Mfalme ‘akiuawa’ huwa inachukua muda mrefu sana Taifa kupona

Mfalme ‘akiuawa’ huwa inachukua muda mrefu sana Taifa kupona

Mkimwaga damu ya namba 1 hamtakaa muwe sawa kama nchi.

Bahati mbaya kijiti akapokea mwanamke. Double laana hii!
Marekani walipomuondoa JFK na kumuweka LBJ mwaka 1963 walidhani wameweza sana. Kina Edgar Hoover walipiga simu kwa Robert Kennedy kumpa taarifa huku wakiwa na furaha sana. Allen Dulles akaanza kumtukana JFK kusema "JFK, that man thought himself a god". Ila baada ya pale Marekani iliingia kwenye taharuki kubwa ambazo zinaigharimu Marekani mpaka leo hii.

JFK alikataa kabisa The Culture of Military Industrial Complex, Uncontrolled CIA na Zionist Influence on American Affairs. Kidiplomasia hakuna Raisi aliwahi kuifanyia makubwa Marekani kama yeye, hasahasa kwenye The Cuban Missile Crisis. Kiufupi kipindi cha JFK ndicho ambacho Middle East hakukuwa na vita.

Lee Kuan Yew aliwahi kusema Marekani chini ya JFK ingekuwa na mwelekeo mzuri sana. Ila ndiyo vile, wahuni walimhujumu. Huwezi kumuondoa kiongozi mkubwa vile halafu nchi isilipie hata kidogo. Baada ya JFK haya yakaanza kutokea:

1. Kuanguka kwa mfumo wa dhahabu (Collapse of the Gold Standard)
2. Marekani kushindwa vita Vietnam, wakifa maelfu.
3. Raisi kupewa skendo za ajabu hadi kujiuzulu.
4. Raisi wa awamu moja.
5. Nchi kuongozwa na taasisi za kiusalama siyo wananchi.

Mengi mno yameikumba Marekani baada ya JFK, fuatilia mwenyewe utaona tu!
 
Kaka RRONDO nimefurahi sana kukuona mzima. Juzi hapa nilitaka hadi kuanzisha uzi kuuliza kama uko salama. Kukuona hapa mzima napata faraja.

Kiufupi ni kwamba MUDA NI MSEMA KWELI hasahasa kwa kinachoendelea kipindi hiki. CCM wanaweza kudhani tatizo lao ni Samia na akitoka nchi itatulia kumbe wapi. Matatizo ni makubwa mno na yana mzizi mrefu. Siasa za 2015-2021, zilichangwa vibaya mno kwa kuangalia matumbo na leo. Hawakuzingatia kesho kitatokea nini.

I hope I'm wrong, lakini Tanzania yetu is headed for a very bigger crisis. Mbaya zaidi ni kwamba baadaya Mzee Mkapa kufariki nchi imekuwa haina BABA MLEZI ambaye anaweza kusema au kukemea kitu na watu wote wakaacha na kuogopa.
Mkapa angewezaje kukemea haya yaliyo tokea October 29 hali ya kuwa yeye mwenyewe alisha fanya hayo hayo huko zanzibar?
Kiufupi rais yeyote watz kiapo chake cha kwanza ni kihakikisha maslahi ya ccm yana simama alafu ya nchi ndo yafuate.
 
Ni kama unaleta mada ndani ya mada. Mada haijadili kifo kama adhabu.
Sawa! kwanini mnawaombea msiowapenda wafe? na inafikia mtu kufurahia kifo cha asiyempenda,
au imefikia sasa Kila anaekufa mnasema kauliwa as if mshaona daftari la uhai la Kila mtu!
Kwamba Fulani uhai wake kaandikiwa afe 2060 kwanini kafa kabla.
 
Andiko zuri mkuu, nakumbuka nili wahi kumwambia Kiranga kuwa mkapa ndio alikuwa Godfather wetu aliye baki.

Angalau ali tufikiria na kujaribu kubadilisha meza, tukampata jiwe licha ya kwamba hakuwa mkamilifu.

Mkapa ali mvumilia chekibobu licha ya kubanwa mbavu muda mwingine, chekibobu akajiona yuko above the law na kushindwa kumvumilia jiwe ona tunavyo uma meno leo hii.
Kuna kikao fulani kiliwahi kufanyika mwaka 2014, walikuja watu wengi wasomi wa ndani na nje ya nchi. Mzee Mkapa alikuwa mgeni rasmi. Walimshambulia maswali mengi mno, lakini yule Mzee alikataa kabisa kumshambulia CHEKI-BOBU na akasema wazi, hawezi kukanyaga vidole vya mtu. Miaka ya mwanzo CHEKI-BOBU alimfanyia vituko sana Mzee Mkapa lakini yule alitulia tu.

Kuna kipindi alianza kutembelea balozi za nchi mbalimbali baada ya kuambiwa zinamilikiwa na Mzee Mkapa. Alienda Afrika Kusini na maksudi kuomba auziwe jengo la ubalozi maana tunalipa gharama nyingi. Wakamuambia mbona ni la Mtanzania mwenzako Mhindi. Muhindi kuitwa akabanwa akasema jengo siyo lake ni la Mzee. CHEKI-BOBU kwa madaha akapiga simu kwa maksudi kwa Mzee kumuuliza kama jengo ni lake, na Mzee akakataa.

Basi CHEKI-BOBU akalitaifisha kuwa mali ya ummah. Alifanya hivyo kwa baadhi ya nchi. Kipindi hicho na Kiwila ikapamba moto, Mzee akabanwa akarudisha. Lakini ulikuwa huwezi kumkuta yule Mzee anaingilia majukumu ya mwenzake wale kutaka kumhujumu. Walipishana wazi-wazi kwenye gesi ya Mtwara ambapo CHEKI-BOBU akiwepo Mtera Iringa mwaka 2014 alitishia wazi-wazi kwamba wanaosababisha vurugu "Wenye pembe kubwa tutazikata" akimtishia Mzee.

