Mh. Mnyika kwa hili umepotoka!...

Mh. Mnyika kwa hili umepotoka!...

nachoona hapa ni matunda ya multiple ID,mwanzinsha mada na baadhi ya wanaomuunga mkono naamini ni mtu moja anapigia upatu huu wizi wa magamba,tunasema hivi hizo pesa ni akiba zetu na tutazichukua tunapozihitaji! Kama unabisha subiri bunge likatae kurekebisha hiyo sheria uone tutakachofanya...kwa hili tupo tayari kwa lolote hata mvue nguo hatutakubali.nimemaliza...

Kama mleta hoja ninamuunga mkono hili lina tatizo gani. Mimi nimemuunga mkono lakini nimemponda alipopotoka na kusema kuwa wabunge wana PENSION wakati alitakiwa aseme ni GRATUITY.

Mbona wewe MTK kakuunga mkono kwa hii post yako, au nawe una multiple ID!!
 
1) Kama 90% ya mshahara haumtoshi mfanyakazi, na kama 10% ni makato ya shuruti kwa ajili ya pensheni (na sio fao), lakini bado mfanyakazi huyo anaamini hiyo 10% (+10% ya mwajiri) itamsadia basi apewe. Ina maana then tatizo liko mahali pengine, UDUNI WA MISHAHARA.

Tatizo ni uduni wa mishahara, hasa katika sekat rasmi ni bayana. Laiti kama hawa wafanyakazi wangekuwa na pato la wastani lenye kukidhi mahitaji muhimu mathalan ya nyumba, chakula, malazi, afya na elimu ni wazi wasingekuwa na utashi kwa umma wao wa kwenda kudai mafao pindi ajira zao zinapokoma. Na pengine wangekuwa na miradi halali ya kuwaingizia vipato hata kabla ya ajira zao kukoma.

Hivyo mgogoro huu kwangu ni kiashiria kingine cha sera (hasa za kiuchumi na kisiasa) zilizoshindwa. Haitwakiwi kuweka viraka bali ni kufanya total and complete overhaul ya sera na mifumo nchini.

2) Kama kusudio la zuio la kisheria ni jema hasa kwa wafanyakazi (?), kwa nini serikali ilifanya usiri mkubwa ktk mchakato na hatimaye uidhinishwaji wa sheria hiyo?

3) Ni muhimu tukapewa uhalisia (facts) i.e. independent and thorough financial viability of those provident/social funds. Lazima kuna walakini kwenye going-concern za haya mashirika. Tumesikia ripoti za CAG zikigusia madudu lakini sio ktk ujumla na ukubwa wake. So lazima kwanza tujue afya ya hayo makapu ya "hifadhi" i.e. uchotaji!
 
Naomba tuwa wakweli. 1 John 3:18-20 “Dear children, let us not love with words or tongue but with actions and in truth. This then is how we know that we belong to the truth, and how we set our hearts at rest in his presence whenever our hearts condemn us. For God is greater than our hearts, and He knows everything”
Hatuna ajira zenye uhakika hapa Tanzania. Maisha ni magumu especially kwa vijana. Unamaliza university kama una bahati utapata ajira baada ya muda mfupi. Lakini waliyowengi wanakaa kijiweni muda mrefu bila ajira. Si hivi tuu pia ajira nyingi ni za muda mfupi. Once ajira moja inapoisha mpaka kupata nyingine inachukua muda. Kwa mtazamo huu ni vema fao la kujitoa liendelee kuwepo tuu. Naungana na Hon.Mnyika na watanzania wengine kuomba ili jambo lipite. Acha watu wawe huru kuchukua fedha zao na kwenda kuanzisha chochote wanachopenda kufanya. Ona mabenki yanatoa mikopo kwa riba kubwa na kwa upendeleo. Je watu wanapata wapi mitaji? watu wataweza vipi kujiajiri?
Mwisho nawaachia neno hili:-

Ephesians 5:15-17 Be very careful, then, how you live — not as unwise but as wise, making the most of every opportunity, because the days are evil. Therefore do not be foolish, but understand what the Lord’s will is. ”
 
Mnyika ange raise hii concern yake wakati hii sheria ikipitishwa. Nashangaa hakufanya hivyo. Sijui anataka ijadiliwe tena upya kwa mantiki ipi.

Naye pia tumweke kwenye hilo kundi la BENDERA FUATA UPEPO!!

Kwa nini usimchukulie kama ni mbunge Muungwana kuliko wote kwa kukubali kwamba alifanya kosa na sasa anataka kurudia mchakato ili kufanya marekebisho?
 
Inawezekana ukawa sahihi ila hili neno " kusaka cheap popularity" ni neno la kucopy na kupest kutoka kwa watu wasiofikiri bila wewe kulifanyia editing, kwani hadi mtu kuwa mbunge tena sehemu kama jimbo la ubungo je huyu si maarufu?
 
......Najua nitashambuliwa....... .

