuwaona wadau wakuu yaani Key stakeholders ambao ni wafanyakazi wenyewe. Hivyo Acha kudandia gari mbele utakanyagwa. MNYIKA KAZA BUTI TUPO PAMOJA ACHANA NA WAVJINGA HAWA WACHACHE WANAOTAFUTA UMAARUFU KUTOKA SERIKALINI KINGUVU ILI WAACHIWE BIASHARA ZAO WAKWEPE KODI. KODI WATALIPA KAMA WAFANYAKAZI TUNAVYOLIPA NA MICHANGO YETU TUTAICHUKUA.
 
Mkuu usione labda namsema mh. Mnyika out of nowhere. Kusema anatafuta cheap popularity maana yangu ilibase kwanye mambo makuu matatu.

1. Muswada huu wa mabadiliko ya sheria uliopitishwa bungeni mwaka huu, mwezi wa Aprili, hardly miezi minne mpaka leo. Najiuliza kwa mbunge makini kama Mh. Mnyika alikua wapi wakati wakiujadili mpaka leo ajitokeze kuonekana "mtetezi wa wafanyakazi?" What if wafanyakazi wasingeraise the alarm!

2. Hoja hii iliibuliwa na Mh. mbunge wa kisarawe kama jambo la dharura, na spika aliamuru Mtoa mada ailete hoja yake rasmi, lirudishwe kwenye kamati husika, kamati ikutane na wadau wote, halafu kamati imshauri spika on the way forward baada ya kukutana na wadau.

3. Mh. Mnyika mara nyingi kama sio zote, amekua ni mtu wa kufanya kazi kwa data za uhakika na huwa namkubali sana kwa kufanya homework. Ajabu kwenye hili, mara baada ya kikao kuahirishwa kakutana na waandishi wa habari na anaongelea kutafuta sahihi za wabunge!!!... Yani jambo la kitaaluma analitreat kisiasa. jambo litalo impact maisha ya maelfu ya wazee siku za usoni analichukulia kama masihara na kitu cha kushangiliwa kama umefunga goli.

Hivi wewe Sober umetumwa na Magamba kuja kumshambulia JJ Mnyika na kutu CONFUSE sisi wafanyakazi?
1. NSSF na PPF angalia website zao wanatoa mafao ya kujitoa.
2. Katika nchi kama Tanzania ambayo inflation rate ina stand > 20% kumwambia mtu aliyestaafu na miaka eg 35 asubiri miaka 20 ndiyo uchukue mafao yake ni WIZI WA MCHANA KWEUPE.
3. Kuhusu MNYIKA alikuwa wapi wakati sheria hiyo inapitishwa April 14, 2012 Mbona Mnyika amelitolea ufafanunuzi vizuri hili, serikali iliwachezea WABUNGE KEKUNDI NA KEUSI. Una maana wewe hujasoma hayo maelezo au ndiyo umetumwa na MASHETANI wenzako kuhalalisha wizi wa pesa zetu.

MAELEZO YA MNYIKA WAKATI SHERIA HII INAPITISHWA
Naomba kumjibu mtoa maoni wa saa 3:56 swali lake: ‘mlikuwa wapi wakati haya yanapitishwa? Sio wapinzani, sio chama tawala... wote mlishiriki kutukandamiza.”, kwa kurejea taarifa yangu ya tarehe 3 Agosti 2012 kwa umma kuwa:

“Ikumbukwe kwamba kifungu cha kufuta mafao ya kujitoa kilichozua mgogoro hakikuwepo wakati muswada uliposomwa kwa mara ya kwanza bungeni tarehe 1 Februari 2012 bali kiliwasilishwa kupitia jedwali la marekebisho ya Wizara lililowasilishwa tarehe 13 Aprili 2012 bila malengo na madhumuni yake kuelezwa kwa ukamilifu.

Kupitishwa kwa kifungu hicho kumethibitisha maneno niliyoyatoa bungeni kuwa tumefika hapa tulipo kutokana na ‘uzembe wa bunge na wabunge’ na kwa hili pamoja na mchango nilioutoa bungeni kwa maandishi siku hiyo juu ya haja ya kuwa mfumo mpana zaidi wa pensheni na hifadhi ya jamii (universal pension and social security) pamoja na kuwa sikuunga mkono kifungu husika kilichoingizwa kinyemela naomba radhi kwa wananchi wa Ubungo na wafanyakazi kwa kutokuwasilisha jedwali la marekebisho kupinga kifungu hicho kuingizwa.