Kiufupi JPM na CHEKI-BOBU walipwaya mno kwenye hili somo la STOICISM. Kuna kipindi tuliwaambia watu kwamba JPM kuna mambo anafanya hatakiwi kushangiliwa. Ndiyo tunapambana na rushwa, lakini kuna nyenzo nyingi na hili taifa bado ni changa sana abadilike. Wafuasi walitufurumushia matusi na kusema sisi ni tarumbeta za mafisadi.

================================================================================
Binafsi huwa naamini kitu kimoja hapa Tanzania: Mzee Mwinyi ndiye Raisi pekee wa Tanzania ambaye amekufa A Natural Death na kifo chake hakina minong'ono. Amekufa kwenye uzee mwema mno, ameshuhudia kijana wake kawa Raisi na amakufa kila mtu akiwa anampenda.

Mzee Nyerere, Mzee Karume, Mzee Mkapa na Mzee Magufuli vifo vyao vimejaa sana minong'oni ambayo inatia ukakasi, hata kama walikufa vifo vya kawaida kweli. Lakini vifo vyao vyote vinatokea wakiwa kwenye fukuto fulani la kisiasa au mabadiliko makubwa ya utawala wa nchi.

Yote tisa, mtawatia moyo watanzania, lakini siasa ni sayansi na ukikosea kanuni ni lazima ikulambe. JPM aliongwa akashupaza shingo. SSH anaonywa anashupaza shingo. Cheki-Bobu anaonywa akae mbali aridhike anashupaza shingo. Well !Nature Has a Bad Way of Fixing Things.

Suala la muda tu
 
Heshima yako MALCOM LUMUMBA usipotee sana. Katika kipindi kigumu kama hiki vijana wanahitaji hekima na busara za watu wenye akili kubwa kama wewe.
Ni kweli kabisa..

Na sijui watu kama Nguruvi3, Mag3, Mzee Mwanakijiji, Doctor Mama Amon wako wapi. Hata wakija huja kwa kubipu sana wakati taifa liko kwenye hali tete. Hata kule kwenye jukwaa la Great Thinkers hawaposti chochote kwa siku nyingi sana. Mzee Nguruvi3 uko wapi rafiki? Mada zako kule GT zimetulia kwa miezi mingi bila mwendelezo

Nyie wazee waheshimiwa njooni tu hukuhuku kwenye Jukwaa la Siasa - jukwaa la vurugu mechi lililo na mchanganyiko wa kila aina ya watu wajinga, wapumbavu, wapuuzi, walevi, wanafiki na wapiga propaganda tu wa kutetea pande zao bila facts, machawa nk

Nyie njooni tu. Shusheni nondo. Kwa uzoefu wangu, machawa mara nyingi huwa irrelevant kwenye mada nyingi zilizoenda shule kama hii kwa sababu wanakuwa hawana cha kuchangia. Hata wakiweka tusi, basi linakuwa irrelevant kwa kuwa linakuwa linaelea hewani tu kupingana na ukweli halisi...!!

Asante sana ndugu MALCOM LUMUMBA kwa elimu nzuri katika makala nzuri iliyochambuliwa
 
Mkapa angewezaje kukemea haya yaliyo tokea October 29 hali ya kuwa yeye mwenyewe alisha fanya hayo hayo huko zanzibar?
Kiufupi rais yeyote watz kiapo chake cha kwanza ni kihakikisha maslahi ya ccm yana simama alafu ya nchi ndo yafuate.
Mkapa alimkemea Cheki-Bobu na Mtandao mwaka 2015 kuhusu kumuweka Membe unadhani angeshindwa kukemea ujinga wa SSH ??? Mkapa alisema kabisa wakate Lowassa na wakamkata na akatia mkwara kama mtu hataki atoke na wote wakakinywea. Binafsi naamini kabisa Mzee Mkapa angekuwepo hai wakati wa kifo cha JPM 2021, siasa za Tanzania zingekuwa za tofauti sana sanaa.

Ushawishi wa Mzee Mkapa ulikuwa ni mkubwa sana hapa nchini na huko nje. Kukupasha tu, hata kipindi kile Kagame na Jakaya wanaparurana, Mzee Mkapa alisafiri kwenda Kigali, Membe akalalamika kwamba lazima aambiwe wamezungumza nini, ila mambo yakatulia vizuri na uhasama ukafa. Kiufupi kifo cha Mkapa hakina tofauti na The Dismissal Chancellor Otto Von Bismarck. (If you know you know)
 
Andiko zuri mkuu, nakumbuka nili wahi kumwambia Kiranga kuwa mkapa ndio alikuwa Godfather wetu aliye baki.

Angalau ali tufikiria na kujaribu kubadilisha meza, tukampata jiwe licha ya kwamba hakuwa mkamilifu.

Mkapa ali mvumilia chekibobu licha ya kubanwa mbavu muda mwingine, chekibobu akajiona yuko above the law na kushindwa kumvumilia jiwe ona tunavyo uma meno leo hii.
Mkapa ndo anaye takiwa kulaumiwa kwa kupindua meza 2015 mwisho wa siku akatuletea Jpm ambaye alikuwa mshamba wa siasa.
Uelekeo wa siasa za tz ulianza kubadilika baada ya magufuri kuingia madarakani.
(1)Alizima bunge lisioneshwe live.
(2)Akazuia vyama vya siasa kufanya mikutano.
(3)Akaanzisha utamaduni wa kuteka na kuuwa wakosoaji wa serikali.
(4)akanzusha utamaduni wakuhonga wanasiasa wa upinzani ili wahamie ccm.
(5)Akaanzisha utamaduni wa kupitisha wagombea wa ccm bila kupingwa huku wapinzani wakikatwa.
Yaani tuseme kiufupi jpm alikuja kuvuruga mambo mengi sana ambayo watangulizi wake waliyajenga kwa damu.
Kiufupi kila kinacho endelea sasa mzizi mkuu ni siasa za magufuri.
Na mbaya zaidi watu wenye akili walisema sana kuwa haya mambo aliyo yaasisi magufuri yataligharimu taifa kwa miaka mingi hata baada ya yeye kufa mkaishia kuwaita vyeti feki sijui mafisadi.
 