Mimi naamini huwezi kushambuliwa, umetoa hoja then wengine watasoma na pia watatoa hoja, ukiwa na mashaka ya kushambuliwa utaanza kuogopa kusema some of the issues unazofikiri kwa kuogopa kushambuliwa. Nimeona hapo tu, nikaanza kupata taabu kuendelea kusoma hoja zako.
 
  • Thanks
Reactions: MI6
Nne, hii hadithi ya kupotosha ya Life Expectancy ya mtanzania ni miaka 53. Ni kweli Life expectancy ni miaka 53, ila ukokotaoji wake unapatikana kwa average ya vifo vyote nchini kwa mwaka. sasa kwa nchi kama yetu ambapo kuna vifo vingi sana vya watoto chini ya umri wa miaka mitano, si ajabu vikashusha life expectancy at birth. Lakini kama life expectancy ingetazamwa wakati wa umri wa kuanza kazi, say 20yrs, utakuta watanzania wengi wanafika miaka 65 na kuendelea... Hivyo si sahihi kusema watu wanakufa at 53 halafu mafao yatatolewa at 55yrs( hapa naona kuna gap kubwa mno ya uelewa wa hii concept).

Hapa kuna theory of life expectancy na Reality of life expectancy.

Kama kuna muda muafaka wa kubadilisha sheria hii na iwe sasa kwa maana, kadri siku zinavozidi kwenda ndo ambavyo muda wa kuishi unavopungua (No theory here it is FACT).

Kwa mtu aliajiriwa serikalini hawezi kuelewa Mnyika anamaana gani jamani.ipo siku watu watamkumbuka tu.
 
Hujishangai kuona wewe ndio umekurupuka bila kuja na data za kuunga mkono hoja na umeishia kukandia tu!

Mkuu nakupongeza kwa kuchambua kitaalam, huu ndo ukweli, sema siku hizi kupinga kila kitu imekuwa ndo style yetu.

Ni mazoea tu, watu akibadilisha walichokizoea hata kama ni kwa faida yao watakuwa wagumu tu.

Hawa kina Mnyika wanakurupuka tu, si unakumbuka hata ile ya nauli ya feri wao ni kupinga tu bora wapate attention ya watu.
 
Mtoa mada, kama kweli uhalisia ungekua kama unavyotiririsha hoja yako humu, kila mtu angekuwa mhamasishaji wa sera za mifuko hii. Umeleta mfano wa wazee wa majuu wanavyokula pensheni yao Zbar, mama yangu ni 'mla' pensheni kwa sasa lakini huko kujilaza kwenye hizo pwani za Zbar atakusikia tu kwenye radio pamoja na pensheni yake!
 
Sober,

Mbona na wewe unavuruga sasa. Ukiangalia post zako zote mimi ndiye nimekupa LIKES nyingi kuliko mtu yeyote humu. NImekupa LIKES kwa sababu unaongea kitaalamu kabisa na uko sahihi kwa kila hoja kiasi kwamba nimelazimika kuamini kwamba wewe ni mmoja wa staff wa PPF maana ungekuwa NSSF usingeongelea ile 5%.

Unachoharibu hapa kuhusu wabunge kuna jambo nilitegemea mtaalamu wewe ulieleze kitalamu kama mengine. Ubunge ni uwakilishi na wala si kazi au ajira. NImeona kuna mahala umembana jamaa aliyekusakama kutumia neno KUPOTOKA. Nakubaliana na wewe uko sahihi lakini pia kuna neno linatakiwa pia kupewa tafsiri sahihi ya kiswahili, nalo ni MSHAHARA WA MBUNGE.

Anachopewa mbunge si mshahara. Wanaobisha basi wanieleze tofauti ya Diwani na Mbunge nini nini? Mimi naona tofauti ni idadi ya wanaowakilishwa lakini concept ni ileile uwakilishi.

Hivyo, tusaidiane kutafuta neno zuri ili anachopewa mbunge kisiitwe mshahara, maana ukikiita kuwa ni mshahara ndipo unakaribisha misconception kwamba kama kuna mshahara wa mbunge basi kuna pension ya mbunge.

Hiki ulichosema kuwa mbunge akimaliza miaka mitano ile hela anapewa anapeleka kwenye kampeni ya uchaguzi hakiitwi PENSION, bali kinaitwa GRATUITY.

Ni hilo tu, otherwise niatendelea kukupa LIKES maana sijaona wa kukuzidi hoja katika unayoeleza. Uko sahihi kabisa endelea kutuelimisha.
Nimeshindwa kuendelea kusoma baada ya kufikia maneno niliyoyakuza na kuyapaka rangi nyekundu!.
Nidadafulie vizuri maana nasikia wabunge waliopita walipewa kiinua mugongo cha 40,000,000/= kila mmoja ni kweli au la!.
Na hapo kwenye blue jamani kidhungu kinani ni naniiiiii....... eheee MAMBO!.
 
ayo mambo ni sawa lakn uwez sema m2 amepotoka..ndoja na mm nseme ww umepotea..kwanza kbsa uwez fanansha tz na nch nyngne..2po nyuma sana..tz kla k2 siasa, bibi yangu hal leo anamiaka 70 na uche, ajapewa chake..tz systm imecorrupt mojomba,...mishahara dun maisha yenyewe mafub makato yenyewe upew..
 