Izingatiwe kuwa ili kurekebisha hali hiyo tarehe 27 Julai 2012 kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani niliitaka Serikali itoe maelezo maelezo kuhusu taarifa zilizotolewa bungeni tarehe 13 Aprili 2012 kuwa wafanyakazi ikiwemo wa migodini kupitia vyama vyao walihusishwa kutoa maoni yaliyopelekea kufutwa kwa fao la kujitoa (withdrawal benefits); suala ambalo Chama Cha Wafanyakazi wa Migodini (TAMICO) kililikanusha.

Hata hivyo, Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya Hotuba yake tarehe 28 Julai 2012 hakutoa majibu yoyote bungeni kuhusu suala hilo hali ambayo imesababisha migongano kuendelea katika migodi mbalimbali kuhusu madai hayo hali ambayo kwa taarifa nilizozipata tarehe 1 na 2 Agosti 2012 inaweza kusababisha migomo migodini. Kufutwa kwa fao la kujitoa kumelalamikiwa pia na wafanyakazi na wadau wa hifadhi ya jamii katika Jimbo la Ubungo na katika taifa kwa ujumla.

Hata hivyo, suala hili na tukio husika litumike kama rejea ya bunge na wabunge kuikatalia Serikali kuwasilisha marekebisho yenye athari kubwa kipindi cha mwisho na hivyo wabunge kukosa fursa ya kupata maoni ya wananchi na pia Serikali itakiwe kuomba radhi kufuatia kulipotosha bunge kuwa wadau wa hifadhi ya jamii hususan wafanyakazi na vyama vyao walishirikishwa na kuridhia wakati ambapo wamejitokeza na kukanusha madai hayo yaliyotolewa na Wizara bungeni.

Kwa upande mwingine kufutwa kwa mafao ya kujitoa msingi wake haupo kwenye marekebisho ya sheria yaliyofanyika tarehe 13 Aprili 2012 pekee bali ni udhaifu katika mfumo mzima wa kisera na kisheria wa hifadhi ya jamii nchini hali ambayo inahitaji wadau kutaka mabadiliko makubwa.”

Tuendelee na mkutano.
John Mnyika
 
Hii ya kukutana na wataalam kaka naona uipe nafasi kubwa ili ijadiliwe from the point of view ya mwanachama. Tuone kimahesabu mtu akijitoa na kibaki kupata pension ni wapi ana pata faida na hifadhi kama dhana nzima inavyosema.

Nashukuru sana Sober na wachangiaji wengine kwa michango yenu. Nitatafuta wasaa wa kusoma yote kwa ajili ya kupata maoni. Kwasasa tunaendelea na mkutano mpaka saa 11 jioni kwa ajili ya kupata maoni ya moja kwa moja katika masuala ambayo nimeomba yafanyiwe uchambuzi, mnaweza kurejea kupitia:JOHN MNYIKA: MKUTANO WA MTANDAONI KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA HIFADHI ZA JAMII KWA HATI YA DHARURA KUREJESHA FAO LA KUJITOA

Nimepitia kwa haraka haraka hoja za wanaopinga nisiwasilishe muswada wa marekebisho ya sheria za hifadhi ya jamii kwa kile kinachoelezwa kuwa ni kukinzana na dhana ya malengo ya hifadhi ya jamii ya kutoa pensheni uzeeni, pia hoja za kupinga muswada usipelekwe kwa hati ya dharura bila kwa kuwa muswada husika wa kuwa haujatokana na mawazo ya watalaamu. Ni vizuri tu Sober na wengine mkarejea mchango wangu bungeni tarehe 13 April 2012 siku marekebisho husika yalipopitishwa ambapo nilitaka marekebisho ya ziada ambayo serikali haikuyaleta kwenye muswada wala marekebisho, aidha pitieni taarifa yangu kwa umma ya tarehe 3 Agosti 2012 ambayo mnaweza kuirejea kupitia: JOHN MNYIKA: Muswada binafsi kwa hati ya dharura: Marekebisho ya Sheria za Hifadhi ya Jamii kuhusu namna kinachoitwa 'marekebisho yaliyositisha fao la kujitoa' yalivyofanyika. Aidha, katika taarifa hizo nimeweka bayana kuwa "kufutwa kwa mafao ya kujitoa msingi wake haupo kwenye marekebisho ya sheria yaliyofanyika tarehe 13 Aprili 2012 pekee bali ni udhaifu katika mfumo mzima wa kisera na kisheria wa hifadhi ya jamii nchini hali ambayo inahitaji wadau kutaka mabadiliko makubwa". Nashukuru katika michango yenu nanyi mmeeleza baadhi ya marekebisho yanayopaswa kufanyika.