Lazima wakilipie walichokianzisha na hali haitotulia coz ardhi ishakunywa damu ya mteule na wananchi wake..!!

Damu zitawalilia kila siku na hazitonyamaza, kama taifa tutapitia kipindi kigumu sana..!!
 
Mkapa ndo anaye takiwa kulaumiwa kwa kupindua meza 2015 mwisho wa siku akatuletea Jpm ambaye alikuwa mshamba wa siasa.
Uelekeo wa siasa za tz ulianza kubadilika baada ya magufuri kuingia madarakani.
(1)Alizima bunge lisioneshwe live.
(2)Akazuia vyama vya siasa kufanya mikutano.
(3)Akaanzisha utamaduni wa kuteka na kuuwa wakosoaji wa serikali.
(4)akanzusha utamaduni wakuhonga wanasiasa wa upinzani ili wahamie ccm.
(5)Akaanzisha utamaduni wa kupitisha wagombea wa ccm bila kupingwa huku wapinzani wakikatwa.
Yaani tuseme kiufupi jpm alikuja kuvuruga mambo mengi sana ambayo watangulizi wake waliyajenga kwa damu.
Kiufupi kila kinacho endelea sasa mzizi mkuu ni siasa za magufuri.
Na mbaya zaidi watu wenye akili walisema sana kuwa haya mambo aliyo yaasisi magufuri yataligharimu taifa kwa miaka mingi hata baada ya yeye kufa mkaishia kuwaita vyeti feki sijui mafisadi.
Alichokifanya Mzee Mkapa mwaka 2015, hakina utofauti na alichokifanya Mzee Nyerere 1995.

Walivuruga michakato ya kidemokrasia ndani ya chama kwa ubabe na wakapenyeza watu wao kwenye nafasi za Uraisi kisha hao watu wakawageuka vibaya sana. Mzee Mkapa alimgeuka Mzee Nyerere hadi kupelekea Mzee Nyerere kulia machozi na kujuta sana. Dakika zake za mwisho JPM alimgeuka Mzee Mkapa vibaya sana hadi kupelekea Mzee Mkapa kuwa na majonzi sana.

Mzee Mkapa alikuwa akiomba wakutane, bwana JPM anamkwepa Mzee Mkapa.
=============================================================================
Bottom Line: At Every Action There Is An Equal Opposite Reaction. Ukivuruga mchakato wowote wa haki na kuharibu mzani wa nguvu (Balance of Power) ni lazima ile kwako. Mzee Nyerere alimchukia Malecela, Kolimba, Kombe na wengine waliotaka mabadiliko, akatumia mabavu ila baadaye akajuta. Mzee Mkapa naye akakata watu kibabe akamuweka JPM na baadaye akajuta. Dhambi ambazo Mzee Mkapa alimtendea Mzee Nyerere tokea 1995-1999 ndizo hizohizo na yeye alitendewa na JPM kuanzia 2015-2019.

AND BY THE WAY: Mkapa na Samatta ndiyo wazee waliowahi kutoka waziwazi na kumwambia JPM ukweli mchungu mbele ya uso wake, jambo ambalo hakuna Mtanzania aliyediriki kulifanya. Hata Cheki-Bobu alikuwa anapiga majungu kimafumbo tu, hakuna na ujasiri wa kumvaa JPM. Mkapa na Samatta Rubbed It on His Face. They Bruised His Ego.

Maisha ndivyo yalivyo. Dunia siyo ya Baba Yako ishi kwa Unyenyekevu Mkubwa. SSH na Cheki-Bobu na wapinzani wao wakubwa wataenda kujifunza somo gumu mno, ambapo hata akiingia Nchimbi au mwingine nchi bado itakuwa haijatulia. Itachukua muda mrefu kidogo kurudi tulipokuwa mwanzo.
 
Mkapa alimkemea Cheki-Bobu na Mtandao mwaka 2015 kuhusu kumuweka Membe unadhani angeshindwa kukemea ujinga wa SSH ??? Mkapa alisema kabisa wakate Lowassa na wakamkata na akatia mkwara kama mtu hataki atoke na wote wakakinywea. Binafsi naamini kabisa Mzee Mkapa angekuwepo hai wakati wa kifo cha JPM 2021, siasa za Tanzania zingekuwa za tofauti sana sanaa.

Ushawishi wa Mzee Mkapa ulikuwa ni mkubwa sana hapa nchini na huko nje. Kukupasha tu, hata kipindi kile Kagame na Jakaya wanaparurana, Mzee Mkapa alisafiri kwenda Kigali, Membe akalalamika kwamba lazima aambiwe wamezungumza nini, ila mambo yakatulia vizuri na uhasama ukafa. Kiufupi kifo cha Mkapa hakina tofauti na The Dismissal Chancellor Otto Von Bismarck. (If you know you know)
Halafu watu wengi hawajui kutangulizwa kulianzia kwa Mwana Lupaso ili wammalize na dikteta.!!
 
