Mr George Francis
Senior Member
- Jun 27, 2022
- 186
- 212
MGAWANYO WA MALI ZA FAMILIA BAADA YA MUME NA MKE KUACHANA.
SEHEMU YA 2
Mgawanyo wa mali za familia baada ya mume na mke kuachana unapaswa ufanyike kwa kuzingatia haki, ili kila mmoja apate kile anachostahili bila upendeleo.
Katika kupima mchango au jitihada za mume au mke juu ya upatikanaji wa mali za familia kumekuwa na mitazamo mbalimbali.
Kwenye kesi ya
ZAWADI ABDALLAH vs IBRAHIM IDDI [1981] TLR 311
Kulikuwa na Mitazamo miwili kama ifuatavyo;
(1). Lazima kuwe na mchango wa mojakwamoja wa mume au mke wa kifedha, mali au kazi katika upatikanaji wa mali husika.
•Hivyo kazi za nyumbani na malezi ya watoto havipaswi kuhesabiwa kama mchango juu ya upatikanaji wa mali husika.
=Huu ni mtazamo wa kihafidhina. Ni mtazamo wa kizamani na usioendana na mazingira au mahitaji ya sasa. Mtazamo huu sio sahihi.
(2). Sio lazima kuwe na mchango wa mojakwamoja wa kifedha, mali, au kazi katika upatikanaji wa mali husika za familia.
•Hivyo kazi za nyumbani na malezi ya watoto ni lazima kuzingatiwa na kutamburika kama mchango muhimu katika upatikanaji wa mali husika.
=Huu ni mtazamo huria. Ni mtazamo wa kisasa na unaoendana na mahitaji ya sasa. Mtazamo huu ni sahihi.
Kutokana na mtazamo huria, shughuri za nyumbani zinazofanywa na mke au mume zinatamburika mchango au jitihada za pamoja katika upatikanaji wa mali za familia.
Ndoa inapovunjika mwanandoa anayo haki juu ya mali za familia hatakama hakutoa mchango wa kifedha wa mojakwamoja juu ya upatikanaji wa mali husika.
Mume kuwa na kazi inayompatia kipato kikubwa kuliko mke au mke kuwa na kazi inayompatia kipato kikubwa kuliko mume hakupaswi kuwa sababu ya upande mwingine kukosa haki katika mgao wa mali za familia baada wawili hao kuachana.
BI HAWA MOHAMED vs ALLY SEFU [1983]TLR 32
Ni kesi ya kihistoria kuhusiana na mgao wa mali za familia.
Mahakama ya Rufani iliamua kwamba
"Kwasababu ustawi wa familia ni muhimu katika utendaji wa shughuri za kiuchumi za familia hivyo ni muhimu kuziangalia kazi za nyumbani anazofanya mke au mume kama sehemu ya mchango au jitihada juu ya upatikanaji wa mali husika."
NB: MGAO WA MALI SIO LAZIMA UWE 50%/50%
Je, unapenda kujua ni kwanini?
Inaendelea....
Prepared By
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Contacts: 0713736006
SEHEMU YA 2
Mgawanyo wa mali za familia baada ya mume na mke kuachana unapaswa ufanyike kwa kuzingatia haki, ili kila mmoja apate kile anachostahili bila upendeleo.
Katika kupima mchango au jitihada za mume au mke juu ya upatikanaji wa mali za familia kumekuwa na mitazamo mbalimbali.
Kwenye kesi ya
ZAWADI ABDALLAH vs IBRAHIM IDDI [1981] TLR 311
Kulikuwa na Mitazamo miwili kama ifuatavyo;
(1). Lazima kuwe na mchango wa mojakwamoja wa mume au mke wa kifedha, mali au kazi katika upatikanaji wa mali husika.
•Hivyo kazi za nyumbani na malezi ya watoto havipaswi kuhesabiwa kama mchango juu ya upatikanaji wa mali husika.
=Huu ni mtazamo wa kihafidhina. Ni mtazamo wa kizamani na usioendana na mazingira au mahitaji ya sasa. Mtazamo huu sio sahihi.
(2). Sio lazima kuwe na mchango wa mojakwamoja wa kifedha, mali, au kazi katika upatikanaji wa mali husika za familia.
•Hivyo kazi za nyumbani na malezi ya watoto ni lazima kuzingatiwa na kutamburika kama mchango muhimu katika upatikanaji wa mali husika.
=Huu ni mtazamo huria. Ni mtazamo wa kisasa na unaoendana na mahitaji ya sasa. Mtazamo huu ni sahihi.
Kutokana na mtazamo huria, shughuri za nyumbani zinazofanywa na mke au mume zinatamburika mchango au jitihada za pamoja katika upatikanaji wa mali za familia.
Ndoa inapovunjika mwanandoa anayo haki juu ya mali za familia hatakama hakutoa mchango wa kifedha wa mojakwamoja juu ya upatikanaji wa mali husika.
Mume kuwa na kazi inayompatia kipato kikubwa kuliko mke au mke kuwa na kazi inayompatia kipato kikubwa kuliko mume hakupaswi kuwa sababu ya upande mwingine kukosa haki katika mgao wa mali za familia baada wawili hao kuachana.
BI HAWA MOHAMED vs ALLY SEFU [1983]TLR 32
Ni kesi ya kihistoria kuhusiana na mgao wa mali za familia.
Mahakama ya Rufani iliamua kwamba
"Kwasababu ustawi wa familia ni muhimu katika utendaji wa shughuri za kiuchumi za familia hivyo ni muhimu kuziangalia kazi za nyumbani anazofanya mke au mume kama sehemu ya mchango au jitihada juu ya upatikanaji wa mali husika."
NB: MGAO WA MALI SIO LAZIMA UWE 50%/50%
Je, unapenda kujua ni kwanini?
Inaendelea....
Prepared By
Mr George Francis
Email: mr.georgefrancis21@gmail.com
Contacts: 0713736006