Nitarejea kutoa maoni yangu kuhusu hoja ambazo tumetofautiana kimtizamo kwa kuwa kwa sasa ninachofanya nikuchukua tu maoni mbalimbali. Kuhusu kushirikisha wataalamu, hili kwangu ni kipaumbele, ndio maana nimeandika rasmi kwa Katibu wa Bunge kutaka kupewa ushauri wa kitaalamu wa kutafsiri matakwa ya wafanyakazi na ya wadau wote muhimu wa sekta ya hifadhi ya jamii kuwa marekebisho ya sheria yenye maslahi kwa umma. Mpaka sasa ninapozungumza, hatujaandaa muswada wa sheria, wala kuwasilisha taarifa ya muswada huo yenye kueleza malengo na masuala mengine ya msingi. Nilichowasilisha ni kusudio, na katika taarifa yangu kwa umma nimeeleza bayana kwamba nimetoa wiki moja ya kupata maoni ikiwemo ya kitaalamu kabla ya kwenda hatua inayofuata. Uamuzi wa kukusanya saini, ni kupata wabunge ambao wanaona haja ya marekebisho ya dharura ili hatua huo ushauri wa kitaalamu na hatua nyingine ziweze kufanyika kwa haraka zaidi kuepusha migogoro inayoanza kujitokeza. Naendelea kupokea maoni.
 
Hivi wewe Sober umetumwa na Magamba kuja kumshambulia JJ Mnyika na kutu CONFUSE sisi wafanyakazi?
1. NSSF na PPF angalia website zao wanatoa mafao ya kujitoa.
2. Katika nchi kama Tanzania ambayo inflation rate ina stand > 20% kumwambia mtu aliyestaafu na miaka eg 35 asubiri miaka 20 ndiyo uchukue mafao yake ni WIZI WA MCHANA KWEUPE.
3. Kuhusu MNYIKA alikuwa wapi wakati sheria hiyo inapitishwa April 14, 2012 Mbona Mnyika amelitolea ufafanunuzi vizuri hili, serikali iliwachezea WABUNGE KEKUNDI NA KEUSI. Una maana wewe hujasoma hayo maelezo au ndiyo umetumwa na MASHETANI wenzako kuhalalisha wizi wa pesa zetu.

MAELEZO YA MNYIKA WAKATI SHERIA HII INAPITISHWA
Naomba kumjibu mtoa maoni wa saa 3:56 swali lake: ‘mlikuwa wapi wakati haya yanapitishwa? Sio wapinzani, sio chama tawala... wote mlishiriki kutukandamiza.”, kwa kurejea taarifa yangu ya tarehe 3 Agosti 2012 kwa umma kuwa:

“Ikumbukwe kwamba kifungu cha kufuta mafao ya kujitoa kilichozua mgogoro hakikuwepo wakati muswada uliposomwa kwa mara ya kwanza bungeni tarehe 1 Februari 2012 bali kiliwasilishwa kupitia jedwali la marekebisho ya Wizara lililowasilishwa tarehe 13 Aprili 2012 bila malengo na madhumuni yake kuelezwa kwa ukamilifu.

Kupitishwa kwa kifungu hicho kumethibitisha maneno niliyoyatoa bungeni kuwa tumefika hapa tulipo kutokana na ‘uzembe wa bunge na wabunge’ na kwa hili pamoja na mchango nilioutoa bungeni kwa maandishi siku hiyo juu ya haja ya kuwa mfumo mpana zaidi wa pensheni na hifadhi ya jamii (universal pension and social security) pamoja na kuwa sikuunga mkono kifungu husika kilichoingizwa kinyemela naomba radhi kwa wananchi wa Ubungo na wafanyakazi kwa kutokuwasilisha jedwali la marekebisho kupinga kifungu hicho kuingizwa.