Mkapa alimkemea Cheki-Bobu na Mtandao mwaka 2015 kuhusu kumuweka Membe unadhani angeshindwa kukemea ujinga wa SSH ??? Mkapa alisema kabisa wakate Lowassa na wakamkata na akatia mkwara kama mtu hataki atoke na wote wakakinywea. Binafsi naamini kabisa Mzee Mkapa angekuwepo hai wakati wa kifo cha JPM 2021, siasa za Tanzania zingekuwa za tofauti sana sanaa.

Ushawishi wa Mzee Mkapa ulikuwa ni mkubwa sana hapa nchini na huko nje. Kukupasha tu, hata kipindi kile Kagame na Jakaya wanaparurana, Mzee Mkapa alisafiri kwenda Kigali, Membe akalalamika kwamba lazima aambiwe wamezungumza nini, ila mambo yakatulia vizuri na uhasama ukafa. Kiufupi kifo cha Mkapa hakina tofauti na The Dismissal Chancellor Otto Von Bismarck. (If you know you know)
Basi maamuzi ya mkapa hayakuwa sahihi kwetu kama taifa hasa kwa kutuletea mtu kama magufuri.
Maana kila kinacho endelea sasa muasisi wake ni magufuri wenda angemuacha Rowasa akawa rais kusinge asisiwa siasa za ubabe na kutekana.
Alafu mkapa hana usafi wowote kiasi cha kuwa mfano kwa wengine maana hata yeye amejaa damu za watz kwenye mikono yake.
 
Alichokifanya Mzee Mkapa mwaka 2015, hakina utofauti na alichokifanya Mzee Nyerere 1995.

Walivuruga michakato ya kidemokrasia ndani ya chama kwa ubabe na wakapenyeza watu wao kwenye nafasi za Uraisi kisha hao watu wakawageuka vibaya sana. Mzee Mkapa alimgeuka Mzee Nyerere hadi kupelekea Mzee Nyerere kulia machozi na kujuta sana. Dakika zake za mwisho JPM alimgeuka Mzee Mkapa vibaya sana hadi kupelekea Mzee Mkapa kuwa na majonzi sana.

Mzee Mkapa alikuwa akiomba wakutane, bwana JPM anamkwepa Mzee Mkapa.
=============================================================================
Bottom Line: At Every Action There Is An Equal Opposite Reaction. Ukivuruga mchakato wowote wa haki na kuharibu mzani wa nguvu (Balance of Power) ni lazima ile kwako. Mzee Nyerere alimchukia Malecela, Kolimba, Kombe na wengine waliotaka mabadiliko, akatumia mabavu ila baadaye akajuta. Mzee Mkapa naye akakata watu kibabe akamuweka JPM na baadaye akajuta. Dhambi ambazo Mzee Mkapa alimtendea Mzee Nyerere tokea 1995-1999 ndizo hizohizo na yeye alitendewa na JPM kuanzia 2015-2019.

Maisha ndivyo yalivyo. Dunia siyo ya Baba Yako ishi kwa Unyenyekevu Mkubwa.
Yaa hapo nimekuelewa Mzee wangu ni mtu mwenye madini hasa.
 
Mkapa alimkemea Cheki-Bobu na Mtandao mwaka 2015 kuhusu kumuweka Membe unadhani angeshindwa kukemea ujinga wa SSH ??? Mkapa alisema kabisa wakate Lowassa na wakamkata na akatia mkwara kama mtu hataki atoke na wote wakakinywea. Binafsi naamini kabisa Mzee Mkapa angekuwepo hai wakati wa kifo cha JPM 2021, siasa za Tanzania zingekuwa za tofauti sana sanaa.

Ushawishi wa Mzee Mkapa ulikuwa ni mkubwa sana hapa nchini na huko nje. Kukupasha tu, hata kipindi kile Kagame na Jakaya wanaparurana, Mzee Mkapa alisafiri kwenda Kigali, Membe akalalamika kwamba lazima aambiwe wamezungumza nini, ila mambo yakatulia vizuri na uhasama ukafa. Kiufupi kifo cha Mkapa hakina tofauti na The Dismissal Chancellor Otto Von Bismarck. (If you know you know)
We mzee uko nondo Sana 🙏🙏🙏
 
Mwaka 235 A.D kule Roma aliuwawa Kaisari aitwaye Severus Alexander. Aliuwawa kwa hila za majasusi wake waitwao The Praetorian Guard ambao walikuwa ndiyo kikosi cha ulinzi na ujasusi cha watawala wa Roma. Mtu ulikuwa huwezi kutawala Roma bila kutumia hichi kikosi.

Makaisari wa Roma walikuwa wanaheshimika kama miungu (Demi-gods), na hata kuwagusa ilikuwa ni sawa na kupingana na amri ya miungu. Utulivu na mafanikio ya dola la Roma, ulitegemea sana uimara wa kiti cha Kaisari. Makaisari wengi wa Roma kabla ya mwaka 235 A.D walikuwa ni lazima watokwe kwenye familia kubwa Roma (Roman Aristocracy) ambapo walifundishwa mambo ya utawala na siasa tangu wadogo.

Severus Alexander alivyoingia kwenye kiti alianza kufanya mabadiliko makubwa sana ya kiuchumi, kisheria na kisiasa ambayo yaliifanikisha mno Roma ndani ya muda mfupi. Japo alikuwa na udhaifu mwingine mkubwa kwamba, alikuwa ni mtoto wa mama (Mama's Boy) ambaye hakuwa na uzoefu wowote wa vita. Hivyo alisoma mambo ya vita bila kwenda uwanja wa vita kama ilivyokuwa lazima kwa vijana wote wa Roma.

