Mgomo wa madaktari - Updates

kazi ipo. Unapodili na wasomi yahitaji umakini.
 
Wachukue mafaili warudi nyumbani na this time hamna atakayewaita kazini.
 

ROBOSOME Wewe ni mamluki unakula pesa za umma na magamba afu unajifanya kuitetea serikali...hivi wewe hujiulizi kwa nini siku hizi umeme unakatika bila wananchi kupewa taarifa? Unazani huo ndo uwajibikaji wa serikali yako? Ninawasiwasi hata makazi yako inawezekana yapo mikocheni kwa mawaziri.....AKILI ZAKO CHANGANYA NA ZAKE!
 
Waziri mkuu alipokutana na madaktari huko nyuma alitoa impression kwamba ki-msingi ameelewa na kukubaliana na madai ya madaktari. Na alienda mbele zaidi kwa kutangaza kuwa amewasimamia katibu mkuu na mganga mkuu (correct me if I am wrong) kutokana na tuhuma mbalimbali. Na hili la waziri mkuu na naibu wake alisema liko chini ya rais.

Sasa weeks chache baadae anakuja na taswira nyingine kabisa. Ndani ya hizi weeks (tangu akutane na madaktari) Pinda amegeuka toka kwenye taswira ya 'kiongozi wa watu' na kuwa Mtawala asiyeambilika.

Kumfukuza waziri wa afya na naibu hakuifanyi serikali ionekane dhaifu bali serikali itaonekana sikivu, iliyokamaa na kutambua kuwa mamlaka yake yanatoka kwa wananchi, hivyo kama wananchi (madaktari) wanasema fulani hafai basi serikali yao (serikali ya wananchi) inatakiwa iheshimu maamuzi ya wananchi. Lakini anachofanya Pinda ni sawa na kuutangazia umma wa Tanzania serikali ni ya watu wachache kwa ajili ya wachache. Na ndio maana hata hao wachache wakiugua wanaenda India na sio mwananyamala wala Muhimbili. Hii sio sahihi hata kidogo lakini ndio mtaji wa Pinda.

Kwa upande mwingine nahisi serikali hawajifunzi chochote, na wana-understimate hasira za wananchi (sio madaktari tu). Huu mgomo unaweza kugeuka balaa. Sidhani kama utaishia kwa madaktari peke yao. Kama serikali haitajimbua basi wasishangae sekta nyingine wakaanguna na madaktari. Mgaya hatoweza kuzima moto. Mwenye macho haambiwi tizama.
 
Kinachonishangaza ni jinsi ambavyo watu humu ndani wanona kuwa Madaktari wana haki kwa kila wanachokisema. Tunajua umuhimu wao katika jamii lakini wao wasijione kuwa bora kuliko watumishi wengine serikalini. How do you demand kwamba Waziri lazima aondoke na unataka kweli aondolewe? This is holding the government at ransom. walitaka Mtasiwa na KM waondoke wakaondoka, tena masikini KM akampoteza mama yake in the process. Ndugu zangu Madaktari, mgomo si suruhisho la kila kitu. Hebu fikiria roho za maskini wangapi wanakufa kwa sababu ya migomo yenu. Hamna hata Kwaresma nyinyi? Hiki mnachokifanya ni kwa manufaa ya nani kama sio nyinyi na matumbo yenu? Mna tofauti gani na mafisadi? I hate ufisadi lakini hili mnalolifanya ni well out of control and I will never support this. Doctors must be declared as enemy number one of the common mwananchi! Mkielezwa mnaanza kubwaga matusi humu, well sishangai kwani kama mnaruhusu watu kufa mahospitalini ili mifuko yenu itune, then matusi is just a drop of water in the indian ocean. As we stand, Doctors wanalipwa kuliko cadre yoyote serikalini; mnataka mlipwe kama wabunge????? For this one, doctors you sack!!!
 
temeke hospital mbna mgomo. Na Wagonjwa watishia kuwapiga madaktari. Hii ni NEWSHOUR ya ITV.
 
:embarassed2: yametufika wa-tz kwa kukosa hekima na busara ya kutatua matatizo yetu wenyewe mpaka waje wazungu. AIBUUU
 
Hii itawaamsha watanzania na kudai haki zao kwa serikali legelege
 
Sasa hivi nimetoka kukutana na muajiliwa wa muhimbili.....kaniambia
---siku ya leo hakukuwa na huduma yoote isipokuwa ya watoto pekee
---madkatari hawapo kabisa.....wameshinda kwenye vikao..
kaniambia kwa kweli hali ni mbaya sana.....
 

Wewe usilete habari za umeme kwenye habari za madaktari. Huo umeme si wanakula fedha Tanesco ambao wako watu kama wewe pale, wasiojuwa kuwajibika, wasiojuwa kutenda kazi kusukumia mpira kwa waziri, waziri ndio anaendesha mitambo ya Tanesco? wewe kuwa makini kidogo, wacha kufikiri kwa kutumia kingine zaidi ya kichwa chako.
 

nchi hii inahitaji ukombozi wa kweli sio wa kuwaondoa mawaziri, wakati viongozi wote ni wabovu. Mabadiliko ni ccm itoke mkuu. Unakataa nn kwamba madaktari hawatumiwi na kundi fulani na wamekuwa affected na mob psychology. Haiwezekani wakampa masaa 72 rais atekeleze kuwawajibisha mawaziri kwa matakwa ya madaktari. Wangetumia busara ku-finalize madai yao. Na huko kuto tumia busara kujiona uko sahihi kumbe uko-wrong ni mob-psychology.
 


Waacheni wagome serikali yenyewe imejaa wezi tu wanagawana raslimali za taifa hili. watu wachache wanavimbiana matumbo. Hivi mtu amuoshe mgonjwa vidondo aokoe maisha. wengine wanakufa mikononi mwao wakijaribu kuokoa na nk unampa 20,000 posho then mtu anasinzia bungeni kujamba tu mle ndani unampa 70,000 sijui 200,000 then kwa hawa unasema si haki yao. Daktari kajipinda kasoma kajitolea kuokoa nafsi ila hana dhamani. Daktari na mwalimu si watu wa kudharauliwa kabisa. Midude yenyewe haijali kisa inatibiwa India shwani zao. Kwani huyo waziri ana ulazima gani wa kuwa waziri kama watu wake hawamtaki?????????????????????? Democracy ifanye kazi. hata kwenye makampuni mkijikusanya wafanyakazi 20 mkaandika barua hamumtaki meneja lazima abadilishwe au aondolewe. Utaongozaje mtu ambaye hataki umuongoze? Madaktari wameshasema hawamtaki Waziri period they better **** him off.
 

Si hivyo mkuu..Raisi tumempa ridhaa ya kuteua mawaziri kumsaidia yeye katika majukumu yake ya kila siku. ma Dr. wako chini ya wizara ya afya wana matatizo ambayo yanahitaji kusimamiwa na wizara yao husika. sasa basi yasipotatuliwa wanakosa imani na ngazi husika za wizara akiwema waziri wao. kwa maana hiyo haiingii akilini kufanya mazungumzo na yuleyule aliyeshindwa muda wote. ndio maana kipengele cha hao waheshimiwa kupigwa chini faster kikawa mbele, then mazungumzo yaendelee sawa mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…