Mnyika anacho fanya ni kupeleka hoja ili kila mtu au mbunge ajaribu kuangalia kwa kina zaidi kwani bungeni hakuna malaika.

Naamini kuna wabunge wengi wa ccm wanajua kufikiri bila kujali nani kaleta hoja na kufikia maamuzi mazuri! Kwani hiyo hoja ukumbuke ilipitishwa na binadamu si malaika kwa hiyo wanaweza kufikiria upya!

Kuna wachangiaji wanasema Mnyika alishindwa kuzuia mswada usiwe sheria kwa sababu wabunge wa wapinzani ni wachache. Swali, je sasa hivi anavyopeleka hoja bungeni wabunge wa upinzani wameshakuwa wengi kuliko wa CCM?
 
Na kama kweli sisi ni waigaji wa mambo mema kwa nini tusiige hili la PSPF ya Swaziland?

bigBox1_04.gif

[TD="class: headFont, colspan: 3"] PSPF[/TD]

[TD="width: 4"][/TD]
[TD="colspan: 5"]

[TD="bgcolor: #FFFFFF"] [TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="class: contentheading, width: 100%"] Withdrawal Benefits [/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]
printButton.png
[/TD]
[TD="class: buttonheading, width: 100%, align: right"]
emailButton.png
[/TD]
[TABLE="class: contentpaneopen"]
[TR]
[TD="colspan: 2"]
One can withdraw if the service is under 10 years and get interest of 8% per annum. This is paid as a lump sum.
[/TD]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
[/TD]
[/TR]
[/TABLE]
 
Mnyika anawakililisha mawazo yake na pia ya kundi kubwa la wafanyakazi wa mshahara wa kima cha chini na ambao hawana hakika ya ajira za kudumu. Hivi mnawafikiria wale wanaofanya kazi ya manamba kwa wahindi?
Mfano, I was working with certain institution ya wahindi kwa contract ya miaka 2, na nilikuwa nachangia NSSF, baada ya mwaka 1, nimepata kazi kwa govt, nachangia LAPF. sasa is it fair kuniambia nisubiri mpaka miaka 30 ijayo nikachukue 4M NSSF? waangalie sera zao. ni kweli mpo wataalam, lakin sisi wengine sio majuha wa kushindwa kufanya simple analysis. Ni wizi huo, mbona hamgusii maelelezo ya CAG kuhusiana na afya ya hiyo mifuko? Na kwanini hilo fao litolewe sasa na si enzi za Mkapa au Mwinyi. Ninyi wataalam hamkuwepo?

hapo kwenye RED ndipo nimegundua upeo finyu wa uelewa wa jambo hili. Wewe una contact ya miaka miwili ilikuwaje hadi ukapeleka NSSF.
 
ayo mambo ni sawa lakn uwez sema m2 amepotoka..ndoja na mm nseme ww umepotea..kwanza kbsa uwez fanansha tz na nch nyngne..2po nyuma sana..tz kla k2 siasa, bibi yangu hal leo anamiaka 70 na uche, ajapewa chake..tz systm imecorrupt mojomba,...mishahara dun maisha yenyewe mafub makato yenyewe upew....
 
Hivi hizo pesa wanazo kaa nazo NSSF unapochukua unapewa na riba?
 
Hii mifuko inasaidia sana kwa wazee wetu, kila mwezi wanapata kiasi kidogo hata kama ni kidogo ila kinasaidia sana tofauti na ukiwa umestaafu halafu huna uhakika hata wa Ths mia,, Angalia wazee wa Africa Mashariki wanavyopata shida...

Mnyika amekurupuka katika hili
 
hapo kwenye RED ndipo nimegundua upeo finyu wa uelewa wa jambo hili. Wewe una contact ya miaka miwili ilikuwaje hadi ukapeleka NSSF.

SIYO upeo finyu, ni uzoefu wake, pia nadhani anatusaidia kuelewa mamba ambayo ni zaidi na yale tunayoelewa, mimi pia nimeona watu wakipeleka NSSF wakiwa na mikataba ya mwaka 1, miwili, nk. actually ninachokusudia kusema ni kwamba, tusione mchango wa mtu kwa mtazamo wa ufinyu, lets see if that what you call ufinyu can contribute to what we know.Na pale tunapoona mwingine hajaelewa vizuri au hajaelewa kama sisi tulivyoelewa, tujenge hoja itakayofanya tuelewe sawa. mimi binafsi napenda the way watu wanavyokuwa na mitazamo tofauti, I really enjoy, and I like your constructive contributions.
 
Back
Top Bottom