Hili tatizo ndilo lilimletea changamoto kwasababu alishindwa kusimamia nidhamu ya jeshi lake. Wanajeshi walikuwa wanafanya vitu vya hovyo lakini yeye kwakutokuwa na uelewa akawa anafanya nao mijadala tu. Watawala kabla yake walikuwa wanafahamu siasa za jeshi na waliweza kulidhibiti. Severus Alexander akiwa kijana mdogo alizidiwa na jeshi, kisha yeye na mama yake wakauwawa.

Baada ya kuuwawa, jeshi likamuweka madarakani askari mwenzao Maximius Thrax kama Kaisari mpya. Huyu hakuwa ametokea familia za watawala, na alikuwa hana elimu ambayo ingemsaidia kutawala. Katika utawala wake Roma ikaanza kuporomoka na ambapo kwa miaka 50 nchi haikuwa na mfalme anayeweza kumaliza muda bila kuuwawa na wanajeshi au majasusi. Hiki kipindi wanahistoria wanakiita The Third Century Crisis.

==================================================================
Kila nchi huwa na utaratibu wake wa kiutawala. Huo utaratibu ukivunjwa lazima madhara makubwa yawepo. Kwenye The Third Century Crisis walikuwepo watu zaidi ya 50 waliouwawa kwa kutaka kukalia kiti cha Kaisari ndani ya kipindi cha miaka 50. Kiufupi Roma ilikuwa imejaa vurugu kama utekaji, mauaji ya kutisha, vita, rushwa na dola kugawanyika.

==================================================================
IKO HIVI: Tokea mwaka 1961-2021, Tanzania imekuwa ikishikiliwa na kiti cha Uraisi. Raisi ni Baba, Raisi ni Mfalme, Raisi ni mungu-mtu, Raisi ni Jalala la lawama, Raisi ni alama ya umoja wa kitaifa na Raisi ni nguzo ya matumaini. Hii ndiyo Tanzania aliyoijenga Mzee Nyerere. Raisi anaweza akawa na madhaifu lakini tunamsitiri na kumstahi tukiwa na matumaini kwamba atamaliza muda wake halafu atakuja mwingine kurekebisha.

Ukweli mchungu ni kwamba miaka ya 1960's-1980's bara la Afrika liligubikwa na mapinduzi na muaji ya Maraisi. Mzee Nyerere alipona mara nyingi. Siyo kwamba alikuwa na nguvu, lakini watu wa ndani ya vyombo vya dola walikuwa wanamchukulia kama BABA YAO MZAZI. Wengi walijiuliza kwamba Mzee Nyerere akitoka nini kitafuata ???

Hata alipokuja Mzee Mwinyi ambaye Mzee Nyerere na kina Imran Kombe walimfanyia vimbwanga vingi kwasababu walikuwa hawamkubali, ukweli mchungu ulikuwa ni kwamba lazima amalize muda wake. Hili lilikuwa siyo suala la majadiliano bali mustakabali wa nchi.

Tatizo likaja mwaka 2005 alipoingia kaingia Cheki-Bobu Ikulu. Alivurunda mno nchi ikafika hadi kipindi wakafanya jaribio la kumleta Dikteta kurekebisha. Cheki-Bobu na udhaifu wake wote alivumiliwa na muda wake ukaisha. Mwaka 2015, aliingia Dikteta kwelikweli. Alifanya makubwa ndani ya muda mfupi huku akiacha vilio na maumivu mengi pia.

==================================================================
Bahati mbaya sana, wengi hawakumpenda na hawakumvumilia ambapo ilitakiwa mwaka 2025 awe anaondoka madarakani. Mbaya zaidi Tanzania kuna utamaduni wa pande mbili kupokezana miaka 10/10. Hivyo ni lazima Raisi amalize muda wake, mpende au msipende. Utamaduni huu ndiyo umeleta utulivu na amani kwa kipindi kirefu nchini.

Anaweza akaingia mvaa kobasi akasemwa sana, lakini hawezi kutolewa kwasababu lazima Raisi amalize muda wake. Kama hamumpendi msingepitisha jina lake kule NEC. Hivyo hata Wagalatia watasema na kutoa matamko, lakini hawafanyi jambo la kijinga kwasababu wanafahamu zamu yao itakuja.

Huu utaratibu unaweza kuonekana ni una ufedhuli mwingi lakini ndiyo ambao unafanya kazi kwa taifa changa kama letu (The Only Practical Method to Ensure Political Stability). Ni lazima mzani uwiane (Balance of Power), usipowiana ni lazima mtapata matatizo.

==================================================================
SHIDA INAANZA HAPA: Watu walio karibu na Raisi masaa 24/7/365 ni Majasusi na Wanajeshi. Hawa ndiyo humsaidia Raisi kutawala. Hapa Tanzania hili kundi tokea mwaka 1964 hadi 2021 lilijengwa kwa dhana kwamba Raisi hagusiki, hata iweje. Raisi ni mungu-mtu. Raisi ni Nchi. Raisi ni Baba. Hivyo kama kumdhuru subirini amalize muda wake ndiyo mtamgusa lakini mkimgusa akiwa madarakani mtayumbisha nchi nzima. Hili hata wale wenye falsafa tofauti ndani ya mfumo walikuwa wanakubaliana.

Baada ya mwaka 2021 utaratibu ulibadilika vibaya mno. MKUU WA NCHI aliguswa, kukawa na minong'ono, huku mahasimu wake wakajisifu hadharani kwamba "Sasa Bahari Iko Shwari" na kutamba kwa kejeli nyingi. Hakuna aliyewakeme. Miaka michache baadaye tunasikia minong'ono kwamba MKUU WA NCHI kweli alihujumiwa.

Ndiyo alikuwa Dikteta, Ndiyo alikosea mambo mengi tu. Lakini kwanini mlimpitisha mkifahamu tabia zake fika. Kwanini hamkusubiri amalize muda wake kama ambavyo mlimvumilia CHEKI-BOBU aliyekuwa anafanya mambo ya ajabu Ikulu yenye madhara makubwa kwa nchi ???