Izingatiwe kuwa ili kurekebisha hali hiyo tarehe 27 Julai 2012 kwa nafasi yangu ya Waziri Kivuli wa Nishati na Madini kwa niaba ya Kambi Rasmi ya Upinzani niliitaka Serikali itoe maelezo maelezo kuhusu taarifa zilizotolewa bungeni tarehe 13 Aprili 2012 kuwa wafanyakazi ikiwemo wa migodini kupitia vyama vyao walihusishwa kutoa maoni yaliyopelekea kufutwa kwa fao la kujitoa (withdrawal benefits); suala ambalo Chama Cha Wafanyakazi wa Migodini (TAMICO) kililikanusha.

Hata hivyo, Waziri wa Nishati na Madini wakati wa majumuisho ya Hotuba yake tarehe 28 Julai 2012 hakutoa majibu yoyote bungeni kuhusu suala hilo hali ambayo imesababisha migongano kuendelea katika migodi mbalimbali kuhusu madai hayo hali ambayo kwa taarifa nilizozipata tarehe 1 na 2 Agosti 2012 inaweza kusababisha migomo migodini. Kufutwa kwa fao la kujitoa kumelalamikiwa pia na wafanyakazi na wadau wa hifadhi ya jamii katika Jimbo la Ubungo na katika taifa kwa ujumla.

Hata hivyo, suala hili na tukio husika litumike kama rejea ya bunge na wabunge kuikatalia Serikali kuwasilisha marekebisho yenye athari kubwa kipindi cha mwisho na hivyo wabunge kukosa fursa ya kupata maoni ya wananchi na pia Serikali itakiwe kuomba radhi kufuatia kulipotosha bunge kuwa wadau wa hifadhi ya jamii hususan wafanyakazi na vyama vyao walishirikishwa na kuridhia wakati ambapo wamejitokeza na kukanusha madai hayo yaliyotolewa na Wizara bungeni.

Kwa upande mwingine kufutwa kwa mafao ya kujitoa msingi wake haupo kwenye marekebisho ya sheria yaliyofanyika tarehe 13 Aprili 2012 pekee bali ni udhaifu katika mfumo mzima wa kisera na kisheria wa hifadhi ya jamii nchini hali ambayo inahitaji wadau kutaka mabadiliko makubwa.”

Tuendelee na mkutano.
John Mnyika

kwa nchi zilizoendelea ujiwa huna ajira au unasubiria kupata kazi sehemu nyingine kuna kitu kinaitwa Unemployment benefits unapewa ili kujikimu. na hili fao la kujitoa linachukua kabisa nafasi ya kusaidia mfanyakazi aliyeachishwa kazi akiwa chini ya umri huo aweze kutafuta namna ingine ya kujiajiri kwa kutumia akiba yake ya PPF au NSSF. jaribuni kuwa watafiti hata wewe uliyeandika report hii umekurupuka
 
Mafao ya kujitoa ni muhimu sana sawa na kwa nchi zilizoendelea wanavyoweza kutoa malipo ya unemployment benefits. hayo ni majina tu. hata nchi zingine wanawawezesha wafanyakazi kupitia mifuko hiyo ya hifadhi za jamii kwa njia nzuri...jiulize vitega uchumi vya PPF au NSSF vinamfaidisha vipi mwanachama? hakuna hata scheme iliyotengenezwa kumweshesha mfanyakazi apate mkopo kwa dhamana ya akiba yake iliyopo kwenye mifuko ya hifadhi za jamii. uliyeandika hapa jaribu kufanya utafiti usiandike tu mambo. ndio maana rushwa haitaisha nchi hii kwani maandalizi ya pensheni ni hafifu....ili ujenge Nyumba hapa Tz lazima uwe mfanyakazi mwizi mifuko hii inashindwa kusaidia hata Mortgage ili mwanachama apate makazi yaani nyumba na usafiri. mwanakimbilia kutoa mafao ya kipindi ambacho hazikusaidia kama mazishi na kipindi umezeeka na pesa inakuwa haina thamani halisi. ...anagalia wazee wa EA community wengine walilipwa cheque ya shilingi 500.
 
Back
Top Bottom