=================================================================
Tokea mwaka 2021 yametokea muaji makubwa ya kutisha kuwahi kutokea hapa Tanzania. Hayatakuwa mwisho kwasababu mzani wa madaraka haujakaa sawa. Mbaya zaidi imefahamika kwamba MKUU WA NCHI naye anagusika vizuri na haliwezi kutokea jambo lolote lile kubwa. Historia inaonesha kwamba mara nyingi mapinduzi makubwa, huzaa mapinduzi mengine. Nchi huchukua muda mrefu mno mpaka ije kutulia:

  • Mwaka 1651 waingereza walipindua mfalme wao na kumnyonga ila nchi ilikuja kutulia mwaka 1688 baada ya kuanzisha utaribu mpya wa kiutawala.
  • Mwaka 1789 wafaransa walipindu mfalme wao na miaka zaidi ya 30 nchi ilijaa damu na vita, ikaja kutulia mwaka 1814.
  • Mwaka 1776 makoloni 13 ya Marekani yaliasi dhidi ya Mfalme, na nchi ilikuja kutulia mwaka 1815 baada ya kumaliza ugomvi na Muingereza.
==================================================================
Hata hapa Afrika mchezo ni uleule tu:

RWANDA: walimfukuza Mfalme Kigeri ila mpaka leo kila utawala mpya umeingia kwa kumwaga damu. General Kayibanda, General Habyarimana na General Kagame, wote wameingia kwa bunduki. Ila makosa yalianza kule kwa Mfalme Kigeri.

UGANDA: walianza na kumtoa Mutesa. Akaja Obote akatolewa. Akaja Amini akatolewa. Akarudi Obote akatolewa. Sasa yuko Museveni naye akiondoka haijulikani Uganda itakuwa kwenye hali gani. Hakuna anayeweza kuvaa viatu vya Museveni.

ZIMBABWE: nako ni hivyo-hivyo tu. Mubage alitolewa akaingia Munangagwa.

NIGERIA: walau kipindi hiki wametulia na wanapokezana kimakabila na kidino

==================================================================
Tanzania na Kenya, MUNGU alitupendelea mno. Jinsi tulivyokuwa tunayaangalia madaraka (Approach Towards Leadership) mbali na madhaifu yetu mengi imakuwa ni kuvumiliana mno (Tolerance). Siyo kwamba sisi tuna kitu cha ziada kuliko wenzetu lakini tuna kiwango kikubwa cha kuvumiliana.

GHANA, South-Africa na Botswana ni mataifa ambayo yameanza kukomaa hapa Afrika linapokuja suala zima la kuvumiliana kisiasa. Sisi hapa Tanzania tunarudi miaka ya 60's kuishi maisha ambayo hatukuyaishi. Maisha ya machafuko (Political Instability). Kitakachotokea Tanzania kipindi hiki ni kwamba kiti cha Uraisi kitatingishwa mno kwa miaka mingi, hata huyu wa sasa akitoka.

Tumeshatengeneza BAD PRECEDENT, na kutulia mpaka pande zote ziumie na kupata hasara kubwa ndiyo tutarudi kuwa kawaida. Ila kwasababu NOBODY IS SAFE. Kiufupi hata uweke wanajeshi barabarani, muda wako utafika tu. Mlichokianzisha mwaka 2021 lazima mkinywee, tena mtakinywea vibaya sana.

Siasa ndivyo ilivyo, historia imejaa ushahidi wa hichi nachokisema kuanzia Rome, The Rashidun Caliphate, Mongol Empire, Tang Dynasty n.k Kumuua mfalme (Mzuri au Mbaya) na machafuko yasitokee huwa ni nadra mno.

====================================================​
The Rashidun Caliphate imenikumbusha kuuwawa kwa kiongozi wa Dola ya Kiislamu Swahaba Uthmaani ibn Affaan (RadhiyaAllahu 'anhu) kulileta matatizo na mgawanyiko mkubwa katika Umma na athari zake mpaka Leo zimeathiri Uislamu
 
Mwaka 235 A.D kule Roma aliuwawa Kaisari aitwaye Severus Alexander. Aliuwawa kwa hila za majasusi wake waitwao The Praetorian Guard ambao walikuwa ndiyo kikosi cha ulinzi na ujasusi cha watawala wa Roma. Mtu ulikuwa huwezi kutawala Roma bila kutumia hichi kikosi.

Makaisari wa Roma walikuwa wanaheshimika kama miungu (Demi-gods), na hata kuwagusa ilikuwa ni sawa na kupingana na amri ya miungu. Utulivu na mafanikio ya dola la Roma, ulitegemea sana uimara wa kiti cha Kaisari. Makaisari wengi wa Roma kabla ya mwaka 235 A.D walikuwa ni lazima watokwe kwenye familia kubwa Roma (Roman Aristocracy) ambapo walifundishwa mambo ya utawala na siasa tangu wadogo.

Severus Alexander alivyoingia kwenye kiti alianza kufanya mabadiliko makubwa sana ya kiuchumi, kisheria na kisiasa ambayo yaliifanikisha mno Roma ndani ya muda mfupi. Japo alikuwa na udhaifu mwingine mkubwa kwamba, alikuwa ni mtoto wa mama (Mama's Boy) ambaye hakuwa na uzoefu wowote wa vita. Hivyo alisoma mambo ya vita bila kwenda uwanja wa vita kama ilivyokuwa lazima kwa vijana wote wa Roma.

Hili tatizo ndilo lilimletea changamoto kwasababu alishindwa kusimamia nidhamu ya jeshi lake. Wanajeshi walikuwa wanafanya vitu vya hovyo lakini yeye kwakutokuwa na uelewa akawa anafanya nao mijadala tu. Watawala kabla yake walikuwa wanafahamu siasa za jeshi na waliweza kulidhibiti. Severus Alexander akiwa kijana mdogo alizidiwa na jeshi, kisha yeye na mama yake wakauwawa.

Baada ya kuuwawa, jeshi likamuweka madarakani askari mwenzao Maximius Thrax kama Kaisari mpya. Huyu hakuwa ametokea familia za watawala, na alikuwa hana elimu ambayo ingemsaidia kutawala. Katika utawala wake Roma ikaanza kuporomoka na ambapo kwa miaka 50 nchi haikuwa na mfalme anayeweza kumaliza muda bila kuuwawa na wanajeshi au majasusi. Hiki kipindi wanahistoria wanakiita The Third Century Crisis.

==================================================================
Kila nchi huwa na utaratibu wake wa kiutawala. Huo utaratibu ukivunjwa lazima madhara makubwa yawepo. Kwenye The Third Century Crisis walikuwepo watu zaidi ya 50 waliouwawa kwa kutaka kukalia kiti cha Kaisari ndani ya kipindi cha miaka 50. Kiufupi Roma ilikuwa imejaa vurugu kama utekaji, mauaji ya kutisha, vita, rushwa na dola kugawanyika.

==================================================================
IKO HIVI: Tokea mwaka 1961-2021, Tanzania imekuwa ikishikiliwa na kiti cha Uraisi. Raisi ni Baba, Raisi ni Mfalme, Raisi ni mungu-mtu, Raisi ni Jalala la lawama, Raisi ni alama ya umoja wa kitaifa na Raisi ni nguzo ya matumaini. Hii ndiyo Tanzania aliyoijenga Mzee Nyerere. Raisi anaweza akawa na madhaifu lakini tunamsitiri na kumstahi tukiwa na matumaini kwamba atamaliza muda wake halafu atakuja mwingine kurekebisha.

Ukweli mchungu ni kwamba miaka ya 1960's-1980's bara la Afrika liligubikwa na mapinduzi na muaji ya Maraisi. Mzee Nyerere alipona mara nyingi. Siyo kwamba alikuwa na nguvu, lakini watu wa ndani ya vyombo vya dola walikuwa wanamchukulia kama BABA YAO MZAZI. Wengi walijiuliza kwamba Mzee Nyerere akitoka nini kitafuata ???

Hata alipokuja Mzee Mwinyi ambaye Mzee Nyerere na kina Imran Kombe walimfanyia vimbwanga vingi kwasababu walikuwa hawamkubali, ukweli mchungu ulikuwa ni kwamba lazima amalize muda wake. Hili lilikuwa siyo suala la majadiliano bali mustakabali wa nchi.

Tatizo likaja mwaka 2005 alipoingia kaingia Cheki-Bobu Ikulu. Alivurunda mno nchi ikafika hadi kipindi wakafanya jaribio la kumleta Dikteta kurekebisha. Cheki-Bobu na udhaifu wake wote alivumiliwa na muda wake ukaisha. Mwaka 2015, aliingia Dikteta kwelikweli. Alifanya makubwa ndani ya muda mfupi huku akiacha vilio na maumivu mengi pia.

==================================================================
Bahati mbaya sana, wengi hawakumpenda na hawakumvumilia ambapo ilitakiwa mwaka 2025 awe anaondoka madarakani. Mbaya zaidi Tanzania kuna utamaduni wa pande mbili kupokezana miaka 10/10. Hivyo ni lazima Raisi amalize muda wake, mpende au msipende. Utamaduni huu ndiyo umeleta utulivu na amani kwa kipindi kirefu nchini.

Anaweza akaingia mvaa kobasi akasemwa sana, lakini hawezi kutolewa kwasababu lazima Raisi amalize muda wake. Kama hamumpendi msingepitisha jina lake kule NEC. Hivyo hata Wagalatia watasema na kutoa matamko, lakini hawafanyi jambo la kijinga kwasababu wanafahamu zamu yao itakuja.

Huu utaratibu unaweza kuonekana ni una ufedhuli mwingi lakini ndiyo ambao unafanya kazi kwa taifa changa kama letu (The Only Practical Method to Ensure Political Stability). Ni lazima mzani uwiane (Balance of Power), usipowiana ni lazima mtapata matatizo.

==================================================================
SHIDA INAANZA HAPA: Watu walio karibu na Raisi masaa 24/7/365 ni Majasusi na Wanajeshi. Hawa ndiyo humsaidia Raisi kutawala. Hapa Tanzania hili kundi tokea mwaka 1964 hadi 2021 lilijengwa kwa dhana kwamba Raisi hagusiki, hata iweje. Raisi ni mungu-mtu. Raisi ni Nchi. Raisi ni Baba. Hivyo kama kumdhuru subirini amalize muda wake ndiyo mtamgusa lakini mkimgusa akiwa madarakani mtayumbisha nchi nzima. Hili hata wale wenye falsafa tofauti ndani ya mfumo walikuwa wanakubaliana.

Baada ya mwaka 2021 utaratibu ulibadilika vibaya mno. MKUU WA NCHI aliguswa, kukawa na minong'ono, huku mahasimu wake wakajisifu hadharani kwamba "Sasa Bahari Iko Shwari" na kutamba kwa kejeli nyingi. Hakuna aliyewakeme. Miaka michache baadaye tunasikia minong'ono kwamba MKUU WA NCHI kweli alihujumiwa.

Ndiyo alikuwa Dikteta, Ndiyo alikosea mambo mengi tu. Lakini kwanini mlimpitisha mkifahamu tabia zake fika. Kwanini hamkusubiri amalize muda wake kama ambavyo mlimvumilia CHEKI-BOBU aliyekuwa anafanya mambo ya ajabu Ikulu yenye madhara makubwa kwa nchi ???

=================================================================
Tokea mwaka 2021 yametokea muaji makubwa ya kutisha kuwahi kutokea hapa Tanzania. Hayatakuwa mwisho kwasababu mzani wa madaraka haujakaa sawa. Mbaya zaidi imefahamika kwamba MKUU WA NCHI naye anagusika vizuri na haliwezi kutokea jambo lolote lile kubwa. Historia inaonesha kwamba mara nyingi mapinduzi makubwa, huzaa mapinduzi mengine. Nchi huchukua muda mrefu mno mpaka ije kutulia:

  • Mwaka 1651 waingereza walipindua mfalme wao na kumnyonga ila nchi ilikuja kutulia mwaka 1688 baada ya kuanzisha utaribu mpya wa kiutawala.
  • Mwaka 1789 wafaransa walipindu mfalme wao na miaka zaidi ya 30 nchi ilijaa damu na vita, ikaja kutulia mwaka 1814.
  • Mwaka 1776 makoloni 13 ya Marekani yaliasi dhidi ya Mfalme, na nchi ilikuja kutulia mwaka 1815 baada ya kumaliza ugomvi na Muingereza.
==================================================================
Hata hapa Afrika mchezo ni uleule tu:

RWANDA: walimfukuza Mfalme Kigeri ila mpaka leo kila utawala mpya umeingia kwa kumwaga damu. General Kayibanda, General Habyarimana na General Kagame, wote wameingia kwa bunduki. Ila makosa yalianza kule kwa Mfalme Kigeri.

UGANDA: walianza na kumtoa Mutesa. Akaja Obote akatolewa. Akaja Amini akatolewa. Akarudi Obote akatolewa. Sasa yuko Museveni naye akiondoka haijulikani Uganda itakuwa kwenye hali gani. Hakuna anayeweza kuvaa viatu vya Museveni.

ZIMBABWE: nako ni hivyo-hivyo tu. Mubage alitolewa akaingia Munangagwa.

NIGERIA: walau kipindi hiki wametulia na wanapokezana kimakabila na kidino

==================================================================
Tanzania na Kenya, MUNGU alitupendelea mno. Jinsi tulivyokuwa tunayaangalia madaraka (Approach Towards Leadership) mbali na madhaifu yetu mengi imakuwa ni kuvumiliana mno (Tolerance). Siyo kwamba sisi tuna kitu cha ziada kuliko wenzetu lakini tuna kiwango kikubwa cha kuvumiliana.

GHANA, South-Africa na Botswana ni mataifa ambayo yameanza kukomaa hapa Afrika linapokuja suala zima la kuvumiliana kisiasa. Sisi hapa Tanzania tunarudi miaka ya 60's kuishi maisha ambayo hatukuyaishi. Maisha ya machafuko (Political Instability). Kitakachotokea Tanzania kipindi hiki ni kwamba kiti cha Uraisi kitatingishwa mno kwa miaka mingi, hata huyu wa sasa akitoka.

Tumeshatengeneza BAD PRECEDENT, na kutulia mpaka pande zote ziumie na kupata hasara kubwa ndiyo tutarudi kuwa kawaida. Ila kwasababu NOBODY IS SAFE. Kiufupi hata uweke wanajeshi barabarani, muda wako utafika tu. Mlichokianzisha mwaka 2021 lazima mkinywee, tena mtakinywea vibaya sana.

Siasa ndivyo ilivyo, historia imejaa ushahidi wa hichi nachokisema kuanzia Rome, The Rashidun Caliphate, Mongol Empire, Tang Dynasty n.k Kumuua mfalme (Mzuri au Mbaya) na machafuko yasitokee huwa ni nadra mno.

====================================================​
Asante sana mkuu Kwa madini kama haya.. Nakula zangu hapa Ngoma.. pembeni cappuccino.. Tunaangalia namna watavyo amua kuamlizana wenyewe
 
Basi maamuzi ya mkapa hayakuwa sahihi kwetu kama taifa hasa kwa kutuletea mtu kama magufuri.
Maana kila kinacho endelea sasa muasisi wake ni magufuri wenda angemuacha Rowasa akawa rais kusinge asisiwa siasa za ubabe na kutekana.
Alafu mkapa hana usafi wowote kiasi cha kuwa mfano kwa wengine maana hata yeye amejaa damu za watz kwenye mikono yake.
CCM inavuna matatizo iliyoyapanda kuanzia miaka ya 60's. Maamuzi mengi ya wazee wetu hayakuwa sahihi. Kupindisha Demokrasia na kuhujumu mabadiliko kwa kutumia taasisi za kijasusi, kipolisi na kijeshi hakukuwa sahihi. Mwaka 1995 baada ya Mzee Nyerere kutumia mabavu kukanyaga Demokrasia akidhani anaokoa nchi, madhara ndiyo tunayavuna leo hii. Taasisi zetu za usalama zilionjeshwa damu za watanzania ili kupata madaraka na ukajengeka utamaduni mbaya mpaka leo.

Kila napoanzisha mada kusema madhaifu ya Mzee Nyerere wajamaa huwa wanakuja kunibagaza. Lakini ukweli ni kwamba ili kuitoa nchi hapa ilipo ni lazima tupitia milango ambayo tuliingilia. Kuanzia muungano mwaka 1964, katiba mwaka 1977, vyama vingi 1995. Pamoja na kupitia sera nyingi ambazo zinatengeneza sheria ambazo zimezalisha taasisi za kiutawala ambazo zinatuongoza hii leo.

Bila kukubali kujitazama kwenye kioo na kutambua matatizo yetu yaanza tokea awamu ya kwanza hatuwezi kufika popote kama nchi.
 
Back
Top Bottom